Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

mwanasiasa,
naona jamaa anamuota "Jasusi"!!

Jasusi, ulimfanya nini huyu ndg?
 
Hapo ndipo mtajua kwamba Mzee Ndesa si mbabaishaji sasa .CCM wanaanza kuumana ni kazi kubwa .
 
mzee Ndesamburo,ulidhani unazima moto,kumbe ulikuwa ndio unaumwagilia petrol,je una semaje?kama kamati ilihongwa ina maana bunge limehongwa,na wewe ukaamua kwa mihasira yako kujitoa katika kamati,ambapo ungewaku ndani ya kamati unge stand better chance ya kutetea,kwa hoja ya ko ya kamati amabo ni bunge kuhongwa kwanini basi hata katika hilo bunge lenyewe usijiuzuru?kuonyesha kuwa bunge lenyewe wala rushwa?niliuliza siku moja je wewe mwenyewe katika kugombea ubenge huku honga?au katika hiyo kamati na wewe hukuvuta?Ushahidi wa tape upo acha zionyeshwe,ndipo utakapoona kuwa ni wazi kuwa ulikuwa unatetea kwa kutumia uchagga wako,wachagga ache kutugawa,wewe ndesamburo wakati Mengi anatoa kanda yake ya uongo wa kutumia dakika chake si ulikuwepo?Na Adam Malima alipoonyesha kanda ambayo ni the same na ya Ndesamburo si uliona?Ipi ilikuwa ya Uongo?Jibu ni kuwa ya Mengi ilifanyiwa EDITTING nyingi kupunguza muda,Mengi tukubali tusikubali anatumia vyombo vyake VIBAYAAAAAAA!!!

Watu wengine walizaliwa bila aibu, hawajali kama wanaandika hoja za kipuuzi na kuziweka hadharani. Au kwa sababu hawatumii majina yao? Na hawa ndio wanaojitapa kwa hili na lile, eti wasomi! Ona thinking capacity yake. Mzee wa London kweli amedhalilisha ubongo wake...Yaani haoni mantiki ya kitendo cha Ndesa? Shit!
 
Ni uoga wa jina maana anadhani Jasusi ni kijana wa RO hapa JF. Hapa vijana wa RO ni kama TTJ na wengine nitawajia baadaye lakini si Jasusi .
 
Nina washangaa watu .Wanataka aongelewe kwa issue ipi inayo mgusa moja kwa moja ? Labda kwa issue ya magazeti yake kuacha kuandika habari muhimu ya leo ya Maandamano kama vile hayakutokea ama waandishi hawakufika huko Jangwani .
 
Wapinzani wataka ufisadi, rada, mikataba,vichunguzwe

Muhibu Said na Patricia Kamelemeta

VYAMA vitano vya upinzani, jana vilihitimisha maandamano ya kupinga madai ya ufisadi nchini kwa kutaka iundwe tume huru itakayochunguza namna dola za Marekani milioni 12 zilivyolipwa kwa wakala aliyehusika na ununuzi wa rada ya mabilioni ya shilingi.

Mbali na hilo, vyama hivyo vya upinzani vimependekeza tume hiyo kuchunguza vigogo waliohusika katika sakata hilo na kuwachukulia hatua iwapo watathibitika kuhusika na suala hilo pamoja na kuipitia mikataba yote yenye harufu ya rushwa.

Akihutubia mkutano wa hadhara mara baada ya maandamano hayo katika viwanja vya Jangwani, jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema kuundwa kwa tume hiyo kutasaidia kuwarejeshea wananchi imani kwa serikali dhidi ya wasiwasi wa kuwepo kwa rushwa katika ununuzi wa rada hiyo.

"Ufisadi unatisha. Ahadi ya tano ya TANU ilisema: Rushwa ni adui wa haki, sitatoa wala sitapokea rushwa...Tunahitaji tume huru ya watu walio safi iundwe, waweze kupitia mikataba inayonuka rushwa, waeleze hizo fedha zimeibwa wapi, nani aliyehusika na wachukuliwe hatua," alisema Profesa Lipumba na kuongeza: "Tunahitaji fedha hizo zirejeshwe mara moja".

Alipendekeza Mhadhiri wa zamani wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Issa Shivji kuwa miongoni mwa watu wanaostahili kuunda tume hiyo akisema kwamba ni mtu safi anayeweza kufanya kazi hiyo kwa uadilifu na uaminifu wa hali ya juu.

Profesa Lipumba alisema anashangaa kuona hadi sasa Serikali inapata kigugumizi kwa kushindwa kumkamata wakala aliyehusika na ununuzi wa rada hiyo wakati baadhi ya vyombo vya habari vya Uingereza vimekwisha kusaidia kutaja jina lake halisi, umri na mahali ziliko ofisi za mtu huyo hapa nchini.

"Ilipaswa huyu bwana awe amekamatwa, anaisaidia polisi, Takuru (Taasisi ya Kuzuia Rushwa nchini), aeleze alishirikiana na wakubwa gani," alisema Profesa Lipumba na kuongeza:

Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP), John Cheyo, aliwataka Watanzania kuchukizwa na kitendo cha matumizi mabaya ya fedha za ununuzi wa rada hiyo na kuonya kuwa iwapo ufisadi na rushwa vitaendelea, nchi itaendelea kuwa maskini, tegemezi na kuwakamua wananchi kwa kuwatoza michango isiyokwisha.

"Ukiona mtu anachukua fedha zetu, kasirika na uchukue hatua mara moja," alisema Cheyo na kuongeza: "Tukiendelea na hali ya ufisadi na rushwa, nchi itaendelea kuwa maskini, tegemezi na changia changia".

Mbunge wa Jimbo wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, alishutumua kitendo hicho ambacho alidai kinaonesha ni kwa jinsi gani nchi inavyotawaliwa, kuongozwa na rasilimali za nchi kutumika vibaya.

Alisema anashangaa kuona serikali inadiriki kutumia Sh80 bilioni kununua majengo ya Quality Group Limited huku ikijidhalilisha kwa kuiomba Jumuiya ya Kimataifa msaada wa Sh 83 bilioni.

"Tangu mwaka 2004, nchini kumekuwa na matumizi mabaya ya fedha za umma, mwaka jana vyombo vya habari viliripoti suala hilo, lakini serikali imeshindwa kuchukua hatua," alisema Kabwe.

Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF), Juma Hamad Rashid, aliwataka wananchi kutoishia kutoa taarifa za rushwa Serikalini na kuwataka kufanya hivyo pia kwa vyama vya upinzani ili taarifa hizo ziweze kufikishwa bungeni, kuwapo uwajibikaji na umma na dunia waweze kuelewa.

Naye Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema wapinzani watahamasisha kuonyesha Watanzania upungufu uliomo ndani ya muswada wa sheria ya vyombo vya habari na akawataka waungane kuupinga muswada huo.

Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party, Augustine Mrema Alisema anamuonea huruma Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo kutokana na kauli yake ya kuwatuhumu wabunge kwa ulaji rushwa kwa kuwa yanaweza yakamkuta mabaya.

Licha ya kuandaliwa na vyama vitano vikuu vya upinzani, maandamano hayo yaliyoanzia katika makutano ya Barabara za Morogoro na Mandela yalihudhuriwa na watu wachache kinyume na ilivyotarajiwa.

Pia Ndesamburo ambaye awali aliahidi kuhudhuria na kueleza kwa undani sakata lake la kuwahusisha na rushwa wajumbe wa kamati ya haki, maadili na madaraka ya bunge, hakuweza kutokea na hakukuwa na taarifa zozote juu ya kutokuwapo kwake.

Mkutano huo pia uliambatana na mgawo wa pilau na maji, vilivyoandaliwa na kamati ya maandalizi ya maandamano kwa waliohudhuria.
 
In his thread up there Habari Leo seem to be trying to present a nice potrait of Mengi!!
Does Mengi's mishaps ever documented??
 
Bunge, serikali vyashutumiwa kwa kumkingia kifua mfanyabiashara




Zitto Kabwe


na Mwandishi Wetu


VIONGOZI wa serikali na wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wameshutumiwa kumlinda mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya kiasia, anayedaiwa kupora fedha za mifuko ya jamii nchini.


Wameshutumiwa kuwa wameshindwa kumchukulia hatua mfanyabiashara huyo na kumlinda asijadiliwe ndani ya Bunge, hata baada ya kubainika kuwa ametumia pesa za umma vibaya.


Madai hayo yalitolewa juzi na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara wa vyama vya upinzani uliofanyika Viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam, kulaani mpango wa ununuzi wa rada unaodaiwa kugubikwa na rushwa.


Kabwe alisema tayari Mtanzania huyo mwenye asili ya kiasia amekwishaweka kibindoni kiasi cha sh bilioni 83, fedha za wafanyakazi wanazokatwa kuchangia mifuko hiyo ya hifadhi ya jamii.


“Ndani ya mwaka mmoja, kuna skendo ya ubadhirifu wa sh bilioni 83 katika Serikali ya Rais Kikwete na ameshindwa kutoa maelezo kuhusu skendo hiyo… hili linatia shaka.


“Mwaka jana serikali ilikwenda kuomba msaada wa fedha za kufanikisha bajeti yake katika Jumuiya ya Ulaya (EU), ikapewa sh bilioni 80, wakati kuna Muasia amechukua sh bilioni 83 za Watanzania, amekaa nazo, lakini serikali haina pesa, inalazimika kwenda kuomba kwa wafadhili, hii ni akili gani?” alihoji Kabwe.


Alisema kashfa ya kuliwa kwa fedha za mifuko ya hifadhi ya jamii, ilianza mwaka 2004, ambako Tanzania ilianza kukithiri kwa matumuzi mabaya ya fedha za wananchi, huku wahusika wa kashfa wakionekana kuwa na kinga maalumu kutoka kwa wakubwa, ya kutokamatwa au kuchunguzwa na taasisi yoyote ya serikali.


Akizungumzia jinsi pesa hizo zilivyochukuliwa, Kabwe alisema, Februari 2004, Muasia huyo alikopa sh bilioni sita kwa ajili ya kununua maghala yaliyokuwa yakimilikiwa na NSSF.


Alisema, siku chache baada ya kununua maghala hayo, aliyauza tena kwa NSSF kwa gharama ya sh bilioni 47, jambo ambalo linatia shaka kuwa, huo ni mpango uliopagwa kwa ajili ya kuihujumu NSSF pamoja na wanachama wake.


“Aidha, hakuna Mtanzania anayejua kama hizo bilioni 47, bado ziko nchini au zimekwishahamishiwa nje ya nchi. Serikali inalijua jambo hili vizuri, lakini imekaa kimya, hata rais hathubutu kuhoji, inashangaza,” alisema Kabwe.


Alisema, muda mfupi baadaye, Muasia huyo alikwenda PSPF na kudai kuwa ana jengo la ghorofa mbili analiuza na kwamba ndani ya muda wa wiki moja, bodi ya PSPF ilikaa na kukubali kulinunua jengo hilo.


Kabwe alisema, anazo taarifa kuwa bodi ya PSPF ilikubali kununua kampuni nzima ya Quality Plaza badala ya jengo la ghorofa mbili na siku kumi kabla ya kununuliwa kwa kampuni hiyo, thamani yake ilipanda kwa sh bilioni sita zaidi.


“Sijui wajumbe wa bodi ya PSPF walitumia vigezo gani kukubali kununua kampuni nzima bila kufanya tathmini na kubaini ilikuwa na madeni kiasi gani, pamoja na mambo mengine ya msingi kabla ya kuinunua kampuni kama hiyo,” alisema Kabwe.


Alisema baada ya kugundua kashfa hiyo, wabunge walijaribu kuhoji ndani ya bunge jinsi fedha za mifuko hiyo zinavyoishia kwa Muasia huyo, lakini Spika wa Bunge aliupiga ‘stop’ mjadala huo, kwa maelezo kuwa suala hilo liko mahakamani.


“Tulipogundua kashfa hiyo, tulihoji ndani ya bunge kulikoni, ajabu, tukapigwa zengwe, tukaambiwa kesi iko mahakamani. Tulipofuatilia tukagundua kesi iliyoko mahakamani ni ya kuvunjiana heshima baina ya wafanyabiashara wawili.


Naye Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour, Augustine Mrema, alisema anamuonea huruma Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo kwa kuibua kashfa ya rushwa ambayo inawagusa viongozi wakuu wa serikali.


Mrema alisema ingawa Ndesamburo ameonyesha ujasiri wa hali ya juu, lakini anamuonea huruma, kwa sababu ana hakika atakiona cha mtema kuni kwa kuwatuhumu wabunge wenzake kuwa, wamehongwa ili wapindishe ukweli katika kesi inawayowakabili Adamu Malima na Reginald Mengi.


“Ninamuonea huruma Ndesamburo, ingawa amepasua ukweli kuwa ziwa la mama linanyonywa na mtoto wa kambo, lakini nina hakika atakiona cha mtema kuni!... nchi inateketea hii… inakwisha, na mimi nitaendelea kulia na CCM,” alisema Mrema.
 
Tunangoja majibu ya Serikali hapa maana wanadhani watu tumelala. Huyu Manji kawapa nini lakini hawa watu ? Kiasi cha pesa hadi ana maamuzi kwenye Nchi tya watu more than 30m ?
 
Ndio shida ya kuwapa nchi maamuma, wanachojua ni kugawa mali kwa marafiki mwalimu (RIP) alituonya lakini wameingia kwa mlango wa nyuma, sasa tuna kazi ya kuwaondoa tena kwa ARI MPYA, NGUVU MPYA NA SPEED MPYA NA WALE WASIOTAKA ITABIDI WAONDOKE NAO; HATUWEZI KUKUBALI UKOLONI MAMBOLEO.
 
Sioni sababu ya kumjadili Mengi...unless kama kuna "hidden agenda ya 2010". Kama kuna mbio za jumba jeupe...basi na aseme then tuendelee. Otherwise naona hakuna mpya hapa.
 
If need be, let us discuss him as business institution but not as a person. Otherwise we will be off-track.

Why in Tanzani we dont have so many Mengi's as compared to other EAC countries like Uganda and Kenya ?. With this trend do we have anything to gain in EAC ?
 
NIPATAPO WASAA KUWA HUKO VIJIJINI, HUWA NAJARIBU KUAMSHA WAZEE WANGU NA NDUGU ZANGU WALIOLALA. MWANZO HAWAKUWA WANANISIKILIZA WALIONA KAMA NAPOTEA NATAKA KUFIA JELA! KIDOGO KIDOGO WALIANZA KUNIFUATA MMOJA MMOJA KUTAKA KUJUA KAMA NINAYOSEMA NIKWELI!!
NA TANGU NIMEKUWA MWANA FORUM 9ndani ya nyumba) NAONA UJUMBE WANGU WANAUPOKEA KWA UMUHIMU WAKE KIASI KWAMBA KILA WIKI WANASUBIRI MPYA KUTOKA CHUNGUNI...

WENZANGU, EBU TUWAAMSHE HAWA WAPIGA KURA WA 2010....
 
Mimi nina watu zaidi ya 100 wengine wao ni ignorant lakini wameanza kuamka . Nina wakati nyeti kweli kweli na sasa kazi ni kubwa kila kukika unasikai Mzee Lunyungu tupe Baba hata kidogo toka kwenye chungu . Nategemea sana JF kuwapa info lakini hata mimi sijambo nazipata jikoni hapa hapa Magogoni kwa hiyo tuendelee .
 
JF inageuka na kuwa nguzo muhimu sana ya mapambano dhidi ya ufisadi. Hili ni eneo la kihistoria, kila siku historia inaandikwa, ukamavu wa watu unaongezeka, hofu iko milangoni mwa watawala dhaifu na wachafu. Tukaze uzi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom