Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

mkurugenzi wa TMA tar 1/march/2015 tuliona kwenye magezeti akiwahimiza wakulima walime mazao yenye kustahimili ukame kwani mvua za masika za msimu zitakuwa chini ya wastani maeneo ya Pwani.
 
Vp sehemu za bunju+ununio+majohe, hali ikoje huko??? Tunahitaji updates
 
ImageUploadedByJamiiForums1430981620.550652.jpg ImageUploadedByJamiiForums1430981639.018093.jpg
 
Serikali lazima ilaumiwe kwani hata ile sheria ya kujenga mita sitini kutoka baharini haaifuati. Kutokujenga sehemu za wazi hawazifuati (huko ndiko maji yanapumulia). Kuna sheria ya kutokujenga mabondeni watendaji wanaruhusu! Mikondo ya maji haitakiwi kuzibwa lakini wananchi wanaziba na serikali inaangalia tu!
Tunahitaji serikali ya kisayansi na kama ni kuhamisha watu wahamishwe kwa gharama, waliojenga sehemu za wazi wavunjiwe mifereji ijengwe sehemu husika nchi nzima.
Ukiwa na miundo mbinu mizuri hata mafuriko yakija huwa yanaondoka baada ya muda mfupi.
 
Yaani nyinyi wananchi mjenge holela na kuziba mitaro, mjenge sehemu za maji kupita, mvua ije maji yashindwe kupita, muilalamikie Serikali? Seriously?
 
Ifike wakati watu waende nje ya mji, kwani lazima kuonekana unakaa mjini ili hali unaishi kwenye bwawa la maji ya chooni???????? nyumba nyingine ni kinyaa lakini mtu anang'ang'ania hapo hapo kisa yupo karibu na kariakoo ni ujinga huo sasa. hapo serikali ya ccm haihusiki.

Kama wewe ni mmoja wa watunga sera kinachotakiwa ni ku-create Kariakoo nyingine huko nje ya mji. Lkn watunga sera wetu wanajiangalia wao wanatoka wapi/ wanakaa wapi basi kwingine wanasahau kabisa na ndo maana watu wanawafuata huko huko wakisema tutabana hapa hapa. Kulikuwa na mradi wa "satelite cities" Luguruni-Kibamba, Goba, Bunju lakn nafikiri umekufa kwani hakuna kinachoendelea. Pia kuna corridor wajua "Mtwara Corridor ilikuwa kipindi cha nani weye?, Je wajua Bagamoyo corridor ilikuwa kipindi gani?, unakumbuka maendeleo ya Mwanga (umeme, barabara za lami n.k) ilikuwa kipindi cha nani weye? Je Katavi everything Chuo kikuu, Mkoa, barabara za lami? Tafakari. hatuna sera ya kitaifa yaliyopo ni maigizo tu!
 
Yalah! Pole yao kwa matatizo. Maisha Bora kwa kila Mtanzania.
 
Ifike wakati watu waende nje ya mji, kwani lazima kuonekana unakaa mjini ili hali unaishi kwenye bwawa la maji ya chooni???????? nyumba nyingine ni kinyaa lakini mtu anang'ang'ania hapo hapo kisa yupo karibu na kariakoo ni ujinga huo sasa. hapo serikali ya ccm haihusiki.

Upo sahihi Apologise lady, tunaoishi maeneo ya Kimara, Mbezi, Pugu na kwingine nje ya mji huwezi kusikia tunaathirika na mafuriko...masista dudu na mabishoo wa mjini ndio wanalia na kusaga meno😀
 
Last edited by a moderator:
11025707_560461290762690_5363877423202717052_n.jpg
Huwezi kuamini lakini ni ukweli.. Lori Tani 20 limesombwa na mto Darajani Kinyerezi... this is now na mvua inaendelea km kawaida.
 
Kiongozi anapozungumza bila amani kwa sababu anaamini kabisa kuwa anayozungumza yeye mwenyewe hayaamini, na anajua anaowaambia hawayaamini, na yeye pia haaminiki,
Inapofikia wakati wa kutoa maamuzi magumu anakohoa!
Pia Kwenye matatizo anatabasamu,
Nini maana yake?
 
Back
Top Bottom