Wanaomshauri Mzee Mkapa wanakosea sana,kila mtu anataka kuona Mkapa anakwenda Mahakamani.Kila kitu kipo wazi,(ushahidi wa kutosha upo) ataumbuliwa na wenzie aliokuwa nao serikalini.Lakini hali hii isihamishe juhudi za kutaka kujua pesa za umma za EPA zimeibiwa vipi?,hawa waungwana wamekuwa wajanja kukwepa maswala kwa kuzua habari mpya, moto moto.Wawakilishi wetu Bungeni wawe macho na hawa majangili,kila issue ipewe nafasi sawa ya kujadiliwa kwa uwazi.
Mkapa ni Fisadi,na kwa kuwa ameamua kwenda Mahakamani kila kitu kitakuwa nje!Anajivua nguo mwenyewe,wala msiwazibe macho watoto,waacheni waone sinema ya bure..Kuna ushahidi tosha wa yeye,Mrs,Nico na Mbuna Family kuhusika na Mradi wa kiwira.Judge Bomani na akina Zitto watakuwa mashahidi hapa,yale waliyoyaona Mbeya (Kiwira) yasiwe siri tena,kila kitu kiwekwe hadharani,ili hawa watu wahukumiwe kwa udhalimu wao.
Muungwana JK kama kweli utawala wako hauna Ubia usiwaonee haya hawa Majangili,acha sheria ichukue mkondo wake..Vinginevyo nawe utazomewa na kupigwa mawe kwa kuwalinda hawa wezi unaowaita wastaafu.Hivi serikali yako imefanya nini toka iingie Madarakani?kila siku tunaona kashfa mpya,kama nawe Uongozi umekushinda,achia ngazi si lazima umalize 10yrs,Historia itakuandika vizuri,kwa kuwa Rais wa kwanza kukaa madarakani Term moja..