Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Yes anatembea na Msafara usiopungua gari tatu na piki piki moja ya kuongoza Msafara.
Ni gharama juu ya gharama!!

Inafaa tuwasaidie hao vijana maana sijaona kosa lao; wamejaribu kutumia uhuru wao pasipo kukashifu mtu! Kwani kuna kesi dhidi ya mkapa au bado ni tetesi??
 
Zamani enzi zetu ilikuwa ukiwa huna kazi/umekosa kazi nyingine ndio unaenda upolisi, siku hizi ikoje?
 
Hii ndio shida polisi wetu wanafanya kazi kwa hisia. Ukiwauliza hawa vijana wamevunja sheria gani utakuta wala hawajui. Sasa kwa mfano kama hao vijana wangeamua kumshangilia wakati akipita wangewakama?
Kosa la kuhatarisha Amani.Mathalani kama wangempiga Risasi Rais mstaafu unaju Madhara yake ni yapi.
 
Hii ndio shida polisi wetu wanafanya kazi kwa hisia. Ukiwauliza hawa vijana wamevunja sheria gani utakuta wala hawajui. Sasa kwa mfano kama hao vijana wangeamua kumshangilia wakati akipita wangewakama?

Kitila,

Swali gumu sana hili. Nimekuwa napiga vita swala la polisi kutumiwa na viongozi wa serikali (hata wastaafu) kwa mambo ya ajabu kama haya kwa muda sasa hapa.

Ni makosa makubwa, inaonekana walitaka hao vijana wasifie tu na kupiga vigelegele kuwa mkubwa kapita.

Pambaffff kabisa!
 
Kama yeye sio fisadi anasubiri nini sasa kukanusha tuhuma hizo. Hivi hajui kama uongo ukiachwa kwa muda mrefu hugeuka kuwa ukweli? Kama hana dhambi anazotuhumiwa kuwa nazo aongee hadharani na kukanusha or else we'll make his life more and more miserable!
 
Hii ndio shida polisi wetu wanafanya kazi kwa hisia. Ukiwauliza hawa vijana wamevunja sheria gani utakuta wala hawajui. Sasa kwa mfano kama hao vijana wangeamua kumshangilia wakati akipita wangewakama?

Kwi kwi kwi kwi.... yani unanivunja mbavu, yani hapa wanaonyesha upumbavu wao kabisa, hawana tofauti na wale mbwa wao kiakili, mbwa akiambiwa kamata tu.. kwisha habari..... mbiiiiooooo.... sbb bwana mkubwa kasema. BADO KABISA.....SHAME....
 
Aaaahhhh!!! Big Ben huo ndio utamu wa utandawazi bwana....Baba ukifanya utumbo ndani ya nyumba kuna siku watoto wako mwenyewe watakuzomea ndio mambo yalivyo...Polisi si just watch dogs ni lazima kuna kibaraka wa huyo fisadi kawapa amri kukamata then kesho hao hao wanalia lia mishahara haitoshi mara nyumba za full suit (bati kila mahali) zina joto kumbe wanaosababisha hali ngumu wanawalinda wenyewe... Bravo na ni mwanzo mzuri message was sent and delivered correctly!!!Poleni vijana ndio gharama za mapambano hizo na sisi tutamzomea hata humu JF...
 
Kajipatia jina baya kweli! Mwenzie Mzee Mwinyi akipita watu hushangilia "rukhsa rukhsa rukhsa rukhsa!"
 
Hivi:

a. Kama walikuwa kwenye msafara wakaona watu wanapiga kelele "Fisadi" "Fisadi" wanapoteremka na kufanya msako, wanajuaje walioawakamata NDIYO waliosema "fisadi"?

Kwa uzoefu wangu wa vijana wakijiweni,wanafahamika sana na pale ndipo huwa Mzee Mkapa huwa anpita kila mara kama akiwa hapa Dar. na ujue ile kona ni kona ambayo inaenda kwenye Nyumba za Mawaziri,hivyo watu wa Usalama ni kibao na wao ndio watakuwa wamewapa taarifa Polisi kwasababu ndiyo kazi yao kubwa

b. Je kama vijana hawa wangesimama na kupiga kelele "Mtukufu" "Mtukufu" ni hatua gani wangechukuliwa au zawadi gani wangepewa?

Wasinge weza kumwita Mzee Ben Mtukufu sababu yeye siyo Mtukufu na kamwe halikataa kuitwa hivyo.angekasirika.
c. Uhuru wa maoni ni pamoja na uhuru wa maoni ya kijinga. Katiba haisemi mahali popote kuwa maoni yatakayotolewa na wananchi lazima yawe mazuri au yanayopendeza ili yakubaliwe.

Ibara ya 18 inayotoa uhuru huo inasema hivi
18
.-(1).Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati


Sheria zingine za nchi zinasemaje kuhusu ulinzi wa Rais Mstaafu ambazo wewe Mwanakijiji hauzijui??​


d. HIvi wanazojela za kutosha? Maana tukianza hii movement ya "Fisadi" "Fisadi" wataweza kweli kuwasweka watu ndani au watalazimika kutumia njia "kali" zaidi... ?​

Hawawezi kuwapeleka Jela zaidi ya kwuahoji na kujua lengo lao ni nini​
 
Kwa uzoefu wangu wa vijana wakijiweni,wanafahamika sana na pale ndipo huwa Mzee Mkapa huwa anpita kila mara kama akiwa hapa Dar. na ujue ile kona ni kona ambayo inaenda kwenye Nyumba za Mawaziri,hivyo watu wa Usalama ni kibao na wao ndio watakuwa wamewapa taarifa Polisi kwasababu ndiyo kazi yao kubwa

Hawa watu wa usalama kama wakianza kukamata watu wanaomzomea Mkapa kuwa ni fisadi basi wajiandae for a very long ride!

Wasinge weza kumwita Mzee Ben Mtukufu sababu yeye siyo Mtukufu na kamwe halikataa kuitwa hivyo.angekasirika.

Yeye ni mwizi na fisadi tu na kukasirika ni dhambi ndogo sana kwake ukilinganisha na mengine makubwa aliyofanya.


Ibara ya 18

sheria zingine za nchi zinasemaje kuhusu ulinzi wa Rais Mstaafu ambazo wewe Mwanakijiji hauzijui??



hawawezi kuwapeleka Jela zaidi ya kwuahoji na kujua lengo lao ni nini

Kuzomea mwizi hakuhitaji kuhojiwa na polisi ili ijulikane lengo ni lipi. Lengo ni kumwaibisha mwizi na shetani (shame the devil).
 
Sasa watu wamekazana ajitokeze ajibu shutuma hizo ataongea nn??zaidi ya kusema ngoja uchunguzi ufanyike baasi tunabaki tumeduwaa ni bora kutumia nguvu ya umma namna hii ya kuzomea zomea mpaka ajisikie vibaya kuwa tumemchoka na UFISADI wake sasa hao vijana watafunguliwa kesi gani hapo naomba msaada wanasheria...
 
Kajipatia jina baya kweli! Mwenzie Mzee Mwinyi akipita watu hushangilia "rukhsa rukhsa rukhsa rukhsa!"

Mbona wanao mwita mzee Mwinyi RUKSA RUKSA wakamatwi???si sifa aliyo jingea na huyu BEN si FISADI sasa wanausalama walitaka aitwe vp??wkt wao wenyewe wanashindwa kumpeleka kwenye sheria.
 
Kuzomea mwizi hakuhitaji kuhojiwa na polisi ili ijulikane lengo ni lipi. Lengo ni kumwaibisha mwizi na shetani (shame the devil).
Hata kama Mzee Mkapa ni Mwizi(Hapa mahakama haijaamua) ila jua ya Kwamba bado ni Rasi Mstaafu tu..other thing reamin Constant.

Wewe unadhani kama angepita kiongozi mstaafu wa upinzani watu wakaanza kumzomea,viongozi wa juu wanatembea na mtoto wako huku wakimghasi..Polisi wakikaa kimya unadhani italeta picha nzuri??
 
Heri hao vijana waaachiwe huru mapema maana magazeti ya kesho ndo yatakoleza vichwa vya habari ili kumchokonoa ajitetee kwa nini yeye si fisadi.
 
Hata kama Mzee Mkapa ni Mwizi(Hapa mahakama haijaamua) ila jua ya Kwamba bado ni Rasi Mstaafu tu..other thing reamin Constant.

Hakuna aliyekataa kuwa si Raisi mstaafu ila tu kwa sasa ameongezewa cheo kingine cha mwizi na fisadi mkapa - got it!

Wewe unadhani kama angepita kiongozi mstaafu wa upinzani watu wakaanza kumzomea,viongozi wa juu wanatembea na mtoto wako huku wakimghasi..Polisi wakikaa kimya unadhani italeta picha nzuri??

Kama kiongozi mstaafu wa upinzania akifanya ufisadi kama wa Mkapa mimi nitakuwa wa kwanza kumzomea na kumrushia mawe kila mara akipita kwenye "kijiwe" changu!
 
Hata kama Mzee Mkapa ni Mwizi(Hapa mahakama haijaamua) ila jua ya Kwamba bado ni Rasi Mstaafu tu..other thing reamin Constant.

Wewe unadhani kama angepita kiongozi mstaafu wa upinzani watu wakaanza kumzomea,viongozi wa juu wanatembea na mtoto wako huku wakimghasi..Polisi wakikaa kimya unadhani italeta picha nzuri??

Toka lini kuzomea ni kosa?
Kuna sheria inayokataza kuzomea?
Kama ipo iweke hapa maana itakuwa ni moja ya unjust laws
Na kama ipo, application yake ikoje? Kwa mfano nikikuzomea wewe kwa kumtetea Mkapa polisi watanikamata au ina apply tu pale "wakubwa" wanapozomewa? Please tell me...
 
...sasa hao vijana watafunguliwa kesi gani hapo naomba msaada wanasheria...
Msaada mwingine kwa wanasheria, yapasa kusaidia hao vijana walishitaki Jeshi la vibaraka kwa kuwaweka kizuizini pasi kosa lolote! Wakileta kisingizio cha uzururaji then watuambie wametoa ajira ngapi baada ya kusababisha maisha ya vijijini kuwa magumu?!
 
Kwa uzoefu wangu wa vijana wakijiweni,wanafahamika sana na pale ndipo huwa Mzee Mkapa huwa anpita kila mara kama akiwa hapa Dar. na ujue ile kona ni kona ambayo inaenda kwenye Nyumba za Mawaziri,hivyo watu wa Usalama ni kibao na wao ndio watakuwa wamewapa taarifa Polisi kwasababu ndiyo kazi yao kubwa

Ni sheria gani inayowapa kazi Usalama wa Taifa kuingilia kati protest halali ya wananchi? Mtu yeyote wa Usalama wa Taifa anayeingilia uhuru wa mwananchi kupinga au kujishughulisha na shughuli ya kupinga kidemokrasia jambo lolote afisa huyo anavunja sheria ya Usalama wa Taifa ya 1996.



Wasinge weza kumwita Mzee Ben Mtukufu sababu yeye siyo Mtukufu na kamwe halikataa kuitwa hivyo.angekasirika.

point yangu ni kumwita jina lolote lile la sifa siyo lazima liwe mtukufu; kama kumwita mtu "fisadi" unakamatwa je kumwita jina la sifa nini kinafanyika na kwanini?



Ibara ya 18 inayotoa uhuru huo inasema hivi

Uhuru hautolowi na ibara yoyote ile, kwani uhuru ni tunu ya Mwenyezi Mungu kwa mwanadamu; hakuna serikali inayoweza kutoa uhuru huo. Jukumu la serikali ni kutambua uhuru huo. Bahati mbaya umenukuu kipengele cha Katiba ambacho kimefanyiwa mabadiliko angalia toleo jipya la Katiba uone kipengele hicho kinasemaje sasa. Hilo toleo la 2000 la Katiba haliko sahihi.


Sheria zingine za nchi zinasemaje kuhusu ulinzi wa Rais Mstaafu ambazo wewe Mwanakijiji hauzijui??​

Ulinzi wa Rais unahusiana vipi na mtu kuita "Fisadi".? Jukumu la ulinzi wa viongozi ni kuhakikisha kiongozi asidhurike siyo asikasirike au kukasirishwa. Jukumu la wananchi ni kuhakikisha viongozi wao wanakasirika! Ni kwenye nchi ya kidikteta tu ndiko wananchi wanatakiwa kuhofia viongozi wao kukasirika kwani wakikasirika watawakamata na kuwesweka lupango.


Hawawezi kuwapeleka Jela zaidi ya kwuahoji na kujua lengo lao ni nini​
[/QUOTE]

Lengo lao mbona ni dhahiri; walitaka kutoa maoni yao ambayo ni kumuita Rais mstaafu "fisadi". Zaidi ya hapo ni kujaribu KUPANDIKIZA maoni zaidi ya kile kilichosikika.
 
Back
Top Bottom