Mchungaji aliyetekwa aeleza mateso na kwenda kutupwa porini ashindwa kutembea "Mengine tuyaache "

Mchungaji aliyetekwa aeleza mateso na kwenda kutupwa porini ashindwa kutembea "Mengine tuyaache "

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Kristo lililopo Mtaa wa FFU, Kata ya Murieti, Steven Jacob Gumbo (35) ambaye iliripotiwa ametekwa na ‘Watu Wasiojulikana’ Mei 16, 2025 amezungumza na Wanahabri na kueleza kuwa Watu waliomchukua walijitambulisha kuwa ni Askari Polisi na wanamhitaji kwa ajili ya mahojiano

Amesema Watu hao walimchukua kwa nguvu huku wakimpiga, akapelekwa sehemu ambayo hakuifahamu na kuingizwa kwenye chumba kisha kuanza kumshambulia

Ameongeza “Naomba nisiongee mengi, sababu ya kutekwa ni ishu za Mtandao. Walichukua maelezo, wakanipeleka porini West Kilimanjaro, wakachukua simu yangu na kunitaka nifute video zangu zote, wakazungumza vitu ambavyo siwezi kuvisema kwa sasa kisha wakanitelekeza hapo.”

VIDEO: KUSAGA TV

Pia soma:
~
Mchungaji Mwl Steven Jacob atekwa na watu wasiojulikana
~ Mwl. Steven Jacob aliyedaiwa kutekwa na watu wasiyojulikana apatikana Kilimanjaro akiwa amepigwa
 
Kosa lake anahisi ni nini hadi kutekwa. Nina imani kuna jambo limewaudhi waliomteka
 
Mmh pole sana mtumishi wa Mungu
Sisi bado tuko kwenye ujima tusubiri kizazi cha vilembwe wetu labda wanaweza kuikomboa nchi hii siye tukae kimya hatuwezi kujipigania hatuna umoja
 
Hajapigwa huyo… waliowahi kukutana na bwana pepsi huwa hawaongei
 
Daaa kumbe ni huyu jamaa!!Huwa anatoa sana nondo,Nakumbuka ile moja alimkosoa yule Mtumishi mwenzake wakule Kitunda..Ukute ni wenyewe kwa wenyewe sio Jamaa zetu.
 
Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Kristo lililopo Mtaa wa FFU, Kata ya Murieti, Steven Jacob Gumbo (35) ambaye iliripotiwa ametekwa na 'Watu Wasiojulikana' Mei 16, 2025 amezungumza na Wanahabri na kueleza kuwa Watu waliomchukua walijitambulisha kuwa ni Askari Polisi na wanamhitaji kwa ajili ya mahojiano

Kupata matukio ya nyuma kuhusu watu wasiyojulikana ingia hapa: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Amesema Watu hao walimchukua kwa nguvu huku wakimpiga, akapelekwa sehemu ambayo hakuifahamu na kuingizwa kwenye chumba kisha kuanza kumshambulia.

Ameongeza "Naomba nisiongee mengi, sababu ya kutekwa ni ishu za Mtandao. Walichukua maelezo, wakanipeleka porini West Kilimanjaro, wakachukua simu yangu na kunitaka nifute video zangu zote, wakazungumza vitu ambavyo siwezi kuvisema kwa sasa kisha wakanitelekeza hapo."

 
Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Kristo lililopo Mtaa wa FFU, Kata ya Murieti, Steven Jacob Gumbo (35) ambaye iliripotiwa ametekwa na 'Watu Wasiojulikana' Mei 16, 2025 amezungumza na Wanahabri na kueleza kuwa Watu waliomchukua walijitambulisha kuwa ni Askari Polisi na wanamhitaji kwa ajili ya mahojiano

Amesema Watu hao walimchukua kwa nguvu huku wakimpiga, akapelekwa sehemu ambayo hakuifahamu na kuingizwa kwenye chumba kisha kuanza kumshambulia.

Ameongeza "Naomba nisiongee mengi, sababu ya kutekwa ni ishu za Mtandao. Walichukua maelezo, wakanipeleka porini West Kilimanjaro, wakachukua simu yangu na kunitaka nifute video zangu zote, wakazungumza vitu ambavyo siwezi kuvisema kwa sasa kisha wakanitelekeza hapo."
DAAH, UMEJITAHD, KUNA WENGNE WALIRUDI WAKAPELEKEWA WAANDISHI WA HABARI LAKN HAWAKUSEMA..

samahani hvo vitu walikuwa wanaongea nini?
 
Kuna wakati hawa wanaotenda hivi vitendo wapaswa kulipwa kadili ya vitendo vyao hapa hapa duniani ili wengine washuhudie na kujifunza.
 
Back
Top Bottom