Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Mkuu JMUSH,

Taratibu na shule za watu mkuu.Mmeku na mimi nitakupa siku saba u-withdrawal statement yako ya kuhusisha utumbo wowote na Galanos.Kwi kwi!

P Diddy alisema chuo na kila mtu anajuwa ndugu Zitto alisoma mlimani...Masatu akaleta utani wake wa ki ccm akasema ni madrassa...Sasa na mimi nikajiuliza labda amechanganya Galanos ama Usagara..I ama not sure lakini nadhani Zitto alisomea kati ya shule hizo huko Tanga.
So huna haja ya kunipa siku saba kuhusiana na utumbo wowote ule.
 
Hili suala la kuanza ugomvi na Mengi, Masha atalijutia for a long time.

Countdown inaendelea..... tik tak tik tak tik tak tik tak..................
 
Hela za UFISADI ni kama kula Nyama ya MTU. Kuna VIONGOZI ni akina RAMA MLA WATU wa hela za Watanzania ila hawajajijua tu. Kibaya zaidi ukiwakamata wanalalamika na kuanza kudai "nirudishie kichwa changu....."
Masha kaniangusha sana. Nilishaanza kujenga imani kubwa sana kwake. Tulitegemea atamuonyesha mfano Zitto nini maana ya kulifanyia kazi taifa. Nilitegemea aonyeshe mapenzi kwa nchi yake kuzidi Dr. Slaa (sala ya Tanzania). Nakubaliana na watu wanaosema kuwa "kama haya angelisema Kingunge au Mramba, tusingeliona BIG DEAL". Ila kwa Masha, inauma sana kugundua kumbe hata angelikuwa Rais, ndiyo tungelikuwa tumeleta Mugabe wetu Tanzania.
Najua kuwa hata akiacha Uwaziri, bado ataendelea kula KUKU. Ila mtu asikudanyanye. Hawa watu kama PESA wanazo. Kinachowasumbua zaidi ni POWER. Kama mtu haamini basi kamuulizeni Mkapa, Yona au Mramba, nini maana ya kukosa POWER. Wanasema, ukiona wanaume wanagombana ujuwe ni vitu vitatu tu "sex, money and Power..". Ndiyo maana huu ugomvi mkubwa. Mengi ana pesa, Masha ana Power. And the winer is ........ ohh, subiri kwanza, Mengi hana power? Mhhh, media nayo ni 0.5 Power, .................
 
Hebu Tujadili Hatua (kama zipo) ambazo Waziri Masha anaweza kumchukulia Mengi kama alivyoahidi bila kuvunja sheria.

Mimi naona moja au mbili tu...kumtegea Gazeti lake lichemke kisha walifungie. Au kumsingizia anauza bithaa feki (kama alivyofanyiwa Bakhresa na ngano yake mwaka 1996). Wadau kuna lingine ndani ya uwezo wa Waziri Masha analoweza kumfanyia Mr Mengi na IPP?
 

Hebu Tujadili Hatua (kama zipo) ambazo Waziri Masha anaweza kumchukulia Mengi kama alivyoahidi bila kuvunja sheria.

Mimi naona moja au mbili tu...kumtegea Gazeti lake lichemke kisha walifungie...

Yebo Yebo

Masha hahitaji kumtega Mengi na magazeti yake. Ameshasema ameharibu tayari kwa kutumia vyombo vyake vya habari kuleta hatari.

Hilo jambo nadhani tumelikosa katika huu mtafaruku mzima, kwa sababu, kwanza, wamali wa Waziri walikuwa wanatupurukusa, wanatu distract, kwa kusema tumshukuru kwa kurudi nchini kututumikia. Hilo nadhani tumelijibu, tumelimaliza. Lakini sababu nyingine ya kupurukuswa na kushindwa kuangalia vina vingine vya sakata hili ni kwamba sidhani kama tulikuchunguza sana kilichotamkwa na Masha hasa hasa:

``Hizi ni tuhuma nzito...Unapoituhumu serikali na unapomtuhumu waziri, ni lazima uwe na uthibitisho….Siyo tu aendelee kueleza hivi hivi tu, aje na amseme waziri huyo ni nani; na aje na ushahidi. Asipothibitisha tutamchukulia hatua.´´

``...Uhuru wa vyombo vya habari si kuvitumia kutangaza vitu ambavyo vinaleta athari katika jamii, hivyo tutaliangalia suala hilo na mimi kama waziri ninayesimamia usalama ndani ya nchi, ninawajibika moja kwa moja katika jambo hili´´

``…Asipoleta ushahidi wake ndani ya siku saba, serikali ina wanasheria wake, watapitia sheria zinasemaje ili ichukue mkondo wake hawezi kutoa madai mazito eti kwa vile ana vyombo vya habari, ni hatari...´´

``...Asitumie vyombo vya habari kutoa tuhuma kwa serikali. Ni kweli serikali inatambua kuwa kuna uhuru wa vyombo vya habari, ingawa uhuru hauna budi kutumiwa ipasavyo na si kutoa taarifa zisizo sahihi. Hii ni serikali si serikali ya kuifanyia mchezo.´´

``…Kama ni kweli Mengi ametumiwa ujumbe wa maneno ya kumtishia kuuawa, anatakiwa kuwa mkweli na muwazi huku akiwa na vithibitisho. ...madai yake ni mazito lakini kwa sababu ana ushahidi wa kuhujumiwa na waziri mmoja kijana, tutamuomba atupe ushahidi wa kuhujumiwa na waziri mmoja kijana, na leo namuandikia barua ili atulete.´´

Sasa, ukiweka pembeni utetezi ulioletwa na rafiki wa utotoni wa Waziri, wakitubeza tushukuru amerudi nyumbani kututumikia, na pia tukiahirisha maswali juu ya unyuma wa Waziri kuhusu alivyoweza kukwepa kujiunga JKT kabla ya chuo kikuu, tena akiwa na madarasa ya shule 10 badala ya 13 kama wengine, nadhani baadhi ya maswali na makamio dhidi ya hatua yake hii yana majibu ndani ya alichosema.

Kuna hili la Masha amemlenga Mengi kama nani, raia ? Utaona Masha kasema tatizo hapa ni kwamba mlengwa anatumia penyenye aliyonayo na vyombo vya habari kusema vitu vya kichochezi. Kwa hiyo Mengi hapa hajalengwa kama raia, na pia hapo hapo kuna jibu la swali la kosa ni nini hasa: uchochezi.

Hilo la kwanza na pili. La tatu ambalo limejibiwa hapo ni hili la usahihi wa nguvu yake kuhusika hapa: kasema usalama uko chini yake. Kwa hiyo maswali ya wakuu wengi hapa kwamba itakuwaje hawakuachiwa ma DPP na ma IGP na AG na wakuu wa tarafa na shina waongee hilo Masha kashasema usalama uko chini yake. Watume mkuu wa kituo au mkuu wa magereza, au mkuu wa kaya ya Wakwere, wote hawa ni eneo chini ya himaya ya usalama. Mkuu wa masuala ya usalama, kama alivyosema, ni yeye.

Kama ambavyo Mkuchika alichukua mikononi swala la uchochezi wa magazetini kama mkuu wa masuala ya uchapishaji habari, hapa Masha anachua mikononi swala la shutuma za kichochezi zinazohusiana na kutishia usalama wa raia yeye akiwa kama mkuu wa mambo ya usalama wa raia.

Kwa hiyo kosa ni uchochezi wa mwanahabari, mmiliki wa vyombo vya habari, Mengi. Kumbuka Mengi amechapisha matamko yake - hakunukuliwa na mwingine, na third party - yeye mwenyewe amechapisha, ametoa tamko ndani ya gazeti lake.

Hivyo ndivyo Masha atakavyomshitaki mchapishaji Mengi, nadhani. Hatahitaji kumtega tena.
 
wandugu,

..mpaka sasa hivi nashangaa kwamba waandishi wa habari hawajamuuliza Reginald Mengi kama alifikisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu au Raisi. zaidi, kama alifikisha malalamiko yake kwa wakubwa hao, alipata response gani?

..vinginevyo napata matatizo na Mengi kuendelea kufanya identity ya aliyemtishia maisha kuwa ni siri. Mengi lazima aelewe uzito wa nafasi yake ktk jamii ya Watanzania.

..kwa madai haya ya Mengi jamii inaweza kuwahisi vibaya Mawaziri wote vijana ktk cabinet ya Kikwete. tena kuna uwezekano hata wale "wazee-vijana" nao wakaanza kuhisiwa vibaya.

..binafsi napenda Waziri aliyemtishia maisha Reginald Mengi ajulikane na achukuliwe hatua za kisheria. naamini Waziri huyo ana kesi ya jinai ya kujibu.
 
wandugu, ..mpaka sasa hivi nashangaa kwamba waandishi wa habari hawajamuuliza Reginald Mengi kama alifikisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu au Raisi. zaidi, kama alifikisha malalamiko yake kwa wakubwa hao, alipata response gani?

Kuna namna nyingi za kufikisha malalamiko kwa hao wakuu na mojawapo ya uwazi na ukweli ni huu aliotumia Mengi. Hata sisi humu ndani kwa tunatumia JF na ninaamini tunafikisha ujumbe si kwa serikali tu bali kwa watanzania wote. Njia nyingine na ailyoitumia Mengi ni kulifikisha hili swala polisi na anadai alifanya hivyo. Sasa hapa sijui tatizo lako ni nini ?

..vinginevyo napata matatizo na Mengi kuendelea kufanya identity ya aliyemtishia maisha kuwa ni siri. Mengi lazima aelewe uzito wa nafasi yake ktk jamii ya Watanzania.

Kama bado una matatizo basi sijui unataka kifanyike kitu gani. Mh. Zitto, MP keshamtaja au una tatizo kuhusu nafasi ya Mbunge na mfanya biashara katika jamii ya Watanzania ?

..kwa madai haya ya Mengi jamii inaweza kuwahisi vibaya Mawaziri wote vijana ktk cabinet ya Kikwete. tena kuna uwezekano hata wale "wazee-vijana" nao wakaanza kuhisiwa vibaya.

'The guilty are always afraid' Naamini anayejihisi amekwisha kujianika kwa matendo na matamshi yake. Kama ni kuhisiwa tu binafsi nawahisi asilimia kubwa tu ya mawaziri wetu kuwa wanajihusisha na vitendo vya aibu visivyo na maslahi kwa taifa including mwenye kaya.

..binafsi napenda Waziri aliyemtishia maisha Reginald Mengi ajulikane na achukuliwe hatua za kisheria. naamini Waziri huyo ana kesi ya jinai ya kujibu.

Well ameshajulikana - swali ni nani amchukulie hatua za kisheria kama mkuu wa maafande kisha kuwa mtuhumu, mtuhumiwa, mshitaki, mwendesha mashtaka na hakimu vyote kwa pamoja. Halafu eti kasomea sheria na kawahi kufanya kazi WB

My take - Kwa siku hizi mbili nimekuwa nje ya ukumbi na duh malumbano si malumbano !! Nawashukuru wote mliosimama kidete kuita koleo koleo na kumkoma nyani - kwa kuwa mwisho wa siku mchele na pumba hujitenga taratibu na kilaini. Asante Kuhani, Fundi Mchundo, Yo yo, mama, jmushi1 na wengine wote ambao sikuwataja for taking a lead role in getting to bottom of this saga. Kama nilivyosema awali hivi vita dhidi ya mafisadi si lelemama na wengine humu tutajikuta tunatumiwa bila kujua na hili linasikitisha. Kazi kweli kweli.
 
Mag3,

..sintopenda kumhusisha Zitto Kabwe ktk sakata hii. namesoma alichokisema lakini nadhani ili kutu-complicate suala hili ni vizuri tukaiacha kauli yake kama ilivyo.

..Mengi ndiye anapaswa kumtaja Waziri aliyemtishia maisha. kama amepeleka taarifa polisi that is good step. sasa maadam ameamua kuushirikisha umma ktk matatizo yake, basi ni bora akawa open zaidi kwa kutueleza ushahidi aliowapa Polisi, na hatua ambazo Polisi wamemwambia watachukua, na stage waliyofikia.

..kwetu sisi tunaoamini katika haki na utawala wa sheria Waziri aliyemtishia Mengi bado hajajulikana. zaidi ikiwa Mengi atamtaja itabidi hatua za uchunguzi zifuatwe ili kubaini kama ni kweli anahusika na kupanga hujuma dhidi ya Mengi.

NB:

..Waziri yeyote atakayetajwa na Mengi atapaswa kujiuzulu nafasi yake, ili uchunguzi ufanyike kwa haki na uwazi.
 
I can't wait for wednesday/thursday when the Masha ultimatum expires and he does nothing.

This is chess not checkers Masha.
 
Asante...... mama...., na wengine wote ambao sikuwataja for taking a lead role in getting to bottom of this saga.


Mama hastahili asante, hakuna substance yeyote aliyocontribute zaidi ya kutoa thanks. Hivyo basi naungana na wewe kuwashukuru wote waliochangia mjadala huu.
 
CHADEMA yanunua kesi ya Mengi, Masha
• Mbowe ashtuka Masha kumtisha Mengi


na Edward Kinabo




CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeinunua kesi ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, dhidi ya Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, kwa kusisitiza kuwa kina ushahidi kutoka kwenye vikao nyeti vya serikali kuwa waziri huyo kijana ndiye aliyepeleka hoja ya kutaka mfanyabiashara huyo afilisiwe.

Hali hiyo ilibainishwa jana na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Mbowe aliithibitishia Tanzania Daima kwamba chama chake kina ushahidi wa kuaminika kutoka kwenye vikao nyeti vya serikali kwamba Waziri Masha ndiye aliyeishauri serikali ipange mkakati wa kumfilisi Mengi kwa lengo la kuvidhoofisha vyombo vyake vya habari visiendelee kuibua na kuandika habari zinazohusu ufisadi.

Alisema mwelekeo wa suala hili unamnyima Waziri Masha haki ya kuzungumza na hapaswi kujitetea wala kusema chochote zaidi ya kuviachia vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi yake kwa uhuru.

"Kitendo cha Waziri Masha kumpa Mzee Mengi amri ya kuwasilisha ushahidi ndani ya siku saba kinashangaza, kwani Waziri huyo hana mamlaka kisheria ya kudai ushahidi na badala yake chombo chenye mamlaka ya kudai ushahidi ni mahakama," alisema Mbowe. Mwenyekiti huyo alisema kama serikali inaona imeonewa au imechafuliwa katika suala hilo, iende ikashitaki mahakamani na si vinginevyo.

"Waziri hana mamlaka ya kisheria ya kudai kupelekewa ushahidi. Chombo chenye mamlaka hayo ni mahakama. Kama wao (serikali) wanaona wameonewa au wamechafuliwa waende mahakamani, kama ni uongo waende wakashtaki kama walivyokimbilia mahakamani kwenye sakata la mgomo wa walimu," alisisitiza Mbowe.

Kwa mujibu wa Mbowe, Waziri Masha ameendeleza rekodi ya mawaziri wengine wa Serikali ya Awamu ya Nne ya kupenda kukurupuka na kupayuka hovyo bila kutafakari kwa makini na matokeo yake ni kuvuka mipaka ya mamlaka waliyonayo.

"Na hii imekuwa ni tabia ya Mawaziri wa Kikwete ya kukurupuka na kupayuka hovyo bila kutafakari kwa umakini hadi wanavuka mipaka ya mamlaka yao. Waziri hana mamlaka ya kudai apelekewe ushahidi……hiyo ni kazi ya mahakama," alisema Mbowe.

Alisema mtu au chombo chochote kinachopinga ufisadi kinahitaji kulindwa kwa gharama yoyote badala ya kutishwa na serikali.

Aliitaka serikali kutumia vyombo vyake kufanya mambo ya maana na yenye maslahi kwa taifa . "Serikali itumie vyombo vyake kufanya mambo ya maana na yenye maslahi kwa taifa. Jambo hili la kumfilisi Mengi halina tija. Serikali inataka kuwawajibisha wananchi badala ya wananchi kuiwajibisha serikali. Serikali iache mchezo wa kutisha raia wake, iache kuwahujumu raia wa nchi. Jukumu la serikali ni kupambana na uhalifu si kufanya uhalifu dhidi ya raia wake wema," alisema Mbowe.

Alisema inasikitisha kuona serikali inataka kumshughulikia Mengi kwa kumfilisi bila kujali mchango mkubwa wa vyombo vyake vya habari na biashara katika kupambana na ufisadi na kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Alionya kuwa iwapo serikali itamfilisi Mengi kama alivyopendekeza Waziri Masha, uchumi utaathirika kwa pato la taifa kushuka kwa sababu itapoteza mapato ya kodi zinazotozwa kwenye makampuni ya mfanyabiashara huyo.

"Kumfilisi Mengi ni kuathiri ajira….hata uchumi wa nchi unaweza kuathirika. Ni wananchi wangapi wameajiriwa kwenye makampuni yaliyo chini ya Mengi…….Watanzania wengi watapoteza ajira. Pato la taifa linaweza kushuka…..serikali itapoteza mapato ya kodi inayopata kutoka kwenye makampuni anayoyamiliki Mengi. Serikali iache mchezo wa kushugulikia raia wake na kudai kuwa inawalinda," alitahadhalisha Mbowe.

Juzi Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe, alisema ana ushahidi kuwa Waziri Masha, ndiye aliyepeleka hoja ya kumhujumu Mengi katika vikao vya juu vya serikali.

Zitto alisema yeye hana sababu ya kumtetea Mengi ila hawezi kunyamaza kuona Mtanzania anayeipenda nchi yake na kulazimika kupinga ufisadi, anafanyiwa hujuma. Naye Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa, jana alinukuliwa na vyombo kadhaa vya habari akimtaka Waziri Masha kuviacha vyombo vya upelelezi vifanye uchunguzi wake.

Kuibuka kwa sakata hilo kunatokana na Mengi kumtuhumu Waziri mmoja kuwa ameagiza abambikiwe kodi bandia ya kiasi kikubwa atakachoshindwa kulipa ili hatimaye afilisiwe.

Mengi akizungumza na vyombo vya habari wiki iliyopita, alimtuhumu waziri huyo ambaye hakumtaja jina, kuwa amekuwa akitumiwa ujumbe wa vitisho kutokana na vyombo vyake vya habari kuwa mstari wa mbele katika kupinga ufisadi.

Kutokana na hatua hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, kupitia mkutano wake na waandishi wa habari, alimpa Mengi siku 7 awe amekwisha wasilisha vielelezo vya kuthibitisha madai yake kwake yeye (Masha), vinginevyo atamchukulia hatua za kisheria.

Akijibu amri ya Masha, Mengi alisema yupo tayari kutupwa jela ikithibitishwa kuwa amedanganya na kumwomba Masha pia aseme kama atakuwa tayari kujiuzulu iwapo ukweli utathibitika.

Hata hivyo juzi jumapili, Masha alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa hayuko tayari kujiuzulu kwa sababu nia yake ya kuwaagiza polisi kufanya uchunguzi inalenga kumlinda Mengi.

Alisema kutokana na taarifa ambayo Mengi aliipeleka kituo cha polisi cha Oysterbay, polisi wameamua kuifanyia uchunguzi ili kuhakikisha maisha yake yanakuwa salama.

Alisema, hata kama hawamuamini, basi waupeleke huo ushahidi kwa Rais au Waziri Mkuu kuuonyesha na kama ikibainika kama ni kweli yeye ndiye anayemhujumu Mengi, basi atajiuzulu.

Alidai kuwa yeye hakusema kuwa atamshughulikia Mengi kama alivyonukuliwa kwenye baadhi ya magazeti ila alisema kuwa sheria itachukua mkondo wake kama ikibainika kuwa tuhuma zilizotolewa ni za kweli.
 
CHADEMA yanunua kesi ya Mengi, Masha• Mbowe ashtuka Masha kumtisha Mengi


na Edward Kinabo




CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeinunua kesi ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, dhidi ya Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, kwa kusisitiza kuwa kina ushahidi kutoka kwenye vikao nyeti vya serikali kuwa waziri huyo kijana ndiye aliyepeleka hoja ya kutaka mfanyabiashara huyo afilisiwe.

Hali hiyo ilibainishwa jana na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Mbowe aliithibitishia Tanzania Daima kwamba chama chake kina ushahidi wa kuaminika kutoka kwenye vikao nyeti vya serikali kwamba Waziri Masha ndiye aliyeishauri serikali ipange mkakati wa kumfilisi Mengi kwa lengo la kuvidhoofisha vyombo vyake vya habari visiendelee kuibua na kuandika habari zinazohusu ufisadi.

Alisema mwelekeo wa suala hili unamnyima Waziri Masha haki ya kuzungumza na hapaswi kujitetea wala kusema chochote zaidi ya kuviachia vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi yake kwa uhuru.

“Kitendo cha Waziri Masha kumpa Mzee Mengi amri ya kuwasilisha ushahidi ndani ya siku saba kinashangaza, kwani Waziri huyo hana mamlaka kisheria ya kudai ushahidi na badala yake chombo chenye mamlaka ya kudai ushahidi ni mahakama,” alisema Mbowe. Mwenyekiti huyo alisema kama serikali inaona imeonewa au imechafuliwa katika suala hilo, iende ikashitaki mahakamani na si vinginevyo.

“Waziri hana mamlaka ya kisheria ya kudai kupelekewa ushahidi. Chombo chenye mamlaka hayo ni mahakama. Kama wao (serikali) wanaona wameonewa au wamechafuliwa waende mahakamani, kama ni uongo waende wakashtaki kama walivyokimbilia mahakamani kwenye sakata la mgomo wa walimu,” alisisitiza Mbowe.

Kwa mujibu wa Mbowe, Waziri Masha ameendeleza rekodi ya mawaziri wengine wa Serikali ya Awamu ya Nne ya kupenda kukurupuka na kupayuka hovyo bila kutafakari kwa makini na matokeo yake ni kuvuka mipaka ya mamlaka waliyonayo.

“Na hii imekuwa ni tabia ya Mawaziri wa Kikwete ya kukurupuka na kupayuka hovyo bila kutafakari kwa umakini hadi wanavuka mipaka ya mamlaka yao. Waziri hana mamlaka ya kudai apelekewe ushahidi……hiyo ni kazi ya mahakama,” alisema Mbowe.

Alisema mtu au chombo chochote kinachopinga ufisadi kinahitaji kulindwa kwa gharama yoyote badala ya kutishwa na serikali.

Aliitaka serikali kutumia vyombo vyake kufanya mambo ya maana na yenye maslahi kwa taifa . “Serikali itumie vyombo vyake kufanya mambo ya maana na yenye maslahi kwa taifa. Jambo hili la kumfilisi Mengi halina tija. Serikali inataka kuwawajibisha wananchi badala ya wananchi kuiwajibisha serikali. Serikali iache mchezo wa kutisha raia wake, iache kuwahujumu raia wa nchi. Jukumu la serikali ni kupambana na uhalifu si kufanya uhalifu dhidi ya raia wake wema,” alisema Mbowe.

Alisema inasikitisha kuona serikali inataka kumshughulikia Mengi kwa kumfilisi bila kujali mchango mkubwa wa vyombo vyake vya habari na biashara katika kupambana na ufisadi na kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Alionya kuwa iwapo serikali itamfilisi Mengi kama alivyopendekeza Waziri Masha, uchumi utaathirika kwa pato la taifa kushuka kwa sababu itapoteza mapato ya kodi zinazotozwa kwenye makampuni ya mfanyabiashara huyo.

“Kumfilisi Mengi ni kuathiri ajira….hata uchumi wa nchi unaweza kuathirika. Ni wananchi wangapi wameajiriwa kwenye makampuni yaliyo chini ya Mengi…….Watanzania wengi watapoteza ajira. Pato la taifa linaweza kushuka…..serikali itapoteza mapato ya kodi inayopata kutoka kwenye makampuni anayoyamiliki Mengi. Serikali iache mchezo wa kushugulikia raia wake na kudai kuwa inawalinda,” alitahadhalisha Mbowe.

Juzi Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe, alisema ana ushahidi kuwa Waziri Masha, ndiye aliyepeleka hoja ya kumhujumu Mengi katika vikao vya juu vya serikali.

Zitto alisema yeye hana sababu ya kumtetea Mengi ila hawezi kunyamaza kuona Mtanzania anayeipenda nchi yake na kulazimika kupinga ufisadi, anafanyiwa hujuma. Naye Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa, jana alinukuliwa na vyombo kadhaa vya habari akimtaka Waziri Masha kuviacha vyombo vya upelelezi vifanye uchunguzi wake.

Kuibuka kwa sakata hilo kunatokana na Mengi kumtuhumu Waziri mmoja kuwa ameagiza abambikiwe kodi bandia ya kiasi kikubwa atakachoshindwa kulipa ili hatimaye afilisiwe.

Mengi akizungumza na vyombo vya habari wiki iliyopita, alimtuhumu waziri huyo ambaye hakumtaja jina, kuwa amekuwa akitumiwa ujumbe wa vitisho kutokana na vyombo vyake vya habari kuwa mstari wa mbele katika kupinga ufisadi.

Kutokana na hatua hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, kupitia mkutano wake na waandishi wa habari, alimpa Mengi siku 7 awe amekwisha wasilisha vielelezo vya kuthibitisha madai yake kwake yeye (Masha), vinginevyo atamchukulia hatua za kisheria.

Akijibu amri ya Masha, Mengi alisema yupo tayari kutupwa jela ikithibitishwa kuwa amedanganya na kumwomba Masha pia aseme kama atakuwa tayari kujiuzulu iwapo ukweli utathibitika.

Hata hivyo juzi jumapili, Masha alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa hayuko tayari kujiuzulu kwa sababu nia yake ya kuwaagiza polisi kufanya uchunguzi inalenga kumlinda Mengi.

Alisema kutokana na taarifa ambayo Mengi aliipeleka kituo cha polisi cha Oysterbay, polisi wameamua kuifanyia uchunguzi ili kuhakikisha maisha yake yanakuwa salama.

Alisema, hata kama hawamuamini, basi waupeleke huo ushahidi kwa Rais au Waziri Mkuu kuuonyesha na kama ikibainika kama ni kweli yeye ndiye anayemhujumu Mengi, basi atajiuzulu.

Alidai kuwa yeye hakusema kuwa atamshughulikia Mengi kama alivyonukuliwa kwenye baadhi ya magazeti ila alisema kuwa sheria itachukua mkondo wake kama ikibainika kuwa tuhuma zilizotolewa ni za kweli.
 
"Alisema, hata kama hawamuamini, basi waupeleke huo ushahidi kwa Rais au Waziri Mkuu kuuonyesha na kama ikibainika kama ni kweli yeye ndiye anayemhujumu Mengi, basi atajiuzulu."


The million dollar question hapa ni je waziri masha ataiheshimu hii kauli yake siku ya siku?...
 
Ati kwa JK tena? Mimi naona hata Shein anaweza kuchukua uamuzi wa busara kwenye hili kuliko Jk,yaani ile hofu ya shein tu,inatosha kumlazimisha shein atende haki kwa kupaniki.Lakini Jk itaku ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu
 
CHADEMA wanafuatilia mjadala huu hapa JF kwa makini sana inaonekana.
 
Mzee FMES, mimi nakubaliana na wewe kwamba saga la EPA halijaanza jana. Lakini nataka tuangali reaction ya Mh. Masha pindi waandishi wanapotaka kuangalia kama ana skeleton kwenye closet.

Kwanza unakumbuka kuhusu yeye kulitishia gazeti ambalo liliripoti ajira ya Ridhiwani na IMMA, wakati ule yeye alikuwa ashajiuzulu kuifanyia kazi IMMA.

Leo hii tunaona movement yake ya chinichini ya kutaka kuziba mdomo IPPMEDIA. Nadhani huitaji kuwa msoma mashitaka ndio ujue kwamba mshika kibendera atakiwa anyooshe bendera yake.

Sijasema Masha anahusika na EPA moja kwa moja, sema nimesema hii reaction yake inasababisha nirecall maamuzi yangu ya mwisho kwamba Masha hausiki na EPA. Ninachotaka kuona ni more scrutiny kwa Mh. Masha.

- Sikiliza mkuu, sitetei anything foolish kutoka Lau, kama waziri lakini siwezi kumhukumu kwa kumchukia bila sababu za msingi majungu na unafiki, kama kuna ukweli wa kuhusu kuhusika kwa Lau na EPA, basi uwekwe ukithibitishwa nitakua wa kwanza kusema wazi kwamba ajiondoe, lakini sio maneno ya mitaaani yasiyokwisha, ambayo yalianza kabla hata mimi sijazaliwa na majungu ya viongozi.
 
Kwa vile zimebaki siku tatu tu kufikia kikomo cha siku saba zilizotolewa na Waziri Masha, nadhani wakati huu tusisumbuke kutafuta historia za key-players wa hii saga; badala yake, tusubiri siku hiyo ifike ili ukweli uanze kutolewa. Tukitaka kujadili historia zao, ni afadhali tuanzishe thread nyingine kule kenye folder ya Celebrities.

Nina imani kuwa kambi ya Masha inajiandaa vya kutosha kuhakikisha kuwa Mengi anakiona cha moto asipotoa ushahidi ndani ya siku saba, na kambi ya Mengi nayo inajitahidi kukusanya ushahidi wa kuthibitisha madai yao. Nadhani kambi hizo mbili zitakapoanza kupambana kwa facts ndipo mjadala utakapokuwa na maana kwa watanzania wote kwani mvutano huo unahusu maslahi ya demokrasi, utawala bora na utii wa sheria kwa watanzania wote. Kumtetea au kumponda mtu kutokana na matendo ama tabia yake ya zamani hakusaidii lolote katika mjadala huu kwa sasa hivi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom