Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

watan
kosa kubwa tulilofanya watanzania wakati wa ubinafsishaji ni kuwapa wahindi viwanda ..leo wamevigeuza magodown na havizalishi....bora tungewapa wazawa kama kina mugishangwe ,mengi....na wengine...

Usiseme watanzania; waliofanya hii blunder ni Mkapa na CCM.
 
..je,umejiuliza kama hao wazazi nao wana adabu?

..we mama anapakuwa chakula anaweka mezani. baba kwa ulafi wake anawahi mapande yote mazuri ya nyama,tena karibia zote!. hao watoto kesho wakimwambia "baba acha ulafi" watakuwa na kosa gani?

..btw,muwe mnakumbuka kunawa mnapokula!

..unaongelea malezi? yapi? haya ya kuwafundisha watoto wetu jinsi ya kula rushwa na kujilimbikizia mali nyingi kwa muda mfupi?

..nani analipeleka taifa pabaya? baba/mama au mtoto?

..... JF imejaliwa vichwa utadhani ni group ya "wise (wo)men" wanaoendesha masuala ya kila siku ya Marekani?!!!!
 
mkapa yes...juu juu.

tangu lini mahakama zikahamia kijiweni!!???..alivyosema warioba leo sawa...kinga ya rais ni political..na kuliko kuendelea kumtuhumu tu wampeleke mahakamani haraka akajibu huko..sio kumzomea..

...na hili la kumdhalilisha ndio kikwete alilokuwa analitaka kama shukrani yake ....baada ya kumsaidia kumwangusha salim...,lakini si haki!!

mkapa anayo mazuri na pia anayo mabaya...kama kikwete anaona haya mabaya yana jinai ampeleke mahakamani haraka au kama hilo haliwezekani na akae kimya!!!!..yeye na watu anaowatumia kumchafua mtangulizi wake..ili tusipate muda wa kumuongelea yeye!!!

..talking about camps,bro?

..wakati wenu wa kutesa ulishapita! sasa msubiri mteswe!

..kuna usemi usemao "shukrani ya punda,mateke"
 
Kama bado Mkapa anahudhuria ibada ningeomba kujua ni kanisa gani?
Kuna kila sababu ya kuwashawishi waumini husika wamfukuze kanisani mpaka pale atakaporudisha mali aliyoiba yeye na washirika wake. Vita hii lazima iende mbali. Kile kiti cha enzi anachopewa kanisani lazima anyang'anywe. Kwani iliandikwa, "Nyumba yangu sio pahali pa wezi na wanyanganyi" maana nyumba ya ibada. Leo iweje mnyanganyi na muuwaji mkapa aruhusiwe kuingia kanisani? Ujumbe huu naomba umfikie paroko wa mkapa na mshikaji wake Polycarp Pengo.

Naomba fedha zote alizochangia kanisani arudishiwe kwani ni fedha haramu hazina baraka mbele ya mwezi Mungu.

Mkapa tubu dhambi umrejee muumba wako, wewe tayari ni mzee, unaumwa miguu, siku za kuishi ni miaka sabini , themanini ni bonasi.

Pengo, Pengo, Pengo sikusikii kabisa kuhusu huyu jamaa. Tuambie na lazima ueleze jamii moja kwa moja kwamba unayemsema ni Mkapa.

Je ikitokea wananchi wakaenda kanisa analosali halafu kuzomea wakati anaingia na kutoka kanisani, je waumini wakaamua kuanza kumnyooshea vidole mle kanisani watakamatwa?
 
Naunga mkono kitendo cha vijana hawa, wengi wanafanya hivyo hata kama hawapati nafasi ya kupayuka. Inawezekana mawe yalikuwa mbali.

Hatutawazoemea tu, ikifika wakati, tutawakaanga
 
....well said ...tena over all the places in dar azomewe MASAKI...na pale hakuna kituo cha polisi karibu zaidi ya obay...hao polisi walijuwaje kuwa mkapa akipita atazomewa ili mara moja wakamate watu kijiweni...kama sio hao watu waliozomea ni planned na mwisho wa siku hakuna kesi....propaganda za kijinga kabisa za kikwete na cronies wake..inasikitisha sana,lowassa amezomewa mara ngapi ..mbona naye hawajakamatwa..thats propaganda!!.....mkapa asizomewe mjini au kwenye traffic lights na vijana waliokata tamaa ..azomewe, of all the places in dar, MASAKI..lets be serious jamani!!!

..bro phil,

..acha guessing kama za HRC dhidi ya BO!

..we pale unapafahamu?au unaongea tu?. kwa taarifa,pale wanakaa vijana wengi wanaotafuta/fanya kazi maeneo yale. pia,kuna vibanda vya lishe!. so u can guess ni tabaka lipi la watu lina hang at that corner!. be so informed!.

mkapa angemfanyia hivo mwinyi tungefika ..hivi mnayajua yaliyokuwamo kwenye ripoti ya warioba jamani!!!..ingefunuliwa mwinyi asingepona....dereva gani anaangalia nyuma tu...si tutagonga jamani!!!

..ya mwinyi yalishapita!. unataka kusema JK kaloga wananchi wote waiseme na kuichunguza serikali iliyopita?. unataka kusema,JK kawahonga au kula njama na kina dr.slaa & co. kufumua uozo uliokuwa katika hilo genge!

..acha kumsingizia JK. ushawahi kushika sufuria la moto wewe? sasa,hizo issue ni sawa na kushika sufuria la moto kwa bare hands!........nothing can be done,and it's sad for u guys....

nchi inaelekea ndiko siko kwa kuteka akili za wenye akili nyepesi!!!

..mlitakiwa kujua kwamba kuna kuumwa tumbo au kuharisha,usiponawa mikono wakati wa kula!

..after this,tanzania will be a better place! trust me!
 
Hata kama Mzee Mkapa ni Mwizi(Hapa mahakama haijaamua) ila jua ya Kwamba bado ni Rasi Mstaafu tu..other thing reamin Constant.

Wewe unadhani kama angepita kiongozi mstaafu wa upinzani watu wakaanza kumzomea,viongozi wa juu wanatembea na mtoto wako huku wakimghasi..Polisi wakikaa kimya unadhani italeta picha nzuri??


Mie nashangaa haswa...hivi huyu "Gembe" ni mzalendo na ni mtanzania kweli??? Maana naona argument zake juu ya ufisadi wa Mkapa ni very emotional, biased and unrealistic...Au ndio nyie mlopandikizwa na hawa mafisadi hapa JF ili ku-neutralize soo zao??

"Gembe", whoever you are...you are either (1) Clueless (2)Kibaraka wa Mkapa (3)Mtoto/Ndugu yake Mkapa or...(4) FISADI!!!
 
Ni rais mstaafu. Ni lazima tumuheshimu. we do not want to set a bad precedent. Kama anatuhumiwa wanaomtuhumu wampeleke mahakamani. Kumzomea haisaidii na ni kuvunja sheria!!

..hiyo bad precedent wamei-set wenyewe!
 
Maoni yangu ni kuwa sasa ni wakati wa kuanza kuangalia uwezekano wa kuchagua viongozi wapya pamoja na marekebisho makubwa ya kikatiba!
Wapya kabisa ambao hawajawahi kufanya kazi kwenye awamu zilizopita, na wala hawajuani na nobody alieko kwenye rank za uongozi!
Hapo taifa litazaliwa upya! Na maybe nuru mpya kuanza kuonekana!
Hawa viongozi wetu ni kama kabila la tofauti kabisa ndani ya Tanzania( or like aliens) ambalo liko absolutelly out of touch huku likilindwa na dola!
Na wao sio kama sisi hilo tusijidanganye! Wanajuana wenyewe kwa wenyewe na sasa ni wengi mno(from awamu ya kwanza till now) kiasi cha kufikia namba kubwa yenye uwezo wa kujenga tabaka la tofauti la kinyonyaji na kifisadi ndani ya Tanzania!
Wanaoana wenyewe kwa wenyewe, wanapeana madaraka wenyewe kwa wenyewe, na pia kupeana kazi na tenda wenyewe kwa wenyewe
Ni wengi kiasi cha kwamba hata mafao wanayoendelea kuyapata(mara baada ya kustaafu) yamekuwa mzigo mwingine tena wa kifisadi wenye kuendelea kuwaweka mafisadi kwenye viwango vya juu in definetly in leau of the poor people's tax money and our own resources!
Hawa watu ni tofauti kabisa na hata mazungumzo yao yanaonyesha!
Halafu wasaidizi wao nao ni tabaka moja tu na ndio maana hata (wanapowaandikia hotuba zao) wanazotoa zinaonyesha kuwa wako dunia nyingine kabisa ya tofauti! Mfano wa ile ya Muungwana huko Singida!
Yani mtaani hawajui kabisa kinachoendelea!
Maisha yao yote wako serkalini halafu tunategemea walete mabadiliko!?
Tunaota!
 
Je ikitokea wananchi wakaenda kanisa analosali halafu kuzomea wakati anaingia na kutoka kanisani, je waumini wakaamua kuanza kumnyooshea vidole mle kanisani watakamatwa?

..mamvi anafahamu vizuri hii kitu!
 
..mamvi anafahamu vizuri hii kitu!

yah mamvi a.k.a wakuvanga analijua fika na akafikia hata kujitetea mazishini. Hivi wale jamaa walomzomea wakuvanga pale white sands nao walikamatwa nini?

Je imefikia wapi kwa hawa vijana waliokamatwa?wameshaachiwa? kwa dhamana au hawana kesi? kwa yeyote mwenye kujua jamani, isije ikawa hawa vijana mashujaa wanaendelea kusotea mahabusu
 
Maoni yangu ni kuwa sasa ni wakati wa kuanza kuangalia uwezekano wa kuchagua viongozi wapya pamoja na marekebisho makubwa ya kikatiba!
Wapya kabisa ambao hawajawahi kufanya kazi kwenye awamu zilizopita, na wala hawajuani na nobody alieko kwenye rank za uongozi!
Hapo taifa litazaliwa upya! Na maybe nuru mpya kuanza kuonekana!
Hawa viongozi wetu ni kama kabila la tofauti kabisa ndani ya Tanzania( or like aliens) ambalo liko absolutelly out of touch huku likilindwa na dola!
Na wao sio kama sisi hilo tusijidanganye! Wanajuana wenyewe kwa wenyewe na sasa ni wengi mno(from awamu ya kwanza till now) kiasi cha kufikia namba kubwa yenye uwezo wa kujenga tabaka la tofauti la kinyonyaji na kifisadi ndani ya Tanzania!
Ni wengi kiasi cha kwamba hata mafao wanayoendelea kuyapata(mara baada ya kustaafu) yamekuwa mzigo mwingine tena wa kifisadi wenye kuendelea kuwaweka mafisadi kwenye viwango vya juu in definetly in leau of the poor people's tax money and our own resources!
Hawa watu ni tofauti kabisa na hata mazungumzo yao yanaonyesha!
Halafu wasaidizi wao nao ni tabaka moja tu na ndio maana hata (wanapowaandikia hotuba zao) wanazotoa zinaonyesha kuwa wako dunia nyingine kabisa ya tofauti! Mfano wa ile ya Muungwana huko Singida!
Yani mtaani hawajui kabisa kinachoendelea!
Maisha yao yote wako serkalini halafu tunategemea walete mabadiliko!?
Tunaota!

Wakuu kama kuna mwenye data za gharama zote za hawa viongozi wote wastaafu kuanzia awamu ya kwanza na bajeti yake iwekwe hapa ili tuanze kuijadili na tuone kwamba kwanini tuendelee kuwalipa watu huku wakitu sweka lupango all the time na wakitukebehi huku tukiteketea!
NO STONE SHOULD BE LEFT UNTURNED!
 
Maoni yangu ni kuwa sasa ni wakati wa kuanza kuangalia uwezekano wa kuchagua viongozi wapya pamoja na marekebisho makubwa ya kikatiba!
RAIA MWEMA FRONT PAGE LEO SOMA, KWENYE MTANDAO WARIOBA ANAKILI VIONGOZI WETU NI DHAIFU,MZEE MUSHI SASA NI WAKATI WA KUKAMPENI JK TERM MOJA YAMTOSHA AKIONGEZA TU HAPENDEZI KWA AFYA YAKE.
 
Finally leo, Warioba naye anasema Mkapa aende mahakamani, ili mahakama iamue kama anayo hiyo kinga, na kesi zake zianze maana ni nyingi sana, heshima kwa Warioba kwa hili yaaani kusimama at the right political time ili kuhesabiwa!

according to the dataz, mkulu ana ishu nyingi sana za ufisadi, na hasa alizokuwa akizisaini dakika za mwisho wakati anaondoka, wabunge wengi wa kamati mbali mbali za bunge wanaojua ukweli nasikia wameanza kutishiwa kwa message za simu kuwa watauliwa au wataipata,

Naomba kuwaambia wale wanaotuma hizo message, kwamba you do not know what is coming your way, maana mngejua saa hizi mngeanza kutayarisha either kukimbia nchi, au mawakili wa kuwatetea, maana saa mbaya saa imefika ya ukombozi wa wananchi na mali za taifa ni lazima zirudi hata kama nusu maana tunajua mmeshazitumia sana!

Lakini at this stage, Yesuuuu na Maria! mahakamani hakukwepeki!
 
Finally leo, Warioba naye anasema Mkapa aende mahakamani, ili mahakama iamue kama anayo hiyo kinga, na kesi zake zianze maana ni nyingi sana, heshima kwa Warioba kwa hili yaaani kusimama at the right political time ili kuhesabiwa!

according to the dataz, mkulu ana ishu nyingi sana za ufisadi, na hasa alizokuwa akizisaini dakika za mwisho wakati anaondoka, wabunge wengi wa kamati mbali mbali za bunge wanaojua ukweli nasikia wameanza kutishiwa kwa message za simu kuwa watauliwa au wataipata,

Naomba kuwaambia wale wanaotuma hizo message, kwamba you do not know what is coming your way, maana mngejua saa hizi mngeanza kutayarisha either kukimbia nchi, au mawakili wa kuwatetea, maana saa mbaya saa imefika ya ukombozi wa wananchi na mali za taifa ni lazima zirudi hata kama nusu maana tunajua mmeshazitumia sana!

Lakini at this stage, Yesuuuu na Maria! mahakamani hakukwepeki!

Mkuu,

Warioba, Mwinyi, Kawawa, Msuya, Butiku wote wameshaonyesha kutoridhishwa kwao na mafisadi akiwamo fisadi Mkapa kutochukuliwa hatua zozote. Inaelekea sasa tatizo ni huyo muungwana maana haingii akilini yeye kama Rais wa nchi pamoja na kuwa na nguvu ya dola bado anafanya usanii tu. Mimi nina wasiwasi kwamba naye ana mambo yake ya kifisadi ndio yanamfanya awe mwoga kusimama kidete ili kuwachukulia hatua mafisadi wote akiwamo Mkapa.

Huu ulikuwa ni wakati mzuri sana wa yeye kurudisha credibility yake kwa Watanzania ambayo imeanguka vibaya sana, lakini inaelekea hana uwezo wa kufanya hivyo kwa wasi wasi aliokuwa nao kuhusiana na madhambi yake ambayo labda mafisadi wanayajua na wako tayari kuyaanika hadharani.
 
Field Marshall Es,
Mkuu heshima mbele hakika hii ni moja ya kipaza sauti kwa wananchi....
Hata hivyo mimi nafikiria nje ya box hili la NDIVYO TULIVYO maanake siku zote tunategemea mtu wa kubeba msalaba.. hadi sasa hivi simuoni hata mtu mmoja zaidi ya kelele za kina Petro kukata masikio ya askari watumishi tu wa Heron...

Hivyo basi mimi nadhani ipo haja kubwa ya kuanza mbiu ya kumtafuta kiongozi atakayeweza kuleta mabadiliko ktk maswala haya ya Ufisadi. Kiongozi ambaye atakuwa tayari kuwaahidi wananchi kuwa pindi akipewa Urais atachukua jukumu la kufufua kesi zote zinazohusiana na Ufisadi. Aanze kujinadi toka sasa hivi. Mtu ambaye bila woga atakuwa tishio la wazi kwa serikali hii kiasi kwamba serikali wataanza kufanya ovyo zaidi kama mfa maji...jambo ambalo litaamsha wananchi wengi zaidi hasa wa vijijini kuona maonevu ya serikali yetu kabla ya 2010...kwa sbababu kama kitendo hiki kidogo cha kumzomea Mkapa kimeweza kujibiwa na serikali yetu bila kutumia busara nadhani palke itakapo fikia mapambano ya kikweli serikali hii itachanganyikiwa..
Kumbuka swala la Zitto alipofungiwa Bunge ni habari ambayo ilifika hadi vijijini na hivi sasa serikali inaomba Mungu kila siku swala la Buzwagi na EPA liote magugu, lakini bado linezidi kustawi pasipo matunda...

Matunda hayawezi patikana ktk serikali hii hata siku moja.. Tunajidanganya, haiwezekani hata kidogo unless Mkapa afariki dunia jambo ambalo hakuna Mtanzania analiombea.. Huyu alikuwa rais wetu, mzazi wetu na hakuna anayemtakia kifo ni upumbavu kuomba haya hasa wakati kama huu, isipokuwa sheria itakayo rudisha uzalendo ndani ya serikali yetu. na haki hiyo haiwezi patikana bila kuwepo na mtu wa kubeba msalaba huo na sisi kina Yakhe tutasimama nyuma yake hata kama tutaanza kuitwa magaidi wasiotumia silaha...
Mimi naomba sana viongozi wapinzani ndani ya CCM hao kina Warioba, viongozi wa Chadema, CUF, NCCR, Mageuzi, TLP na vyama vinginevyo woteee kwa pamoja jikusanyeni kumwondoa adui yetu huyu mkubwa UFISADI...
Huu ndio wakati wa kumpata mtume wa kweli... na kama Dr. Slaa yupo tayari ni bora kujiandaa toka sasa hivi kuanza kutangaza madhara haya ya UFISADI kwa wananchi kwa sababu ushahidi tayari umeshapatikana na yeyote yule atakaye taka kwenda mahakamani kushtaki ati amekashfiwa basi na aende kwani huko ndiko tunakokutaka. Hii ndio nafasi yetu pekee kujibu mapigo kwa sababu serikali hii imeshindwa kuyafikisha maswala haya mahakamani kwa mlango wa mbele na sababu kubwa wao ndio wahusika.. hivyo mchezo wote ni kuwavuta wenyewe wajifunge kamba kutaka haki yao, na mahakamani tutakwenda na ushahidi wetu huu mdogo ambao bila shaka utafungua mengi zaidi...

Kama alivyosema Warioba, waandishi wa habari hawawezi kumhukumu mtu na hii habari ya kutaka Mkapa ajieleze ni hadithi ya kitoto sana ambayo mtu kama Mkapa hawezi kujifunga kamba - he is smart than that!.
Wajibu wetu ni kuwashtakia wananchi ktk mikutano yote na hapo watakapo dai mahakama ndipo tutakapojua mwanaume nani!
 
Mkuu Bubu,

Kwa mwananchi yoyote mwenye akili timamu, ukiiangalia hii ishu ya ufisadi wa Mkapa na wenziwe kwa kina na upepo wa siasa unavyokwenda sasa hivi, ni kwamba it only a matter of time tu kabla muungwana hajanawa mikono na kuwaachia wanaoweza kuendelea nayo kwenye sheria,

Hebu niambie ni miracle gani muungwana anaweza kuifanya at this time kuwaokoa Mkapa na wenziwe? Kwanza historia haiko upande wake, maana sio siri kuwa ana tabia ya kukubali only under massive political pressure, ambayo sasa inakuwa pushed upande wake kutoka kila kona ya bongo, wafadhili tayari wamesharukia treni, kwa wale mlio karibu na Mkapa mfahamisheni kuwa according to the dataz toka jana wakulu wengi wa taifa wamekuwa kwenye furaha kubwa kusikia amezomewa mtaaani, ninasema kwa jina la Miungu yangu yote kuwa hakuna hata mmoja aliyechukizwa, wala kusikitishwa na hicho kitendo, if anything wengi wameonyesha kushitushwa kuwa vijana waliomzomea wameshikwa! Je umesikia kuna hata kiongozi mmoja mzito aliyejitokeza kuwalaaani wale vijana waliomzomea Mkapa?

Ohhhh! Yes, watu wa Mkapa msijidanganye, kisiasa kitendo cha jana cha Mkapa kuzomewa sio kidogo na ukubwa wake unaongezwa sana na the fact kwamba, kisiasa za taifa lolote duniani ilitakiwa by leo viongozi wetu wa juu wa taifa wajitokeze na kumpa Mkapa a strong support kwa kuwalaaani wale vijana waliomzomea, nafikiri Mkapa ni mtu mzima wa kuelewa hii simple lakini very strong political message, kuwa saaa imekaribia sasa ya yeye kupelekwa kwa Pilato ambaye anajitayarisha kunawa mikono kwa kisingizio cha kilio cha wananchi hakiwezi tena!

Time is up kwa mafisadi, hakuna msamahaa vijana waliomzomea wameanza sisi watu wazima ni kumalizia tu and it is coming!
 
Field marshall Es,
Binafsi bado siamini kuwa wakati umefika wala umekaribia naona kama vile tunatazama dalili ya Kiyama...Mkuu sioni mwanga ktk bao langu hata kidogo kwa mtaji huu..
Kama hatapatikana mtu wa kuubeba msalaba huu mkuu wangu itachukua miaka 20 mingine kwa sababu ya maneno yako wewe Mwenyewe - VIONGIZI WETU ni REFLECTION YETU..
Ni kawaida ya mdanganyika kusahau.. na tutakuja sahau kama tulivyosahau madai mengi yaliyotangulia. Hili linahitaji muda tu na ndicho KIkwete anachosubiri hadi sasa na kila kinapotokea kitu atatupaka mafuta ya kumwondoa ama kujiuzuru kwa mtu huyo..
Hivi sasa nani anamtazama Lowassa ama Karamagi kama sio wao kuwepo bungeni?..viongozi wengine wote kina Meghji na Chenge baada ya kujiuzuru imetoka, hakuna hadithi nyingine zaidi..
Tabia hii mimi inanitisha zaidi na wapo wanaosifia Uongozi huu kwa kuwatema viongozi mafisadi..kiasi kwamba inanikumbusha kile kimila cha mzazi kumfukuza mwanae bila kumpeleka ktk vyombo vya kisheria pindi anapofanya vitendo jinai...tena basi humtetea inapofikia swala hili kuwa wazi hali kamfukuza na pengine hata kumkana kuwa mtoto wake..
Yaani ile adhabu ya kumkana mtu pekee inatosha kabisa na kutegemea dunia itakuja kumfunza..
Bila shaka ktk kesi hii ya Mkapa, vijana hao wataondolewa huko jela waliko baada ya kupewa kipigo cha kisawasawa wakiambiwa hawana adabu (mila zetu)...
Na Kikwete hawezi kubabaika zaidi hatua hizi ndogo zinakubalika na baadhi ya wadanganyika..
Kumbuka mkuu aliposema mwacheni Mzee wetu apumzike, kila mtu alikaa kimya na nadhani imeshapita miezi kama sio mwaka..
Hivyo basi ni kitu gani haswa kinachokupa tumaini kuwa Ufisadi utakuja kuishia mahakamani?...
Binafsi naona jiko litasafishwa na mapishi yataendelea kama kawaida, unless tupate mtu atakaye livalia njuga swala hili kisiasa..
Kesho 2010 iwe pigo kubwa kwa chama kuwaacha mafisadi wazidi kutanua....
Nashangaa sana kuona JK hasikii kilio cha wananchi akitubeza kama vile Mugabe.. malipo yake yatakuwa highly paid!
 
Mkandara,

Nakuunga mkono. tunahitaji Mtu kama Mrema wa 1995. Huyu mtu ajiandae sasa. Ningeshauri (samahani makada) kuwa huyu mtu atokee Bungeni na awe Mbunge wa CCM, asapotiwe na upinzani aanze ziara ya nchi nzima. Awaelimishe wananchi kuhusu UFISADI.

Huu sio wakati wa CCM vs Chadema au CUF au NCCR ni wakati wa WaTanzania wote kuamka!
 
Back
Top Bottom