Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,292
- 10,391
- Lakini ukamuhakikishia uwaziri Tanzania, sasa tofauti iko wapi?
Haujui tofauti ya World bank na uwaziri wa Tanzania? Yeyote yule, ili mradi awe raia wa Tanzania na atimize masharti husika anaweza kuwa waziri. Hakuna interview wala kuambiwa upeleke reference kwenye uwaziri wa Tanzania. Ile ni political post. Rais wa Jamhuri ya Tanzania ana mamlaka yote ya kumpa yeyote yule anayemuona atamfaa uwaziri. Hakuna kwenda kuomba kibali cha bunge wala nini.
World Bank wanaangalia uwezo wako kitaaluma. Kuna viwango unavyotakiwa kutimiza ( elimu, uzoefu wa kazi n.k.).Unafanyiwa interview. Unaombwa ushahidi wa uliyoyadai katika maombi yako. Mara nyingi mnagombea wengi. Kinachozingatiwa ni nani katika waombaji ndiye anayekidhi zaidi mahitaji ya taasisi ya World Bank ( si ya rais wa WB). Huyu ndiye anayechaguliwa. Bahati mbaya umeneja wa Amusement Park si moja ya sifa zinazotakiwa katika World Bank. Unadhani huo umeneja unaoutetemekea ungekuwa na maana angeacha kuuweka kwenye C.V. yake? Mtu ambaye ameweka hata shule ya msingi aliyesoma!
Bottom line ni kuwa Masha hajawahi kuajiriwa World Bank. Kwa hiyo hajawahi kuacha kazi World Bank kama ulivyotaka kutuingiza mkenge.
- At best irrelevant na chuki pamoja na wivu, nothing new kwa wale tunaelewa vizuri.
Don't flatter yourself. Chuki na wivu viko wapi katika haya niliyoyasema? Kwa nini nikuchukie au nikuonee wivu mtu ambae simjui? Kwa sababu ulikuwa unamwendesha Masha? Kwa sababu unamjua Masha? Kitu gani hasa kinakufanya uamini kuwa Fundi Mchundo anakuonea wivu?
Ulichotaka tuamini kimeonekana si kweli. Basi kuwa mtu mzima na kubali kuwa uliteleza. Kilio chako kuwa haupendwi na unachukiwa haki-hold water anymore. Tetea hoja yako au nyamaza. Ni hicho tu.