Naomba Msaada: Nyumba yetu inakaribia kuuzwa

Naomba Msaada: Nyumba yetu inakaribia kuuzwa

Ishi na watu vizuri hapa mjini. Kama mama mdogo anasumbua huyo mama mdogo anatulizwa tulii kama maji ya mtungini. Upo tayari?
 
Kama inataka kuuzwa chap. Anzeni na caveat kabla ya kuanza kutengeneza kesi na ushahidi kwanini isiuzwe.
Ukishaweka caveat, zingatia muda ni one year lazima muwe mmesha anazisha kesi.
 
Yaani umeolewa unataka mali ya mama yako alioachiwa na mme wake na akawalea yeye kiwa single mother hadi mkaolewa na wewe uza nyumba ya mmeo dadeki kitoto vya Kinondoni kijinga sana

USSR
Akiuza halafu baadae wamtunze kwa hela nyingine ilhali hela ya hapo ingemtunza.
 
Hapana. Wosia ambao ni mirathi iliweka bayana kwamba mama ni msimamizi tu wa mirathi lakini nyumba isiuzwe kwa namna yoyote zaidi ya kufanyia biashara pekee.

Mtu akiandika mirathi/wosia akiwa na akili zake timamu basi hakuna namna mtu mwingine anaweza ku challenge.
Kwanini mnalazimisha nyumba isiuzwe?
Si mshakua watu wazima nyie?
Kwanini msipambane na wenzi wenu nao wawaachie urithi?

Hivi mama yenu mnamsumbua hivyo, vipi akifariki mkabaki peke yenu si mtachinjana?
 
Kwanini mnalazimisha nyumba isiuzwe?
Si mshakua watu wazima nyie?
Kwanini msipambane na wenzi wenu nao wawaachie urithi?

Hivi mama yenu mnamsumbua hivyo, vipi akifariki mkabaki peke yenu si mtachinjana?
Shida unafikiria karibu akiuza, soon ataanza kuwasumbua hao hao watoto zake wamlee
 
1. Umiliki wa Nyumba

  • Ingawa jina lilisajiliwa kwa mama yenu kwa sababu ya mazingira ya kihistoria (kesi ya uhujumu uchumi), mali hii kiuhalisia ni mali ya baba yenu kwa kuwa ndiye aliyeinunua, na ushahidi ni mirathi aliyoiandika akabainisha mali ni ya watoto na si ya mama binafsi.
  • Kwa mujibu wa Sheria ya Mirathi (Probate and Administration of Estates Act, Cap 352 R.E 2002 – Tanzania), mali yoyote aliyokuwa akimiliki marehemu inapaswa kugawanywa kulingana na mirathi au kama hakuna, kwa urithi wa kisheria.

2. Kuhusu Mirathi na Faili la Mahakama

  • Faili la mirathi haliwezi kupotezwa kiholela, kwa sababu nyaraka za mirathi ni rekodi rasmi za Mahakama na huhifadhiwa kwenye Registry.
  • Ikiwa kweli jalada limepotea, unaweza kuomba upya Mahakama kutoa nakala ya uamuzi na hati za mirathi kupitia “certified copies” kwani kila jalada lina namba (probate file number).
  • Ikiwa mama alipewa nakala yake na inasemekana imepotea, bado Mahakama inabaki na wajibu wa kuhifadhi nakala. Kama hakuna, basi jambo hilo linaweza kufikishwa kwa Mahakama Kuu – Kitengo cha Ardhi au Mirathi kwa malalamiko ya upotevu wa faili.

3. Haki ya Mama Kuamua Kuuza

  • Kwa mujibu wa wasia, mama hakuwa mmiliki halisi bali msimamizi wa mali kwa ajili ya watoto.
  • Kwa hiyo, mama hana mamlaka ya kuuza mali kinyume na masharti ya mirathi (kwa mfano wasia kusema "mali zisiuzwe").
  • Kama atajaribu kuuza, hiyo ni kuzidisha mamlaka (breach of trust) na watoto wana haki ya kuzuia kwa kufungua shauri la kuzuia uuzaji (injunction).

4. Hatari ya Ushawishi na Udanganyifu

  • Ushawishi kutoka kwa mdogo wake unaweza kupelekea undue influence – jambo ambalo Mahakama inaweza kuzuia endapo nyinyi mtawasilisha ushahidi.
  • Historia ya hati kuchukuliwa benki tayari ni dalili ya hatari, hivyo mnapaswa kuchukua hatua haraka kisheria.

5. Mambo ya Kufanya Hivi Sasa

  1. Nendeni Mahakama (ambapo mirathi ilifunguliwa) muombe namba ya jalada na nakala ya hukumu / hati ya mirathi (probate or letters of administration).
  2. Fungueni shauri jipya kama jalada limepotea, mkieleza kuwa kuna jaribio la mama kuhamisha mali kinyume na mirathi.
  3. Ombeni amri ya Mahakama ya kuzuia uuzaji (injunction) mpaka suala la umiliki na mirathi liamuliwe upya.
  4. Kama hamna uaminifu na hakimu wa eneo, pelekeni suala Mahakama Kuu – Probate and Administration Registry ili lisimamiwe juu.
  5. Hifadhi ushahidi wote (nakala za wasia, ushahidi kuwa baba ndiye alinunua nyumba, na ushahidi wa ulaghai wa hati huko nyuma).
 
Ana miaka 74, mimi ni ke,
Niko kwangu
Tunaye kaka mmoja ambaye kwa sasa maisha yake yameyumba hivyo anamshawishi mama auze nyumba ya familia ampe mtaji, hata hivyo hajawah kukanyaga mahakamani zaidi alitutumia ujumbe kwa simu kuwa nyumba inauzwa.
Iteni kikao cha familia msuluhishe hili.
 
Hapana. Wosia ambao ni mirathi iliweka bayana kwamba mama ni msimamizi tu wa mirathi lakini nyumba isiuzwe kwa namna yoyote zaidi ya kufanyia biashara pekee.

Mtu akiandika mirathi/wosia akiwa na akili zake timamu basi hakuna namna mtu mwingine anaweza ku challenge.
HUO WOSIA ISIUZWE KULIKUWA NA MWANANSHERIA AMA WALIENDA MAHAKAMAN??

NA MASHAHIDI WIALIKUWA WANGAP

TUANZIE HAPA
 
KAMA MKO 5
WA 3 WAKILAZIMISHA IUZWE IMEKWISHA HIOO

KAMA.WAKO WAWILI WANATAKA KUUZA NA NA WATATU WAMEKATAA ..M AM A YENU HAGUSI HIO NYUMBA
 
Habarini ndugu.

Sisi tumezaliwa wa5 ke4 me1 na wote tuna miaka 40+, baba yetu alifariki 89 aliacha mali chache ikiwemo nyumba iliyopo katikati ya mji, nyumba hiyo baba aliinunua ila aliandika jina la mama kwakuwa alishtakiwa kwa kesi ya uhujumu uchumi hivyo alifanya hivyo ili kuinusuru isitaifishwe, na kabla hajafariki aliandika mirathi msimamizi ni mama kuwa mali zote ni za watoto na zisiuzwe na alisema nyumba hiyo ni ya biashara hivyo chcht kitakachopatikana ni kwa ajili ya mama na wanae ila mama akiamua kuondoka kuolewa aache kila kitu aolewe.

Tumekuwa na baadhi tuna miji yetu hatutegemei chochote kutoka ktk mali zilizoachwa na mzee, na baadhi tunafanya biasharea ktk nyumba hiyo na zaidi tunampa mama kodi km wapangaji ili aweze kupata mahitaji yake pasipo kututegemea sisi. Na tuliamua hivyo ili aishi kwa utulivu sababu umri wake ni mkubwa sana hana uwezo wa kufanya biashara yoyote tena. Ghafla mama ametaka kuuza nyumba tukamzuia, akaenda mahakamani tukaitwa hakimu akasema file la mirathi limepotea na nakala aliyopewa mama pia imepotea kwahy anampa mama haki ya kuuza nyumba na mama anasema wazi kuwa hakimu ni rafiki yake hivyo atamsaidia.

Sababu za mama kutaka kuuza nyumba ni ushawishi toka kwa mdogo wake ambaye alishaiba hati wakati baba anaumwa ilikuwa bank alimshikia rafiki yake mdhamana kwa kesi ya mauaji na alishinda kesi mama mdogo akachuku hati akaichukulia mkopo nyumba ikauzwa na bank ila baadae ilirudishwa baada ya kustakiana na mama yetu. sasa mama mdogo amerudi anamshawishi mama auze wafanye biashara ilhali mama hana uwezo huo, Naombeni msaada je file linaweza kupotea mahajamani?,na tutafanyaje tupate haki mana mirathi pekee ndio inathibitisha nyumba ilinunuliwa na baba.
Kwa maelezo Yako, hiyo mahakama inampa vipi uhalali wa mama yenu kuuza nyumba ambayo hakuna ushahidi kwamba ni yake( hati za kumiliki hazikutilewa mahakamani),,,ila kama nyinyi mlitoa ushahidi kwamba nyinyi ni watoto wake na hiyo nyumba ni yake basi ana haki ya kuiuza.

Mnaloweza kufanya ni kukata rufaa kupinga nyumba isiuzwe, au mumshawishi kwa upendo awashirikishe na nyinyi kwenye hatua zote za kuiuza na akubali.
 
Habarini ndugu.

Sisi tumezaliwa wa5 ke4 me1 na wote tuna miaka 40+, baba yetu alifariki 89 aliacha mali chache ikiwemo nyumba iliyopo katikati ya mji, nyumba hiyo baba aliinunua ila aliandika jina la mama kwakuwa alishtakiwa kwa kesi ya uhujumu uchumi hivyo alifanya hivyo ili kuinusuru isitaifishwe, na kabla hajafariki aliandika mirathi msimamizi ni mama kuwa mali zote ni za watoto na zisiuzwe na alisema nyumba hiyo ni ya biashara hivyo chcht kitakachopatikana ni kwa ajili ya mama na wanae ila mama akiamua kuondoka kuolewa aache kila kitu aolewe.

Tumekuwa na baadhi tuna miji yetu hatutegemei chochote kutoka ktk mali zilizoachwa na mzee, na baadhi tunafanya biasharea ktk nyumba hiyo na zaidi tunampa mama kodi km wapangaji ili aweze kupata mahitaji yake pasipo kututegemea sisi. Na tuliamua hivyo ili aishi kwa utulivu sababu umri wake ni mkubwa sana hana uwezo wa kufanya biashara yoyote tena. Ghafla mama ametaka kuuza nyumba tukamzuia, akaenda mahakamani tukaitwa hakimu akasema file la mirathi limepotea na nakala aliyopewa mama pia imepotea kwahy anampa mama haki ya kuuza nyumba na mama anasema wazi kuwa hakimu ni rafiki yake hivyo atamsaidia.

Sababu za mama kutaka kuuza nyumba ni ushawishi toka kwa mdogo wake ambaye alishaiba hati wakati baba anaumwa ilikuwa bank alimshikia rafiki yake mdhamana kwa kesi ya mauaji na alishinda kesi mama mdogo akachuku hati akaichukulia mkopo nyumba ikauzwa na bank ila baadae ilirudishwa baada ya kustakiana na mama yetu. sasa mama mdogo amerudi anamshawishi mama auze wafanye biashara ilhali mama hana uwezo huo, Naombeni msaada je file linaweza kupotea mahajamani?,na tutafanyaje tupate haki mana mirathi pekee ndio inathibitisha nyumba ilinunuliwa na baba.
Mzee wenu alioacha ni wosia au milathi? Mama ana haki kuuza mali yake..
 
Ushauri, kaeni kikao bila mama kubalianeni kuinunua ila ibaki kuwa Mali ya familia, baadaye kaeni kikao na mama muombe awauzie na process zote za manunuzi za kisheria zifanyike.
 
Inasikitisha sana kuona jukwaa au jf imevamiwa na watu waliokosa weledi kwenye mambo ya msingi na badala yake wanakimbilia kuzodoa....na hata kutukana........

Mimi najaribu kumuelewa mtoa mada katika angle nyingine kabisa!!

Jambo la wazi ambalo wengi hamlielewi ni kama vile huyo mama anakaribia kutapeliwa kwa mlango wa nyuma!!

Historia ya awali ya huyo mama mdogo ni kuwa alishawahi kufanya dhuruma lakini mahakama ikanusuru nyumba!!!

Achaneni na wajinga wajinga wa humu na nadhani ungejaribu kuwaona wataalamu wa sheria wakupe mwanga!!!!

Huyo mama kama akitapeliwa ni wazi kuwa atarudi kuwa mzigo wenu nyinyi watoto!!
 
Hilo file number 9 la mwaka 1989 ni file la mahakamani? Kama ndio basi fika masijala ya mahakama husika au fika mahakama ya juu yake kudai upewe nakala ya hiyo hukumu. Humo utakuta mali zote husika zimeandikwa.
Mimi sio mwanasheria Ila nimekushauri hivi kutokana tu na uzoefu na mambo kama haya nilivoona kwa wengine.
Suluhisho lako la mwisho wewe n ndugu zako kama mnaamini mama amepungukiwa uelewa na anataka kufanya maamuzi yasiyo sahihi basi ni kufungua kesi kuomba mahakama itoe zuio la kuuza mali maana muuzaji Hana akili timamu na kuwa ameshawishiwa/kupotoshwa.

Asante.
Asante ndugu
 
Back
Top Bottom