Uko sahihi kabisa.
Mimi husali Kisunni katika msikiti wa Kishiia pale Mtaa wa India na Morogoro Road.
Napapenda kwa kuwa kuna vyoo visafi, na msikiti unaendeshwa vizuri. Kuna gari la mgonjwa, kuna daktari, kuna madrassa na tuition ya kufundisha watoto wao, jioni msikiti unakuwa sehemu ya kufanya sherehe tofauti za kwao na kuna usalama wa vitu vyako na usafi wa hali ya juu.
Sijakutana na ubaguzi wowote na sijakatazwa kusali kisunni. Ila Ijumaa, wanatoa hotuba kwa Kihindi halafu baadae kwa Kiswahili. Sisi tunatoa kwa Kiarabu pale upanga makaburini halafu kwa Kiswahili.
Miaka hiyo ni ya 80 na mpaka leo hamna msikiti wowote unaendeshwa vizuri kama wa Kishiia, kwa maoni yangu, hasa kuhusu usafi wa vyoo.
(Sijaona bado msikiti wa Kisunni chenye choo cha kukaa).