Mafinga ni mji wa kibiashara lakini nyumba za kulala wageni nyingi ni chafu

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Jan 24, 2019
28,394
81,877
Kwa wale wasio ufahamu huo Mji; kwa ufupi tu uko ndani ya Mkoa wa Iringa (Kilomita chache kutoka Iringa mjini kama unaelekea Mbeya, Njombe au Ruvuma), uko ndani ya Wilaya ya Mufindi, na ni mji maarufu kwa biashara ya mbao na pia nguzo! Maana uko jirani na kiwanda maarufu cha Sao Hill.

Kwa kweli huu Mji ni mdogo tu lakini uko busy sana kibiashara, na ikumbukwe maeneo ya pembezoni mfano Madibira, Sadani, Mgololo, na pia Mufindi yote kwa ujumla; huutegemea huu mji kwenye suala zima la mahitaji yao muhimu ya kila siku.

Ingawa huu Mji umekuwa ukipokea wageni wa kila aina kila siku kwa ajili ya kununua mbao, nguzo, na mahitaji mengine, umekuwa na upungufu wa nyumba za wageni zenye hadhi. Kiukweli nyumba nyingi za kulala wageni (Lodges + Guest Houses) zilizopo Mafinga ni chafu!

Kwanza mablanketi yao huwa hawafui (ifahamike hili eneo lina baridi mwaka mzima, hivyo lazima ujifunike blanketi). Mara kadhaa nimelazimika kulala Iringa mjini, kwa sababu tu ya huu udhaifu wa nyumba za wageni pale Mafinga.

Hivi shida ni nini kwa wamiliki wa nyumba za wageniza Mafinga? Au ni kwa sababu mnapata faida kubwa kupitia short time? Maana hizo bar zenu maarufu, pamoja na night clubs chache zilizopo; si haba!

Kwa kweli nawashauri mbadilike. Kama vipi pandisheni hata bei za vyumba, huku mkiboresha pia huduma. Kwa kweli mablanketi yeni ni machafu sana. Mtakuja kuwasababishia wateja wenu magonjwa ya ngozi kwa sababu zinazoweza kuzuilika.
 
Karibu sana mafinga
Jaribu kulala guest house at least inayoanzia elfu 30 za kitanzania hizo 20 au 15 ni majanga
Naomba unitajie kwa kweli. Maana hata sizifahamu. Karibia lodge 2 nilizolala nilikumbana na mablanketi machafu, na yenye harufu kali! Na hivyo kuishia tu kujifunika shuka.
 
Kwa wale wasio ufahamu huo Mji; kwa ufupi tu uko ndani ya Mkoa wa Iringa (Kilomita chache kutoka Iringa mjini kama unaelekea Mbeya, Njombe au Ruvuma), uko ndani ya Wilaya ya Mufindi, na ni mji maarufu kwa biashara ya mbao na pia nguzo! Maana uko jirani na kiwanda maarufu cha Sao Hill.

Kwa kweli huu Mji ni mdogo tu lakini uko busy sana kibiashara, na ikumbukwe maeneo ya pembezoni mfano Madibira, Sadani, Mgololo, na pia Mufindi yote kwa ujumla; huutegemea huu mji kwenye suala zima la mahitaji yao muhimu ya kila siku.

Ingawa huu Mji umekuwa ukipokea wageni wa kila aina kila siku kwa ajili ya kununua mbao, nguzo, na mahitaji mengine, umekuwa na upungufu wa nyumba za wageni zenye hadhi. Kiukweli nyumba nyingi za kulala wageni (Lodges + Guest Houses) zilizopo Mafinga ni chafu!

Kwanza mablanketi yao huwa hawafui (ifahamike hili eneo lina baridi mwaka mzima, hivyo lazima ujifunike blanketi). Mara kadhaa nimelazimika kulala Iringa mjini, kwa sababu tu ya huu udhaifu wa nyumba za wageni pale Mafinga.

Hivi shida ni nini kwa wamiliki wa nyumba za wageniza Mafinga? Au ni kwa sababu mnapata faida kubwa kupitia short time? Maana hizo bar zenu maarufu, pamoja na night clubs chache zilizopo; si haba!

Kwa kweli nawashauri mbadilike. Kama vipi pandisheni hata bei za vyumba, huku mkiboresha pia huduma. Kwa kweli mablanketi yeni ni machafu sana. Mtakuja kuwasababishia wateja wenu magonjwa ya ngozi kwa sababu zinazoweza kuzuilika.
Sio kwamba unakwenda lodge za low budget bloangu?
 
Mimi hua nafanya hivi nikifika sehemu namwambia bodaboda anipeleke sehemu nzuri ya kulala wageni yenye kiasi kadhaa
Wale bodaboda wanajua vizuri sehemu nzuri.
Sasa wewe ndugu unajiona wa town unaingia gest za barabarani unazoziona wewe
 
Swala Hilo watu wengi wanalalamika Sana me na nahisi labda hata udogo wa mji unachangi unajua mji ukitanuka huduma Zina sambaa Sana na zinakuwa na ushindani mkubwa Sasa imagine mji ukitoka kinyanambo c hadi changalawe km 14 umemaliza vitu vyote vimebanana hapo lazima iwe shida na hotel ambazo angalau ni Merlin na pop corn tofauti na miji ya iringa na makambako hii imesambaa Sana na huduma za lodge ni nzuri kwa nini mtu asiende kulala huko mafinga inatakiwa wabadilike watapitwa hata na nyororo
 
Ujumbe huu uwafikie wafanyakazi wa hizo nyumba,wamiliki na vibarua wao.Wasisahaulike viongozi wa kata zote wakiongozwa na WEs,Mkurugenzi wa Mji huo awahimize HO/maafisa afya kwa ufuatiliaji wa bampa to bampa.Usafi mwingine wanaweza.Huo unawashinda nini?
 
Karibu sana mafinga
Jaribu kulala guest house at least inayoanzia elfu 30 za kitanzania hizo 20 au 15 ni majanga
Ingawa kuzitaja ni kama matangazo ya biashara kibaguzi lakini ni bora iwe hivyo.Hilo litasaidia wasiotajwa kwa usafi wabadilike.Hamna namna ya kuwasaidia.
 
Kwanza mablanketi yao huwa hawafui (ifahamike hili eneo lina baridi mwaka mzima, hivyo lazima ujifunike blanketi). Mara kadhaa nimelazimika kulala Iringa mjini, kwa sababu tu ya huu udhaifu wa nyumba za wageni pale Mafinga.
Hii inaweza kuwa fursa ya kuanzisha Modern Dry-cleaning mpwa
 
Back
Top Bottom