Jinsi tulivyoumia leo kwangu ni ishara Ten Hag anafanya kazi kubwa sana. Nikikumbuka miezi 6 tulipokuwa na hapa tulipo. Nani angeweza kufikiri hata tukifungwa mechi 3 mfululizo bado tupo top 4?
Binafsi I'm very grateful so far, Arsenal, City na L'pool hizi ni timu ambazo benchi la ufundi lipo kwa zaidi ya misimu mitatu. Hatuwezi kujilinganisha nao kwa sasa, benchi letu la ufundi ndio kwanza wana miezi 6 tu.
Naona mwanga ndani ya msimu ujao. Msimu huu top 4 na kikombe kimoja yatakuwa mafaniko makubwa sana na mahala tulipotoka msimu mmoja nyuma. Japokuwa nilianza kujipa moyo wa kufanya kitu ila Arsenal wapo serious msimu huu.