Bull Bucka
Member
- Oct 5, 2023
- 34
- 46
Jijini Dar es Salaam na maeneo mengine nchini Tanzania, suala la makubaliano kati ya mwenye nyumba na mpangaji ni jambo la kawaida. Makubaliano haya hujumuisha mambo mengi kama vile kodi, malipo ya huduma za nyumba, na masuala mengine yanayohusiana na kukaa kwenye nyumba ya kupanga. Hata hivyo, kuna baadhi ya wenye nyumba ambao huenda zaidi kwa kumuwekea mpangaji sharti la aina ya wageni wa kumtembelea.
Njoja niwape stori kwanza. Mwaka 2017, niliamua kuishi kwenye nyumba moja maeneo fulani huko Goba, Dar es Salaam. Mwenye nyumba naye alikuwa anaishi hapo, na tukiwa tayari kwenye mkataba wa kupanga, hakunipa taarifa yoyote kuhusu sharti la kutoleta wageni wa jinsia tofauti.
Mwenye nyumba alianza kuonesha wasiwasi juu ya wageni wa kike waliokuwa wakija kunitembelea. Alifanya mambo kama kuniangalia kwa jicho la tatu kila wageni wa kike walipokuja. Yaani alikuwa hadi akisimamisha shughuli zake ili kujiridhisha kama walikuwa wageni aliowahi kuwaona awali au ni wageni wapya.
Siku moja, alinitolea uvivu na kuniambia kuwa wageni wa kike wamekuwa wengi sana kwenye nyumba. Nilimuuliza ikiwa kuna siku nilivunja amani au niliwahi kusababisha fujo na kelele zisizo za kistaarabu, na jibu lake lilikuwa "hapana." Tatizo lake na wageni wa kike eti ni kwamba nitawaharibu wanae kwa kushuhudia vitendo vya “kimalaya”. Cha! Nilichoka.
Hata hivyo sikukaa kimya. Nilimkumbusha mwenye nyumba kuwa watoto wake wanahitaji kufundishwa kuhusu ustaarabu na kuheshimu watu na wasiige mambo ya kipuuzi hata wakiwa huko shule. Nilimkumbusha kuwa ana jukumu hilo la kutekeleza kwa wanae na si kwa kumzuia mpangaji kuleta wageni.
Nilisisitiza pia kuwa si kila mwanaume au mwanamke anayekuja kumtembelea mpangaji anakuja kwa lengo la kufanya mambo ya kimapenzi. Baadhi ya wageni ni marafiki wa kawaida, ndugu, au jamaa ambao wanataka kutembelea na kufurahi pamoja. Nilimwambia kuwa si sahihi kuvunja ustaarabu na uhuru wa mpangaji kwa kisingizio cha kuwalinda watoto wake.
Lakini pia nilimwambia kuwa bado mimi ni kijana na nipo katika mchakato wa kutafuta mwenza wa maisha. Kwa hiyo, baadhi ya wageni wa kike, mbali na marafiki na familia, wanaweza kuwa wanawake ambao ninafikiria kuwa huenda nikaoa siku za usoni, kwahiyo hakupaswa kuninyima fursa ya kupenda na kupendwa. Sijui alitaka niishi vipi mzee yule. Sema alijitahidi kunielewa.
Wenye nyumba, kuweka mazingira ya kukodisha ambayo yanawapa wapangaji uhuru wa kufanya maamuzi kuhusu wageni wao ni muhimu sana. Hii inahitaji uelewa wa utofauti wa tamaduni, imani, na mienendo ya kijinsia.
Kuwapa wapangaji nafasi ya kuwa na wageni au marafiki bila kuwahukumu au kuwabagua ni ni jambo la msingi sana. Pia, ni muhimu kuondoa ubaguzi wa kijinsia na kuacha watu wa jinsia tofauti kuwa na mahusiano ya urafiki au kufanya shughuli pamoja bila kutafsiriwa kwa dhana za ngono. Cha!
Njoja niwape stori kwanza. Mwaka 2017, niliamua kuishi kwenye nyumba moja maeneo fulani huko Goba, Dar es Salaam. Mwenye nyumba naye alikuwa anaishi hapo, na tukiwa tayari kwenye mkataba wa kupanga, hakunipa taarifa yoyote kuhusu sharti la kutoleta wageni wa jinsia tofauti.
Mwenye nyumba alianza kuonesha wasiwasi juu ya wageni wa kike waliokuwa wakija kunitembelea. Alifanya mambo kama kuniangalia kwa jicho la tatu kila wageni wa kike walipokuja. Yaani alikuwa hadi akisimamisha shughuli zake ili kujiridhisha kama walikuwa wageni aliowahi kuwaona awali au ni wageni wapya.
Siku moja, alinitolea uvivu na kuniambia kuwa wageni wa kike wamekuwa wengi sana kwenye nyumba. Nilimuuliza ikiwa kuna siku nilivunja amani au niliwahi kusababisha fujo na kelele zisizo za kistaarabu, na jibu lake lilikuwa "hapana." Tatizo lake na wageni wa kike eti ni kwamba nitawaharibu wanae kwa kushuhudia vitendo vya “kimalaya”. Cha! Nilichoka.
Hata hivyo sikukaa kimya. Nilimkumbusha mwenye nyumba kuwa watoto wake wanahitaji kufundishwa kuhusu ustaarabu na kuheshimu watu na wasiige mambo ya kipuuzi hata wakiwa huko shule. Nilimkumbusha kuwa ana jukumu hilo la kutekeleza kwa wanae na si kwa kumzuia mpangaji kuleta wageni.
Nilisisitiza pia kuwa si kila mwanaume au mwanamke anayekuja kumtembelea mpangaji anakuja kwa lengo la kufanya mambo ya kimapenzi. Baadhi ya wageni ni marafiki wa kawaida, ndugu, au jamaa ambao wanataka kutembelea na kufurahi pamoja. Nilimwambia kuwa si sahihi kuvunja ustaarabu na uhuru wa mpangaji kwa kisingizio cha kuwalinda watoto wake.
Lakini pia nilimwambia kuwa bado mimi ni kijana na nipo katika mchakato wa kutafuta mwenza wa maisha. Kwa hiyo, baadhi ya wageni wa kike, mbali na marafiki na familia, wanaweza kuwa wanawake ambao ninafikiria kuwa huenda nikaoa siku za usoni, kwahiyo hakupaswa kuninyima fursa ya kupenda na kupendwa. Sijui alitaka niishi vipi mzee yule. Sema alijitahidi kunielewa.
Wenye nyumba, kuweka mazingira ya kukodisha ambayo yanawapa wapangaji uhuru wa kufanya maamuzi kuhusu wageni wao ni muhimu sana. Hii inahitaji uelewa wa utofauti wa tamaduni, imani, na mienendo ya kijinsia.
Kuwapa wapangaji nafasi ya kuwa na wageni au marafiki bila kuwahukumu au kuwabagua ni ni jambo la msingi sana. Pia, ni muhimu kuondoa ubaguzi wa kijinsia na kuacha watu wa jinsia tofauti kuwa na mahusiano ya urafiki au kufanya shughuli pamoja bila kutafsiriwa kwa dhana za ngono. Cha!