Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

...Kuelekeza tuhuma moja kwa moja kwa polisi kwa ajali za mabasi sio sahihi

...Kuna tamaa binafsi(madereva,makondakta na wenye mabasi) kuna ubovu wa mabasi, kuna matatizo ya barabara zetu, uchovu, ulevi, uzembe wa watu wengine watumiao barabara zaidi ya mabasi na sababu nyingine chungu nzima. Hivyo kabla ya kunyosha kidole na kupanyuka ni vema ukaangalia kwa kina ni vitu vingapi vinavyosababisha ajali.

Sina takwimu za kiutafiti juu ya sababu za ajali za mabasi. Lakini kuna moja nalijua:

Sababu moja ya msingi ya Wananchi kufa kwenye mabasi ni Wananchi.

Umeshasikia dereva amegeesha chupa ya bia pembeni ya gia huku anaendesha na Wananchi waangalia ?

Dereva anashindana, anaendesha upande wa kulia wa barabara mbele kuna kuna curve au mshuko hamuoni kuna nini kinakuja halafu Wananchi wamekaa tu!

Unamuogopa dereva kumwambia utatuua? Au kuomba kushushwa pale pale unapoingia kwenye basi ukaona chupa ya bia imefunguliwa kabla ya safari ? Au kuripoti kwa mmiliki wa mabasi kwamba tajiri umeajiri wauaji ? Au kuripoti kwingine?

Abiria tunaogopa kumkoromea dereva?
 
Mwikimbi,
Nilishasafiri kwa basi hilo kutoka Shinyanga hadi Tabora mwaka huu. Kama ulivyosema ni kweli kabisa. Nilikuwa naenda Sikonge, ila kwa kuwa mvua ilinyesha sana Tabora, na uwanja ukawa umelowa lowolowo basi ndege ikitua ni kuwa haitwaweza kupaa. Kufika Shinyanga jamaa wa Precion air wakatukatia ticket ya hilo bus. Ila niseme ukweli mmoja. Jamaa pamoja na kuweka hadi abiria waliosimama, ule mzani wa TANROAD ulikuwa unawapa sana headache kuwa wakizidisha mizigo na abiria basi watalipa faini kubwa sana. Dereva alijitahidi sana kufuata sheria. Tulipotoka kituo cha mabasi tulienda Petrol Station na hapo tulishushwa wote wakati jamaa ana-FUEL gari. Tuliambiwa kuwa ndiyo sheria. Hakuendesha kwa speed ya ajabu pamoja na kuwa kwenye barabara safi sana kuja Nzega. Kufika Nzega hapo kivumbi kilianza. Ila jamaa alikuwa anaendesha taratibu sana ukichukulia mvua ilivyonyesha iliharibu sana barabara. Asubuhi yake nilienda kituo cha mabasi Tabora na kupanda basi moja la ajabu. Hilo Bus tulijazwa kama Mahindi kwenye gunia. Nilipoingia ndani sikuamini kuona kuwa pamoja na mizigo kuwekwa chini ya abiria, kulikuwa kuna tundu hadi unaona ardhi. Body ya gari ilikuwa imepigwa welding na kuwekwa viraka kibao. Ila maadamu mtu unaenda kwenu na huna jinsi, niliingia hivyo hivyo. Mama mmoja alisahau mizigo na akaomba wamrudishie nauli. Jamaa walimfanyia ushenzi sana hadi nikaamua kumrudishia mimi nauli hiyo. Pamoja na dhuruma hiyo na abiria kujazwa kama mahindi, ndani ya hilo basi alikuwemo POLISI WA WILAYA YA SIKONGE na alishuhudia mama akilia kwa uchungu mkubwa sana. Ajabu analilia dola nane tu, umasikini mbaya nyie? Mungu bariki dereva alikuwa akiendesha kulingana na UBOVU wa barabara. Ukiona Traffic barabarani basi ujuwe mwisho wa mwezi. Sasa hapa nawapa hongera sana Madreva wale. Ila uongozi wote wa hiyo kampuni wanahusika moja kwa moja katika KUJAZA abiria. Wasijifanye kuwa hawajui. Si wanaona idadi ya ticket kuwa kubwa kuzidi uwezo wa basi? Ahh, zikija fedha nyingi ni mswano tu kwa PESA HAZIBANANI
 
Bandiko lako ni zuri, na sio mara ya kwanza kuwepo na bandiko kama hili hapa JF, Iwapo kweli u msafiri na mkereketwa wa usafiri wa mabasi hapana shaka ungekuwa umeyaona hayo mabandiko ambayo yamejaribu kuzungumzia kwa kina ajali za mabasi na kutoa mapendekezo kadha wa kadha.

Kuelekeza tuhuma moja kwa moja kwa polisi kwa ajali za mabasi sio sahihi na wala hakuna ushahidi wowote wa nguvu kwa hilo, kwani wanaoathirika na ajali hizo ni abiria pamoja na mwenye basi.

Mada ulizoandika kuhusu ajali nyingi ni kutoa shutuma ama kwa Polisi au kwa mmiliki wa chombo hicho kama kwenye bandiko la " Gari la Sumry lililokuwa linatoka Dar kwenda Mbeya limepata ajali Makambako "




Kuna tamaa binafsi(madereva,makondakta na wenye mabasi) kuna ubovu wa mabasi, kuna matatizo ya barabara zetu, uchovu, ulevi, uzembe wa watu wengine watumiao barabara zaidi ya mabasi na sababu nyingine chungu nzima. Hivyo kabla ya kunyosha kidole na kupanyuka ni vema ukaangalia kwa kina ni vitu vingapi vinavyosababisha ajali.

Zaidi hata ubora wa mabasi yenyewe umekuwa ni mjadala hapa JF kuhusiana na ongezeko la ajali kama ilivyajadiliwa katika bandiko hili

Nikirudi kwenye listi yako mabasi yote uliyoyataja hapo juu yamewahi kupata ajali...Kwa mfano Fresh ya Shamba ajali zake nyingi zilitokea katika barabara ya DSM - MBY kuliko DSM -AR. Ajali hizo ni pamoja na basi moja la Fresh ya Shamba kuteketea kwa moto likiwa njiani kwenda Mbeya.


hapana. fresh ya shamba iliungua pale korogwe wakati abiria wanapata lunch pale . alikuwa na bima na watu walifidiwa, huwezi kulinganisha ajali hizi, na hawa wenzetu wanaoua kila siku aidha kwa spidi kubwa au kuanguka kwenye mitaro wakikimbilia abiria. tukiwa wakweli bila kujali maslahi binafsi, ajali zitapungua na itakuwa kama nchi nyingine.
 
Kuna ajalimbaya imetokea maeneo ya milima ya Sekenke Kijiji cha Shelui ambapo basi la Zuberi Trans liliokuwa likitoka Mwanza kupata ajali majira ya saa 5 asubuhi na kuua zaidi ya watu 30 baada ya kutumbulia mtoni.

Tunaelekea mwisho wa mwaka ambapo ajali nyingi hutokea. Mungu awape nafuu walionusurika.
 
Mungu awarehemu na awape nguvu na faraja wafiwa wote,mkono wa rehema uwafunike majeruhi wote
 
Pole sana kwa ngudu, marafiki na jamaa wa marehemu lakini pia Taifa kwa ujumla.
 
Ukweli ni kuwa basi hilo la Zuberi lenye nambari za usajili T 677 AGJ limepinduka baada ya break zake kushindwa kufanya kazi.

waliokufa katika ajali hii ni 17 na wengine 35 wamejeruhiwa na basi lilikuwa likitoka Dar es Salaam kuelekea Mwanza, lililala Singida kutokana na magari kukwama katika barabara hiyo.

Dereva ambaye hajafahamika, usiku kabla ya ajali alilalamika kwa askari wa usalama barabarani kuwa basi hilo ni bovu na kwamba breki zake zilikuwa hazifanyi kazi sawasawa, lakini abiri walimshupalia na ikabidi eti hiyo asubuhi aanze safari.

Ni kwamba baada ya kufika katika mlima huo na kuanza kuteremka, breki za gari zilishindwa kufanya kazi na katika kuliokoa akalipeleka kilimani lakini likavuka kilima na kutumbukia kwenye kurongo ambali urefu wake unakadiriwa kuwa kilometa hamsini.

end
end
 
Last edited:
Jamani inasikitisha sana najua ndungu zangu washosha NG'OMBE wamekufa wengi!
Hili basi huwa linakimbia mno!jamani chanzo cha ajali ni nini?
 
Kuna ajalimbaya imetokea maeneo ya milima ya Sekenke Kijiji cha Shelui ambapo basi la Zuberi Trans liliokuwa likitoka Mwanza kupata ajali majira ya saa 5 asubuhi na kuua zaidi ya watu 30 baada ya kutumbulia mtoni.

Tunaelekea mwisho wa mwaka ambapo ajali nyingi hutokea. Mungu awape nafuu walionusurika.

Hivi wewe mleta habari unaijua barabara ya kwenda MWANZA?sasa hapo shelui kuna mto gani?
 
Ukweli ni kuwa basi hilo la Zuberi lenye nambari za usajili T 677 AGJ limepinduka baada ya break zake kushindwa kufanya kazi.

waliokufa katika ajali hii ni 17 na wengine 35 wamejeruhiwa na basi lilikuwa likitoka Dar es Salaam kuelekea Mwanza, lililala Singida kutokana na magari kukwama katika barabara hiyo.

Dereva ambaye hajafahamika, usiku kabla ya ajali alilalamika kwa askari wa usalama barabarani kuwa basi hilo ni bovu na kwamba breki zake zilikuwa hazifanyi kazi sawasawa, lakini abiri walimshupalia na ikabidi eti hiyo asubuhi aanze safari.

Ni kwamba baada ya kufika katika mlima huo na kuanza kuteremka, breki za gari zilishindwa kufanya kazi na katika kuliokoa akalipeleka kilimani lakini likavuka kilima na kutumbukia kwenye kurongo ambali urefu wake unakadiriwa kuwa kilometa hamsini.

end
end

Poleni wafiwa na majeruhi kwenye ajali hii mbaya kabisa, hilo Kolongo ni Km 50 ama ulikuwa unaimanisha 50 M?
 
Hivi wewe mleta habari unaijua barabara ya kwenda MWANZA?sasa hapo shelui kuna mto gani?


Hata kama hajui si amekuletea habari na umejua nini kinaendelea?? Na hao wanaojua si wameshakuelekeza zaidi au unataka kuleta malumbano yasiyo na misngi?? Kani ungekaa kimya ni nani angekucheka au ungekatika sikio?? Grow up na ujenge tabia ya kushukuru pale unapoletewa habari.
 
[/COLOR]

Hata kama hajui si amekuletea habari na umejua nini kinaendelea?? Na hao wanaojua si wameshakuelekeza zaidi au unataka kuleta malumbano yasiyo na misngi?? Kani ungekaa kimya ni nani angekucheka au ungekatika sikio?? Grow up na ujenge tabia ya kushukuru pale unapoletewa habari.

mhhhh umemtolea uvivu First lady wetu leo....
 
[/COLOR]

Hata kama hajui si amekuletea habari na umejua nini kinaendelea?? Na hao wanaojua si wameshakuelekeza zaidi au unataka kuleta malumbano yasiyo na misngi?? Kani ungekaa kimya ni nani angekucheka au ungekatika sikio?? Grow up na ujenge tabia ya kushukuru pale unapoletewa habari.

Siwezi kukaa kimya kama habari yenyewe ina utata!basi kutumbukia mtoni ilhali hakuna mto!lazima niulize i dare to talk openly!
 
[/COLOR]

Hata kama hajui si amekuletea habari na umejua nini kinaendelea?? Na hao wanaojua si wameshakuelekeza zaidi au unataka kuleta malumbano yasiyo na misngi?? Kani ungekaa kimya ni nani angekucheka au ungekatika sikio?? Grow up na ujenge tabia ya kushukuru pale unapoletewa habari.

Hapo chukua five, maana wengine mentali zetu zimekaa kichokozi na kichokonozi hata kama habari inajieleza wazi ili mradi tuweke vidole vyetu kwenye keyboard tu.
 
Dah, poleni wafiwa na poleni sana majeruhi.........hivi hizi hadithi za kusema abiria walilazimisha dereva kuendesha gari hata dereva alipodai kuwa breki zake haziko sawa.........zina ukweli?......au ndio kuamisha lawama!!......sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu akiambiwa gari bovu atalazimisha dereva aendeshe tu........na hata dereva mwenyewe akiendesha atakuwa na matatizo fulani..........
 
Siwezi kukaa kimya kama habari yenyewe ina utata!basi kutumbukia mtoni ilhali hakuna mto!lazima niulize i dare to talk openly!

Kama habari ina utata itaendelea kuwa tata mpaka hapo utata utakapoondolewa na mtu mwenye taarifa kamili either witness au vyombo vya usalama vyenye authority ya kutoa taarifa kamili kwa sasa tunachojua ni kwamba kuna watanzania wenzetu wamepata ajali wakiwa njiani kuelekea mwanza na kuna vifo na majeruhi- Tunachopaswa kufanya hivi sasa ni kuwaombea majeruhi ahueni na waliotutoka mungu awape pumziko la milele na pole kwa wafiwa
 
Siwezi kukaa kimya kama habari yenyewe ina utata!basi kutumbukia mtoni ilhali hakuna mto!lazima niulize i dare to talk openly!


Mama wa kwanza Unaruhusiwa kuongea wazi lakini huna sababu ya kumkosoa mwenzako eti ooh unaijua njia ya Mwanza wewe ooh hiki na hiki, haya we unaijua vizuri hiyo njia tuletee habari basi ( Hebu angalia mwenzako alivyotumia kumuelewesha mtoa habari sahihi kuwa anafikiri ni 50 M na si 50 KM) ukiongea ka upole utaeleweka lakini si kwa kupayuka as if upo kwenye taarabu. N'way yawezekana ni hulka yako bwana maana jina lenyewe linaji identfy........
 
kama habari ina utata itaendelea kuwa tata mpaka hapo utata utakapoondolewa na mtu mwenye taarifa kamili either witness au vyombo vya usalama vyenye authority ya kutoa taarifa kamili kwa sasa tunachojua ni kwamba kuna watanzania wenzetu wamepata ajali wakiwa njiani kuelekea mwanza na kuna vifo na majeruhi- tunachopaswa kufanya hivi sasa ni kuwaombea majeruhi ahueni na waliotutoka mungu awape pumziko la milele na pole kwa wafiwa


ahsante kaka....
 
Back
Top Bottom