Bwana alitoa na leo ametwa jina lake lihimidiwe na kila goti lipigwe kwake. Roho zao zipumzike kwa amani . Lakini hapo Singida kunanini jamani? mara Basi la Mohamed Trans limewaka moto mara watoto wameuwawa kinyama why? kwanini? tujiulize jamani,ikiwezekana huyo Kamanda wa polisi wa Mkoa kashindwa kazi aachie ngazi,SAA 4.30 USIKU MABASI HAYATAKIWI KUENDELEA NA SAFARI VIPI HILI LILIKUWA LINAENDELEA NA SAFARI KAMA KAWAIDA? Manyoni kuna trafic pale,wameliruhusu vipi kwa muda huo?.
Mungu awarehemu marehemu wote, na majeruhi wapate ahueni haraka. Hizi ajali zisizokwisha kwa kiasi kikubwa zinasababishwa na MAFISADI, kwani chanzo cha kuwa na barabara mbovu na madereva wasioheshimu sheria ni rushwa iliyozaa ufisadi usiomithirika.
Hivi Watanzania tutaendelea kutoa pole mpaka lini? Haiwezekani tatizo moja linajirudia na kujirudia lakini kama nchi hakuna jambo la maana tunalochukua kupambana na hizo ajali. Tutaendelea kulia mpaka lini?
Pole kwa waliofiwa na pia walioumia. Tunawaombea mupate nafuu haraka iwezekanavyo.
ni kweli kuna ajali lakini kuna siri kubwa sana kuhusu ajali zinazofanywa na haya mabasi. nasikia mwenye nayo ameanza tabia za kuhonga ili ajali zifichwe. last month nilisafiri na gari la sumry from mbeya kwenda dar, mabasi haya yana mwendo kasi ajabu, halafu hakuna ustarabu barabarani
sidhani kama atafanywa lolote kwa kuwa akina kova walikuwa wanaponea kwake pale mbya
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.