Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Mag3,
Jibu lako rahisi sana.. Alichofanya JK ktk kikao hicho ndicho alichofanya Sitta Bungeni. Sasa kama Sitta analaaniwa kwa kulifanya Bunge kuwa sehemu ya kuibua mashitaka, kuendesha kesi na kutoa hukumu, badala ya kuwa chombo cha kutunga sheria,” Unafikiri JK kafanya nini pale mkutano mkuu wa chama ambacho ni tofauti na Sitta?..

JK kaachia vurugu lipambe ktk mkutano muhimu wa chama... tumeona mashtaka, kuendeshwa kwa kesi, na hukumu zikitolewa badala ya kupanga mikakati endelevu ya chama..lengo lake ni ktk kutaka mafisadi wajitokeze kama Sitta alivyowakoroga Mafisadi bungeni.

Unless unataka kunambia Sitta hakujua alichokuwa akifanya Bungeni hivyo yawezekana kabisa hata JK hakufahamu jinsi ya ku deal na swala hilo ktk kikao hicho. Na hata kama hakujua kumbuka agenda hizi hupitiwa na baraza klabla hawakubali ziwekwe mbele.. pale mchezo ulishapangwa mkuu wangu.. ruksa haikutoka bure!

JK kama mwenyekiti angeweza kabisa kuiondoa mada hiyo ktk agenda za mkutano lakini aliachia wazi kama alivyokuwa akiachia Sitta habari za mafisadi..Jmimi nadhani JK kawavuruga CCM kuliko hata Sitta bungeni kwani sasa hivi uhasama wao uko nje nje..wanajua nani yuko upande gani.
Umenipata mkuu wangu...
Haaa! upo right! JK ni mjanja = Smart; he needs both money and votes; so he has to play his Smart Card both ways: For one side he needs money to steal the votes; in the other side he needs the people (playing as if he is clean)

Yes smart boy - Mjanja
 
Kama kweli JK akiwa mwenyekiti wa Chama, akiwa Rais wa nchi na akiwa mtu mzima, sitegemei kama anaweza kutoa maneno ya kejeli kwa Guninita, tena ndani ya kikao kikubwa cha Chama. Sijui ni kwanini viongozi wetu wasiwe na manners za kuongea.

Inazidu kuonesha kuwa heshima ya vikao vya juu inazidi kupungua. Kama lugha ya kistaarabu haitumiki, inawezekana hata maamuzi yasiwe ya kistaarabu.
 
Wazee na Waheshimiwa wana jamvi

Nikiwa mjumbe wa NEC nisiye na kundi lolote, nawajibika kuweka sawa rekodi moja katika mjadala unaoendelea kuhusu Spika Sitta na kilichotokea ndani ya ukumbi wa mkutano wa NEC.

Baada ya mjadala mrefu ulioshabikiwa sana na wajumbe wengi huku hoja zao zikijiwa bila jazba na wajumbe wachache lakini wanaoheshimika, Spika Sitta alikutana faragha na Mwenyekiti JK, Rais Mwinyi na Kinana. Baada ya faragha ile ambayo bado ni siri, Spika Sitta alipopata nafasi alisema maneno machache sana yenye pointi mbili. Kwanza, aliwashukuru wajumbe kwa kutumia uhuru wao kutoa maoni yao. Pili, alisema anaiachia meza kuu kutafakari yaliyosemwa na pande zote. Kisha alimaliza na kukaa.

Hata kama sikubaliani na baadhi ya misimamo yake, siwezi kusema kuwa aliomba radhi. Lakini pia siwezi sema alikosa watetezi kama inavyoripotiwa. Kulikuwa na hoja nzito, tena nyingine kutoka visiwani zilizomtetea.

Kiroja cha mjadala alikuwa Guninita, Mwenyekiti wa Mkoa wa DSM aliyechemka lakini JK akamzodoa kwa kumwambia "kama ana uchungu na chama mbona alikiacha na kwenda CHADEMA na kuitukana CCM kwa miaka miwili?"

Habari ni hiyo.

Baija

Ninashukuru kwa ufafanizi huu Baija, kwani niliposoma taarifa kuwa Sitta aliomba radhi baada ya yule mwizi ambae pia ni mwenyekiti wa CCm Shinyanga na mafisadi wenzie kuropoka hovyo mkutanoni, sikuelewa sababu ambayo ingemfanya Sitta aombe radhi!! Mtu huomba radhi baada ya kufanya kosa au makosa ,sasa Sitta alifanya kosa gani kuweka bayana baada ya ushahidi kuwa Makamba na Londa walihusika na ufisadi katika halmashauri ya Kinondoni? Je ni kuikosea CCM kuiambia serikali yake kuwa haikuwajibika vilivyo kutekeleza maagizo ya BUNGE kuhusu mafisadi wa RICHMOND?? Kama hivyo ndivyo basi Sitta hana budi kufanya uamuzi wa busara na wa kishujaa juu ya nchi yake kuhusiana na chama cha Mafisadi!!!
 
Kigogo, ni kweli niko Dodoma hata sasa. Ukipenda niweke upande wowote, maana hali ilivyo kwa sasa, kubaki katikati ni hatari zaidi.

SIna hakika kwamba Baija Bolobi ni M-NEC, hii ni kwa sababu humu tumeingia na majina tofauti na yetu halisia, na pia nachelea muamini haya kwani kuna wa-NEC wengi tu walio humu wangeshakanusha mapema

Anyway, tunashukuru kama taarifa hii ni yakweli.... Maana CCM leadership yenyewe inatuchanganya na kama wewe ni M-NEC basi wote mnatuchanganya kwa kuwa rumour mongers, na hii ni mbaya sana kwa Taifa letu

Jisafisheni muwe na kauli moja kama chama

BTW M-NEC wa ID yako, location na signature yako---kaazi sana tu!!!!!!!!!!!
 
Last edited:
Well, pima mwenyewe uamue. Nilikuwa ndani ya kikao. Waandishi wanaoandika kuwa kaomba radhi wanasema "Chanzo chetu cha uhakika ndani ya kikao".

Ni kweli mambo yalikuwa mazito kweli kwa sababu wabaya wa Sitta walipoona hawaungwi mkono kama walivyotaka, na hasa baada ya kuona JK hashtuki na kuwaunga mkono, wakaja na kubwa zaidi: Wakadai Sitta anautaka Urais kupitia bungeni na wakataja matukio kadhaa kuunga mkono madai yao hayo.

Tunakoenda ni giza tupu ndugu zangu. Akina mama wengi wamelia sana ukumbini.

Huu ndiyo ukweli wa mambo, kwamba nchi yetu sasa hivi inaingia kwenye giza nene na la kutisha.

Hili la akina Mama kulia ni kuonyesha wasiwasi wao mkubwa wa hali ya kisiasa nchini ambayo sasa hivi inatisha sana.
 
I really don't care kile CCM wanafanya kwenye mikutano yao na kwa wanachama wao! Hizo ni "party politics". Lakini wanapovuka mpaka wa kuanza kuhoji mambo yanayofanyika Bungeni kwenye vikao vyao vya chama wanavunja mpaka wa uelewa wa uhuru wa mihimili. Hivi ni kitu gani kitawazuia nec kujadili Mahakama Kuu siku Mahakama hiyo ikitoa hukumu ya kuiumiza CCM?

Kosa la Sitta katika hili ni kuentertain malalamiko yanayohusiana na Bunge kujadiliwa kwenye kikao cha CCM. Alitakiwa kuwakatalia pale pale kuwa kama kuna mtu ana issue na yeye kuhusu Bungeni ailete Bungeni; kama siyo Mbunge awasiliane na Mbunge wake wailete Bungeni; na kama ni wabunge wengi wa CCM basi wana kakasi zao kule Bungeni wangeweza kuzungumza na kuchukua msimamo kule. ASINGEKUBALI kabisa kujadili mambo ya Bunge au kuacha watu wamuweke kwenye kona kutokana na nafasi yake ambayo si ya chama.

Kwa kukubali ameshusha hadhi ya uhuruwa USPIKA ni lazima arudishe. Sitarajii Jaji Mkuu kuitwa na CCM na kwenda kuwatolea maelezo ya jinsi gani maamuzu fulani yamefikiwa, kwanini SPIKA akubali?
 
I really don't care kile CCM wanafanya kwenye mikutano yao na kwa wanachama wao! Hizo ni "party politics". Lakini wanapovuka mpaka wa kuanza kuhoji mambo yanayofanyika Bungeni kwenye vikao vyao vya chama wanavunja mpaka wa uelewa wa uhuru wa mihimili. Hivi ni kitu gani kitawazuia nec kujadili Mahakama Kuu siku Mahakama hiyo ikitoa hukumu ya kuiumiza CCM?

Kosa la Sitta katika hili ni kuentertain malalamiko yanayohusiana na Bunge kujadiliwa kwenye kikao cha CCM. Alitakiwa kuwakatalia pale pale kuwa kama kuna mtu ana issue na yeye kuhusu Bungeni ailete Bungeni; kama siyo Mbunge awasiliane na Mbunge wake wailete Bungeni; na kama ni wabunge wengi wa CCM basi wana kakasi zao kule Bungeni wangeweza kuzungumza na kuchukua msimamo kule. ASINGEKUBALI kabisa kujadili mambo ya Bunge au kuacha watu wamuweke kwenye kona kutokana na nafasi yake ambayo si ya chama.

Kwa kukubali ameshusha hadhi ya uhuruwa USPIKA ni lazima arudishe. Sitarajii Jaji Mkuu kuitwa na CCM na kwenda kuwatolea maelezo ya jinsi gani maamuzu fulani yamefikiwa, kwanini SPIKA akubali?
Mkuu, hapana mimi naelewa tofauti ktk swala hili...sidhani kama Sitta ana madaraka hayo inapofikia kikao cha chama..Madaraka yake bungeni yanabakia kama mbunge mwenyekiti wa vikao vya Bunge, lakini pale ktk kikao alikuwa sawa na wajumbe wengine kwa hadhi ya chama..Na wana CCM wana kila sababu ya kuhoji utendaji wake wa kazi aliyokabidhiwa kama mbunge mwakilishi wa chama ktk kiti cha Uspika, pamoja na kwamba anatakiwa kuwa huru na muwazi.
Hawezi kufanya unavyosema wewe hata kidogo kwani atakuwa mtovu wa kikao muhimu cha chama na yawezekana kabisa hata huyo JK angeweza kuhojiwa yeye kulingana na katiba ya chama. Kama chama hakina imani na JK na wanataka kumweka kitimoto basi pale ndipo mahala pake kutafuta no-confidence motion. Hawezi kuwaambia mwenye hoja amfuate Ikulu kwani hizi ni sehemu mbili tofauti.

Nakumbuka kama miaka 10 hivi iliyopita PM wa Canada akiitwa Martin aliwekwa kitimoto na kikao kama hiki wakahoji utendaji wake wa kazi kulingana na mrengo, ilani na sera za chama. Na kweli alikuwa amekishusha chama hadhi na sifa walizojengewa na kiongozi aliyetangulia...baada ya kikao kile haikuchukua muda Martin alijiuzuru...Hakika naweza kusema kesi hii ya Lowassa na JK inafanana sana na kesi ya former PM Chretien na huyo Martin. Njama za martin dhidi ya Chretien zinafanana sana na hizi za Lowassa na RO against JK...

Angalia basi hata baada ya mgogoro huo kwisha na Chretien kupoteza nafasi ile akachukua mchumi aliyesifika kwa kila sifa huyo Martin (Lowassa) matokeo yake Liberal waliharibikiwa kabisa na toka siku hiyo Liberal walipoteza ushindi wao kitaifa na hawajaweza kuurudisha tena.
Hivyo tukumbuke tu ukiwa a good Economist haina maana unaweza kuwa a good leader hata kidogo.. Mimi husema hivi Economist ni sawa na mwandalizi, msafisha meza baada ya watu kula..Hivyo uwezo wake wa maandalizi ya chakula na sherehe nzima haiwezi kumfanya akawa mpishi mzuri.
Tuwe makini sana tunapochagua viongozi wetu, mifano kama hii itumike kama funzo kwetu sisi nchi maskini ambazo bado hatufahamu tofauti kati ya Kongozi bora na msomi.
 
Last edited:
Nasikia kuna uvumi kwamba, Sitta ndiye anaonekana msafi kidogo ndani ya chama. Ikitokea JK hakubaliki mwakani Sitta wanataka awe mbadala. Nawakilisha wakuu.
.. hakubaliki na nani? tatizo hoja ya ufisadi haiwasisimui sana wananchi vijijini, ukweli hawana muda kuifuatilia,ni hoja inayozungumziwa mjini zaidi kwa watu wasiopiga kura,ni bahati mbaya, hata uchaguzi ukifanyika leo asubuhi JK atashinda kwa kura za ajabu. Hata kule Mbeya alikopigwa mawe sio kwa sababu ya kutomtaka bali walikasirika kwa sababu hakusimama. Fuatilia ziara zake za mikoani, hususan vijijini..mugambo wanaruka na kukanyagana. Huo ni upande wa pili wa JK. Hata kama haipendezi, wananchi hawana habari sana ya nini kinachoendelea!
 
Chama Cha Mapinduzi ni chama cha wananchi. Kiongozi yeyote aliye madarakani kwa tiketi ya CCM aelewe kuwa nafasi hiyo aliyonayo ni dhamana aliyopewa kwa ridhaa ya wanachama wa CCM. Haitavumilika wala kukubalika kwa kiongozi yeyote yule anayetokea CCM kutumia nafasi hiyo kwa ajili ya kujijenga binafsi kwa gharama ya kuharibu maadili na maslahi ya chama. Pia ieleweke kuwa Chama cha Mapinduzi kina utaratibu na, viongozi na wanachama waliomakini katika kukabiliana na matatizo yanayoweza kujitokeza ndani na nje ya Chama.
Endapo kiongozi yeyote yule amekwenda kinyume na maadili au maslahi ya Chama basi hana budi kuwa muungwana na kuomba radhi na ajisahihishe. Vinginevyo, arudishe kadi!

Je ina maana CCM si tena Chama cha Wakulima na Wafanyakazi?

Je ina maana Maslahi ya CCM ni ya muimu na yapewe kipaumbele kuliko maslahi ya Taifa na Wananchi wa Tanzania?

Je Maadili na Maslahi ya CCM ni yapi?

Kama CCM ina nguvu na uwezo wa kuijtegemea kivyakevyake, kwa nini inang'ang'ania Katiba ya Tanzania na kulazimisha kila mtu afuate na kusika inachokisema?
 
mi nadhani sasa hivi siasa ya tanzania inaelekea kubaya, halafu wanasiasa wengi hawapendi kuambiwa ukweli, kutoakana na mabaya wanayoyafanya ili kulinda MAOVU YAO. Samweli sitta huwa hapendi unafiki, anakupa live ndio maana wanasiasa wengi hawampendi hasa wale mafisadi
 
Baija Bolobi,
Asante sana kwa taarifa yako. Usipoteze muda kubishana na hao wanaopenda kusoma au kusikia habari zenye vidokezo vya "chanzo chetu, (jina tunaliifadhi)".

Nimeipenda hii siganture yako "Walikuja dhaifu" nami naongeza wakarudi bila ushindi
 
nimesikia asubuhi hii gazeti moja nimeandika kwamba mh Sita anatarajiwa kupewa tuzo kwa kuongoza vikao vya bunge vyema,je hilo nalo halitaleta maafa kwa chama cha ccm ?
 
magazeti ya rostam ndio yaliripoti kuwa sitta ameomba radhi na mhariri wao kibaraka muhingo rweyemamau yule jamaa mwembamba mwenye pua ndefu na sura ya ajabu kibaraka wa rostam na lowassa alikuwapo dodoma na ndio alitunga uongo huo kwa kusaidiana na kibaraka balile mtoto wa mkulima anaye futa viatu vya mafisadi ili apate ugali.kimsingi ni vijigazeti vilevile vya udaku yaani mtanzania na tanzania daima ndio vili exagarate habari hiyo ionekane sitta ameomba radhi ila kimsingi mafisadi wamekwama tena,..
 
Well, pima mwenyewe uamue. Nilikuwa ndani ya kikao. Waandishi wanaoandika kuwa kaomba radhi wanasema "Chanzo chetu cha uhakika ndani ya kikao".
Ni kweli mambo yalikuwa mazito kweli kwa sababu wabaya wa Sitta walipoona hawaungwi mkono kama walivyotaka, na hasa baada ya kuona JK hashtuki na kuwaunga mkono, wakaja na kubwa zaidi: Wakadai Sitta anautaka Urais kupitia bungeni na wakataja matukio kadhaa kuunga mkono madai yao hayo.

Tunakoenda ni giza tupu ndugu zangu. Akina mama wengi wamelia sana ukumbini.

Nimepima Mwenyewe ila nashindwa kukutofautisha wewe Baija na hao waliosema Chanzo chetu cha uhakika ndani ya kikao kwa sababu kama wewe umeshindwa kujitaja iweje uwalaumu walioshindwa kutaja Chanzo?
 
Mr PhD,

Ivi huyo mhariri wa kihaya a.k.a muhingo i wish to see his face phisycaly ni mhaya wa aina gani kwanza? na ananjaaa kiasi gani ni mnafiki sana huyo mhariri nasikiaaga mambo yake hatufai huyo, kazi kuwachanganya watanzania iyo isue imezunguka nchi nzima kwa muda mchacche sana, ila wakae wakijua hawatoshinad hao MAFISADI kamwe,Muda wao ndio umekwisha by the way hayo magazeti huwa siyanunui kabisa.
 
Mkuu Baija Bolobile,'wamekuja wamelegea', (am I assuming correctly your full JF name?) nakufagilia makofi wa wa wa wa wa wa wa !!!!!!!!!. To be sincere CCM ilikuwa inachezea kaa la moto na safari hii one mistake I doubt kama Chama kingekuwa na ujanja wa kuchomoa. Kudos kwa Jakaya kuliona hili na kuamua afunike kombe shaitwani apite,kama kapita hajapita hilo sasa ni suala la sisi sote kusubiria. Ushauri wa bure,na huu si kwa CCM tu bali ni kwa vyama vyote,tujifunze kuangalia tunapojikwaa na si pale tunapoangukia.
 
Last edited:
magazeti ya rostam ndio yaliripoti kuwa sitta ameomba radhi na mhariri wao kibaraka muhingo rweyemamau yule jamaa mwembamba mwenye pua ndefu na sura ya ajabu kibaraka wa rostam na lowassa alikuwapo dodoma na ndio alitunga uongo huo kwa kusaidiana na kibaraka balile mtoto wa mkulima anaye futa viatu vya mafisadi ili apate ugali.kimsingi ni vijigazeti vilevile vya udaku yaani mtanzania na tanzania daima ndio vili exagarate habari hiyo ionekane sitta ameomba radhi ila kimsingi mafisadi wamekwama tena,..

Mkuu PhD heshima mbele kwanza ,Weka kwanja lako chini ndo uingie jamvini.Mambo ya kuingia jamvini na kwanja na tupa ya kunolea aaaahaa nachoka kabisa.Kuna siku utaamua kumwaga damu za watu humu jamvini ACHA HIZO!!
 
Back
Top Bottom