Lete ushahidi hapa. Usilete roumars tu!
Usiwe mvivu wa kufikiri na kufuatilia habari. fuatilia upatikanaji wa Kagera Sugar jinsi kilivyouzwa.
mambo yote huanza hapa na kusemwa kuwa ni udaku,Mradi wa vitambulisho vya Membe ulianza hapa hapa unaweza kuuona www.raiamwema.co.tz aliuleta GT akasemwa kuwa ni mshuzi.
Suzane Mungy kupewa ukurugenzi TBC ilianza hapa na kusemwa kuwa ni uvumi ulioletwa na Mtalii.
Membe na kampeni zake za urais zilianza hapa hapa ikasemwa kuwa ni uvumi.
Mizange Pinda kuwa atakuwa waziri mkuu ilianza hapa hapa.
Sijawahi kuandika jambo la uzushi hapa JF hasa la kumsingizia Mkapa. kwanini nitaje Kagera Sugar baada ya kuona watu wanajishughulisha na kijishamba wakati jamaa ana kiwanda kamili.
Orodha ya mafisadi ililetwa ikasema ni uzushi na Richmond aliifuatilia Mwanakijiji na ikasema kuwa ni mzushi hana hoja.
ilitakiwa ufanye utafiti na kuja kusema huu ni udaku au uvumi.
Mkapa yupo Kagera Sugar wengi wanajua.bwana Fisadi hujui kuwa Mramba anamili shirika la ndege?