Mkapa above the law?: Allegations

Haya ni yaliyotokea miaka ile, enzi zile hoja za wana Jambo/Jamii zilijaa uchambuzi wa hali ya juu.
 
Imeripotiwa hivi karibuni kuwa Mwenyekiti wa CCM wa Taifa Bw. Ben Mkapa kwamba yeye hakubaliani na uamuzi wa Mahakama ulioruhusu uwepo wa wagombea huru.

Binafsi sijafurahishwa kuwa hakuna mwandishi aliyeamua kumhoji Mkapa kwa kina inakuwaje yeye na chama chake wamejiweka kuwa ni walinzi wa sheria zetu na katiba yetu badala ya mahakama? Haya mambo ya kudharau mahakama kwa wazi namna hii yatatufikisha pabaya!

Na tuangalie ni yepi mabaya yaliyotendeka chini ya utawala wa Mkapa sasa!
14 years Ago.
 
Dah!

Enzi za Tafiti then Jadili kabla hajawa Selemani 😄

Mzee Tibwilitibwili

FMES kabla hajawa Le Mutuz

Na Bw. Fukiraduni kabla hajawa Fairplayer.

I really miss the halcyon days of JamiiForums.
 
Dah!

Enzi za Tafiti then Jadili kabla hajawa Selemani 😄

Mzee Tibwilitibwili

FMES kabla hajawa Le Mutuz

Na Bw. Fukiraduni kabla hajawa Fairplayer.

I really miss the halcyon days of JamiiForums.
Mazee Nyani Ngabu, yaani we acha tu ndugu yangu hahahahah
 
Haya ni yaliyotokea miaka ile, enzi zile hoja za wana Jambo/Jamii zilijaa uchambuzi wa hali ya juu.
Nyerere, alimjua Mkapa tena nje ndani, tena kwa karibu sana,

kwa sababu alikuwa akimjua Lowassa kwa karibu sana, ingawa hakuwa mtoto wake wala ndugu yake, wala kiongozi aliyefanya naye kazi kwa karibu, mpaka akamkatalia urais, sasa iweje kuwa hakumjua Mkapa aliyekuwa waziri wake wa nje?

Watanzania inabidi tukubali ukweli, kwamba tumekuwa wajinga for too long, ndio maana tunakazania kuitangaza JF kwa nguvu zote tulizonazo, ni kwa sababu tunajaribu kuamshana kutoka kwenye usingizi mzito sana tulionao, Mkapa alikuwa Elimu na Sayansi, nani aliyekuwa hajui kilichokuwa kikiendelea huko betweeen Mkapa na Mahalu? Eti mnasema Mwalimu, alikuwa hamjui Mkapa? Wakuu tunaambiwa kuwa kipindi cha Mwinyi, hata Usalama walikuwa wamechoka na kuamua kumpa Mwalimu, info zote za serikali na ndio maana wakampa hata za Lowassa, na za Ikulu kuwa pango la kufanyia biashara haramu, sasa mnataka kutuambia kuwa kwenye hizo info hazikuwepo za Mkapa?

Mwalimu, alimpigia makelele Mwinyi, kuwa ni mwizi, lakini hakutuomba msamaha wananchi kwa kutuchagulia kiongozi mbovu, the next thing akarudia tena mchezo wake na kutuchagulia Mkapa again mambo yakawa yale yale, lakini akanyamaza kimyaa, sasa leo maa-pologists mnasema hakumjua Mkapa? Eti Mwalimu hakujua kuwa CCM ilishindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 1995 kule visiwani?, sasa kama alijua hilo how could you put past him kuwa hakumjua Mkapa? Mbona hakusema kitu kwenye ishu ya Zanzibar kama kweli alikuwa ni malaika kama wengi hapa mnavyotaka tuamini? hivi wakuu kweli tunaelewa maana ya siasa na mwanasiasa au tunabahatisha tu?

Wewe kweli ni rais wa nchi, watoto wako wote wanasoma bongo, waziri wako wa nje watoto wake wanasoma US toka wakiwa watoto wadogo, tena in the middle ya siasa ya ujamaa, wakati wananchi wanakula njano na foleni ya kipande cha sabuni mbuni, halafu unasema kuwa humjui waziri wako wa nje? Vijana hebu muache haya masiala, wewe kweli unaamini kuwa Mkapa aliandika mali zake zote? wananchi wa bongo tulikuwa tumelala sana usingizi, matokeo yake tukaruhusu aliyeamka Mwalimu na alioamka nao kina Mkapa, kutuchezea na bado tunaendelea kuchezewa, ndio kwanza tunajaribu kuamka, lakini bado kazi ni nzito saana ya kuamshana, ndio maana ni lazima tuitangaze JF kwa nguvu zote, maana huwezi ingia hapa ukaendelea kulala!

Mwalimu, alale pema peponi, lakini alikuwa akimjua tena vizuri sana Mkapa, kuliko hata sisi wananchi, lakini tunasahau kuwa Mwalimu, alikuwa ni mwanasiasa, alikuwa pia akiangalia legacy yake ambayo ilishamiri sana under Mkapa, Nyerere Foundation imewika under urais wa Mkapa, na sio Mwinyi, hebu nyie Nyerere apologists tuambieni zile shillingi millioni 300 ambazo Mkapa alikuwwa akitoa kwa hiyo foundation alikuwa akizitoa wapi? au under what budget? Mwinyi, na kundi lake walikataa kata kata kumpa Mwalimu hizo hela, na kuna wakati Mwalimu, alikuwa bado ana demand kusafiri kwenye ndege ya rais na Mwinyi alikuwa akikataa, lakini yote haya aliyafanya under Mkapa, kwa hiyo si kweli kabisaa kuwa kwa kumchagua Mkapa, Mwalimu alikuwa hajui anachofanya no way wakuu!

Tunasema kuwa Mwalimu, hakuwa mfisadi, lakini hakuwa na tatizo na mafisadi waliokuwa wakimsujudia, Mkapa included, kusema Mwalimu, hakumjua Mkapa ni very naive thinking kama sio kujua what makes siasa na wanasiasa, to be politicians, siasa sio dini wakuu au charity, siasa ni utawala na power ndani yake, na pia tukumbuke kuwa power siku zote huwa ina-corrupt hata wachungaji kina Mtikila!

Maisha yanakwenda kasi sana😄😄

Eti huyu ni Lemutuz saizi mpanga mikakati wa Makonda

Enzi hizo akili zilikua zimesambaa mwili mzima sio kama saizi zimebaki tumboni tu
 
The guy was a dictator in kind. Hii sera ya polisi ya shoot to kill imeanzia kwake, mauaji ya Mwembechai, mauaji ya Ungua na Pemba January 21 na 22 2001, ukiachilia mbali watu waliokuwa wanauwawa na majambazi kisha majambazi hawajulikani, unakumbuka stori ya Dr. Ouko?(upande wa kenya), Unakumbuka watu kama akina Horace Kolimba?. Jamaa alikuwa anatumia iron fist kunyamazisha wanaompinga. Na huyu jamaa ndiyo rais mstaafu anayeishi kwenye wasiwasi mkubwa wa kuburuzwa kwenye mahakama kama nchi itaongozwa na mtu asiyeweza kumlinda.

Alikuwa anajua fika kuwa ili awe salama ni lazima CCM iwe na control ya bunge, unapokuwa na wabunge wasio na vyama wengi (Kama mfumo wa wagombea huru ungepita) basi ni rahisi kuondolewa kinga na kufikishwa kizimbani na kama rais aliyepo madarakani atakulinda, na yeye anaweza kuwa victim kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani.
14 years back, Hataree sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom