Aleikum Salaam.
Mimekusoma vizuri.
Naam. Kuna madrassa tofauti ya dini.
Nashukuru Mungu, nimetembea Uturuki, Indonesia, Brunei Darusallam na Malaysia. Huko kote kuna ilmu tofauti na pia ni utamaduni tofauti.
Indonesia, Brunei na Malaysia, watoto wa kiume wanatahiriwa wakiwa wakubwa (miaka 5-8) na kufanywa sherehe kubwa. Wa kike, pia kuna Sunna inafanywa, hawawakati bali wanatoboa tundu dogo na sindano katika "clitoris"kitu ambacho hatufanyi kwa watoto wa kike nyumbani.
Uturuki "ameen" huisikii ukisali. Hawaitumii. Lakini Mimi naisema kimazoea nikiwa Istanbul.
Na kama nilivyoandika, wanatumia perfume wakienda kusali Asia, wanaamini kuwa lazima wanukie na kupendeza wakienda kusali, japo wanajifunika na nguo maalum ya kusalia, kwa mbali utafikiri ni mabohora wa Tanzania.
Kila la kheri.