Naomba Msaada: Nyumba yetu inakaribia kuuzwa

Naomba Msaada: Nyumba yetu inakaribia kuuzwa

Ana miaka 74, mimi ni ke,
Niko kwangu
Tunaye kaka mmoja ambaye kwa sasa maisha yake yameyumba hivyo anamshawishi mama auze nyumba ya familia ampe mtaji, hata hivyo hajawah kukanyaga mahakamani zaidi alitutumia ujumbe kwa simu kuwa nyumba inauzwa.
Yamkini kumbe Mama mdogo mnamsingizia isije kuwa huu mpango wote ni huyo Kaka yenu.
 
2025 -43 = 1982
Baba alifariki 1989
Mzee alimwachia mama watoto 5 wakiwa wadogo sana, amepambana mpaka nyie kufikia kuwa na miji yenu.

Ameona hiyo pesa mnayompatia ya kudunduliza kila mwezi haimtoshelezi, na umri umesogea sana.

Mwacheni afaidi mali zake akiumalizia uzee wake.
Ewaaaahh!! Mwana kwetu.
Hao watoto mama yao kuna kitu kaona, hao trust me akifa huyo mama bila kuuza nyumba watachinjana..!! 😹

Mama aache kula pension aliyochiwa na mumewe awaendekeze mijitu mizima isiyowaza kutafuta jasho lao.
 
Ana miaka 74, mimi ni ke,
Niko kwangu
Tunaye kaka mmoja ambaye kwa sasa maisha yake yameyumba hivyo anamshawishi mama auze nyumba ya familia ampe mtaji, hata hivyo hajawah kukanyaga mahakamani zaidi alitutumia ujumbe kwa simu kuwa nyumba inauzwa.
Sio mamdogo tena? 😹😹
Wewe muongo muongo.
Itoshe kusema mama auze hiyo nyumba ikimpendeza ampe kila mmoja chochote kitu mtauana akifa…!!
 
Kwanza watoto kulea wazazi ni tatizo lakini mzazi kuuza mali zake halafu alelewe na watoto ni tatizo kubwa zaidi.
Huyo mzazi kuna kitu kaona, lakini pia sio mbaya kuuza nyumba yake ikiwa watoto wakubwa wanajitegemea..!!
 
Sisi tumezaliwa wa5 ke4 me1 na

Mama amezeeka anataka kwenda kuwekeza wapi ktk umri huo, kama siyo ushauri mbaya wa mama yenu wadogo.

Nyumba katikati ya mjini ni mali kubwa na nyumba na kiwanja chake ni asset / mtaji endelevu inayoongezeka thamani na kutoa fursa kwa watoto na wajukuu kuingia katika mikataba minono na matajiri au mabenki huku mkiingiza kipato endelevu, makazi ghorofani ya kukodisha, kuishi n.k ikiwa mtaingia mikataba sahihi.

Mama kuuza nyumba mjini kati kisha kwenda kujenga majoring ktk uzee huo ni kosa kubwa dhidi ya legacy ya mtaji aliyowawekea nyie na mama yenu na watoto wenu.

Mstueni mama yenu, endeleeni kumtunza katika umri wake mkubwa hadi mwisho wa maisha yake ili asisikilize maneno ya nduguze ambao ni wazee pia kiumri.

Tutalalamika kuhusu familia za kina Dewji, Gulamali, Mengi n.k zenye utajiri. Utajiri huongezeka pale mali kama hizo zinapotunzwa zirithishwe kwa watoto ili legacy iendelee ya utajiri endelevu.

Kwanini siku zote waswahili haturithishi vizazi, tunadai kila kizazi kianze moja ktk kutafuta utajiri ?
 
Ewaaaahh!! Mwana kwetu.
Hao watoto mama yao kuna kitu kaona, hao trust me akifa huyo mama bila kuuza nyumba watachinjana..!! 😹

Mama aache kula pension aliyochiwa na mumewe awaendekeze mijitu mizima isiyowaza kutafuta jasho lao.
Ni kweli kabisa.
Wao wasimamie tu uuzwaji wa hiyo nyumba ili mama asipigwe, awakatie kidogo na wao. Huyo mwanaume anashindwa kwenda kupambana kwa ajili ya familia yake yeye kazi kumlia timing bi.mkubwa.
 
Mama mdogo sio ndugu yako na endapo kama yeye ndio kizuizi na mshawishi basi chezeni na akiri yake! Mbona Hilo jepesi Sana? Mshawishi ndio mvunjifu wa haki zenu na Mali zitapotea kwakuwa yeye Ana ushawishi hivyo, mama mdogo sio ndugu yenu, narudia tena huyo ni ndugu wa mama yenu ni bora mumtie uchizi kabisaaaa nyambafu huyo.
 
Mama amezeeka anataka kwenda kuwekeza wapi ktk umri huo, kama siyo ushauri mbaya wa mama yenu wadogo.

Nyumba katikati ya mjini ni mali kubwa na nyumba na kiwanja chake ni asset / mtaji endelevu inayoongezeka thamani na kutoa fursa kwa watoto na wajukuu kuingia katika mikataba minono na matajiri au mabenki huku mkiingiza kipato endelevu, makazi ghorofani ya kukodisha, kuishi n.k ikiwa mtaingia mikataba sahihi.

Mama kuuza nyumba mjini kati kisha kwenda kujenga majoring ktk uzee huo ni kosa kubwa dhidi ya legacy ya mtaji aliyowawekea nyie na mama yenu na watoto wenu.

Mstueni mama yenu, endeleeni kumtunza katika umri wake mkubwa hadi mwisho wa maisha yake ili asisikilize maneno ya nduguze ambao ni wazee pia kiumri.

Tutalalamika kuhusu familia za kina Dewji, Gulamali, Mengi n.k zenye utajiri. Utajiri huongezeka pale mali kama hizo zinapotunzwa zirithishwe kwa watoto ili legacy iendelee ya utajiri endelevu.

Kwanini siku zote waswahili haturithishi vizazi, tunadai kila kizazi kianze moja ktk kutafuta utajiri ?
Yani ndugu inaumiza sana aisee, toka baba afariki na mirathi aliyoacha hakuna mtoto yyt ambaye amesema apewe mgao bali tuliona ni vyema kila baba alichoacha mama aendelee kusimamia na kodi ya nyumba zote anakusanya yeye kwa matumizi yake binafs ya chakula mavazi na kila atakacho, yani from no were ameshauriwa eti kwakua umri umeenda sana auze nyumba kiasi cha pesa ajenge nnyumba ndogo chanika na nnyingn afanye biashara. Yani unaona kabisa mwisho wa hili inaumiza mno
 
Sio mamdogo tena? 😹😹
Wewe muongo muongo.
Itoshe kusema mama auze hiyo nyumba ikimpendeza ampe kila mmoja chochote kitu mtauana akifa…!!
Shida ni kuwa umetanguliza kuongea sana kuliko kuelewa nilichoandika. Nidanganye ili i jitahidi kufungua ufahamu utanielewa.
Nimesema kashauriwa na mama mdogo auze nyumba na kaka ameafiki hilo sbb anataja apewe mtaji na dada zake tumepinga.
Umenielewa sasa?
 
Shida ni kuwa umetanguliza kuongea sana kuliko kuelewa nilichoandika. Nidanganye ili i jitahidi kufungua ufahamu utanielewa.
Nimesema kashauriwa na mama mdogo auze nyumba na kaka ameafiki hilo sbb anataja apewe mtaji na dada zake tumepinga.
Umenielewa sasa?
Sasa si bora iuzwe sasa kuliko mama yenu akifa, ushafikiria nini kitatokea km huyo kaka yenu mkubwa anataka iuzwe pia?
 
Sasa si bora iuzwe sasa kuliko mama yenu akifa, ushafikiria nini kitatokea km huyo kaka yenu mkubwa anataka iuzwe pia?
Kila kitu ni kwa utaratibu sio kihuni.
Inaweza ikauzwa ama isiuzwe hata mama akiea hayupo
 
FATILIRN ARISE N SHINE
USIKU SAA TATU

WIKI IJAYO NJOON KAWE CHUKUENI MAJI NA MAFUTA YANENEEE MUNGU HAJASHINDWA

UKISIKIA UKOMBOZI WA ARDHI NJOO NA UDONGO WA HAPO KWENU CHUKUA CHANGANYA OMBEA IMILIKIE MALI KUWA YENU N JESUS NAME

UTANIPA MATOKEO
Wwe nae unaleta masihara kwenye vitu vya kisheria, mirathi iko kisheria na si kimaombi ya huko kanisani!!
 
1. Umiliki wa Nyumba

  • Ingawa jina lilisajiliwa kwa mama yenu kwa sababu ya mazingira ya kihistoria (kesi ya uhujumu uchumi), mali hii kiuhalisia ni mali ya baba yenu kwa kuwa ndiye aliyeinunua, na ushahidi ni mirathi aliyoiandika akabainisha mali ni ya watoto na si ya mama binafsi.
  • Kwa mujibu wa Sheria ya Mirathi (Probate and Administration of Estates Act, Cap 352 R.E 2002 – Tanzania), mali yoyote aliyokuwa akimiliki marehemu inapaswa kugawanywa kulingana na mirathi au kama hakuna, kwa urithi wa kisheria.


2. Kuhusu Mirathi na Faili la Mahakama

  • Faili la mirathi haliwezi kupotezwa kiholela, kwa sababu nyaraka za mirathi ni rekodi rasmi za Mahakama na huhifadhiwa kwenye Registry.
  • Ikiwa kweli jalada limepotea, unaweza kuomba upya Mahakama kutoa nakala ya uamuzi na hati za mirathi kupitia “certified copies” kwani kila jalada lina namba (probate file number).
  • Ikiwa mama alipewa nakala yake na inasemekana imepotea, bado Mahakama inabaki na wajibu wa kuhifadhi nakala. Kama hakuna, basi jambo hilo linaweza kufikishwa kwa Mahakama Kuu – Kitengo cha Ardhi au Mirathi kwa malalamiko ya upotevu wa faili.


3. Haki ya Mama Kuamua Kuuza

  • Kwa mujibu wa wasia, mama hakuwa mmiliki halisi bali msimamizi wa mali kwa ajili ya watoto.
  • Kwa hiyo, mama hana mamlaka ya kuuza mali kinyume na masharti ya mirathi (kwa mfano wasia kusema "mali zisiuzwe").
  • Kama atajaribu kuuza, hiyo ni kuzidisha mamlaka (breach of trust) na watoto wana haki ya kuzuia kwa kufungua shauri la kuzuia uuzaji (injunction).


4. Hatari ya Ushawishi na Udanganyifu

  • Ushawishi kutoka kwa mdogo wake unaweza kupelekea undue influence – jambo ambalo Mahakama inaweza kuzuia endapo nyinyi mtawasilisha ushahidi.
  • Historia ya hati kuchukuliwa benki tayari ni dalili ya hatari, hivyo mnapaswa kuchukua hatua haraka kisheria.


5. Mambo ya Kufanya Hivi Sasa

  1. Nendeni Mahakama (ambapo mirathi ilifunguliwa) muombe namba ya jalada na nakala ya hukumu / hati ya mirathi (probate or letters of administration).
  2. Fungueni shauri jipya kama jalada limepotea, mkieleza kuwa kuna jaribio la mama kuhamisha mali kinyume na mirathi.
  3. Ombeni amri ya Mahakama ya kuzuia uuzaji (injunction) mpaka suala la umiliki na mirathi liamuliwe upya.
  4. Kama hamna uaminifu na hakimu wa eneo, pelekeni suala Mahakama Kuu – Probate and Administration Registry ili lisimamiwe juu.
  5. Hifadhi ushahidi wote (nakala za wasia, ushahidi kuwa baba ndiye alinunua nyumba, na ushahidi wa ulaghai wa hati huko nyuma).
Mkuu asante sana, najaribu kukuinbox bila mafanikio. Naomba ukiona hii reply yangu please naomba uniinbox. 🙏🙏🙏
 
Mwanzo alisema anataka kujenga nyumba nyingine chanika, sasa anasema anataka kuhamia kijijini akafuge kuku ndiyo maelezo aliyotoa mahakamanii hivi majuzi.
mama ako atapgwa tukio na mdogo wake huyo.
Kufuga kuku sio lelemama
 
Tujikumbushe mali ni za baba na mama maana wa ndio waliozitafuta na sio za watoto.
Kwenye mali wengi wanafikiri ni za mwanaume tu na je kama hiyo nyumba alinunua mama yenu ndio ikaandikwa jina lake hamuoni mtakuwa mnamdhulumu mama yenu??
Hakununua mama sababu hakuwa na kazi yoyote, baba ndio alikuwa mfanyakazi meneja wa breweries.
 
Back
Top Bottom