Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

ni kweli kuna ajali lakini kuna siri kubwa sana kuhusu ajali zinazofanywa na haya mabasi. nasikia mwenye nayo ameanza tabia za kuhonga ili ajali zifichwe. last month nilisafiri na gari la sumry from mbeya kwenda dar, mabasi haya yana mwendo kasi ajabu, halafu hakuna ustarabu barabarani

sidhani kama atafanywa lolote kwa kuwa akina kova walikuwa wanaponea kwake pale mbya

WATU wawili wamefariki dunia baada ya basi la Kampuni ya Sumry walilokuwa wakisafiria kutoka Dar es Salaam kwenda Tunduma, mkoani Mbeya kupinduka.

Basi hilo T587 ARY Nissan, lilipinduka juzi, saa 8 mchana katika eneo la Kinyanambo A, mjini Mafinga, Wilaya ya Mufindi, baada ya kumgonga mwendesha baiskeli na kusababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi wengine 23.

Akielezea tukio hilo, mmoja wa abiria aliyekuweo kwenye basi hilo, Rehema Mwakalonge (47) mkazi wa Mbalizi Mbeya, alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendesha baiskeli ambaye alikuwa akionyesha kuyumba barabarani.

Alisema baada ya mwendesha baiskeli huyo kukosa mwelekeo, dereva alijitahidi kumkwepa ilishindikana na kusababisha basi hilo lililokuwa kwenye mwendo kasi kupinduka.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mufindi, Dk Deogratias Masawe, alisema majeruhi 23 ndio waliofikikshwa hospitalini hapo kupatiwa matibabu.

Hata hivyo, alisema hali za majeruhi watatu kati ya hao ni mbaya huku dereva wa basi hilo, Oscar Bango (43) amekatwa mguu mmoja kutokana na kupondeka vibaya katika ajali hiyo.

Kwa upande wake, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Crausy Mwasyeba, aliwataja waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni mwendesha baiskeli aliyesababisha ajali hiyo, Tija Nyangwa (18), mkazi wa Kinyanambo B na Joyce Chikwanda (26), mfanyabiashara na mkazi wa jijini Dar es Salaam.

Mwasyeba alisema basi hilo baada ya kumgonga mwendesha baiskeli liliangukia ubavu na kulala katikati ya barabara kuu ya Iringa -Mbeya.

Source: Tz Daima
 
ni kweli kuna ajali lakini kuna siri kubwa sana kuhusu ajali zinazofanywa na haya mabasi. nasikia mwenye nayo ameanza tabia za kuhonga ili ajali zifichwe. last month nilisafiri na gari la sumry from mbeya kwenda dar, mabasi haya yana mwendo kasi ajabu, halafu hakuna ustarabu barabarani

sidhani kama atafanywa lolote kwa kuwa akina kova walikuwa wanaponea kwake pale mbya

Mimi nilikuwa nawaheshimu sana sumry ukilinganisha na sabco mwendo wao sio mbaya sana. Sasa tukimbilie wapi jamaani!!!!!!!!!Scandinavia ndio basi tena,du !!!!!!!!!!
 
Hizi ajali kunatakiwa kuwekwe mpango wa kudumu na kudetermine the root cause. LAKINI SIKU ZOTE HUWA TUNAKURUPUKA MFANO NI KUWEKA VITU VINAITWA CHECK POINTS KIBAO AMBAVYO HAVISAIDII MAANA JAMAA WANAKAMATA KITU KIDOGO BASI LINARUHUSIWA. NIONAVYO MIMI CHUO CHA USAFIRISHAJI KIANDAE COURSE MAALUM KWA MADEREVA WOTE YA DEFENSIVE DRIVING NA PIA IWE NI LAZIMA KUFUZU HIYO ILI UPEWE LESENI. HALAFU PIA TBS/ERB WELL SINA UHAKIKA KAMA TUNA CODE OF STANDARDS TZ INAYODEFINE BASI MAANA NAONA KAMA KILA MTU ANAJITENGENEZEA KAMTINDO KAKE MENGINE KAMA PANZI, BOARD NZIMA NI FIBERS, SPACING KATI YA KITI NA KITI HAIELEWEKI, VIOO VINAFLAP NA KUPIGA MAKELELE SAFARI NZIMA.

HIVYO BASI FROM THE DESIGN POINT OF VIEW KUWE NA STANDARDS NA ZIWE WAZI KUHUSU JE BASI LA ABIRIA NI NINI? US HII IPO INTO MUNICIPAL LEVEL TUNAWEZA PIA KUCOPY NA KUPASTE KAMA TULIVYOFANYA KWENYE SHERIA ZA KAZI.
 
Faraja ya Mungu iwe na familia zotezilizo katika majonzi na masumbufu kutokana na ajali hii.
 
halafu huyu sumry ni mbunge katika moja ya majimbo ya mkoani rukwa

hapana, yule mbunge wa chadema mpanda kati mh.arf sumnry? Siyo mmiliki wa haya mabasi

mmiliki wa haya mabasi ni mkereketwa wa ccm wa muda mrefu, ni mwekezaji wa miradi mbalimbali mkoani rukwa, na ana asili ya asia kama kawaida

madereva wake ni jeuri kupita kiasi, wakiendesha spidi wakionywa hawasikii kwa ajili ya kiburi cha hawa mmilikaji wake ambaye amewakeka polisi mfukon i
 
Ajali inayozungumziwa ni ya pili kwa wiki hii

ya kwanza ilitokea mafinga juzi , na jana ni hii ya makambako

waandishi wa habari naona bado wnampamba mmiliki kuwa eti mpanda baiskeli ndo alisababisha ajali. Wanaofahamu mafinga, kinyananmbo ni eneo la miji wa mafinga, speed limit pale ni 30km/hr, na makambako pia ni mjini

nategemea kuanzisha thread hapa kujadili ajali za barabarani na vyanzo vyake, na kuwataja wamiliki wa mabasi wanaoshirikiana na waandishi wa habari kuficha ajali hizi
 
Ajali inayozungumziwa ni ya pili kwa wiki hii

ya kwanza ilitokea mafinga juzi , na jana ni hii ya makambako

waandishi wa habari naona bado wnampamba mmiliki kuwa eti mpanda baiskeli ndo alisababisha ajali. Wanaofahamu mafinga, kinyananmbo ni eneo la miji wa mafinga, speed limit pale ni 30km/hr, na makambako pia ni mjini

nategemea kuanzisha thread hapa kujadili ajali za barabarani na vyanzo vyake, na kuwataja wamiliki wa mabasi wanaoshirikiana na waandishi wa habari kuficha ajali hizi

Ajari imetokea jana na nina hisi ilikuwa mchana kwa nini waandishi wa habari hawaja report hii ajali au Kamanda wa mkoa hajapata taarifa na kuthibisha??? Kuna mkono hapo lazima mlio karibu fuatilieni hili swala ..... watu wamepewa kitu kidogo hapo inanikumbusha ile Ajali ya ABOOD morogoro waandishi walivyo poozwa na maiti nyingine kufichwa hawa waarabu watatumaliza jamani na mabus yao.
 
hapana, yule mbunge wa chadema mpanda kati mh.arf sumnry? Siyo mmiliki wa haya mabasi

mmiliki wa haya mabasi ni mkereketwa wa ccm wa muda mrefu, ni mwekezaji wa miradi mbalimbali mkoani rukwa, na ana asili ya asia kama kawaida

madereva wake ni jeuri kupita kiasi, wakiendesha spidi wakionywa hawasikii kwa ajili ya kiburi cha hawa mmilikaji wake ambaye amewakeka polisi mfukon i

Wrong! Kwanza sijasema kuwa ni Mbunge wa Chadema Arf. Huyu ninae mzungumzia anaitwa Mh Abdallah S. Sumry ni Mbunge wa CCM ( Mpanda Magharibi)
 
Maximum speed ya mabasi si 120km/h? Huo mwendo wa kasi ajabu ukoje?

....kibunango acha kubeza mkuu! natumaini umemwelewa kabisa mwikimbi... ila unataka kumchanganya akili tu.

....speed inaonekana kubwa kulingana na ukubwa/aina ya chombo au njia ipitapo chombo hicho.

....kwenye makazi ya watu, speed 40mh ni kubwa lakini speed hiyo kwenye freeway/motorway ni ndogo. fikiria boat za kwenda Zenji zipepee juu ya maji kwa 90m/h..... hapo si itakuwa noma!

....gari la fani yako/formula 1 likienda kwa speed ya 120km/h litaonekana linaenda speed ya kawaida. lakini speed hiyo hiyo iki-clockiwa na 15ton truck itakuwa ni speed kubwa sana.

....you know wot i mean, baadae.
------------------------------------------------

Nawaombea Wapumzike Pema Peponi Wale Wote walioangamia. Amina.

SteveD.
 
Maximum speed ya mabasi si 120km/h? Huo mwendo wa kasi ajabu ukoje?

Maximum speed kwa barabara za TZ nafikiri ni 80km/h, kama ni hivyo huoni hiyo 120km/h ni kasi ya ajabu?

Kwenye ajali ya jana kafariki Kondakta na wengine kuumia.
 
hili la abood kuficha maiti ni cha mtoto, kuna msafirishaji mwingine mwenye magari ya kubaba mzigo mbeya. yeye kuna wakati gari lake lilivamia wamama 13 waliokuwa wanauza ndizi kando ya barabara ya mbeya -malawi, kiwira section, na wote wakafa, pamoja na ajali nyingine za namna hiyo kwa mmiliki huyu ni nyingi, last time afisa wake alikuwa anatamba kuwa wao huwa hawakamatwi na traffic bila huyu mkubwa wao kutoa ruhusa, kwa kuwa alishamalizana na traffic period! jeuri hii ya kupindisha sheria inapaswa kupigiwa kelele
 
kama mwendelezo wa ujinga wa madereva wetu, leo asubuhi hapa tabora, mohamad trans bus iliyokuwa inaenda mwanza toka tabora, ikifukuzia abiria eti kupiku mabasi mengine ya nbs, na Am, imepinduka vibaya na kuangukia nyumba na maduka ya wafanyibiashara baada ya kuacha njia!, nimeiona imeanguka vibaya, sijajua maafa ni kiasi gani, lakini ni lazima kuna majeruhi wengi.

nitawaletea habari zaidi. lakini mwendolezo huu wa ajali za kujitakia ni tatizo kubwa kitaifa.ni vema kukaweko mjadala wa kitaifa ili kinachochangia ajali hizi kiwekwe wazi. kwa haraka haraha tu kama nilivyowahi kuandika. wamiliki wakubwa wa vyombo hivi vya usafiri ni pete na kidole na jeshi la polisi. ma utasikia hamna hatua yeyote itakaychokuliwa
 
Hawa vichaa watatugharimu maisha yetu mpaka lini? Maana maderev a wanashitakiwa wakati wenye magari wanaachwa ambao ndo wanaajiri madereva vichaa.
Tuanzishe mjadala wa kitaifa kuangalia uwezekano wa kuwafutia madereva leseni pamoja na wamiliki wa mabasi.
Ukiangalia basi la mohamed liligharimu maisha ya rafiki zangu waliokuwa wanasoma UDSM na watanzania wengine wengi tu kw auzembe wa kufukuzana.
Mabasi ya SUMRY yamekuwa yakipata ajali kila kukicha lakini kwa kuwa yanashirikiana na vigogo habari zao hazitangazwi.
Hivi mbona serikali yetu inaongozwa na watu wenye tamaa ya vijipesa vidogo wakati maisha ya watu yanakatika????????Hakuna taifa lililoendelea wakati halikujali maisha ya watu wake.Kama kuna mtu analijua aniambie na hayo maendeleo si ya kudumu maana watu wanaoleta maendeleo maisha yao yako hatarini.
Ukiangalia nchi kama Ireland,hawana lolote zaidi ya watu wao lakini wanaumia sana wanapopoteza mtu mmoja na wanajitahidi isitokee kama kuna uwezekano wa kuzuia.Maana unapompoteza mtu mmoja ambaye may be ni daktari umepoteza resource ambayo itakuchukua more than 25 years to replace na hapo sijapigia financial resources zinazotakiwa kumreplace.
Watanzania tuanzishe mjadala kama alivyosema mwenzetu.
 
Kwahiyo niki kuazima gari, ukaenda ukalewa au ukaendesha kizembe na kupata ajali mimi mwenye gari ndo nishtakiwe?

MODS naomba iende kwenye habari mchanganyiko hii.
 
ajali imeua watu wawili, naona hili haligusi wengi wenu, lakini kama huwezi ku-adress hili ni bure kuzungumzia mambo mengine, just imagine umekaa marekani miaka 20, unakuja kumsalimia mama na baba hapa tabora, unafika tabora salama kwa ndege, lakini kwenu ni sikonge huna namna unapanda basi halafu dereva ambaye alishaambiwa na bosi yake, yaani mmiliki kuwa usiwe na wasiwasi KILa siku niko na RPC, na kwa kujiamini katika kukimbilia abiria anakumwaga kwenye mtaro, na ndoto zako zinaishia hapo.

nimesafiri sana nchi yetu, tihi week from kilimanajro to dodoma shinyanga then atabora-mbeya back to tabora, last week, moshi nairobi kampala -bukoba then mwanza to dsm by road. ukweli ni kuwa laxity inayoonyeshwa na traffic katika tanzania ni hatari hasa kwa mabasi ya abiria. ebu tujiulize kwa nini mabasi haya hayana rekodi za ajali

1 fresh ya shamba, tabgu kuanzishwa mpaka ilivyofilisika?
2 scandinavia(ukiacha ajali chache zilizosababishwa na matairi mabovu, wakafanya utafiti na bridgestone wakawajibishwa

3 hekima bus

4 dar express, ilikuwa na ajali mwanzoni, mrema akiwa waziri akawakomolea, wakapeleka madereva shule na kufukuza wavuta bangi sasa ajali kwao ni historia

hawa ndo vinara wa ajali

1. ngorika bus kule moshi, tunaambiwakiburi anakipata kwa rushwa

2.buffalo linamilikiwa na akina mahita

3.sumry-mfadhili mkuu wa ccm

4.shabiby -mfadhili mkuu wa ccm

5.champion-kama hapo juu

list ni ndefu
 
.... ebu tujiulize kwa nini mabasi haya hayana rekodi za ajali

1 fresh ya shamba, tabgu kuanzishwa mpaka ilivyofilisika?
2 scandinavia(ukiacha ajali chache zilizosababishwa na matairi mabovu, wakafanya utafiti na bridgestone wakawajibishwa

3 hekima bus

4 dar express, ilikuwa na ajali mwanzoni, mrema akiwa waziri akawakomolea, wakapeleka madereva shule na kufukuza wavuta bangi sasa ajali kwao ni historia

hawa ndo vinara wa ajali

1. ngorika bus kule moshi, tunaambiwakiburi anakipata kwa rushwa

2.buffalo linamilikiwa na akina mahita

3.sumry-mfadhili mkuu wa ccm

4.shabiby -mfadhili mkuu wa ccm

5.champion-kama hapo juu

list ni ndefu

Bandiko lako ni zuri, na sio mara ya kwanza kuwepo na bandiko kama hili hapa JF, Iwapo kweli u msafiri na mkereketwa wa usafiri wa mabasi hapana shaka ungekuwa umeyaona hayo mabandiko ambayo yamejaribu kuzungumzia kwa kina ajali za mabasi na kutoa mapendekezo kadha wa kadha.

Kuelekeza tuhuma moja kwa moja kwa polisi kwa ajali za mabasi sio sahihi na wala hakuna ushahidi wowote wa nguvu kwa hilo, kwani wanaoathirika na ajali hizo ni abiria pamoja na mwenye basi.

Mada ulizoandika kuhusu ajali nyingi ni kutoa shutuma ama kwa Polisi au kwa mmiliki wa chombo hicho kama kwenye bandiko la " Gari la Sumry lililokuwa linatoka Dar kwenda Mbeya limepata ajali Makambako "

Kuna tamaa binafsi(madereva,makondakta na wenye mabasi) kuna ubovu wa mabasi, kuna matatizo ya barabara zetu, uchovu, ulevi, uzembe wa watu wengine watumiao barabara zaidi ya mabasi na sababu nyingine chungu nzima. Hivyo kabla ya kunyosha kidole na kupanyuka ni vema ukaangalia kwa kina ni vitu vingapi vinavyosababisha ajali.

Zaidi hata ubora wa mabasi yenyewe umekuwa ni mjadala hapa JF kuhusiana na ongezeko la ajali kama ilivyajadiliwa katika bandiko hili

Nikirudi kwenye listi yako mabasi yote uliyoyataja hapo juu yamewahi kupata ajali...Kwa mfano Fresh ya Shamba ajali zake nyingi zilitokea katika barabara ya DSM - MBY kuliko DSM -AR. Ajali hizo ni pamoja na basi moja la Fresh ya Shamba kuteketea kwa moto likiwa njiani kwenda Mbeya.
 
Back
Top Bottom