Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 71
daktari ni wavivu wa kufikiri
Habari nilizozipokea sasa hivi kwa njia ya SMS kutoka kwa doctor mmoja pale Mhimbili zinasema hivi,nanukuu,"Hii ya sasa ni bab kubwa responce ni 100% MPAKA EMERGENCY,intern ndio wamemaliza kikao chao cha kupeana moyo na specialist ndio wanaanza Russian culture nw..together we can make it" mwisho wa kunukuu sms niliyoipokea.
My take; hivi serikali ina shindana na madaktari kwa ajili ya maslahi ya kisiasa? au inatakiwa kulinda afya za wananchi wake?
Maana kama mawaziri wamelalamikiwa na ni kweli wameshindwa kuwajibika kwa nini waendelee kuwepo hapo?na je inawezekanaje kupokea malalamiko ambayo kimsingi wao ndio wanalalamikiwa na kisha wakayafanyia kazi?
Nawasilisha wadau
ufinyu wa kufikiri....rais hawezi give up kirahisi namna anapgopa kuzarauliwa make akiwapiga chini kesho walim nao watataka minister wao ajiuzulu then; wafanya biashara, uchukuzi etc ila sie wa kipato cha chini tukubali tu yaishe
Madaktari wetu wanatumiwa na vyama vya siasa, mgomo huu ni wa kisiasa zaidi kuliko masilahi. Madaktari hawana uwezo wa kupanga baraza la mawaziri, kazi yao ni kutibu. Inanisikitisha sana kuona madaktari wetu wanafanya upuuzi kama huu.
Kama JK ndiye amewakatalia kujiuzulu basi amewaondolea utu na heshima mbele ya Watanzania na jumuiya ya wasomi Duniani. Nani atawaona ni watu tena? Nani atawaheshimu?Sikuwahi kuhisi kuwa Mponda na Nkya wanagharama kubwa hivi serikalini mpaka JK aliponionyesha.....
Wewe kwa kuwa si mvivu wa kufikiri ukakosa kuwa daktari, ukaamua kuwa gamba!!!daktari ni wavivu wa kufikiri
Hivi talanta anayo daktari tu? Mafisadi wao ndio wana talanta ya kuiba tu ndio maana wanaiba kila siku huku tukikaa kimya kwa kuwa wanatimiza wito wao?Hivi kiapo chao si ni kulinda maisha???? Sasa unalinda maisha ya wagonjwa kwa kuwaacha wafe? So kama Serikali haiwasikilizi, nani aanaathirika na mgomo huu, ni viongozi wa serikali kweli? Huyu Jack and Jill kakosa nini? Shame on you. Mwogopeni Mungu aliyewapa talanta yake na nyinyi mnaifukia!
How much?Kinachonishangaza ni jinsi ambavyo watu humu ndani wanona kuwa Madaktari wana haki kwa kila wanachokisema. Tunajua umuhimu wao katika jamii lakini wao wasijione kuwa bora kuliko watumishi wengine serikalini. How do you demand kwamba Waziri lazima aondoke na unataka kweli aondolewe? This is holding the government at ransom. walitaka Mtasiwa na KM waondoke wakaondoka, tena masikini KM akampoteza mama yake in the process. Ndugu zangu Madaktari, mgomo si suruhisho la kila kitu. Hebu fikiria roho za maskini wangapi wanakufa kwa sababu ya migomo yenu. Hamna hata Kwaresma nyinyi? Hiki mnachokifanya ni kwa manufaa ya nani kama sio nyinyi na matumbo yenu? Mna tofauti gani na mafisadi? I hate ufisadi lakini hili mnalolifanya ni well out of control and I will never support this. Doctors must be declared as enemy number one of the common mwananchi! Mkielezwa mnaanza kubwaga matusi humu, well sishangai kwani kama mnaruhusu watu kufa mahospitalini ili mifuko yenu itune, then matusi is just a drop of water in the indian ocean. As we stand, Doctors wanalipwa kuliko cadre yoyote serikalini; mnataka mlipwe kama wabunge????? For this one, doctors you sack!!!
taarifa zilizonifikia kutoka vyanzo vya kuaminiaka bugando wamebandika tangazo likisomeka hivi
"kutokana na serikali kutokuwa tayari kushughulikia madai ya madaktari ipasavyo sisi madaktari tumesikitishwa sana. Kuanzia leo tarehe 7 machi 2012 saa 2; 00 asubuhi,madaktari wa hospitali ya bugando tunasitisha kutoa huduma zote mpaka hapo serikali itakaposhughulikia madai hayo.
Jumuiya ya madaktari bugando (intern,registrars,residents)
nakala kwa wakuu wa idara,utawala bmc"
muhimbili
emd-kitengo cha wagonjwa wa dharura kimefugwa
opd-wagonjwa wamejaa lakini hawaoni
thetre hazifanyi kazi na maspecialist wapo russian culture to put last nail in the coffin
amana
total tools down
temeke
total tools down
mbeya
wanaendelea pale walipoishi maana mgomo kama kawa
ifakara
total tools down
kcmc
madaktari kutoa tamko muda si mrefu
ikulu kuna mkutano mkubwa unaendelea nitato updates bdae
Mob psychology ime wa-affect madaktari wetu. Natoa ushauri kila mmoja atafakari ni nini anachogomea hasa kama yeye binafsi bila kutegemea vikao vyao wanavyokaa kupeana molali! Kama ni maslahi yake hayajatekelezwa au ni kuto kujiuzuru kwa mawaziri au vyote viwili. Na ukiangalia dai la kuto kujiuzuri/kutowajibishwa mawaziri imemeza madai yao yote ikiwemo ya masilahi yao. Sasa wawe makini katika madai yao wasije wakawa wanatumiwa na kundi fulani bila kujijua? na hii ndio madhara ya mob psychology. Nawashauri waonane na wataalam wapate ushauri?
Mara tu baada ya uchaguzi mkuu kumalizika na Jakaya kuingia Ikulu, chama fulani cha siasa kilitangaza kwamba kitahakikisha nchi yetu haitawaliki tena. Hivyo sintashangaa kuona haya yanayotokea. Lakini wanaokufa kwa kukosa huduma za madaktari si CCM pekee yetu bali Watanzania wote.
Mpaka kieleweke.....JK atakimbia Magogoni.