Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Nadhani hao vijana walitaka kufikisha msj.Chonde chonde polisi msijiingize kwenye hii vita bila kufikiria mara mbili.

I think that's what he deserves until he break the silence.
 
Polisi ni mojawapo ya taasisi ambazo zinabidi kushiriki kwa moyo mmoja katika vita zidi ya mafisadi kwani hawa watazomewa kila sehemu sasa kama polisi watakamata watu na kuwaweka ndani hii itadhoofisha juudi za wananchi za kutaka kuwaumbua mafisadi.
 
Polisi wetu itabidi waende na Kenya ambako Raila alipotoa salamu za wasuluhishi wa mgogoro wao mbele ya Magufuli Wakenya wakazomea sana lilipotajwa jina la Mkapa.
Sio siri tena Mzee wa Lupaso amejivunjia heshima mwenyewe sio kwa Wa TZ pekee,bali ktk ukanda huu wote wa EA.
Kuwakamata vijana wakizomea sio utatuzi maana mwishowe watarusha mawe na hapo ndio BALAA kuu litakapozuka hapa kwetu.
Awe jasiri asimame hadharani atuombe radhi kwa aliyoyatenda na kuwarudishia wananchi masikini wa nchi hii vile vyote alivyowapora yeye na maswahiba wake nina hakika watu watakumbuka na yale aliyowahi kuyatenda kwa uzuri na atasamehewa kama baba aliyepotoka kidogo lakini kajirudi.LAKINI JEURI NA MAJIDAI,WATU WATAENDELEA KUZOMEA TU.
 
Waliomzomea Mkapa wamekosea nini?

Mkapa, aitwe nani kwa kuingia mikataba mibovu ya madini, kubariki uuzwaji wa nyumba za serikali, kuongeza mkataba wa TICTS kinyume na taratibu, kutowawajibisha watendaji wake walioelekea kulega lega katika kazi.

Tanesco kila siku hutoa sh milioni 146 kuilipa Kampuni ya Tanpower Resources Limited ambayo inaaminika kuwa inamilikiwa na Mkapa na Daniel Yona, ambao waliingia mkataba wa kinyonyaji wenye lengo la kujinufaisha zaidi.

Salehe_mohamedi@yahoo.com

TANZANIA DAIMA

Labda aitwe Mtume na Nabii ili tusisakamwe sakamwe na hao polisi.
 
Mkapa graft allegations: JK urged to emulate Zambian example

-What Mkapa and Yona did was a serious criminal offence
-Detractors cite Mwanawasa’s tough stance on Chiluba

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

PRESIDENT Jakaya Kikwete has been urged to emulate his Zambian counterpart, Levy Mwanawasa, by ordering a full-blown investigation into allegations of corruption and abuse of office against former president Benjamin Mkapa.

Following the prosecution and seizure of $60m (approx. 70bn/-) in stolen funds from former Zambian president Frederick Chiluba, opposition leaders and political commentators in Tanzania are now calling for a similar move against Mkapa if the allegations against him are substantiated.

The Leader of the Official Opposition in the National Assembly, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), said President Kikwete should go ahead and give the green light for an official investigation of the former president.

Hamad Rashid told THISDAY in an interview that it was important for the government of the day to thoroughly investigate all corruption allegations against public leaders - both past and present, regardless of position.

’’The government should be very serious about keeping an eye on public leaders in this country, especially those who have secret offshore bank accounts contrary to regulations,’’ he said.

He called on President Kikwete to emulate the examples set by the Zambian and Pakistani governments in taking legal action against former leaders accused of corruption.

Likewise, the CHADEMA secretary general and deputy leader of the opposition in parliament, Dr Wilbrod Slaa, said the moment of truth had come for the government to demonstrate its true commitment and spirit to fight high-level corruption.

’’The government must show with action how determined it is to fight corruption and do away with the politics of protectionism,’’ Slaa said.

The firebrand opposition leader said continued failure by the government to adequately address the allegations against Mkapa would betray a ’’lack of courage and political commitment to fight corruption.’’

He asserted that the former president does not enjoy any immunity from criminal prosecution for actions done in his personal rather than presidential capacity.

’’Basically, the law gives immunity to Mkapa for all actions he did while executing presidential duties. Doing business at State House and calling himself an entrepreneur were not part of his official duties as president,’’ Dr Slaa said.

Mkapa is alleged to have abused public office by using State House as the official address of his private company, ANBEM Limited, for personal financial gain.

And according to Slaa, the fact that Mkapa and his former senior cabinet minister Daniel Yona sold the state-owned Kiwira coal mine to their own joint private company (Tanpower Resources Limited) while they were still in public office constituted ’’a serious criminal offence.’’

Prominent local lawyer and human rights activist Tundu Lissu also insisted that the former president does not have immunity from prosecution on such allegations.

’’There is no such thing as immunity...it just boils down to the question of political commitment and resolve (or lack of it) within the incumbent government to fight grand corruption,’’ said Lissu.

He said the national Constitution was categorical about limits of immunity enjoyed by ex-presidents.

According to Article 46 of the Constitution of the United Republic of Tanzania: ’’It shall be prohibited to institute in court criminal or civil proceedings whatsoever against a person who was holding the office of President after he ceases to hold such office, for anything he did in his capacity as President while he held the office of President in accordance with this Constitution.’’

Lissu asserted that since Mkapa’s private business dealings were not done in his capacity as president, he was liable for criminal prosecution.

The issue of alleged dubious private business dealings by the ex-president and his former cabinet minister were recently raised in the National Assembly by members of parliament from both the ruling CCM and opposition camps.

This prompted the Prime Minister, Mizengo Pinda, to state categorically in the House that the government would make a formal inquiry into the allegations.

Asked yesterday if the government would be ready to prosecute Mkapa in particular if implicated by the allegations, the Minister of State in the President’s Office (Good Governance), Sophia Simba, was non-committal.

’’I can’t answer that question. He (Mkapa) is not necessarily guilty of these accusations we should not just tarnish his image. He has done good things for this country,’’ Ms Simba told THISDAY.
 
’’I can’t answer that question. He (Mkapa) is not necessarily guilty of these accusations we should not just tarnish his image. He has done good things for this country,’’ Ms Simba told THISDAY.

and she is our leader, do still thinks that there is any miracles we should expect from this kind of a leader???? ni kipofu au atajitia ukipofu huyu mama si ni bora wangeishia tu hapa "I can’t answer that question"
 
and she is our leader, do still thinks that there is any miracles we should expect from this kind of a leader???? ni kipofu au atajitia ukipofu huyu mama si ni bora wangeishia tu hapa "I can’t answer that question"

Hawa ndo viongozi wetu, nafikiri rais anapofanya uteuzi wa mawaziri huchagua walio na dalili za ujinga ujinga kama huyu mama
 
By Charles Mullinda anasema wanawasiwasi wanamwogopa Mkapa.

RAIS Jakaya Kikwete na serikali yake, Laurence Masha na Kampuni ya IMMMA, Ridhwan Kikwete na Fatma Karume, wana wasiwasi, lakini Benjamin William Mkapa hana wasiwasi. Nadhani nimepatia.
Nadhani wapo wengine wengi wenye wasiwasi, sababu ni ile ile ya kumuogopa Mkapa. Lakini hawa niliowataja sina shaka kabisa kwamba wana wasiwasi zaidi.
Nadhani watu hawa wana wasiwasi kwa sababu wanaogopa kuchafuliwa majina yao, na mtu pekee anayeweza kuyachafua na wakashindwa kujisafisha ni Mkapa, siku ambayo ataamua kuvunja ukimya na kuzungumzia tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake.
Zisome sababu zinazonifanya nidhani hivyo. Fikiria kama Mkapa atakapokuwa akizungumza madai ya yeye kufumbia macho rafu za waziwazi zilizofanywa na baadhi ya wana CCM waliokuwa wakiwania kuteuliwa kuwa wagombea urais kupitia chama hicho mwaka 2005 na kubainisha kuwa ni kweli aliyeteuliwa kugombea ambaye sasa ndiye rais wetu, yaani Rais Kikwete, alipatikana kwa mizengwe, wananchi watamtazama kwa jicho lipi?

Kwa mfano, Mkapa katika maelezo yake, anatamka kwamba alilamizika kubadili taratibu za upigaji kura wa kumpata mgombea wa CCM kwa makusudi ili kumuwezesha Kikwete ashinde. Anaendelea kueleza kuwa alitaarifiwa kuhusu baadhi ya waliokuwa wakiwania kuteuliwa kuwashawishi wajumbe kwa fedha (rushwa) lakini akakaa kimya kama anavyofanya sasa kwa makusudi tu, halafu anagusia kidogo pia kuhusu kambi moja kutumia silaha ya kuwachafua wagombea wengine ili mgombea wao ashinde, Watanzania watamwelewaje mgombea aliyeshinda?
Hapa ni dhahiri kwamba Mkapa atakuwa amekiri makosa aliyoyafanya, lakini naamini Watanzania wataguswa zaidi na maelezo kwamba uteuzi wa mgombea wa CCM uligubikwa na mizengwe. Kikwete atakuwa amechafuliwa, na nadhani wengi watamuona kama rais aliyeingia madarakani kwa njia zisizo kubalika. Haya, Mkapa huyo huyo siku hiyo kama itatokea kweli, anaeleza kwamba yeye kama rais alikuwa na wasaidizi na washauri waliokuwa wakimsaidia kutekeleza majukumu yake ya urais. Anaeleza kuwa aliwaamini wasaidizi wake hao lakini kwa makusudi waliamua kumwangusha kwa kumshauri vibaya au kufumbia macho baadhi ya vitendo vya ufisadi, halafu anamtaja Rais Kikwete kama mmoja wa waliokuwa wasaidizi wake katika wadhifa wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Itakuwaje hapo?

Nadhani Mkapa anaweza kusema hivyo kwa sababu hata aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, niliwahi kumsikia akijitetea hivyo hivyo baada ya kuandamwa na kashfa ya Richmond. Hapa hata mimi napata wasiwasi, naogopa kwa sababu sijui itakuwaje siku hiyo!
Tuendelee; mimi naamini Mkapa hataishia hapo, atakuwa na maelezo mengi ya kujisafisha yeye binafsi na serikali aliyokuwa akiiongoza kwa sababu inatajwa kuwa ndiyo iliyoulea na kuukumbatia ufisadi. Kama kiongozi mstaafu na mzee mwenye busara za kutosha, anamchagua waziri mmoja ambaye hakuwemo katika baraza lake lakini sasa anatajwa tajwa kuwa kabla hajaingia serikali, kampuni aliyokuwa akiiongoza ilijihusisha na ufisadi. Hamtaji moja kwa moja waziri huyo, anaanzia mbali kidogo kwa kunukuu maelezo ya mmoja wa wakurugenzi wanaoiendesha kampuni hiyo kwa sasa, baada ya vinara wake kadhaa kuteuliwa kuingia serikalini kuitumikia serikali iliyoshinda kwa kishindo uchaguzi mkuu ambao tayari Mkapa atakuwa ameisha uchafua.
Anaeleza miongoni mwa kampuni zilizosaidia kusajili kampuni zinazodaiwa kujihusisha na ufisadi zilikuwa na uhusiano wa karibu na wasaidi wake, hivyo kwa sababu si rahisi yeye kujua kila kitu, inawezekana zilitumia mwanya huo kufanya mambo mabaya yalinayomtia matatani sasa.
Mkapa, kwa kujiamini kabisa kama ilivyo kawaida yake na kwa sauti yake nzito ambayo hupenda kuitumia anapokuwa akizungumzia masuala mazito, anaitaka Kampuni ya IMMMA ambayo mmoja wa wakurugenzi amekwishakiri kuwa iliteuliwa na kampuni mashuhuri ya wanasheria duniani ya Denton Wilde Sapte ya London, kumsaidia mteja wao kusajili Kampuni ya Deep Green Finance Ltd, ikiwaomba wafanyakazi wake wawili, kushikilia hisa moja kila mmoja kwa ajili ya usajili huo.
Anaelezea kushangazwa na kampuni hiyo kuwa ndiyo iliyokamilisha kazi ya usajili wa Deep green Finance Ltd, Septemba 2004 na 2005, ambapo hisa hizo zilizokuwa zikishikiliwa na wafanyakazi wawili wa Kampuni ya IMMMA, zilihamishiwa kwa waliokusudiwa kuwa wanahisa.
Katika hali anayoweza kuieleza kuwa ya kushitushwa na taarifa hizo ambazo labda anasema kuwa alizisoma tu kwenye magazeti, anasema anakubali uchunguzi ufanywe ili kubaini ukweli kuhusu kampuni hii kuhusika kutoa msaada kisheria wa kusajili kampuni iliyokomba mabilioni ya Watanzania.
Nadhani IMMMA wanaomba jambo hili lisitokee, kwa sababu litaibua mapya na yaliyojificha. Najaribu kuota kama itatokea hivyo, naona kuwa Watanzania wataanza kuhoji uhusiano wa watoto wawili wa marais wa taifa hili, Fatma Karume na Ridhiwan Kikwete, na IMMMA.
Watajiuliza, iweje kampuni hii inayodaiwa na imekwishakili kuisaidia moja ya kampuni zinazodaiwa kuiba fedha za Watanzania iwaajiri watoto wa watawala wetu? Amini usiamini, hawatakuwa na habari, na ufafanuzi ulikwisha kutolewa kuhusu ajira au ubia wao katika kampuni hiyo. Watakuwa na wakati mgumu.
Lakini atakayekuwa katika wakati mgumu zaidi ni Masha, mwanasiasa kijana mwenye bahati ya kupata vyeo vikubwa tangu akingali kijana mdogo, ambaye sasa ni Waziri wa Mambo ya Ndani. Na ndiyo maana nikaeleza kuwa nadhani ana wasiwasi, kama yeye pia anawaza kama mimi.
Huenda akawa anakumbuka maswali ya msingi niliyowahi kumuuliza katika moja ya makala zangu kuwa anapaswa kuwaeleza Watanzania kwamba kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge na baadaye kuteuliwa kuwa naibu waziri na sasa waziri kamili, hakuwahi kuhusika hata kwa tone moja na shughuli zozote za kifisadi zinazodaiwa kufanywa na Kampuni ya Deep Green?

Kwamba wakati Deep Green Finance inasajiliwa alikuwa wapi? Serikalini au katika kampuni yake? Wakati inafungua akaunti alikuwa wapi na shughuli zake zilikuwa zipi wakati inachota mabilioni ya fedha zetu kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), alikuwa tayari waziri, mbunge au mkurugenzi wa kampuni hiyo?
Ni maswali mapesi kabisa, kwa sababu majibu yake naamini Masha anayo, lakini katika hali tuliyo nayo, yanataka mtu kuwa na moyo wa chuma kuyajibu, kwa sababu ya mabadiliko ya mioyo ya Watanzania kwa sasa. Ni vigumu kuwaaminisha hata kwa jambo la kweli iwapo unatuhumiwa kwa ufisadi!
Tukubaliane, katika hali kama hii, katika ndoto kama hizi ninazoota nikiwa macho, wasiwasi ni jambo la lazima. Na kama kuna mtu anabisha, basi tumuombe Mungu amuongoze Mkapa kuzungumza kama ninavyofikiri na kuota.
Sijui hiri rijamaa rmemuhoji Mkapa naona kama ni onyo kwa Muungwana dah kaazi kweri kweeri.
 
Hivi jamani huyu mama Simba ni mzima kichwani au waandishi wanazusha mambo asiyosema? Yaani kama haya ndio maneno yake c bora awe anakataa kusema kuliko kutapika utumbo kama huu waziri mzima jamani? Hivi hawa mawaziri jamani huenda ndio wanareflect aina ya rais tuliyenaye? (show me your friends I will tell you who you are). Kama ndivyo basi tumekwisha kinoma maskini hii miaka kumi tutabackslide kinoma.
 
Hivi jamani huyu mama Simba ni mzima kichwani au waandishi wanazusha mambo asiyosema? Yaani kama haya ndio maneno yake c bora awe anakataa kusema kuliko kutapika utumbo kama huu waziri mzima jamani? Hivi hwa mawaziri jamani huenda ndio wanareflect aina ya rais tuliyenaye? (show me your friends I will tell you who you are). Kama ndivyo basi tumekwisha kinoma maskini hii miaka kumi tutabackslide kinoma.


Kuliko tuendelee kuongea hivi wakati wao wanendelea kugonganisha glass mi nadhani tufanye mikakati ya kuelemisha watu zaidi... na mengine mengi yatakayo tusaidia tuyajadidli hapa, maana naona hizi kelele hazi saidii kitu
 
Mkapa amechafuka sana mbele za macho ya jamii ndani na nje ya nchi. Haitamsaidia kuonyesha udhaifu wa serikali ya JK ili kujinusuru. After all mbona serikali ya Zanzibar iliingia madarakani isivyo halali lakini bado inaongoza na kukubalika tu. Watanzania umewasahau wewe? Cha kufanya kwa Mkapa ni kuomba radhi na kuahidi kumsaidia JK kuhakikisha ufisadi wote wa enzi zake unaibuliwa na watuhumiwa wanashtakiwa mahakamani. Kuhusu ufisadi unaomuhusu yeye na familia yake moja kwa moja (kiwira, anben, etc.) anaweza kuomba msamaha kwa kudai kuwa alipotoshwa kwa makusudi kwa kushawishiwa na wasaidizi wake, na kuahidi kurudisha kila kitu serikalini.

Atoe pia ahadi ya kumsaidia Jk kuimarisha chama kwa kukabiliana na makundi ya mafisadi na kutatua mgogoro wa kisiasa zanzibar.

Hapo anaweza kueleweka na kukubalika tena kwenye jamii.
 
Hivi jamani huyu mama Simba ni mzima kichwani au waandishi wanazusha mambo asiyosema? Yaani kama haya ndio maneno yake c bora awe anakataa kusema kuliko kutapika utumbo kama huu waziri mzima jamani? Hivi hawa mawaziri jamani huenda ndio wanareflect aina ya rais tuliyenaye? (show me your friends I will tell you who you are). Kama ndivyo basi tumekwisha kinoma maskini hii miaka kumi tutabackslide kinoma.

Bobby umeshtukia? Mama kadata huyu jamani.



Asked yesterday if the government would be ready to prosecute Mkapa in particular if implicated by the allegations, the Minister of State in the President’s Office (Good Governance), Sophia Simba, was non-committal.

’’I can’t answer that question. He is not necessarily guilty of these accusations we should not just tarnish his image. He has done good things for this country’’

Ameulizwa kama Mkapa ni guilty? Na mtu aliyefanya mazuri hashitakiwi?
 
JK is risking being remembered as an ineffectual and indecisive president who kept smiling and laughing while showering wananchi with empty promises. He needs to toughen up and act now.
 
JK is risking being remembered as an ineffectual and indecisive president who kept smiling and laughing while showering wananchi with empty promises. He needs to toughen up and act now.


You are assuming he is willing!

You are giving him false credit!
 
and she is our leader, do still thinks that there is any miracles we should expect from this kind of a leader???? ni kipofu au atajitia ukipofu huyu mama si ni bora wangeishia tu hapa "I can’t answer that question"
tTATIZO TULIOLO NALO NI KWAMBA GOOD RECORD YA BENN NDIYO INAMPA RUKSA YA KUIBA,HAPA MAMA SOPHIA AME HEAT BEHIND BELT.
 
Hatukubali Mkapa adhalilishwe -Pinda


*Asema wataalamu wetu ni butu kujadili mikataba
*Azungumzia mapokezi ya vigogo waliowajibishwa

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imesema haipo tayari kuona Rais mstaafu Bw. Benjamini Mkapa anadhalilishwa kwa kuzomewa hadharani na haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote atayebainika kufanya hivyo kwani kufanya hivyo ni ukiukaji wa utawala wa sheria.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda alipokutana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari katika mkutano wa kufahamiana na kubadilishana mawazo ambapo pia walipata fursa ya kumuuliza maswali.

Akijibu swali kuhusu taarifa za madai ya kukamatwa kwa baadhi ya watu wanaotuhumiwa kumwita Rais huyo fisadi hivi karibuni, Bw. Pinda hakuthibitisha wala kukanusha jambo hilo lakini alisema kamwe hafurahii kuona Rais Mkapa anazomewa anapopita mitaani.

Bw. Pinda alisema yapo mambo yanaweza kufanywa lakini si sahihi hata kidogo kumzomea kiongozi huyo na kwamba vitendo vya kumdhalilisha kamwe havitaruhusiwa katika nchi inayofuata misingi ya utawala wa sheria.

" Hatuwezi kuwa watu wasiojiheshimu, kwa lengo hilo hapana ! waliomwita mhujumu uchumi huenda tabia yao haikuwa ya Kitanzania. Siwezi kufurahia kuona Mkapa anapita anazomewa hata kidogo ! Yapo mambo yanaweza kufanywa, kumshtaki mtu si tatizo lakini sio sahihi kumhukumu mtu bila taratibu kufikiwa," alisema na kusisitiza;

Vitendo vya kumdhalilisha kama Taifa tuseme hapana ! katika nchi inayoongozwa chini ya utawala wa sheria tusichukue sheria mikononi. Siafiki Rais Mkapa kuzomewa, ana heshima yake ni binadamu anastahili heshima, zipo taratibu zinazotakiwa," alionya

Akijibu swali lililohoji usafi wa mawaziri waliobaki madarakani baada ya Rais Jakaya Kikwete kupangua baraza hilo, Bw. Pinda alisema hawezi kuwathibitisha kwa hilo kwani waliomo serikalini ni binadamu kama watu wengine na kufafanua kuwa jukumu lake kama Waziri Mkuu ni kuhakikisha timu hiyo inafanya kazi kwa maadili yanayokubalika na umma.

Alisema Rais Kikwete anajitahidi kutambua na kuteua viongozi wazuri bali matatizo yanayojitokeza ni wahusika wenyewe wanapoingia kwenye dhamana hizo na kusisitiza kwamba suala la uadilifu vita dhidi ya rushwa ni vita endelevu.

"Rais amejitahidi kutambua watu wazuri lakini wanapoingia wanaanza kuhangaika kuangalia huku na huko. Yapo yaliyotokea siku za nyuma lakini hawa tuliona tutazidi kusisitiza suala la uadilifu. Hii ni vita endelevu. Hakuna rushwa inayotoka mbinguni zote zinatoka humu humu," alisema.

Richomond
Kuhusu swali la nani anaendelea kupokea pesa zinazodaiwa kulipwa kampuni hiyo kila siku na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),Bw. Pinda, alisema kampuni hiyo sasa haipo na majukumu yake yalichukuliwa na Dowans ndiyo inapaswa kuhusishwa kwa hilo.
Hata hivyo, alisema uchunguzi kuhusu mapendekezo yaliyotolewa na Tume teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa zabuni ya Richmond bungeni yanaendelea kufanyiwa kazi na tayari kwenye maeneo mengine utekelezaji unaendelea.

Sambamba na hilo alizungumzia mkataba Kampuni ya Kupakua na Kupakia Mizigo Bandarini ya (TICTS) na kueleza kuwa pamoja na uhalali wake umeonekana kuwa na dosari nyingi.

Bw. Pinda alisema kinacholiumiza Taifa sasa na uwezo hafifu wa wataalam kupitia na kukubaliana juu ya mikataba mbalimbali. Alisema kutokana tatizo hilo serikali itaangalia uwezekano wa kushirikisha kamati huru za wataalam wa masuala ya sheria kupitia na kutoa mapendekezo ya mikataba mbalimbali kabla haijasainiwa, ili kupunguza dosari hizo.


Kugawa Mikoa

Alisema hivi sasa katika ofisi yake kuna maombi mengi ya kugawa mikoa, wilaya majimbo na vijiji. Hata hivyo alisema jambo hilo linahitaji gharama kubwa kwani kuanzisha mkoa mmoja zinahitajika si chini ya sh. bilioni 10 na wilaya ni kati ya sh. bilioni tano hadi sita.

Kuhusu majimbo alisema suala hilo linategemea zaidi ushauri wa Tume ya Uchaguzi kama ina pesa kuweza kuhudumia majimbo hayo mapya.

Aliko Balali
"Ukiniuliza yuko wapi sijui" alisema Bw. Pinda alipoombwa kutoa taarifa za uhakika kuhusu aliko gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania
( BoT) . Alisema Bw. Balali anahitajika kutokana na masuala ya BoT na kurudia kauli ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Salva Rweyemamu kwamba gavana huyo akihitajika si jambo kubwa, atapatikana.

Bei ya Mafuta

Kuhusu ongezeko la bei za mafuta linalochangia kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali, Bw. Pinda alisema Mamlaka ya Udhibiti wa Bei ya Umeme na Maji ( EWURA) inajitajihidi katika suala hili lakini bei inazidi kupanda siku hadi siku.

Alisema serikali inaangalia uwezekano wa kuagiza bidhaa hiyo kiasi kikubwa kwa wakati mmoja hali itakayosadia kushusha bei kwenye vituo vya mafuta.

Mapokezi vigogo

Akijibu swali lililohoji kuwa anajisikia viongozi waliowajibishwa kwa tuhuma za ufisadi kupokelewa kwa makeke majimboni mwao, alisema huo ni mtazamo wa wananchi wao majimboni na kwamba tuhuma hizo haziwaondolei upendo wao. Alisema serikali haina uwezo kuwahukumu kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Bw. Pinda aliwataka watendaji wote wakiwemo mawaziri kuwa wazi kwa vyombo vya habari na kushirikiana kutoa taarifa, binafsi alisema amejipangia utaratibu wa kukutana na wahariri kila baada ya miezi mitatu kujadili na kujibu hoja mbalimbali kwa manufaa ya jamii.


Alivipongeza vyombo hivyo na kueleza kuwa sasa vimeifikisha serikali pagumu kutoka na umakini wa kufuatilia masuala mbalimbali jambo ambalo alisema kuna mambo mengi yanayofanyika sasa ambayo kama vyombo hivyo vingelala yasingefanyika.

" Vyombo vya habari vimetufikisha pagumu tuliomo serikalini, tunafanya kazi mmesukuma mambo, kama 'press' ingelala yasingefanyika " alisema na kuahidi kuwa serikali itajitahidi kuhakikisha uhuru zaidi kwa vyombo vya habari unakuwepo.
 
Hatukubali Mkapa adhalilishwe -Pinda


*Asema wataalamu wetu ni butu kujadili mikataba
*Azungumzia mapokezi ya vigogo waliowajibishwa

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imesema haipo tayari kuona Rais mstaafu Bw. Benjamini Mkapa anadhalilishwa kwa kuzomewa hadharani na haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote atayebainika kufanya hivyo kwani kufanya hivyo ni ukiukaji wa utawala wa sheria.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda alipokutana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari katika mkutano wa kufahamiana na kubadilishana mawazo ambapo pia walipata fursa ya kumuuliza maswali.

Akijibu swali kuhusu taarifa za madai ya kukamatwa kwa baadhi ya watu wanaotuhumiwa kumwita Rais huyo fisadi hivi karibuni, Bw. Pinda hakuthibitisha wala kukanusha jambo hilo lakini alisema kamwe hafurahii kuona Rais Mkapa anazomewa anapopita mitaani.

Bw. Pinda alisema yapo mambo yanaweza kufanywa lakini si sahihi hata kidogo kumzomea kiongozi huyo na kwamba vitendo vya kumdhalilisha kamwe havitaruhusiwa katika nchi inayofuata misingi ya utawala wa sheria.

" Hatuwezi kuwa watu wasiojiheshimu, kwa lengo hilo hapana ! waliomwita mhujumu uchumi huenda tabia yao haikuwa ya Kitanzania. Siwezi kufurahia kuona Mkapa anapita anazomewa hata kidogo ! Yapo mambo yanaweza kufanywa, kumshtaki mtu si tatizo lakini sio sahihi kumhukumu mtu bila taratibu kufikiwa," alisema na kusisitiza;

Vitendo vya kumdhalilisha kama Taifa tuseme hapana ! katika nchi inayoongozwa chini ya utawala wa sheria tusichukue sheria mikononi. Siafiki Rais Mkapa kuzomewa, ana heshima yake ni binadamu anastahili heshima, zipo taratibu zinazotakiwa," alionya

Akijibu swali lililohoji usafi wa mawaziri waliobaki madarakani baada ya Rais Jakaya Kikwete kupangua baraza hilo, Bw. Pinda alisema hawezi kuwathibitisha kwa hilo kwani waliomo serikalini ni binadamu kama watu wengine na kufafanua kuwa jukumu lake kama Waziri Mkuu ni kuhakikisha timu hiyo inafanya kazi kwa maadili yanayokubalika na umma.

Alisema Rais Kikwete anajitahidi kutambua na kuteua viongozi wazuri bali matatizo yanayojitokeza ni wahusika wenyewe wanapoingia kwenye dhamana hizo na kusisitiza kwamba suala la uadilifu vita dhidi ya rushwa ni vita endelevu.

"Rais amejitahidi kutambua watu wazuri lakini wanapoingia wanaanza kuhangaika kuangalia huku na huko. Yapo yaliyotokea siku za nyuma lakini hawa tuliona tutazidi kusisitiza suala la uadilifu. Hii ni vita endelevu. Hakuna rushwa inayotoka mbinguni zote zinatoka humu humu," alisema.

Richomond
Kuhusu swali la nani anaendelea kupokea pesa zinazodaiwa kulipwa kampuni hiyo kila siku na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),Bw. Pinda, alisema kampuni hiyo sasa haipo na majukumu yake yalichukuliwa na Dowans ndiyo inapaswa kuhusishwa kwa hilo.
Hata hivyo, alisema uchunguzi kuhusu mapendekezo yaliyotolewa na Tume teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa zabuni ya Richmond bungeni yanaendelea kufanyiwa kazi na tayari kwenye maeneo mengine utekelezaji unaendelea.

Sambamba na hilo alizungumzia mkataba Kampuni ya Kupakua na Kupakia Mizigo Bandarini ya (TICTS) na kueleza kuwa pamoja na uhalali wake umeonekana kuwa na dosari nyingi.

Bw. Pinda alisema kinacholiumiza Taifa sasa na uwezo hafifu wa wataalam kupitia na kukubaliana juu ya mikataba mbalimbali. Alisema kutokana tatizo hilo serikali itaangalia uwezekano wa kushirikisha kamati huru za wataalam wa masuala ya sheria kupitia na kutoa mapendekezo ya mikataba mbalimbali kabla haijasainiwa, ili kupunguza dosari hizo.


Kugawa Mikoa

Alisema hivi sasa katika ofisi yake kuna maombi mengi ya kugawa mikoa, wilaya majimbo na vijiji. Hata hivyo alisema jambo hilo linahitaji gharama kubwa kwani kuanzisha mkoa mmoja zinahitajika si chini ya sh. bilioni 10 na wilaya ni kati ya sh. bilioni tano hadi sita.

Kuhusu majimbo alisema suala hilo linategemea zaidi ushauri wa Tume ya Uchaguzi kama ina pesa kuweza kuhudumia majimbo hayo mapya.

Aliko Balali
"Ukiniuliza yuko wapi sijui" alisema Bw. Pinda alipoombwa kutoa taarifa za uhakika kuhusu aliko gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania
( BoT) . Alisema Bw. Balali anahitajika kutokana na masuala ya BoT na kurudia kauli ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Salva Rweyemamu kwamba gavana huyo akihitajika si jambo kubwa, atapatikana.

Bei ya Mafuta

Kuhusu ongezeko la bei za mafuta linalochangia kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali, Bw. Pinda alisema Mamlaka ya Udhibiti wa Bei ya Umeme na Maji ( EWURA) inajitajihidi katika suala hili lakini bei inazidi kupanda siku hadi siku.

Alisema serikali inaangalia uwezekano wa kuagiza bidhaa hiyo kiasi kikubwa kwa wakati mmoja hali itakayosadia kushusha bei kwenye vituo vya mafuta.

Mapokezi vigogo

Akijibu swali lililohoji kuwa anajisikia viongozi waliowajibishwa kwa tuhuma za ufisadi kupokelewa kwa makeke majimboni mwao, alisema huo ni mtazamo wa wananchi wao majimboni na kwamba tuhuma hizo haziwaondolei upendo wao. Alisema serikali haina uwezo kuwahukumu kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Bw. Pinda aliwataka watendaji wote wakiwemo mawaziri kuwa wazi kwa vyombo vya habari na kushirikiana kutoa taarifa, binafsi alisema amejipangia utaratibu wa kukutana na wahariri kila baada ya miezi mitatu kujadili na kujibu hoja mbalimbali kwa manufaa ya jamii.


Alivipongeza vyombo hivyo na kueleza kuwa sasa vimeifikisha serikali pagumu kutoka na umakini wa kufuatilia masuala mbalimbali jambo ambalo alisema kuna mambo mengi yanayofanyika sasa ambayo kama vyombo hivyo vingelala yasingefanyika.

" Vyombo vya habari vimetufikisha pagumu tuliomo serikalini, tunafanya kazi mmesukuma mambo, kama 'press' ingelala yasingefanyika " alisema na kuahidi kuwa serikali itajitahidi kuhakikisha uhuru zaidi kwa vyombo vya habari unakuwepo.

Wana kama mwaka tu hivi teh teh teh...Hizi mi naziita bla blah!
 
Hatukubali Mkapa adhalilishwe -Pinda


*Asema wataalamu wetu ni butu kujadili mikataba
*Azungumzia mapokezi ya vigogo waliowajibishwa

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imesema haipo tayari kuona Rais mstaafu Bw. Benjamini Mkapa anadhalilishwa kwa kuzomewa hadharani na haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote atayebainika kufanya hivyo kwani kufanya hivyo ni ukiukaji wa utawala wa sheria.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda alipokutana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari katika mkutano wa kufahamiana na kubadilishana mawazo ambapo pia walipata fursa ya kumuuliza maswali.

Akijibu swali kuhusu taarifa za madai ya kukamatwa kwa baadhi ya watu wanaotuhumiwa kumwita Rais huyo fisadi hivi karibuni, Bw. Pinda hakuthibitisha wala kukanusha jambo hilo lakini alisema kamwe hafurahii kuona Rais Mkapa anazomewa anapopita mitaani.

Bw. Pinda alisema yapo mambo yanaweza kufanywa lakini si sahihi hata kidogo kumzomea kiongozi huyo na kwamba vitendo vya kumdhalilisha kamwe havitaruhusiwa katika nchi inayofuata misingi ya utawala wa sheria.

" Hatuwezi kuwa watu wasiojiheshimu, kwa lengo hilo hapana ! waliomwita mhujumu uchumi huenda tabia yao haikuwa ya Kitanzania. Siwezi kufurahia kuona Mkapa anapita anazomewa hata kidogo ! Yapo mambo yanaweza kufanywa, kumshtaki mtu si tatizo lakini sio sahihi kumhukumu mtu bila taratibu kufikiwa," alisema na kusisitiza;

Vitendo vya kumdhalilisha kama Taifa tuseme hapana ! katika nchi inayoongozwa chini ya utawala wa sheria tusichukue sheria mikononi. Siafiki Rais Mkapa kuzomewa, ana heshima yake ni binadamu anastahili heshima, zipo taratibu zinazotakiwa," alionya

Akijibu swali lililohoji usafi wa mawaziri waliobaki madarakani baada ya Rais Jakaya Kikwete kupangua baraza hilo, Bw. Pinda alisema hawezi kuwathibitisha kwa hilo kwani waliomo serikalini ni binadamu kama watu wengine na kufafanua kuwa jukumu lake kama Waziri Mkuu ni kuhakikisha timu hiyo inafanya kazi kwa maadili yanayokubalika na umma.

Alisema Rais Kikwete anajitahidi kutambua na kuteua viongozi wazuri bali matatizo yanayojitokeza ni wahusika wenyewe wanapoingia kwenye dhamana hizo na kusisitiza kwamba suala la uadilifu vita dhidi ya rushwa ni vita endelevu.

"Rais amejitahidi kutambua watu wazuri lakini wanapoingia wanaanza kuhangaika kuangalia huku na huko. Yapo yaliyotokea siku za nyuma lakini hawa tuliona tutazidi kusisitiza suala la uadilifu. Hii ni vita endelevu. Hakuna rushwa inayotoka mbinguni zote zinatoka humu humu," alisema.

Richomond
Kuhusu swali la nani anaendelea kupokea pesa zinazodaiwa kulipwa kampuni hiyo kila siku na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),Bw. Pinda, alisema kampuni hiyo sasa haipo na majukumu yake yalichukuliwa na Dowans ndiyo inapaswa kuhusishwa kwa hilo.
Hata hivyo, alisema uchunguzi kuhusu mapendekezo yaliyotolewa na Tume teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa zabuni ya Richmond bungeni yanaendelea kufanyiwa kazi na tayari kwenye maeneo mengine utekelezaji unaendelea.

Sambamba na hilo alizungumzia mkataba Kampuni ya Kupakua na Kupakia Mizigo Bandarini ya (TICTS) na kueleza kuwa pamoja na uhalali wake umeonekana kuwa na dosari nyingi.

Bw. Pinda alisema kinacholiumiza Taifa sasa na uwezo hafifu wa wataalam kupitia na kukubaliana juu ya mikataba mbalimbali. Alisema kutokana tatizo hilo serikali itaangalia uwezekano wa kushirikisha kamati huru za wataalam wa masuala ya sheria kupitia na kutoa mapendekezo ya mikataba mbalimbali kabla haijasainiwa, ili kupunguza dosari hizo.


Kugawa Mikoa

Alisema hivi sasa katika ofisi yake kuna maombi mengi ya kugawa mikoa, wilaya majimbo na vijiji. Hata hivyo alisema jambo hilo linahitaji gharama kubwa kwani kuanzisha mkoa mmoja zinahitajika si chini ya sh. bilioni 10 na wilaya ni kati ya sh. bilioni tano hadi sita.

Kuhusu majimbo alisema suala hilo linategemea zaidi ushauri wa Tume ya Uchaguzi kama ina pesa kuweza kuhudumia majimbo hayo mapya.

Aliko Balali
"Ukiniuliza yuko wapi sijui" alisema Bw. Pinda alipoombwa kutoa taarifa za uhakika kuhusu aliko gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania
( BoT) . Alisema Bw. Balali anahitajika kutokana na masuala ya BoT na kurudia kauli ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Salva Rweyemamu kwamba gavana huyo akihitajika si jambo kubwa, atapatikana.

Bei ya Mafuta

Kuhusu ongezeko la bei za mafuta linalochangia kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali, Bw. Pinda alisema Mamlaka ya Udhibiti wa Bei ya Umeme na Maji ( EWURA) inajitajihidi katika suala hili lakini bei inazidi kupanda siku hadi siku.

Alisema serikali inaangalia uwezekano wa kuagiza bidhaa hiyo kiasi kikubwa kwa wakati mmoja hali itakayosadia kushusha bei kwenye vituo vya mafuta.

Mapokezi vigogo

Akijibu swali lililohoji kuwa anajisikia viongozi waliowajibishwa kwa tuhuma za ufisadi kupokelewa kwa makeke majimboni mwao, alisema huo ni mtazamo wa wananchi wao majimboni na kwamba tuhuma hizo haziwaondolei upendo wao. Alisema serikali haina uwezo kuwahukumu kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Bw. Pinda aliwataka watendaji wote wakiwemo mawaziri kuwa wazi kwa vyombo vya habari na kushirikiana kutoa taarifa, binafsi alisema amejipangia utaratibu wa kukutana na wahariri kila baada ya miezi mitatu kujadili na kujibu hoja mbalimbali kwa manufaa ya jamii.


Alivipongeza vyombo hivyo na kueleza kuwa sasa vimeifikisha serikali pagumu kutoka na umakini wa kufuatilia masuala mbalimbali jambo ambalo alisema kuna mambo mengi yanayofanyika sasa ambayo kama vyombo hivyo vingelala yasingefanyika.

" Vyombo vya habari vimetufikisha pagumu tuliomo serikalini, tunafanya kazi mmesukuma mambo, kama 'press' ingelala yasingefanyika " alisema na kuahidi kuwa serikali itajitahidi kuhakikisha uhuru zaidi kwa vyombo vya habari unakuwepo.

loh
 
Back
Top Bottom