Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Ni upuuzi mtupu...wakati wote wako kimya walikuwa kwenye harakati za kuondoa majina ya Mkapa kwenye kampuni hii...kwa mtazamo wao walifikiri ndio ingemaliza hii issue.Lakini jina la mwananwe bado limo,na la mzazi mwenzake(Mbuna),kwa hio bado ataendelea kuhusishwa tu.Yona ndio alimuuzia ile nyumba ya Sea View(Bank M),uhusiano wao unajulikana toka zamani.
 
Hivi waandishi hamkumuuliza kwanini alisita sana kule Dodoma kujibu swali la mashamba yake ya kibaigwa mpaka alipoona maji yamefika shingoni?
 
Binafsi kwa kutumia taarifa hii KCM najiridhisha kwamba kuna ukweli katika taarifa zinazoitwa za udaku, majungu na uzushi ambao mara nyingi mafisadi wamekuwa wakikanusha kwa nguvu kubwa na kutishia kuenda mahakamani.

Labda kwa kushauri vyombo vyetu butu vya Polisi, PCCB na Usalama wafanyie kazi taarifa hii ya KCM kama ushaidi na wachimbe zaidi hata kama watashindwa wanachi tunazo cases ambazo zinatosha kufanya maamuzi. Kama mtarejea taarifa ya mwanzo iliyochimba ufisadi bongo mtagundua link ipo labda tu longolongo na sanaa ichukue nafasi.

Ushindi dhidi ya vita ya ufisadi hauko mbali ni kuendelea kushika bango mpaka kieleweke, tumepata taarifa nyingi ambazo zinatosha kwetu wabongo kuchukua hatua. Hata kuchukia tu bila kuandika inatosha. Huu ni wakati mzuri kwetu watanzania kuchukua hatua, si mahakama wala serikali ni sisi wapiga kura tunatakiwa kuvunja kanuni ilizoeleka (break the rule) serikali na mahakama ifuate tunavyotaka.
 
Talking about backfire, sour grapes bwana naona mmepatikana sasa linyweni sasa mmelikoroga wenyewe hilooooo tena la motooooooooo!

Chaumbeya, heshima yako mkuu mbona unapotea sana brooo!
 
na ile hotel ya Lamada pale Ilala kaipataje? naona Simba ni kati ya waliopendelewa na Mkapa ambao aliwataja huko kwao Lupaso
 
Hivi watu mnakuwa na uhakika na habari mnazoongea ama kuropoka tu.Wao wanaosema Sophia Simba si mke wa Iddi Simba ni majina tu inabidi waache kurupuka na inaonyesha kiasi gani data zao zisivyo na uhakika.

Eti sophia simba ni mke wa idd simba? wewe umepungukiwa kidogo mkuu huyu ni mshikaji wangu long time unasema eti dataz hazina uhakika na yeye ni jirani yangu Dodoma?

Mkuu ninamjua mke wa Idd Simba ni mdogo mno kimwili ukilinganisha na sophia, sophia ni mweupe mke wa simba ni mweusi wote ninawajua sana mkuu kama hamna dataz kaeni pembeni tutawapeni tu! sophia ni bibi wa kk. yaani ninajua mpaka mtoto wake aliyeko jela US lakini simjui sophia?
 
Huyu Tabaro mwnyw mwizi, alishirikiana na wenziwe watatu kule tigo kuiba 900m
 
DPP ndiye kikwazo kumshitaki Mkapa

2008-06-02 09:35:59
Na Simon Mhina


Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, amedai kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ni kikwazo katika kuwafungulia kesi Rais mstaafu Benjamin Mkapa na mkewe Anna Mkapa.

Bw. Mtikila anakusudia kuwafungulia akiwatuhumu kwa kutumia vibaya madaraka na kujimilikisha mali za umma.

Hata hivyo, DPP, Bw. Elieza Feleshi, amepinga malalamiko hayo ya Mtikila na kusisitiza kuwa hazuii raia wala mtu yeyote kufungua mashataka dhidi ya mtuhumiwa anayeona ana kesi ya kujibu.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam hivi karibuni Bw. Mtikila alisema mashtaka dhidi ya Mkapa na mkewe yapo tayari kufikishwa mahakamani lakini imebidi atumie busara ya ziada kwa vile hata akifungua kesi dhidi yao, DPP ataingilia kati suala hilo na kulifutilia mbali.

``DPP ana madaraka makubwa kuliko Rais wa nchi. Anaweza kusema kesi hii isikilizwe na ile ifutwe bila kutoa sababu zozote, jambo hili ni baya sana na halipo katika nchi nyingine,`` alisema.

Alifafanua kwamba kwa kutumia kifungu namba 91 cha Sheria ya Makosa ya Jinai, Mkurugenzi wa Mshataka anapewa mamlaka ya kufuta kesi bila kutoa maelezo wala kujibu hoja, hatua hiyo kisheria huitwa `nolle proseque`.

Hata hivyo, mwanasiasa huyo machachari alisema kwa vyovyote vile lazima Bw. Mkapa na mkewe watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma kadhaa zikiwemo za mgodi wa Kiwira.

Alisema lengo la kufungua kesi hiyo ni kuhakikisha watuhumiwa hao wanafilisiwa mali walizojipatia kwa udanganyifu.

Alipoulizwa ni vipi amepanga kumfungulia kesi Bw. Mkapa wakati anayo kinga ya kikatiba, mwanasiasa huyo alisema si kweli kwamba Rais yupo juu ya sheria.

Alisema ibara ya 46 ya Katiba inazuia Rais asifikishwe mahakamani kwa mambo aliyoyafanya akitekeleza majukumu yake kama Rais kwa mujibu wa katiba.

``Sasa kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei sawa na bure alikuwa anatekeleza majukumu yake ya urais? Kufungua kampuni binafsi na kukopa mkopo usio na dhamana akiwa Ikulu ni majuku ya kirais? Kwa hali yoyote matendo hayo yalikuwa yanahujumu urais,`` alidai.

Alisema hata ingeshindikana kumshitaki Bw. Mkapa, upo umuhimu wa kumshitaki mkewe kwa vile yeye hakuwahi kuwa Rais.

Alisema amepeleka maombi Mahakama Kuu kwa Jaji Kiongozi ili itolewe amri ya kumpunguzia madaraka DPP asiwe na uwezo wa kuwalinda mafisadi kwa kuwafutia kesi bila kutoa maelezo.

Akijibu madai ya Bw. Mtikila , DPP Feleshi alipinga kuwa ni kikwaazwo katika kufungua kesi ya aina hiyo na kusisitiza kuwa mamlaka aliyopewa na katiba ya kufuta kesi yoyote yamelenga kuleta haki. Hata hivyo, hakufafanua.

Alimtaka Mchungaji Mtikila kufungua kesi yoyote kama anataka ili mradi afuate kanuni za kufungua shauri mahakamani.

``Mimi sio kikwazo mbona huyo Mtikila amefungua kesi nyingi na hajawekewa vikwazo?`` Alihoji na kuongeza ``Sijawahi kutumia madaraka yangu vibaya. Sijafuta kesi kinyume na miongozo niliyopewa.``

Akifafanua zaidi alisema inaweza ikatokea kesi na wakati inaendelea ofisi yake ikagundua kwamba mtuhumiwa ni kichaa au ni mtoto hivyo hulazimika kufuta kesi hiyo kwa vile kuendelea nayo ni kupoteza muda kwa vile `mwisho wa siku` mahakama itaitupa.

SOURCE: Nipashe
 
Inatakiwa habari iwe hivi: 'Mkapa ajisafisha kuhusu Kiwira'!
Suala la Kiwira kumsafisha BWM sio sawa.....
BMW toa statement hii: 'Mimi BWM similiki wala sijawahi kumiliki mgodi wa Kiwira........sio mimi wala familia yangu, wala jamaa zangu! Hatujawahi kuwa na masilahi ya aina yoyote mgodi wa Kiwira'....
Ni rahisi kabisa.
 
huyu mama ni fisadi na mpenda sifa mkubwa kwa viongozi wenzake namjua sana ni mtu wa kujikomba komba sana na sijui anategemea nini kwao na sijui ni kwanini alipewa hiki cheo ila ni jukumu letu wana jf kumtangaza wazi kuwa ni KIONGOZI NA MLINZI WA MAFISADI ili popote akipita naye azomewe "kama ni kupona alipona jk bwana",asituletee uzuri hapa!! maana huyu anataka kukwamisha vita yetu.

Kwa nini alipewa hicho cheo ndio sababu alipewa hicho cheo!

Ni Waziri wa Propaganda. Ndio kazi yake. Unamvyomjua Simba ndio Kikwete anavyomjua. Ndio maana akampa hiyo kazi ya Waziri wa Propaganda.

Lazima uelewe, Kikwete sio mwenzako hapa. Ukishangaa watu anaowateu Kikwete ni kutokumuelewa Kikwete!
 
Rais (mstaafu) wa Tanzania Benjamin William Mkapa yuko katika mchakato wa mwisho kuyashtaki magazeti ambayo yamekuwa yakimwandama kwamba ni fisadi.

Habari kutoka ndani ya familia yake zinaeleza kuwa taratibu za kuyashitaki magazeti hayo zimekamilika na kilichokuwa kikisubiriwa ni kutolewa kwa taarifa za awali kwamba yeye na mkewe, mjasiriamali Anna Mkapa hawana hisa katika mgodi wa Kiwira.

Zaidi ya hapo inaelezwa kuwa magazeti yatakayoshikiwa bango ni Kulikoni, Thisday, Mwanahalisi, Mwananchi, Tanzania Daima, Majira na Mtanzania.

Mtoa habari huyo aliyeona makabrasha ya mashtaka hayo ameeleza kuwa kila gazeti litadaiwa bilioni mbili; akieleza kuwa anadai kiasi hicho kwa kuwa angalau kinalinganalingana na hadhi yake ndani na nje ya nchi.

Hivi majuzi kampuni ambayo ilinunua mgodi wa Kiwira wa kuzalisha makaa ya mawe iliibuka na kueleza kuwa Mkapa na mkewe hawana hisa eti kwamba walijitoa muda mfupi baada ya kugundua kuwa ilikuwa ikijiandaa kununua mgodi huo kwa bei ya kutupwa ya sh. milioni 700 (zililipwa 70 kwanza za kukopa kutoka Benki) wakati mgodi wenyewe ukiwa na gharama kubwa ya bilioni 4.

Mawakili sita wamejipanga kwa kazi hiyo, huku mmoja akiwa kutoka Afrika Kusini ambaye anaeleza kuwa mzoefu katika kesi zinazohusu kashfa kwenye vyombo vya habari.
 

Ohh...welcome Mr. Clean...anasubiri Balali afe ndio ainuke na kuongea...
 
mkiona chukizo la uharibifu likisimama PATAKATIFU (Ikulu) mjue ndio mwanzo wa utungu

Muungwana kaza buti kaka
 
Zaidi ya hapo inaelezwa kuwa magazeti yatakayoshikiwa bango ni Kulikoni, Thisday, Mwanahalisi, Mwananchi, Tanzania Daima, Majira na Mtanzania.
I see! Interesting. What if they come out with evidences?

Mtoa habari huyo aliyeona makabrasha ya mashtaka hayo ameeleza kuwa kila gazeti litadaiwa bilioni mbili; akieleza kuwa anadai kiasi hicho kwa kuwa angalau kinalinganalingana na hadhi yake ndani na nje ya nchi.
Hahaha hapa lazima atakuwa Bilionea wa nguvu! I wish I was him.
Hivi majuzi kampuni ambayo ilinunua mgodi wa Kiwira wa kuzalisha makaa ya mawe iliibuka na kueleza kuwa Mkapa na mkewe hawana hisa eti kwamba walijitoa muda mfupi baada ya kugundua kuwa ilikuwa ikijiandaa kununua mgodi huo kwa bei ya kutupwa ya sh. milioni 700 (zililipwa 70 kwanza za kukopa kutoka Benki) wakati mgodi wenyewe ukiwa na gharama kubwa ya bilioni 4.
Red & Bold texts...

Mawakili sita wamejipanga kwa kazi hiyo, huku mmoja akiwa kutoka Afrika Kusini ambaye anaeleza kuwa mzoefu katika kesi zinazohusu kashfa kwenye vyombo vya habari.
I see,,, hata magazeti haya yanaweza kuwapata mawakili zaidi wa kuyasimamia. Uzoefu katika kesi sidhani kama itakuwa tishio kwa magazeti haya.

Let's wait & see...
 
Sagga continue,ila hii wiki ni ya kutuliza mambo tu..na hasa hasa watu msiongelee suala la Balali.Bao lingine la kisigino.

Hivi tumerogwa??tunasahau mapema sana...kwa sasa habari za balali hazipewe nafasi tena..Kaanza mkapa sumaye jana na bado makamba ataongea wiki hii..CCM ni wajanja
 
wametengeneza cinema imekamilika:

Balali kafa

Kiwira mambo yameshakaa sawa

sasa lililobaki na kufunga midomo magazeti ili wasibugudhiwe kamwe
 
Mwaka huu inabidi tuwe makini sana hapa JF....
Sumaye amtetea Mkapa

2008-06-02 09:39:20
Na Mashaka Mgeta


Waziri Mkuu mstaafu, Bw. Frederick Sumaye, ameibuka na kuutetea utawala wa Rais wa Awamu ya Tatu, Bw. Benjamin Mkapa, kuwa uliharakisha maendeleo ya nchi na watu wake.

Kauli hiyo ya kwanza kutolewa na Bw. Sumaye, imekuja huku kukiwa na tuhuma nyingi zinazomkabili Bw. Mkapa, kutokana na madai ya matumizi mabaya ya madaraka alipokuwa rais.

Baadhi ya tuhuma hizo ni kuingia mikataba `feki` na makampuni ya uwekezaji, hasa katika sekta ya madini huku naye akidaiwa `kujiuzia` mgodi, ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ununuzi unaotia wasiwasi wa rada na ndege ya Rais, na madai ya kuwa na mkono katika menejimenti ya kigeni iliyokuwa inaendesha Tanesco, Net Group Solutions.

``Utawala wa Mkapa ulileta maendeleo kwa kasi kubwa sana, na nchi ilikwenda mbele kweli kweli,`` alisema Bw. Sumaye, alipozungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana.

Mkutano huo uliandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Tanzania Leo Limited, inayochapisha gazeti la Tanzania Leo, Bw. Venance Rwegoshora, kukanusha taarifa iliyochapishwa na gazeti hilo, toleo la Machi 31 hadi Aprili 6, mwaka juzi, kuwa Bw. Sumaye, anamiliki akaunti iliyopo nje ya nchi, ikiwa na Sh. Trilioni 10.

Bw. Rwegoshora, alisema baada ya mchakato wa hoja kati ya kampuni hiyo na Bw. Sumaye kushindikana kupitia usuluhishi wa Baraza la habari, suala hilo lilifikishwa mahakamani, ilipobainika kuwa habari hizo zilikuwa za uongo, zilitungwa, zikapotosha na kutokuwa na msingi wowote.

Kutokana na hali hiyo, Mahakama Kuu iliamuru kufanyika kikao cha usuluhishi kati ya pande mbili hizo, na kukubaliwa masuala kadhaa, ikiwemo Tanzania Leo kumlipa Bw. Sumaye fidia ya Sh milioni 100, zitakazolipwa kuanzia kipindi cha kabla ya Desemba Mosi mwaka huu hadi juni mwaka ujao.

Bw. Sumaye, alisema utendaji wa Serikali ya Mkapa, ulikuwa makini, uliozingatia maslahi ya nchi, ingawa kuna uwezekano wa kuwepo viongozi binafsi, waliokiuka misingi na maadili ya utumishi wao.

``Kama kuna viongozi waliokiuka maadili ya utumishi, hawawezi kuwa sababu ya kusema serikali ilishindwa. Tumeambiwa kuna uchunguzi unafanyika, tusubiri matokeo yake na wahusika watashughulikiwa,`` alisema.

Alisema uchunguzi unaofanyika dhidi ya vitendo vya ufisadi vinavyodaiwa kufanyika wakati wa utawala wa Bw. Mkapa, ambapo (Sumaye), alikuwa Waziri Mkuu, unawahusu watu binafsi na si utendaji wa iliyokuwa serikali ya awamu ya tatu.

Miongoni mwa hatua za kiutendaji alizozitetea Bw. Sumaye, ni ununuzi wa rada, iliyoligharimu taifa kiasi cha Sh. bilioni 70.

Alidai kwamba kabla ya ununuzi wake, ndege za kimataifa zilitishia kukatisha safari zake kutokana na kulazimika kuzunguka angani, ili zionekane na waongozaji ndege, kabla ya kuruhusiwa kutua.

``Kwa hiyo ununuzi wa rada ile ulikuwa uamuzi wa msingi na muhimu, sasa kama kuna watu walifanya madudu yao, wanapaswa kushughulikiwa,`` alisema.

Hata hivyo, watanzania wamekuwa hawapingi ununuzi wa rada hiyo, isipokuwa kilichowashangaza ni gharama kubwa ya rada hiyo ya kijeshi, huku ikisemekana kuwa Tanzania ilihitaji rada ya kawaida yenye gharama ndogo.

Licha ya kutoa tathmini hiyo kuhusu utendaji wa serikali ya Bw. Mkapa, waziri Mkuu mstaafu Sumaye, alikataa kuzungumzia utendaji wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete, kwa madai kuwa hana utaalamu wa kufanya hivyo.

``Kwa bahati mbaya, nilipokwenda kusoma Marekani, sikuchukua somo hili la tathmini, hivyo suala hilo tuziachie taasisi kama zile za Chuo Kikuu,`` alisema wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari.

Muda baada ya kumaliza kipindi cha uongozi akiwa Waziri Mkuu, Bw. Sumaye alijiunga katika Chuo Kikuu cha Harvard, nchini Marekani, ambapo alisomea masuala ya uongozi wa umma.

Akizungumzia fidia atakayolipwa na kampuni ya Tanzania Leo, Bw. Sumaye, alisema baada ya kutoa gharama zilizotumika kudai haki yake, sehemu ya `vijisenti` vitakavyobaki atavikabidhi kwa Jukwaa la Wahariri ili kufanya semina ya maadili ya uandishi kwa vyombo vya habari.

Alisema fedha nyingine atazipeleka kufanikisha miradi ya kuwawezesha wasichana wa kabila la Kimasai, kupata fursa zaidi za kujiendeleza kielimu.

Wakati huo huo, Bw. Sumaye, amesema hajiandai kuwania urais, baada ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete.

Bw. Sumaye ni miongoni mwa wanachama 10 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioshindana na Rais Kikwete kuwania nafasi ya kuteuliwa na chama hicho, kuwania urais mwaka 2005.

Wakati Bw. Sumaye akitoa tamko hilo, habari za ndani ya CCM zilinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari hivi, zikidai kuwapo wanasiasa waandamizi, wakiwemo waliowania uteuzi wa kugombea Urais mwaka 2005, kujipanga kushindana na Rais Kikwete, katika uteuzi wa kuwania kiti hicho mwaka 2010.

``Sijiandai kuwa Rais, kwanza sasa hivi tunaye Rais Kikwete tuliyemchagua, sasa hadi atakapotoka madarakani mwaka 2015 mimi niingie tena, yaani kama ni urais nikae miaka 10 mingine, nitapona kweli,`` alihoji bila kufafanua.

Alisema hivi sasa, anakamilisha mipango itakayofanikisha azma yake ya kuwa mwanaharakati wa kuwasaidia viongozi waliopo madarakani katika nchi za Afrika, kupambana na umaskini.

Aidha, Bw. Sumaye, alisema katika kipindi alichokuwa madarakani, hakuwahi kujihusisha na biashara za kimataifa wala kufungua akaunti nje ya nchi.

``Sikuwahi kuwa na akaunti hata ya Dola moja, ama isiyokuwa na fedha kabisa nje ya nchi, ndani ya kipindi chote nilipokuwa Waziri Mkuu,`` alisema wakati akijibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari.

Hata hivyo, alisema hivi sasa anamiliki akaunti moja nchini Marekani, aliyoifungua wakati alipokwenda kusoma katika Chuo Kikuu cha Harvard nchini humo.

Alisema bado anaendelea kuihudumia akaunti hiyo, kutokana na kuwa na shughuli mbalimbali anazozifanya na Chuo Kikuu hicho nchini Marekani, ambazo hata hivyo hakuzitaja.

Pia Bw. Sumaye, alisema hana hofu kuhusishwa na vitendo vya ukiukwaji wa maadili ya utumishi wa umma, akiwa msaidizi wa karibu wa Bw. Mkapa wakati wa utawala wa awamu ya tatu.

``Mkiniandika kama mnavyomwandika (Mkapa) andikeni tu, ali mradi muwe na taarifa za kweli, vinginevyo, hivi sasa mimi ni raia wa kawaida. Mkifanya hivyo kwa kunichafua, tutafikishana mahali pa kusafishana,`` alisema.

Bw. Sumaye, alitetea usiri unaoainishwa katika Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kwamba unasaidia kulinda utu wa mtu.

``Dunia hii kila mtu ana privacy yake (mambo binafsi), kama kuna wasiwasi na kiongozi fulani kuna vyombo vya uchunguzi kupata na kutumia zile taarifa, vinginevyo ukisema iwe kwa kila mtu, itakuwa vurugu,`` alisema.

Hata hivyo, alisema bado kuna haja ya kuangalia mapungufu yaliyopo katika sheria hiyo na kuyarekebisha kwa maslahi ya umma.

Tayari Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta, ameiagiza Kamati ya Kudumu ya Katiba, Sheria na Utawala, kuipitia sheria hiyo na kutoa mapendekezo ya uboreshaji wake.

Kwa upande mwingine, Bw. Sumaye alisema tuhuma dhidi ya ufisadi, zinazowakabili wanasiasa, zina athari kubwa katika maisha yao binafsi.

Alisema athari zake ni kubwa zaidi inapotokea tuhuma hizo `zimepandikizwa` na watu kwa maslahi yao binafsi.

``Hali ikiwa hivyo unaweza kujikuta kila unapopita unazomewa na pengine kupigwa mawe... Watu wakikuona wanasema huyo alikula fedha zetu,`` alisema.

SOURCE: Nipashe

http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/06/02/115635.html
 
Back
Top Bottom