Tukaondoka salama pale, Dada yangu akamwambia anti Sofia ukija Dar uje kunidfundisha kufanya visheti na kahawa yako, nimevipenda. Anti Sofia akaingia ndani akamtolea kopo zima la visheti, yale makopo ya biskuti makubwa. Akamwabia hii ndio biashara yangu kubwa hapa, navitengeneza kwa wingi wanaojua wananipa order, navipeleka sehemu nyingi sana, wewe ulikua hujui hii zawadi yako. Nakupa kwa sababu asingeolewa mamako unagekua mwanangu, kidogo babako anioe, huyo mdigo sijui akampa nini. Tukacheka tukaondoka.
Tulipoondoka kwenye gari nikajua dada yangu anamchokoza mama.
Dada; Anti Sofia anasema baba ilikua amuoe yeye wewe ukamt)roga kidogo akakuoa wewe, eti kweli? Ananesha alikua mzuri kweli?
Mama; Sofia anawatania, tu, amuoe miubwa kweli kwetu yule, kaolewa sisi bado tunasoma msimuone vile ana mwili mzuri. Lakini alikua mzuri mkweli, mpaka sasa mzuri .
Baba Sofia kajiweka pale kibiashara tu, pale anauza visheti Tanzania nzima, halafu hakuna Msomali anapita Chalinze bila kununua mirungi kwake, siku hizi haweki pale, anaweka kule uoande wa pili, kuna watu wake wanamuuzia, zinatembea simu tu, usimuone vile anapesa nyingi sana, yule muewe kamwachia Scania zaidi ya kumi, urithi wa wanawe. Huyomwanae mdogo wa kiume ndio anafanya kazi za kuzitrazama hizo. Hata wewe bwana mkubwa unazijua garizake, huwa zinakuja garage matra moja moja, zile anazokuja nazo Anko Abdi. Zile zote za Sofia na wanawe. Nikasema aaah, nimezijua na huto mwanae nimeshamjua, siku hizi wanzo benz moya mpya wamewachana na Scania kabisa.
Baba: ndio hizo hizo.
Mimi: Kweli ana pedsa, kwanini anakaa huku sasa?
Baba' Atahamia mjini hgivoi karibuni ana nyumba nyingi tu Dar. Hapa anatengeneza pesa nyingi sana, yule Waarabu wote wa Morogoro wanachukua kirungi kwake, magaru ya Wasomali na mengine mengi tu yanayopita hapa yanachukua miringi kwake. Yule kwa siku anafanya ya miilioni wo mpaka ishirini, usimuone vile.
Mama: Wasomali ni hodari sana kwa biashara.
Tukaneda mwndi mzuri tum hatukuchelewa sana tukawa tumeingia Dar, Vimbwanga vikaanzi mtaa wa Msimbazi, maana tulizunguka kupitia Kariakoo, kuna kitu mama alitaka kabla ya kwenda nyumbani. Ikabidi tupite Msimbazi.
Itaendelea.