Naomba Msaada: Nyumba yetu inakaribia kuuzwa

Naomba Msaada: Nyumba yetu inakaribia kuuzwa

Habarini ndugu.

Sisi tumezaliwa wa5 ke4 me1 na wote tuna miaka 40+, baba yetu alifariki 89 aliacha mali chache ikiwemo nyumba iliyopo katikati ya mji, nyumba hiyo baba aliinunua ila aliandika jina la mama kwakuwa alishtakiwa kwa kesi ya uhujumu uchumi hivyo alifanya hivyo ili kuinusuru isitaifishwe, na kabla hajafariki aliandika mirathi msimamizi ni mama kuwa mali zote ni za watoto na zisiuzwe na alisema nyumba hiyo ni ya biashara hivyo chcht kitakachopatikana ni kwa ajili ya mama na wanae ila mama akiamua kuondoka kuolewa aache kila kitu aolewe.

Tumekuwa na baadhi tuna miji yetu hatutegemei chochote kutoka ktk mali zilizoachwa na mzee, na baadhi tunafanya biasharea ktk nyumba hiyo na zaidi tunampa mama kodi km wapangaji ili aweze kupata mahitaji yake pasipo kututegemea sisi. Na tuliamua hivyo ili aishi kwa utulivu sababu umri wake ni mkubwa sana hana uwezo wa kufanya biashara yoyote tena. Ghafla mama ametaka kuuza nyumba tukamzuia, akaenda mahakamani tukaitwa hakimu akasema file la mirathi limepotea na nakala aliyopewa mama pia imepotea kwahy anampa mama haki ya kuuza nyumba na mama anasema wazi kuwa hakimu ni rafiki yake hivyo atamsaidia.

Sababu za mama kutaka kuuza nyumba ni ushawishi toka kwa mdogo wake ambaye alishaiba hati wakati baba anaumwa ilikuwa bank alimshikia rafiki yake mdhamana kwa kesi ya mauaji na alishinda kesi mama mdogo akachuku hati akaichukulia mkopo nyumba ikauzwa na bank ila baadae ilirudishwa baada ya kustakiana na mama yetu. sasa mama mdogo amerudi anamshawishi mama auze wafanye biashara ilhali mama hana uwezo huo, Naombeni msaada je file linaweza kupotea mahajamani?,na tutafanyaje tupate haki mana mirathi pekee ndio inathibitisha nyumba ilinunuliwa na baba.
Kama Mna maisha yenu na mna Mali zenu, muache huyo mama afanye anachohisi ni sahihi .

Sifikirii Kama ni sahihi kugombana kisa hizo takatakata ambazo ni useless.

We tengeneza Maisha yako yasimame Mali kitu gani
 
Kama Mna maisha yenu na mna Mali zenu, muache huyo mama afanye anachohisi ni sahihi .

Sifikirii Kama ni sahihi kugombana kisa hizo takatakata ambazo ni useless.

We tengeneza Maisha yako yasimame Mali kitu gani
Ni kweli tuna mali zetu lakini hii nyumba ni mali ya famili n sio nyumba tuh kuna na mshamba ambayo bab aliacha alitaka kuyauza kinyemel ila ndugu wa bba wakakataa.
 
Haya mambo ndiyo yanayotufanya wazaramo tuonekane hatuna akili .

Sasa mali aliachiwa mama kama msimamizi ,yeye kawalea na sasa mpo kwenye familia zenu ikiwa anahitaji kuuza mali ya mmewe ninyi inawahusu nini ninyi mashangingi wa mjini
Lakini wamuulize akiuza atakaa wapi kama sehemu ya kukaa ina shida kiuhuru,basi wamuhoji anyooshe maelezo asijekwenda kujibana kwa mtu.
 
Mimi sijata

Ka mali wala sijawah kuenda mahakamani nimeitwa zaidi ya mara 3 sikuona sbb ya kwenda, kilichonifanya niombe msada ni hali ya mama ya afya ya akili na mwili, na ni baada ya kutaka kuuza nyumba ya zaid ya mil 250 kwa mil 80, na umri wake ni mkubwa hawezi kufanya biashara wala chcht nyumba hy ndio msaada kwake, na mshauri wake mkuu ni mdogo wake wa kike ambaye alishawah kufoji signatir akachukua mkopo wa nyumba hy hy ikaja kuuzwa na bank. Lengo sio kumdhulumu wala kugombea msli ila ni kuhakikishs hakuna utapeli unafanyika dhidi yake na familia kwa ujumla mana mirathi yeye ni msimamizi na mmiliki pia.
Fanyeni namna yoyote mumzuie mama yenu mdogo kuingilia mambo ya familia yenu?Yeye hana familia yake?
 
Ana miaka 74, mimi ni ke,
Niko kwangu
Tunaye kaka mmoja ambaye kwa sasa maisha yake yameyumba hivyo anamshawishi mama auze nyumba ya familia ampe mtaji, hata hivyo hajawah kukanyaga mahakamani zaidi alitutumia ujumbe kwa simu kuwa nyumba inauzwa.
Okay pole Sana

Naomba umcheki Mwansheria akupe muongozo mzuri Kama upo DSM mtafute Jebra Kambole. Au pascall Mayalla wakupe ushauri wa kisheria .

Then nachona hapo mgepata mshauri mzuri wa Ku-Solve huo mgogoro bila kufika mahakamani


Mfano Kama kaka yenu yupo financially broke , mnaweza kumtafuta mkaongea nae friendly mkaona namna gani mnaweza kumpiga tafu pasipo kuuza Nyumba.

Ila usitumie Ubabe tumia akili sana sio nguvu .

Shida kubwa ya nyie wanawake mnapanic na mnatumia ubabe Sana

So ni vizuri utafute Mwnaume MTU mzima amabaye yupo smart aingilie kati mshauriane namna ya kumtulizamama yenu na huyo kaka yenu .


So Ukiona hizo njia za kidiplomasia zimefeli ndo utumie ubabe
 
Yaani umeolewa unataka mali ya mama yako alioachiwa na mme wake na akawalea yeye kiwa single mother hadi mkaolewa na wewe uza nyumba ya mmeo dadeki kitoto vya Kinondoni kijinga sana

USSR
Hajui uzito wa kukojolewa huyu kama mke na mme achana na hyo tamaa mwachie b mdg aendelez familianya baba mwengn
 
Back
Top Bottom