Maulidi Kitenge aacha kazi ITV/Radio one

Maulidi Kitenge aacha kazi ITV/Radio one

Mtangazaji mkongwe wa michezo kwenye kituo cha Radio one Stereo/ITV ameacha kazi.

Kitenge ambaye amefanya kazi kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na IPP kwa muda wa miaka 14, amedai anakwenda kufanya shudhuli zake binafsi akidai kuwa, hali ya maisha imepanda kwa kiasi kubwa sana na mahitaji ya kimaisha yameongezeka gharama, hivyo inanilazimu kutafuta njia mbadala ya kujiingizia kipato kikubwa zaidi

Source: BONGO 5

Kumbukumbu zangu

Mwaka 2005 nilisoma kwenye gazeti moja hivi (sikumbuki) alisema anampango wa kugombea ubunge ifikapo 2015.

Sijui kama bado ana nia hiyo iliyomlazimu aache kazi au kapata shavu kwingine.

ALL IN ALL: Kila la kheri Maulid Kitenge a.k.a Baba Shadya tutakumiss kwenye kioo.

Umarioo haa sidhani ingawa mke wake mkubwa Eshe Mhidin aliyekuwa TBC sasa yupo UN Sudani huyu mke wapili sijui anafanya kazi gani.

Ni kweli hiyo kazi imemfanya ajulikane na akitoka hapo anaweza kupata opportunity nzuri hata business

Kusomesha watoto ni jambo zuri sana..yaani jitu zima na akili zake eti linasema limejiuzulu!!!! Mxxxxxx halijui tofauti ya kujiuzulu na kuacha kazi!!

Mno na maisha yamepanda ila wakubali wakatae limewatoa wengi kujulikana na kupata opportunities nyingine.

Kawa mstaarabu tu kwa kumsitiri mwajiri wake ila ukweli ni kwamba lile chaka ninalipa kiduchu sana.



Wanalipa kidogo ukilinganisha na sekta gani?
Labda ututajie kima chao cha chini cha mshahara ili tulinganishe na sekta nyingine.

Almost watanzania wanalipwa mishahara midogo iwe serikalini au binafsi .
Watu wanaishi kijanja janja tu,iwe kwa rushwa au wizi na dili nyingine ndio maana watu wakimbila ajira za serikali mana huko ni shamba la bibi la rushwa na wizi.

Mfano tu mfanyakazi wa sekta za kawaida tu za umma bado hajafikisha taking home ya kima cha chini sh.270,000/= kwa mshahara wa mwezi lakini wanabangaiza hivyo hivyo.
Kwa hiyo kulaumu IPP peke yao ni sawa lakini nimulike na mashirika na taasisi nyingine kwani huko nako kuna matatizo hayo hayo.

Cha msingi ni mtu kutafuta fursa ya kujiajiri ili kuongeza kipato vinginevyo utatoka kupitia rushwa na wizi tu.
 
...
Kitenge ambaye amefanya kazi kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na IPP kwa muda wa miaka 14, amedai anakwenda kufanya shudhuli zake binafsi akidai kuwa, hali ya maisha imepanda kwa kiasi kubwa sana na mahitaji ya kimaisha yameongezeka gharama, hivyo inanilazimu kutafuta njia mbadala ya kujiingizia kipato kikubwa zaidi

Nimeipenda hii....mwanaume lazima uwe wazi na mkweli.
 
Kwa kadri ya sheria za kazi, kama emetoa taarifa ya masaa 24 (24hr notice) alitakiwa kurudisha mshahara wa mwezi mzima na siyo nusu mshahara au kuhesabu siku alizofanya kazi.

Ila kwa mtangazaji wa kiwangu cha Kitenge, barua aliyoandika ina mwangwi mzito sana. Kama huyu anaweza kuandika hivi, je wale wa siku hizi watakuwa wanaandikaje barua?
 
du, hivi utangazaji nao unajiuzulu? du naona anawaza siasa, au amepata na yeye post serikalini ya upande wa habari nini? angeandika yah: kuacha kazi basi.
Unaweza kujiuzulu kazi yeyote ile ,ukulima ,ufugaji uvuvi,wazibua karo-mifereji,wazoa taka,wachawi,vibaka,dada wa nyumbani,uchangudoa,pusha wa ngada,ukuwadi yaani zote zinahusu kujiuzulu mkuu!
 
Haha ndio nani huyo.
mo%2B2.jpg
 
Karudisha mshahara! ina maana ITV/radio one hupokea mwanzo wa mwezi siyo mwisho wa mwezi au sijaelewa!
 
Sasa yeye kua na zaidi ya mke mmoja inakuhusu nini? Hizo ni mambo binafsi na makubaliano yake na wake zake.

Wewe Uchiboy. Huoni mapungufu kwa kijana mdogo kkuwa na wake wengi. rekebisha jina lako kwanza
 
Back
Top Bottom