Mtu porii
Member
- Jan 29, 2024
- 34
- 110
Maisha yangu yanaanzia mkoani Iringa katika mtaa wa Semtema A baada ya kuhitimu chuo 2019. Kodi ya geto ikawa imeisha kulingana msukumo wa mwenye nyumba nkaamua kuuza kilicho changu kama kitanda, gesi na redio.
Nikabadil mazingira na kuamua kwenda kuanza maisha mapya Mafinga huku nikiwa sina ndugu wala jamaa. Nimeshuka mafinga kama saa 10 jion hivi wakat naangalia hela yangu ambayo niliuzia vitu siioni, nikajisachi tena na tena ni kwel haikuwepo.
Niliaanza kuzurura mitaa ya Mafinga huku sijui nnakoenda giza lilivoingia nikaingia kwenye pagale ambalo limeezekwa ila halina mlango nikalala zangu, lile baridi la Mafinga nililisikia kwa undani wake yaani usingizi nimepata saa sita halafu saa tisa nimeshtuka hapo ikawa ni kubaki macho had asubuhi.
Asubuhi ilipambazuka nikatafuta kazi bila mafanikio, nkaenda mafundi niwe hata saidia fund napo nilkataliwa, hatimaye usiku uliingia bila kupata chochote cha kutafuna nkarud kwenye pagale langu.
Siku ya pili nikiwa na njaa nkamfata Bibi mmoja nikamwomba ugal mitaa ya kinyanambo A akasema hana ila ananionesha mti wa mapera nakumbuka nlichuma mengi sana nkaenda kwa pagale nkala kidogo nkapata unafuu.
Harakati za kutafuta kazi ziliendelea bila mafanikio nkaamua kurud zangu kwa pagale ile naingia nakuta harufu kumbe mtu kanya ilbd nihame room japo harufu ilitanda nyumba nzima.
Siku ya tatu niliamka mapema sana nkaelekea Kinyanambo A, nkavuka hadi kinyanambo C, kila sehemu nnayoulizia kazi kupakia mbao naambiwa wamejaa, nkaenda kiwanda cha wachina cha kutengeneza singbod naambiwa had niwe na ID ya mjasriamal kile cha magu cha 20000.
Mimi na njaa yangu nikaenda kiwanda cha Mchina mwingin kwa njaa niliyokuwa nayo nilijikuta tu nalia bado nkaambiwa hadi ID. Nikiwa nimekata tamaa nkaamua kuelekea kaskazini kutokea kinyanambo C naifata barabara ilyoelekea porin.
Baada ya kutembea kama nusu saa hv nkaona kiwanda cha nguzo za umeme cha kwihaya nkaenda kuomba kazi huku akili yangu inaniambia hata wakininyima niwaombe nifanye malipo yawe chakula tu.
Ashukuriwe Mungu yule msimamizi kwa jina la Abuu alinikubalia kazi na akanielekeza jinsi ya kuweka Lebo kwenye nguzo na jion nkapewa Elfu 6000. Pia wakawa wameniomba niwe nalala pale mana Nguzo zinatreatiwa usiku na mchana hvo niwe nasaidia kufungua mlango wa mtungi ambao unaingiza nguzo zaid ya 60 kwa ajili ya kupgwa dawa. Mchana nikawa naingiza elfu 6000 na usiku n 10000.
Baada ya mwezi nilienda kupanga na nikawa na maisha yangu.
Nawaasa vijana wezangu msikate tamaa m ilifika hatua nikafikilia had kujiua na had leo naelewa mtu aliyejiua hatupswi kumlaum hata kidogo..hii dunia ina mambo..
🙏🙏
Nikabadil mazingira na kuamua kwenda kuanza maisha mapya Mafinga huku nikiwa sina ndugu wala jamaa. Nimeshuka mafinga kama saa 10 jion hivi wakat naangalia hela yangu ambayo niliuzia vitu siioni, nikajisachi tena na tena ni kwel haikuwepo.
Niliaanza kuzurura mitaa ya Mafinga huku sijui nnakoenda giza lilivoingia nikaingia kwenye pagale ambalo limeezekwa ila halina mlango nikalala zangu, lile baridi la Mafinga nililisikia kwa undani wake yaani usingizi nimepata saa sita halafu saa tisa nimeshtuka hapo ikawa ni kubaki macho had asubuhi.
Asubuhi ilipambazuka nikatafuta kazi bila mafanikio, nkaenda mafundi niwe hata saidia fund napo nilkataliwa, hatimaye usiku uliingia bila kupata chochote cha kutafuna nkarud kwenye pagale langu.
Siku ya pili nikiwa na njaa nkamfata Bibi mmoja nikamwomba ugal mitaa ya kinyanambo A akasema hana ila ananionesha mti wa mapera nakumbuka nlichuma mengi sana nkaenda kwa pagale nkala kidogo nkapata unafuu.
Harakati za kutafuta kazi ziliendelea bila mafanikio nkaamua kurud zangu kwa pagale ile naingia nakuta harufu kumbe mtu kanya ilbd nihame room japo harufu ilitanda nyumba nzima.
Siku ya tatu niliamka mapema sana nkaelekea Kinyanambo A, nkavuka hadi kinyanambo C, kila sehemu nnayoulizia kazi kupakia mbao naambiwa wamejaa, nkaenda kiwanda cha wachina cha kutengeneza singbod naambiwa had niwe na ID ya mjasriamal kile cha magu cha 20000.
Mimi na njaa yangu nikaenda kiwanda cha Mchina mwingin kwa njaa niliyokuwa nayo nilijikuta tu nalia bado nkaambiwa hadi ID. Nikiwa nimekata tamaa nkaamua kuelekea kaskazini kutokea kinyanambo C naifata barabara ilyoelekea porin.
Baada ya kutembea kama nusu saa hv nkaona kiwanda cha nguzo za umeme cha kwihaya nkaenda kuomba kazi huku akili yangu inaniambia hata wakininyima niwaombe nifanye malipo yawe chakula tu.
Ashukuriwe Mungu yule msimamizi kwa jina la Abuu alinikubalia kazi na akanielekeza jinsi ya kuweka Lebo kwenye nguzo na jion nkapewa Elfu 6000. Pia wakawa wameniomba niwe nalala pale mana Nguzo zinatreatiwa usiku na mchana hvo niwe nasaidia kufungua mlango wa mtungi ambao unaingiza nguzo zaid ya 60 kwa ajili ya kupgwa dawa. Mchana nikawa naingiza elfu 6000 na usiku n 10000.
Baada ya mwezi nilienda kupanga na nikawa na maisha yangu.
Nawaasa vijana wezangu msikate tamaa m ilifika hatua nikafikilia had kujiua na had leo naelewa mtu aliyejiua hatupswi kumlaum hata kidogo..hii dunia ina mambo..
🙏🙏