Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,580
- 18,222
Kwani kimaro alikua na kosa gani? Wanasema amekosa adabu? Hivi wananchi hao hao si ndio wakimwona kibaka wanaanza kumkimbiza kwa mawe? Kwa hiyo huko nako ni kukosa adabu?
huyo dogo aache kelele amlete baba yake ajibu tuhuma moja baada ya nyingine mbele ya waandishi wa habari na watanzania kwa ujumla ndio tutamwelewa la sivyo tutamwandama mpaka kaburini. na si yeye tu hata maswahiba wake wakina mramba na wengineo tutawasakama mpaka kieleweke.
HUYU PAMOJA NA YULE BALOZI WALIOMBAGA TENA URAIA NA WALIPEWA MUDA MREFU UMEPITAkumbe castico yuko huko ? huyu si ndo yule alikuwepo kiswandui zanzibar au mwengine ?
na kama ndie ile kesi yake ya uraia imefikia wapi ?
Sio Jambo La Ajabu Kwani Kama Ambavyo Sita Atapopolewa Ndivyo Yeye Atapopolewa,amedandia Mambo Hasiyoyaweza....lazima Atolewe Tena Kwa Aibu.
TATIZO HAO WANANCHI NDIO HAWAMTAKI NA WANASEMA WAZIWAZI.NJOO HUKU VUNJO UAMBIWE HAYO MAMBO.MPAKA MAKANISANI HAWATAKI KUMSIKIA..ALIOANDIKA DIKTETA NI YA KWELI.LABDA MPENI JAMBO DAR.Nguvu ya umma siku zote iwa haishindwi kitu...mkimpiga cheni anagombea kwa kupitia mgombea binafsi CCM kaeni chonjo....na Kimaro kesha jitangazia sifa kwa kupigana na mafisadi.,
Ajibu tuhuma kwa waandishi wa habari, kwani wao wamekuwa mahakama? Kwa nini hiyo serikali ya CCM haitaki kumfikisha mahakamani?
Hata mimi ningekuwa mtoto wake Mkapa ningekuwa na ghadhabu kubwa kabisa na waandishi wa habari kwa sababu wao wamebaki kulia na Mkapa badala ya kuibana serikali imfikishe mahakamani. Kama ni tuhuma, waandishi wa habari wameshaziweka wazi, sioni kilichobaki tena cha kuzungumza kuhusu Mkapa. Kama hatuwezi kuibana serikali imfikishe mahakamani waandishi na sisi tukae kimya waendelea kutesa mtaani na mapesa yao.