Maulidi Kitenge aacha kazi ITV/Radio one

Maulidi Kitenge aacha kazi ITV/Radio one

:hail::hail::hail:.....sawasawa.
Tarehe je!? ina mjadala hapo?

Hiyo barua yake haiko kwenye miundo rasimi ya uandishi wa barua za kiofisi kachanganya changanya sana yaani ameniangusha sana. Tarehe inaweza kuwa upande huo kwa muundo tofauti na huo aliotumia.

Kinachosikitisha anasema ameamua kuacha kazi eti maisha yamekuwa magumu, na hasemi ni wapi anakokwenda ambako maisha yatakuwa mapesi.

Kimsingi ukiamua kusema sababu za kuacha kazi unapaswa kusema pia unakwenda kufanya nini kinyume na hapo utakuwa umeharibu!
 
Mno na maisha yamepanda ila wakubali wakatae limewatoa wengi kujulikana na kupata opportunities nyingine.

aisee nimejisikia vbaya sana...!!!
Mengi anatakiwa aamke sasa!!
Yaani gold zinaondoka zote hizo!!
 
du, hivi utangazaji nao unajiuzulu? du naona anawaza siasa, au amepata na yeye post serikalini ya upande wa habari nini? angeandika yah: kuacha kazi basi.

Hiyo ni job resignation letter yupo sahihi kabisa,tatizo lenu hamtaki kujifunza alafu mnajifanya wajuaji.
 
Kinachosikitisha anasema ameamua kuacha kazi eti maisha yamekuwa magumu, na hasemi ni wapi anakokwenda ambako maisha yatakuwa mapesi.

Kimsingi ukiamua kusema sababu za kuacha kazi unapaswa kusema pia unakwenda kufanya nini kinyume na hapo utakuwa umeharibu!

angesema tu amepata kazi sehemu nyingne yenye malipo mazuri zaidi. maisha magumu halafu uamue tu kuacha kazi bila kuwa na mbadala. hajawa muwazi.
 
....bado sijaona kosa la kiuandishi hapo upande wa Tarehe.
It's an immediate resignation notice,
Suala la kurudisha mshahara halina mjadala, kaliweka sawa sawa.

Mnaohoji template aliyoitumia leteni samples zenu hapa 'tuone' ya nani muafaka, otherwise wengi wenu mnalaumu kiushabiki tu.


#MosKwito !

Kabisa jamaa hakuna halichokosea hata sehemu moja kujiuzuru ni kuachia ngazi na yeye amesema kabisa ameachia ngazi kama mtangazaji/mwandishi radio1/itv
~Ni halali kwa yeye kulipa mshahara nusu maana amefanya kazi siku 18 tena inatakiwa alipe siku 10 tu
~Tarehe na sahihi ni design tu inategemea mtu ataweka vipi zote ruksa.
~Kutoa sababu ya kuacha kazi kwenye barua ni jambo la msingi sana na sababu aliyotoa ina mantiki kwamba mshahara ni mdogo.
 
Mengi anapenda sifa lakini analipa mshahara mdogo sana staff wake halafu mikataba ya kazi inatoka kwa kujuana nimefanya kazi IPP kwa muda nikashindwa
wacha Kitenge atafute maslahi mazuri

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hongera Kitenge kwa kuchukua maamuzi magumu! Kuamua kuondoka sehemu uliyoishi kwa miaka 14 sio jambo jepesi.
 
angesema tu amepata kazi sehemu nyingne yenye malipo mazuri zaidi. maisha magumu halafu uamue tu kuacha kazi bila kuwa na mbadala. hajawa muwazi.

Eti chief! Yani kaniangusha kama mtangazaji. Anasema maisha yamekuwa magumu wakati anakazi je wale ambao hawana watasemaje!

Pengine alitarajia akisema maisha ni magumu mkurugenzi ataongeza cha juu hahahahaha!!! Sijapenda uandishi wake. Ila kupata kazi sehemu nyingine ni vizuri unajifunza zaidi.
 
Eti chief! Yani kaniangusha kama mtangazaji. Anasema maisha yamekuwa magumu wakati anakazi je wale ambao hawana watasemaje!

Pengine alitarajia akisema maisha ni magumu mkurugenzi ataongeza cha juu hahahahaha!!! Sijapenda uandishi wake. Ila kupata kazi sehemu nyingine ni vizuri unajifunza zaidi.

hata mimi sijapenda kabisa..... bora hata angedanganya sababu kuliko hiyo sababu aliyoitoa. ... vizuri kama amepata kazi sehemu nyingne. kufanya kazi sehemu moja miaka 14 yote hiyo ni mingi sana.
 
MTANGAZAJI wa michezo wa Radio One Stereo na ITV, Maulid Kitenge kupitia akaunti yake ya Twitter hivi punde ametangaza kuondoka rasmi katika kampuni hiyo ya IPP baada ya kuitumikia kwa miaka 14. Je, nini maoni yako.
attachment.php
attachment.php
attachment.php

Alikoenda...... BOFYA: Global Publishers
 
hata mimi sijapenda kabisa..... bora hata angedanganya sababu kuliko hiyo sababu aliyoitoa. ... vizuri kama amepata kazi sehemu nyingne. kufanya kazi sehemu moja miaka 14 yote hiyo ni mingi sana.

Naam!! Tumtakie mafanikio huko aendako.
 
Back
Top Bottom