Msikiti wa posta na ubaguzi??

Msikiti wa posta na ubaguzi??

Kuna watoto wadogo mabilioni wamefariki wakiwa wadogo sana, kwa sababu wakunga hawakujua kwamba wanatakiwa kuosha mikono.

Kwa sababu hakukuwa na antibiotics.

Kwa nini Mungu kaumba ulimwengu ambao watoto hawa wasio na hatia wamefariki wakiwa wadogo hivyo wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao hawawezi kufa hivyo?

Watu weusi wamebaguliwa sana. Wameuzwa utumwani. Wameuawa. Wamechinjwa. Wamefanyiwa kila unyama.

Kwa nini huyu Mungu kama kweli ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao ubaguzi wa rangi na unyama wote huu unawezekana kuwepo wakati alikuwa na uwezo wa kuuumba ulimwengu huu kwa namna ambayo ubaguzi wa rangi na unyama ote huu hauwezi kuwepo?
Aisee mkuu unafikiri saba
 
Habari ndo hiyo, Bilal (Muislaam mweusi) ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuadhini (mwito wa kuita Waislaam kwenda/kuingia msikitini kuswali)
Nabii Luqman pia inadaiwa alikuwa ni mtu mweusi kutoka Ethiopia (Abbyssinia) odbg
Bilal yupi huyo? Ama huyu Bilal Mashauzi??
 
Mimi Muafrika. "Kustaarabika" ni kuwa muarabu. Mzizi wa "ku sta arab ika ni kutaka kuwa muarabu.

Sitaki utumwa wa akili wa kutaka kuwa muarabu.

Ndiyo maana hata hizi habari za kuingia msikitini na kusujudu kwa waarabu sizitaki.

Kwa nini nitake kuwa muarabu wakati mimi Muafrika?
Waarabu wengi ni wastaarabu mana wanapenda taarabu-afande sele(mkuki moyoni)
 
Siye waislamu ni vigumu kubaguana. Muislam anaweza kuingia msikiti wowote ambako swala ilimkutia.

Ataingia, Atatawadha, Ataswali , Ataondoka.
Kulingana na mafundisho ya dini ya kiislamu ni vigumu sana kubaguana.

Msikiti wowote hapa duniani ni mahali salama kimwili na kiroho kwa muislamu yeyote.

Nina hakika wewe na uyo aliyekwambia wrote ni wanafiki. Either mna sababu zenu binafsi au mna zile tabia za umbea usio na tija.

Nitashukuru na kukuona wa maana kama utataja jina LA msikiti ili waislam halisi wakahakikishe uyasemayo.
Nani kasema??tena nyie waislamu weusi hamtakiwi uarabuni kabisa..waarabu hawawapendi lakin marekani akiwagonga waarabu mnalia lia na kutaka kuandamana...
Ila afrika ya kati..waislamu weusi wenzenu walikua wanachinjwa... nyie kimyaa...na hata hao waarabu hawakuwasaidia
 
Makundi 72 Yatakayoingia Motoni
Aqiydah
SWALI:
assalam aleikum.amma baad namshukuru Allaah kuniwezesha tena kuandika sula hili ambalo natumai litakuwa bayana kwako kwa uwezo wake Allaah. Naomba uanitajie makundi 73 ambayo Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)(s.a.w) kayabashiria kuwa yataingia motoni ila moja tu na unifafanulie vizuri tofauti zao? Ahsante wajazakAllaahu kheir.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani kwa swali lako hilo kuhusu makundi yaliyotajwa kwa idadi katika Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa yataingia Motoni. Ieleweke kuwa hapa si mahala pake pa kuweza kuyaeleza makundi hayo kufanya utafiti huo itabidi tusiwe ni wenye kujibu maswali wala kufanya kazi wala shughuli nyengine isipokuwa hiyo. Hivyo ni juu ya mwanafunzi kwenda katika vitabu vingi vilivyoelezea hayo.
Kwa kifupi tu kwa kukupa mwangaza kidogo, utayajua yale makundi yaliyo potofu kwa kuona na kujua itikadi zao. Mfano mzuri leo utaona wanaodai kuna mtume baada ya Mtume wa haki na wa mwisho Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), utawaona pia wale wanaowakufurisha Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘anhum) na kuwatukana wake za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), pia utawaona wengine wanaokufurisha Waislam na kuwatoa katika Dini kwa sababu wanaamini kuonekana Allaah Qiyaamah, na wanakufurisha Waislamu kwa sababu ya kufanya baadhi ya maasi, na pia utawaona wengine wanakataa Hadiyth za Mtume na kudai kuwa wao wanafuata Qur-aan pekee, na pia utawakuta wengine wanakwenda kuwaomba watu waliokufa makaburini ili wawasaidie haja zao, na wengi wengine wasio na idadi.
Tutalijua kundi lililookoka na ambalo halipo katika hayo makundi 72, kwa kuitazama ile Hadiyth ya bwana Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo:
((Wamegawanyika Mayahudi katika mapote 71, wakagawanyika Wakristo katika mapote 72 na Ummah wangu utagawanyika mapote 73. Yote hayo yataingia motoni ila moja tu)) Maswahaba waliuliza: Ni lipi hilo, ewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wa Allaah! Akasema: ((Ni lile nililokuwemo mimi na Swahaba zangu)) [Ahmad, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na Ad-Daarimiy].
Kundi hilo litakuwa ni lenye kufuata maagizo ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Makhalifa waongofu (Radhiya Allaahu ‘anhum) na Maswahaba wengine (Radhiya Allaahu ‘anhum) na wema wote waliotangulia (Salafus-Swaalih). Muislam atakayejikita na kuwa imara katika hayo basi atakuwa katika njia nyoofu. Dalili ni nyingi katika Qur-aan na Sunnah. Miongoni mwayo ni kauli ya Aliyetukuka:
((Na anayemtii Allaah na Mtume Wake, bila ya shaka amefanikiwa mafanikio makubwa)) [33: 71].
Pia Amesema Aliyetukuka:
((Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni na Atakufutieni madhambi yenu. Na Allaah ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu)) [3: 31].
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye anatueleza yafutayo katika khutbah yake ya Hijjatul Wadaa: ((Hakika nimewaachia kitu ambacho hamtapotea baada yangu lau mtashikana nacho, Kitabu cha Allaah)) [Muslim].
Sehemu nyengine kasema: ((Kitabu cha Allaah na Sunnah zangu)) [Al-Bukhaariy na Muslim].
Na katika masimulizi ya Abu Najiih al- 'Irbaadh bin Saariyah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba: "Alituwaidhia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyozifanya nyoyo kuingia hofu na macho yakatokwa na machozi. Tukamwambia: "Ewe Mtume wa Allaah! Yaonyesha kama haya ni mawaidha ya kuaga, basi tuusie". Akasema: ((Nawausia kumcha Allaah, Kwani hakika atakayeishi katika nyinyi ataona khitilafu nyingi, basi jilazimisheni kufuata Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa walioongoka, yashikeni kwa magego mambo yao)) [Abu Daawuwd, Ahmad, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na Ad-Daarimiy].
Mambo muhimu ambayo tunayapata katika dondoo za hapo juu ni kuwa, kuwepo kwetu katika kundi litakaloongoka ni kufuata mwendo aliokuwa nao Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Makhalifa wake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na kushikamana nao kivitendo barabara.
Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Atufanye ni wenye kuyashikilia hayo vilivyo ili tuwe ni wenye kuingia katika Rehma Yake na kuwa ni kundi lililosalimika na moto, kundi lililonusurika na ni kundi liliokoka.
Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Atusahilishie hatua zetu katika kuelekea katika mwendo wa sawa na wa haki.
Totally crap...unaandika nonsenses. Hakuna maisha baada ya kifo. Ukibisha lete ushaidi aliyekufa aje atuambie ayo maisha yapoje.
 
Inatia moyo kuona watu wengi zaidi wanajua hili.
Hakuna kitu kibaya kama mental slavery.
Waafrika wengi wana hii kitu..utumwa wa fikra.
Dini zote hizi sio uislamu ama ukristo zimeletwa..
mababu zetu wakazipokea tuu...ukazaliwa...ukamezeshwa . Izo dini zina wenyewe..basi unakuta mwafrika eti yupo ntafia dini yangu..like seriously???

Dini alete mwarabu ama mzungu useme eti "ntafia dini yangu"??? Huezi kua na akili timamu.

Imani yako ndo itayokubeba...naongelea imani yako ktk "right na wrong".
Nafurahi sio muumini wa dini yoyote ile. Napenda imani yangu. Naamini ktk right n wrong ktk maisha.
 
Acha Uongo, hata kama uislam hauruhusu Ubaguzi, Waarabu wanawabagua Wabantu hata katika Ibada.

OVA
Kiufupi waarabu hawawapendi wabantu. ..lakini mwarabu akichapwa na mmarekani basi waislamu wakibantu watalaani na kulia sana na kutishia kuandamana ubalozi wa marekani
 
Hakuna kitu kibaya kama mental slavery.
Waafrika wengi wana hii kitu..utumwa wa fikra.
Dini zote hizi sio uislamu ama ukristo zimeletwa..
mababu zetu wakazipokea tuu...ukazaliwa...ukamezeshwa . Izo dini zina wenyewe..basi unakuta mwafrika eti yupo ntafia dini yangu..like seriously???

Dini alete mwarabu ama mzungu useme eti "ntafia dini yangu"??? Huezi kua na akili timamu.

Imani yako ndo itayokubeba...naongelea imani yako ktk "right na wrong".
Nafurahi sio muumini wa dini yoyote ile. Napenda imani yangu. Naamini ktk right n wrong ktk maisha.
Siku moja natoka kazini naenda kupanda treni nirudi nyumbani. Kutoka ofisini kwangu mpaka kufika kituo cha treni ilikuwa lazima nishushe Wall St. mpaka Broadway. Basi nimefika kona ya Broad St. na Wall St pale kwenye New York Stock Exchange, katikati ya dunia ya watoza ushuru na waabudu fedha, nikamkuta babu mmoja kwa accent yake anasikika kama Mnigeria hivi. Kakomaa anawahubiria New Yorkers injili wamsikilize anawaletea neno la Yesu. Wakati wazungu ndio wanajua uongo wote ulio katika biblia na ndio walioutumia kwa mamia ya miaka kutuibia mali na uhuru wetu.

Nikaona sasa Afrika tumedanganywa mpaka tunafanya reverse evangelism.

Nikafikiria sana nikasema usikute Mnigeria naye anawapiga kivyaje huko kwenye makodi na misaada na kuwaunganishia watu wa kwao waje huku na yeye anachanganya mingo kivyake.

Bottom line habari za Mungu ambaye hawezi hata ku pass a simple logic test ni uongo wa kitoto unaofaa kuachwa kwani unatudumazia maendeleo.
 
Hujajibu la kanisani umelitoa wapi.

Msikiti haubagui kwa msingi wa wanaoingia kwa kuvaa na kutovaa viatu?
Kwa taarifa yako;Dini na mafundisho yake yanaruhusu kuingia msikitini na kuswali ukiwa umevaa viatu,Pale utapohakikisha ni visafi na havina najisi.Zaidi ni katka hali ya ku maintain usafi kwani watu wanapita ktk mazingira tofauti huko watokako.
Je unaweza kuingia Nyumba yenye Zuria ilhali viatu vyako vina tope???
Al Islam Nadhiif.
 
Kwa taarifa yako;Dini na mafundisho yake yanaruhusu kuingia msikitini na kuswali ukiwa umevaa viatu,Pale utapohakikisha ni visafi na havina najisi.Zaidi ni katka hali ya ku maintain usafi kwani watu wanapita ktk mazingira tofauti huko watokako.
Je unaweza kuingia Nyumba yenye Zuria ilhali viatu vyako vina tope???
Al Islam Nadhiif.

Umechelewa sana mjadala. Tumejadili hayo yote awali.

Sasa kwa nini huyo Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hakufanya kwamba ukiingia msikitini tu uchafu wote unaishia mlangoni bila hata kuvua viatu?

Angefanya muujiza huo angeaminika zaidi.

Lakini sasa hivi ama hayupo mnatupiga fix, ama yupo anatubania kutupa favor hata tunapoenda msikitini.
 
Umechelewa sana mjadala. Tumejadili hayo yote awali.

Sasa kwa nini huyo Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hakufanya kwamba ukiingia msikitini tu uchafu wote unaishia mlangoni bila hata kuvua viatu?

Angefanya muujiza huo angeaminika zaidi.

Lakini sasa hivi ama hayupo mnatupiga fix, ama yupo anatubania kutupa favor hata tunapoenda msikitini.

Tatizo wewe unataka Mungu afikiri kibinaadamu, Mungu utashi wake ni huo wa kuona Binadamu anakabiliana na Mazingira yake na hali zake, emeweka utaratibu wa Maisha, akatoa uhuru wa kumuamini na kumkataa ndio maan akampa mwanadamu akili ya utambuzi.

Yeye hanufaiki wala hapungukiwi na chochote kwa kuabudiwa wala kutokuabudiwa.

Vilevile kuhusu majanga yanayotokea ni yeye ndiye aliyeumba, hayo majanga yanafaida zake na hasara zake japo sisi wanaadamu hatupendi.

Kwamfano wewe unauwezo wa kununua nguo mpya na hununui unavaa mtumba, kwa kutokununua bado haikuondolei kwamba wewe huna uwezo bali ndio chaguo lako vivyohivyo Mungu kuumba aina hii ya maisha na dunia (imperfect and bungling) hakumfanyi awe hawezi kuumba vinginevyo.

Mfano mwingine Mwanaume anayeowa mke mmoja na kuzaa watoto wawili kisha kwa sababu zake anamfungu uzazi mkewe, kwa kufanya hivyo haina maana hawezi kuowa mke mwingine na kuzaa watoto wengine. vivyo hivyo Allah kwa kuumba Dunia hii hivi ilivyo haimaanishi hawezi kuumba Dunia isiyo na Matatizo wala Mashaka yoyote.

umeng'ang'ania ati kwanini asiumbe Dunia isiyo na inefficiency? hiyo sio Dunia ni pepo na tayari ameshaiumba Pepo ambayo humo hakuna mashaka wala maradhi wala kufa wala hakuna mwisho.

Nilisha kujibu huko lakini unajitia uziwi na kutokuelewa kwa makusudi.
 
Tatizo wewe unataka Mungu afikiri kibinaadamu, Mungu utashi wake ni huo wa kuona Binadamu anakabiliana na Mazingira yake na hali zake, emeweka utaratibu wa Maisha, akatoa uhuru wa kumuamini na kumkataa ndio maan akampa mwanadamu akili ya utambuzi.

Yeye hanufaiki wala hapungukiwi na chochote kwa kuabudiwa wala kutokuabudiwa.

Vilevile kuhusu majanga yanayotokea ni yeye aliyeumba, hivyo majanga yanafaida zake na hasara zake japo sisi wanaadamu hatupendi.

Kwamfano wewe unauwezo wa kununua nguo mpya na hununui unavaa mtumba, kwa kutokununua bado haikuondolei kwamba wewe huna uwezo bali ndio chaguo lako vivyohivyo Mungu kuumba aina hii ya maisha na dunia (imperfect and bungling) hakumfanyi awe hawezi kuumba vinginevyo.

Mfano mwingine Mwanaume anayeowa mke mmoja na kuzaa watoto wawili kisha kwa sababu zake anamfungu uzazi mkewe, kwa kufanya hivyo haina maana hawezi kuowa mke mwingine na kuzaa watoto wengine. vivyo hivyo Allah kwa kuumba Dunia hii hivi ilivyo haimaanishi hawezi kuumba Dunia isiyo na Matatizo wala Mashaka yoyote.

umeng'ang'ania ati kwanini asiumbe Dunia isiyo na inefficiency? hiyo sio Dunia ni pepo na tayari ameshaiumba Pepo ambayo humo hakuna mashaka wala maradhi wala kufa wala hakuna mwisho.

Nilisha kujibu huko lakini unajitia uziwi na kutokuelewa kwa makusudi.
Wapi nimeng'ang'ania kwa nini Mungu asiumbe dunia isiyo na efficiency?

Hivi unaelewa hata ninachoandika?
 
Back
Top Bottom