NGUMU KUMEZA ...
Kwa wale wapenzi wa gozi/mpira chukua dk 4 kupitiaa ...
GOLDEN BOY MAPUNG'O: MPIRA ULIOTUACHIA UKIWA UMETOBOKA HATUJAUZIBA BADO...
Siku watu waliokaa chini na kujadili mambo mengi kuhusu mpira, huku kwetu tulikuwa Bado hatuja funguka macho, ndio kwanza almasi na dhahabu tulitumia kama kete za draft na bao..... Siku walipokaa tena na kuunda mpira wao, huku kwetu babu zetu walikuwa wanawashangaa wakoloni na familia zao wanapiga piga mpira kila jioni....... Siku walipokaa tena na tena kwaajili ya maboresho ya gozi lile, sisi Bado tuna shangaa na kuendelea kuwaona wakoloni wajinga kwa kupoteza muda wao kukimbia kimbia uwanjani.......
Walichotunyima ni sisi kuwa kama wao, ila walichoturuhusu tu ni sisi kuwaiga wao....... Ndio maana hakuna kilicho andaliwa huku kwetu kikaenda kufanyiwa kazi kule kwao tofauti na nguvu zetu tu, ndio maana kila kitu walikiandaa wao na sisi tukaruhusiwa kutumia Bila kubadilisha ata nukta......
Sheria 17 za gozi lile wanajua wao walipozitoa na ni kwanini wameweka....... Sisi Leo 2017 Bado hatujafika walipopita mwaka 1999... Ndio maana hatua zetu ni ndefu kama mawazo yao lakini ajabu ni kwamba hazigusi chini kama malengo yetu.
Ndio maana nyasi bandia zinafika kwetu sasa ila kwao zilishapita na wameshaziacha.... Ndio maana kucheza michezo usiku wao wameshazoea ila sisi ndio tunajitutumua, ndio maana sheria zao haziitaji vikao vingi, sisi Bado tuna ukakasi, ndio maana Transfer matching system (TMS) tunaanza kuitumia sasa ila kwao ni kitu kizee......
Rangi zetu nyeusi ndivyo zilivyo ambatana na weusi wa maamuzi yetu katika soka, weusi wa mapambano yetu katika soka, weusi wa kujituma katika soka, weusi wa kuridhika na mafanikio kidogo katika soka, weusi wa kupambana na weusi wa ujanja wa kuchuma.....
Ukiachia weusi wetu katika soka Bado Mungu alitujaalia busara, hekima, nguvu, vipaji na upambanaji wa kujitoa...... Ndio maana Zama zile wakitumika kuleta utajiri wa ulaya mababu zetu wale wa kale katika biashara isiyo huru na wao wakatuachia mipira ile waliyokuwa wanaicheza kila siku jioni.....
Wakati tukipishana na wanaojua mipango katika soka, mbinu na namna ya kupiga hatua katika soka, nashukuru Mungu hatukubaki nyuma katika kuwaiga kwa namna moja ama nyingine......
Wao walituletea bablish zenye picha za wachezaji ila sisi tukawanogeshwa na jarida/gazeti la Sun na ligi ya utawala wa wajanja wa bush.
Riziwani Reagan Ridhwani.... Huyu mwanadamu alihusika kunifanya nimiliki daftari lililojaa picha(stika) za wachezaji wa ulaya enzi hizo, ila pia alinifanya kumiliki majarida/gazeti la Sun lililokuwa na ligi pendwa ya picha zenye maneno..... Kupitia yeye nilimuona Golden boy Mapung'o katika ubora kuliko uhalisia wa George Opong Weah, kupitia yeye niliweza kuwafahamu wachezaji watatu tu duniani waliokuwa wakicheza mpira wa miguu huku wakiwa na kofia na hata mawani..... Edger Davies na mawani yake katika picha, ila pia Peter Manyika katika kofia yake na mikono yake katika kurasa za mbele za magazeti, vipi kuhusu Mtaalam wa chimbo na kuopoa kwa fedha mzee Lord lofa na lile kofia lake uwanjani..
Zama hizo ndizo Mimi na Andrea Zlatan Mushi tulikuwa tunahadisiwa kuhusu ubora wa Zama za Sandy Manara Computer huku tukimsoma Golden Boy Mapung'o na umaridadi wake......
Zama hizo ndio ndizo kulikuwa hakuna mashine za kupunguza ukubwa wa jezi na kuwa saizi ya kila mchezaji kutokana na umbo... Na Bado Zama mpaka sasa hatujaweza kuuziba mpira ule uliotuachia.
Imefika mahali sasa tunaweza kukaa kiti kimoja pale taifa na kuwaangalia Brazil na Robinho wake, kuwatizama Ivory coast na Drogba wake, senegal na kamara wao..... Dah Zama zinapita sana tangu Golden boy Mapung'o uondoke, huku mtaani kila jioni baada ya mechi tumekuwa tukisema umeondoka na mpira wako, umeondoka na timu yako umeondoka na mbinu na utaalamu wako.... Hapa mpira ulikuwa una slow pancha.
Zama hizi sasa hakuna tena zile hadithi za Peter Tino, hakuna tena zile soga za Pele wa mwanza ili kina Ramadhani Singano na Hassan Kessy waziige..... Leo maandishi yote na maneno yote yanakuhusu wewe Golden boy Mapung'o na timu yako katika Zama zako......
Tunamisi mpira uliochezwa viwanjani na kidogo ukachezwa mezani, tunamisi mipango iliyokuwa kwenye makaratasi na kidogo kichwani...... Tunakulaumu umeondoka na vitu vyooote ulivyotuandalia.
Ndio maana Leo tunahadisiana tu hadithi mpya za Ludovic wa mbao fc na African Lyon, lakini pia Mubarak Yusuph wa Kagera, Simba na Azam fc...... Tunakukumbuka sana mzee wa bush japo wewe na kizazi chako cha dhahabu mliwatesa kiasi waamuzi kuliko goli la mkono wa Chirwa, offside ya Ajibu na hata kadi tatu za Mohammed.
Golden boy Mapung'o..... Marcio Maximo aliondoka najua unajua, Jan Poulsen aliondoka najua unajua lakini pia Kim Poulsen naye aliondoka pia najua pia hilo unalifahamu...... Kabla hajaja Martin Noij najua unajua Kodi ya mishahara ya waalimu hawa haikuwa katika zile pretty cash za pale maeneo..... Ila pia Bado tumekosa kutambua tofauti ya Serikali na Mamlaka ya mapato katika mishahara unayoijua Golden boy Mapung'o.
Golden boy Mapung'o ule mchezo mtamu wa kombolela naona sehemu kubwa duniani wameshabutua kopo..... FIFA kabutua Infatino, lakini UEFA walizinga ila katibua Cefferin, usisahau swahiba Issah Hayatu alizinga Ahmad Ahmad kabutua...... Sasa kopo limepelekwa Dodoma sadakalawe ipo dar es salaam.
Watu Wengi wanajiuliza kama kuna timu ya kutufikisha ilipotufikisha Bush Stars yako...... Ndoto kila siku zimekuwa ni zile zile na cha ajabu panawahi kukucha na mpira bado hatujauziba.
Timu yetu ya sasa haina Golden boy Mapung'o wa sasa, inamkosa Kipepe, inamkosa baba ubaya lakini pia kiokote, madenge na Lord lofa....... Najiuliza tu nyie mlikujaje najiuliza pia nyie mliondokaje.....? Bush Stars.
Nashukuru kwa kukushuhudia mzee maana ipo siku ntakuja kusimulia juu yako...... Ila sondano, Uzi na patex utusaidie hata kwa mawazo ili tuuzibe na kuucheza.
Macho na ubongo ndio vinaweza kuelewa ila macho pekee hayatoambilia kitu.....