NaimaOmari
JF-Expert Member
- Sep 25, 2007
- 801
- 46
balaa hizo maana sumaye analipwa Ml 100 mwenzangu ohoo ... shauri yenu mtakuwa mashahidi mimi simo
Kitila Mkumbo,
Sam Nujoma Rd inaendelea kwa mwendo wa kusuasua mno,leo wakati natoka zangu Mbezi kuja mjini foleni ikaanzia Africana mpaka Mwenge kwenyewe,mtu unatoka nyumbani 05:50 a.m unafika Posta/Mjini 8:00 a.m!Kufika Mwenge nawakuta wachina na vibarua wao wana majembe na makoleo (as opposed to bulldozers,asphalt pavers and the like) wakijikongoja kujaza udongo na lami...damn it!!
Miundo Mbinu kwa kweli wa ovyo sana!!!
MZEE KAANZA KUISHIWA UVUMILIVU SASA NDIYO SAFI AENDE MAHAKAMANIRais (mstaafu) wa Tanzania Benjamin William Mkapa yuko katika mchakato wa mwisho kuyashtaki magazeti ambayo yamekuwa yakimwandama kwamba ni fisadi.
Habari kutoka ndani ya familia yake zinaeleza kuwa taratibu za kuyashitaki magazeti hayo zimekamilika na kilichokuwa kikisubiriwa ni kutolewa kwa taarifa za awali kwamba yeye na mkewe, mjasiriamali Anna Mkapa hawana hisa katika mgodi wa Kiwira.
Zaidi ya hapo inaelezwa kuwa magazeti yatakayoshikiwa bango ni Kulikoni, Thisday, Mwanahalisi, Mwananchi, Tanzania Daima, Majira na Mtanzania.
Mtoa habari huyo aliyeona makabrasha ya mashtaka hayo ameeleza kuwa kila gazeti litadaiwa bilioni mbili; akieleza kuwa anadai kiasi hicho kwa kuwa angalau kinalinganalingana na hadhi yake ndani na nje ya nchi.
Hivi majuzi kampuni ambayo ilinunua mgodi wa Kiwira wa kuzalisha makaa ya mawe iliibuka na kueleza kuwa Mkapa na mkewe hawana hisa eti kwamba walijitoa muda mfupi baada ya kugundua kuwa ilikuwa ikijiandaa kununua mgodi huo kwa bei ya kutupwa ya sh. milioni 700 (zililipwa 70 kwanza za kukopa kutoka Benki) wakati mgodi wenyewe ukiwa na gharama kubwa ya bilioni 4.
Mawakili sita wamejipanga kwa kazi hiyo, huku mmoja akiwa kutoka Afrika Kusini ambaye anaeleza kuwa mzoefu katika kesi zinazohusu kashfa kwenye vyombo vya habari.
Mimi nafikiri amechukua uamuzi wa busara sana. Madamu serikali yetu kwa niaba yetu imeshindwa kumshtaki acha yeye aende hukohuko ili ukweli ujulikane- kama sisi tukipigwa bao asafishike kiana, yeye akipigwa bao basi tumepona. Hii tabia ya kushtaki watu kwenye internet na kwenye vijiwe binafsi imeshanichosha. Tuna vyombo tumevitumie.
Nafikiri hizi kesi zikianze zitatusaidia ku-concentrate na yale wanayoyafanya akina JK. Nakubaliana na wale wanaosema kuwa tujifunze kuwaadabisha na kuwajibisha viongozi wetu wangali madarakani itatusaidia zaidi. Sasa hivi tunawapa easy ride akina JK; tunasubiri atoke tusikie amenunua Bagamoyo nzima ndipo tuanze.
BTW, kwa wale waliopo Dar, hivi barabara ya Sam Nujoma KM 5 iliyoanza kujengwa Januari 2006 imefikia wapi?
Mkutano huo uliandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Tanzania Leo Limited, inayochapisha gazeti la Tanzania Leo, Bw. Venance Rwegoshora, kukanusha taarifa iliyochapishwa na gazeti hilo, toleo la Machi 31 hadi Aprili 6, mwaka juzi, kuwa Bw. Sumaye, anamiliki akaunti iliyopo nje ya nchi, ikiwa na Sh. Trilioni 10.
Bw. Rwegoshora, alisema baada ya mchakato wa hoja kati ya kampuni hiyo na Bw. Sumaye kushindikana kupitia usuluhishi wa Baraza la habari, suala hilo lilifikishwa mahakamani, ilipobainika kuwa habari hizo zilikuwa za uongo, zilitungwa, zikapotosha na kutokuwa na msingi wowote.
Kutokana na hali hiyo, Mahakama Kuu iliamuru kufanyika kikao cha usuluhishi kati ya pande mbili hizo, na kukubaliwa masuala kadhaa, ikiwemo Tanzania Leo kumlipa Bw. Sumaye fidia ya Sh milioni 100, zitakazolipwa kuanzia kipindi cha kabla ya Desemba Mosi mwaka huu hadi juni mwaka ujao.
Nasema hivi Mlango wameufungua wenyewe sasa hivi kazi inakuja!... Na huyoTaharo ata hara kweli kweli maanake tunataka kwanza uthibitisho wa kila alichokisema, Nina hakika hana labda ziwe zimeghushiwa..
Kuna mtu ananena anasema Sumaye kacheza deal ili kusafishwa na gazeti lile ni mali yake mwenyewe anajiandika , na kujishitaji na sasa anajisafisha baada ya kuona hilo Mkapa naye kaanza .Ni game hii wananchi .Mnakumbuka huko nyuma nilikuja na madai ya CCM kuanza kwa gharama yeyote kujisafisha watu wakasema Lunyungu ni mzushi ? Sasa mnayaona wenyewe hakuna cha magazeti kushitakiwa hapa ni kwamba wahariri wanalambishwa na kufanya deal .Rostam alijaribu akakwaa kisiki sijui ile kesi yake imeishia wapi.