Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Kuna kisa kimoja Cha kweli kabisa naomba Arsis anipe ufafanuzi na Tiba:
Baba yangu ni mgonjwa (maradhi ya akili) wa muda mrefu sana. Maradhi haya yalimpata 1996 nikiwa na umri miaka ..... Kwa kipindi hicho alikua mjasiliamali mdogo huko kijijini na alikua anamalengo ya kuamia mjini Kwa wakati huokwa ajili ya kujitanua kibiashara.

Ugonjwa ulimpata akiwa polini anapasulisha mbao Kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mjini, ghafla akapatwa na hayo maradhi akiwa uko poloni!

Sasa huu ugonjwa una mkangnyiko kutoka na ulivyotokea tunaamini amefanyiwa ushirikina. Kwa kipindi hicho chote watitembea sehem mbalimbali walishindwa baadae wakampeleka hospital akawa anatumia Sindano Kila baadae ya miezi 3. Kuanzia 1998 Hadi 2012 hivi ikawa zile dawa hazisaidii akawa tena Yuko serious sana.

Mwaka 2020 nikazunguka nae Mimi bila mafanikio nikampeleka milembe akapatiwa dawa ambapo hizi dawa alizopewa sasa ni mtihani sana Kwa sababu anatakiwa ameze Kila siku asubihi 3na jioni 1, Hadi Maisha yake yatakapofika mwisho. Kikubwa zaidi zinaua nguvu za kiume.
Kikubwa zaidi sana ni yeye kutotumia dawa hizo na hili hata alipokua anatumia Sindano hilokua ni changamoto kubwa sana. Hii inatokana na kutojitambua kama yeye ana maradhi ya akili.

Sasa hali hapo zamani ilipokua inataka kumtokea alikua anafaham kua siku zijazo atapatwa na hilo tatizo hivyo kama anapesa alikua anampatia mama anamwambia hii ni Ada ya Chama hata kama nikikuomba vipi usinipatie na anaweza akampatia na Pesa nyingine. Sasa Ile hali ikimjia tu anakua na huruma na ukarimu mkubwa sana mtu akija dukani kununua kitu anampatia vingine zaidi au kama Kuna mtu anapita nje anmwita anampatia ama Pesa au Mali kutoka dukani ni hivyo. Ile Pesa aliyokupatia akirudi kwenye hali yake yakawaida anakumbuka vizuri ikipungua hata 100 atakuambia.

Kwa ufupi ugomvi unatokea na hasira zaidi pale anapodai zile Pesa anakua na vitisho vikali na hata kutia kukupiga au kukupiga kabisa. Nilisoma Kwa namna hyo Hadi nikamaliza.

Kwa ufupi Hadi Leo baba yupo ni mgonjwa naomba Arsisi aniambie huu ugonjwa nini chanzo chake na unatibika na kama unatibika anifahamishe wapi atapata tiba.

Nina mengi ya kuongea athari tunazozipata au tuzazopitia kutokana na huu ugonjwa wa baba kama famiia na ukoo Kwa ujumla.
Simba; Yupo mkoa gani kwa sasa?
Simba.
 
Boss

Umenitaka ninukuu hata aya za biblia juu dalili za kuwa adam ndio binadamu wa kwanza

Biblia imeelezea tangua Allah alipoumba ardhi na vilivyomo ndani kisha siku ya saba Mungu akapumzika,kisha akamuumba mwanadamu kwa vumbi.la ardhi kisha akampulizia pumzi ya uhai na kuwa nafsi kamili au nafsi ya uhai

Tusome hapa

Mwanzo 2:7
[7]BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
And the LORD God formed man of the dust of the ground, and breathed into his nostrils the breath of life; and man became a living soul.

Na baada ya hapo adam akajulishwa majina ya vitu vyote na akavifahamu,na kila alivyoviita ndio vikawa majina yake kamili

Baadae biblia inaelezea adam akatiwa usingizi na bwana na akatolewa ubavu wake na kuumbwa mwanamke ambaye atakuwa msaidizi wa adam,huyu ni hawa

Kwahiyo hapa tunaona kabisa kabla ya adam na hawa hakukuwa na kiumbe kinaitwa mwanadamu au binadamu

Kwahiyo qur'an na biblia vyote vinadhibitisha kuwa hakika mwanadamu wa kwanza ni adam

Sasa kwa mara ya mwisho tunakuomba utupe dalili au taarifa nyingine za kuonyesha kuwa kuna binadamu wengine kabla ya adam

Asante
Arsis: Safi kabisa. Hapo umehitimisha niliyoyasema, nilisema Waislam hamuifati qur'an, mnachukua ya kwenye biblia na kuja kutafsiri kwayo.
Umeshindwa kuleta ushahidi wa kua adam ni mtu wakwanza au unao wa Qur'an? Pia Muislam umemtoa wapi Hawa? Au kwenye biblia vile vile?

Kwa mwenye uelewa, umeufanya mjadala kua mwepesi sana.
Arsis.
 
Simba alafu kama nakujua Mimi ni mzaliwa wa tanga nimekulia usagara madrasa nimesoma kwa ustadhat bi mwalimbuzi sijui unamfahamu..?
 
Mnapendana sana! Na wewe ulisema unapenda anavyotupenda☺️
Aminaaaaaaaaaaaaaaaa!💋💋Mungu asema tupendane!❤️❤️❤️
Sema nimesahau ni verse gani kwenye baibo😊!
Story ina pages wakushatroo naenda nazo aste aste ntawafikia tu uzuri nafocus kwenye muendelezo tu hata koments za waja ka sizioni kabisa

Cc Smart911
 
My Life Experience 03

Vitabu vya dini vipo sahihi kwa kiasi isipokuwa watafsiri wa hivyo vitabu ndo wanapindisha mambo.

Djinn ambae wapo kwenye vitabu vya dini ni kweli wameumbwa kwa moto, Pia anaezungumziwa kwenye vitabu vya dini sio hawa ambao ni Chotara/Djinn/Soul/Nafsi bali ni hao ambao wapo kwenye Ulimwengu/Dunia/Sayari ya pili baada ya hii yetu.

Jiulize tu Kiumbe kimeumbwa kwa moto then inakuaje akaweza kukaa na kustahimili katika ulimwengu huu wa kwetu ambao viumbe vyake vimeumbwa kwa udongo?

Djinn wa kwenye vitabu vya dini hafungamani na binadamu, Hata kumuona kwake ni mtihani ingawa wanakuja mara chache na kukaa kwa muda mfupi usiozidi masaa matano katika ulimwengu huu.

Kuna nyota huwa zinachomoza ghafla angani na huwa zina ng'aa sana, Nyota hizi zinaweza kaa ndani ya wiki moja, mbili, tatu na mpaka nne ndio zinatoweka. Nyota hizi zina ashiria kuna binadamu amezaliwa ambae ana nguvu za kimungu ndani yake, Hivyo hawa Djinn halisi ndio huja ulimwengu huu kwaajili ya Binadamu huyo na watakuja mara kwa mara kumuona mpaka Binadamu huyo atakapo fariki.

Wanakuja kumpa Elimu ya Mafumbo, Alama na Maandishi. Hawatoengea nae neno hata moja kwasabau lugha yao na yetu ni tofauti.

Hakuna Binadamu mwenye uwezo wa kuwaita wala kuwa control isipokuwa kwa yule waliye mjia tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom