Mpira ni mbinu. Kwenye mpira hakuna mbinu moja pekee, zipo nyingi.
Kuna wakati defense ya wapinzani inakua imebana sana uwanja na hivyo kuwanyima nafasi ya nyie kushambulia.
Nyakati kama hizo unakua unahitaji winga (Anthony and the likes) anayetanua uwanja ili kuwavuta pembeni walinzi na hatimaye nafasi za kushambulia (spaces) zipatikane.
Kukiwa hakuna uhitaji wa kucheza na mapana ya uwanja, hapo unahitaji winga wa kuingia ndani (Sancho and the likes) ili kuweza kulitumia vema eneo la mbele ya goli la mpinzani.
Unaposema kwamba Anthony ni mchezaji mbaya au asiyefaa maana yake unataka United iwe ni timu inayotumia mbinu moja tu.
Mimi binafsi sioni kama hilo pendekezo lako ni sahihi sana. Tunacheza mechi nyingi, aina tofauti tofauti za wapinzani, tunapaswa kuwa na aina tofauti tofauti za silaha.