Kilichomfukuzisha kazi Maulidi Kitenge Wasafi FM chajulikana

Ambakucha

JF-Expert Member
Aug 16, 2019
277
445
Wadau, kichwa cha habari chajieleza. Mtangazaji Maulidi Kitenge hajaondoka Wasafi FM Radio bali amefurushwa kwa sababu ya safari zake za mara kwa mara nje ya nchi, hususan nchini Marekani.

Kwa mujibu wa chanzo cha ndani kutoka Wasafi FM, Maulidi Kitenge amekuwa akienda nchini Marekani kwa mwaka mara nne jambo ambalo limekuwa likimkera CEO wa Wasafi, Nasibu Abdul 'Diamond'.

"Mfano, Novemba mwaka jana alikwenda Marekani. Januari mwaka huu, wakati Rais Joe Biden anaapishwa akaenda. Machi akaenda tena, mwezi Julai pia akaenda, mpaka unaingia Agosti yuko kule. Diamond akaona jamaa anakuwa nje ya kituo cha kazi muda mwingi, akaamua kumtimua," kilisema chanzo hicho.

"Amekuwa akitumia nguvu kubwa kutuma matangazo yake Wasafi akiwa kule, kama kusoma Magazeti (Kurasa za Magazeti, Chumvi na Ndimu) na Michezo (Sports Arena) ili aoneshe kuwa, hakuna pengo la kazi zake, lakini ukweli ni kwamba, Diamond amekuwa akikereka sana, akashindwa kumvumilia, akamtumia barua ya kumwachisha kazi," kiliongeza chanzo hicho.
 
Wadau, kichwa cha habari chajieleza. Mtangazaji Maulidi Kitenge hajaondoka Wasafi FM Radio bali amefurushwa kwa sababu ya safari zake za mara kwa
Au Diamond ana ona wivu kwann mfanyakazi wake ana kwenda sana Marekani kuliko yeye boss ? ..huu wivu mbaya sanaaaa
😄😄😄 Nilitazama leo akiwa efm live na kasuti kake na sun glass zake .......
 
Tuwe wakweli kwenye hili ukiwa na mfanyakazi ambaye muda mwingi anakuwa nje ya kituo cha kazi ufanisi unapungua
Kipindi cha korona ya kwanza Ulaya wafanyakazi waliruhusiwa kufanya kazi zao nyumbani...ombwe la ufanisi lilionekana wazi
Kwenye ajira kuna taratibu za ruhusa na likizo na zina vikomo vyake... Hili watalielewa tu wale walio katika ajira rasmi na hasa ambazo si za serikali na utumishi wa uma
 
Tuwe wakweli kwenye hili ukiwa na mfanyakazi ambaye muda mwingi anakuwa nje ya kituo cha kazi ufanisi unapungua
Kipindi cha korona ya kwanza ulaya wafanyakazi waliruhusiwa kufanya kazi zao nyumbani...ombwe la ufanisi lilionekana wazi
Kwenye ajira kuna taratibu za ruhusa na likizo na zina vikomo vyake... Hili watalielewa tu wale walio katika ajira rasmi na hasa ambazo si za serikali na utumishi wa uma
kabisa
 
,
19218d5e2c9a0e404abff44fc0c06d98.jpg
 
Back
Top Bottom