Mukuru
Member
- Apr 14, 2009
- 40
- 0
Tumeshuhudia mengi tangu Ndugu Samuel Sitta awe Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kiasi kikubwa amekuwa na tofauti na maspika waliomtangulia kwa jinsi anavyoendesha shughuli zake kama kiongozi wa mmojawapo ya mihimili ya dola. Kuna wanaomsifu kwa utendaji wake na kuna wanaodai kuwa ana 'nguvu ya soda' hivyo tusitarajie lolote jipya zaidi ya 'longolongo' huku akijificha nyuma ya kivuli cha chama chake.
Mtu upimwa uwezo wake pale afikwapo na misukosuko inayohitaji busara na uwezo wa kutetea kile unachoamini kwa masilahi ya wanyonge amabo wameweka imani kwako kama kiongozi wao.
Yaliyojiri katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM yanabainisha kuwa ile slogan ya Ndugu Sitta ya 'kasi na viwango' inawezekana ikagonga mwamba hasa ukizingatia kuwa ikija kwenye suala la 'ulaji' CCM inabakia kuwa CCM bila kujali una wadhifa gani. Kitendo cha Ndugu Sitta kunywea wakati wa kikao cha NEC kinanipa picha kuwa Spika ana hali ya uvuguvugu...ana chembe chembe za uzalendo na pia ana chembe chembe za masilahi binafsi na ya chama....aidha ana chembe chembe za masilahi ya taifa lakini nashawishika kuamini kuwa kiasilimia chembe chembe za utaifa alizonazo ni kidogo mno. Sitashangaa Spika Sitta akigeuka nyuma na kuwa nguzo ya chumvi katika vikao vijavyo vya bunge.
Hayo ni mawazo yangu......wewe unadhani tutarajie lipi kwa Spika Sitta kwa kipindi kilichobakia cha uspika wake hasa ukizingatia "wenye chama" wameshamwonyesha kadi ya manjano?
Mtu upimwa uwezo wake pale afikwapo na misukosuko inayohitaji busara na uwezo wa kutetea kile unachoamini kwa masilahi ya wanyonge amabo wameweka imani kwako kama kiongozi wao.
Yaliyojiri katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM yanabainisha kuwa ile slogan ya Ndugu Sitta ya 'kasi na viwango' inawezekana ikagonga mwamba hasa ukizingatia kuwa ikija kwenye suala la 'ulaji' CCM inabakia kuwa CCM bila kujali una wadhifa gani. Kitendo cha Ndugu Sitta kunywea wakati wa kikao cha NEC kinanipa picha kuwa Spika ana hali ya uvuguvugu...ana chembe chembe za uzalendo na pia ana chembe chembe za masilahi binafsi na ya chama....aidha ana chembe chembe za masilahi ya taifa lakini nashawishika kuamini kuwa kiasilimia chembe chembe za utaifa alizonazo ni kidogo mno. Sitashangaa Spika Sitta akigeuka nyuma na kuwa nguzo ya chumvi katika vikao vijavyo vya bunge.
Hayo ni mawazo yangu......wewe unadhani tutarajie lipi kwa Spika Sitta kwa kipindi kilichobakia cha uspika wake hasa ukizingatia "wenye chama" wameshamwonyesha kadi ya manjano?