Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

nashawishika kuamini kwamba MAFISADI WATASHINDA!
 
Field Marshall Es,

Mkuu wangu huwezi kuwajua wabaya wako bila kuwapa nafasi wakajikaanga wenyewe.. maneno mazito yaliyosemwa against Sitta ni ushahidi tosha wa watu waliopo nyuma ya Lowassa na RO..this is what JK alikuwa akihitaji siku zote.. names!..Tena basi wamepatikana na wengine waliokuwa wamejificha kwa sababu tu walifikiria JK yuko nao pamoja..

FMES, kwa lugha yetu ya kizamani unaitwa borntown,hivi kweli unaamini JK angetaka Sitta atolewe nje angekuwa na mazungumzo naye baadaye!.. Mbona asimshauri Lowassa kuomba msamaha bungeni..JK anamhitaji Sitta na kazi yake kaifanya hasa ktk mkutano huu mkuu kwani prediction za mzee Malecela zilihusiana zaidi na watu wanaotakiwa kusimama Ubunge mwaka 2010. By now wameisha jua wataanzia wapi kufanya usafi kisha mtaambiwa wananchi kuwa wachafu wote wameondolewa!..Na wananchi wasipokaa macho mshindi CCM kwa goli la kilaini utadhani Droba dakika ya 90 kuleta ushindi.

- Very strong analysis Bob, lakini the damage was done mkuu, kama sio hoja ya kumng'oa Makamba kuchomekewa na wapiganaji mle ndani ya kikao, saa hizi Six angekua njiani kurudi Urambo tayari mazee! maana Muungwana ni mazishi bro, halafu umesikia mafisadi walivyomchokonoa Mengi tena! Inasikitisha sana! Bob Muungwana hatabiriki, muulize Mkulu Saeed.

Respect.

FMEs!
 
- Very strong analysis Bob, lakini the damage was done mkuu, kama sio hoja ya kumng'oa Makamba kuchomekewa na wapiganaji mle ndani ya kikao, saa hizi Six angekua njiani kurudi Urambo tayari mazee! maana Muungwana ni mazishi bro, halafu umesikia mafisadi walivyomchokonoa Mengi tena! Inasikitisha sana! Bob Muungwana hatabiriki, muulize Mkulu Saeed.

Respect.

FMEs!

Mkuu unaweza tutajia waliokuwa upande wa six na walio upande wa Muungwana?? muungwana atabirike kivipi wakati group lake linaeleweka ni mtandao halisi yani Lowasa,Ra,Nchimbi nk
 
Naomba Mungu hadithi zako ziwe za uwongo kwani hakuna mtu anayenikatisha tamaa kama wewe. JM anayepanga mikakati ya kuiba kura (busanda) ni hatari sana. Tunapoongea kung'oa mafisadi nadhani na yeye yumo!

- Pole sana mkuu, by the way kwa nini hakuiba kura za Tarime?

Respect.


FMEs!
 
Mkuu unaweza tutajia waliokuwa upande wa six na walio upande wa Muungwana?? muungwana atabirike kivipi wakati group lake linaeleweka ni mtandao halisi yani Lowasa,Ra,Nchimbi nk

- Muungwana ana kundi moja tu sasa hivi nalo ni yeye na Membe, that is it! the rest anacheza tu mchezo wa kuigiza!

Respect.

FMEs!
 
du kembe mil 50 inaweza kufanya mambo mengi kiasi hicho
siamini!!!!!
kweli wajumbe wa nec ccm ni very cheap?????
ndio maana kila siku wanarudi kuwa omba omba, sasa hiyo mil 50 wakigawana itawapeleka wapi
halafu wenzao wanakamua bil 50
Wacheni ushamba huo. Sisi hatubabaiki na vijipesa kama hivyo. Na kwa taarifa yako wajumbe wa Visiwani(sema Zanzibar mara nyengine) are not cheap as you are. Lakini huyo Spika wenu haizungumzii Zanzibar -uzuri- ndiyo anakandiwa hivyo. Tafuta kumbu kumbu kuna wakati fulani Spika aliepita (Msekwa ) alikandiwa hivyo hivyo na wajumbe wa Zanzibar kwa sababu ya hulka yake ya kuisema vibaya Zanzibar. Ni jambo zuri kuwa alijirekebisha. This is food for thought
 
- Muungwana ana kundi moja tu sasa hivi nalo ni yeye na Membe, that is it! the rest anacheza tu mchezo wa kuigiza!

Respect.

FMEs!

Mkuu heshima yako
mie nafikiri muungwana yupo virtually connected na akina Lowasa ,nahisi hilo la kina membe ni changa la macho tu.

Kama kweli angekuwa hayupo na akina Lowasa angekuwa kishawaning'iniza siku nyingi kwanza kabisa kile kitendo cha kuwapeleka kolokoni akina lowasa angepita ktk urais bila kikwazo chochote ,pia angesifika sana kwa rafiki zake akina Obama tatu Tanzania ingekuwa nchi ya kuigwa afrika.Short of that yupo pamoja nao.
 
Last edited:
- Very strong analysis Bob, lakini the damage was done mkuu, kama sio hoja ya kumng'oa Makamba kuchomekewa na wapiganaji mle ndani ya kikao, saa hizi Six angekua njiani kurudi Urambo tayari mazee! maana Muungwana ni mazishi bro, halafu umesikia mafisadi walivyomchokonoa Mengi tena! Inasikitisha sana! Bob Muungwana hatabiriki, muulize Mkulu Saeed.

Respect.

FMEs!
Yote hii ilipangwa babuuu, kama JK angetaka Sitta awe nje hakuna mtu yeyote angepinga lakini kwa ujinga wao walifikiria JK yuko nao na huu ndio mwisho wa makelele ya Sitta bungeni.
Kumbuka mkuu Sitta wa leo sii yule aliyenza na Lowassa au wakati sakata la Richmond linapingwa na Lowassa kuzungumziwa.. Sitta alikuwa mklai hata Zitto kutolewa nje ya kikao lakini baada ya kupata baraka za JK unajua yaliyofuata.

Ilibidi ionekane kuwa JK hayupo na Sitta ili kujaza kokoro..kisha ajabu kutoka kwa Sitta kulikuwa rahisi sana kwani waamuzi hawakuwa tena wajumbe wapinzani ila wazee wa CC kina Mwinyi ambao tayari wanajua kinachofuatia..Mkuu wangu wazee wote wa CCM wanataka JK akawajibishe Mafisadi kukisafisha chama -How na ukubwa wa kundi hilo ndio ilikuwa shida kwani uchaguizi mkuu wa 2010 adui wa kwanza wa CCM ni Mtandao.. wakiwaondoa hao, kazi iliyobakia ndogo sana..
 
Wazee na Waheshimiwa wana jamvi

Nikiwa mjumbe wa NEC nisiye na kundi lolote, nawajibika kuweka sawa rekodi moja katika mjadala unaoendelea kuhusu Spika Sitta na kilichotokea ndani ya ukumbi wa mkutano wa NEC.

Baada ya mjadala mrefu ulioshabikiwa sana na wajumbe wengi huku hoja zao zikijiwa bila jazba na wajumbe wachache lakini wanaoheshimika, Spika Sitta alikutana faragha na Mwenyekiti JK, Rais Mwinyi na Kinana. Baada ya faragha ile ambayo bado ni siri, Spika Sitta alipopata nafasi alisema maneno machache sana yenye pointi mbili. Kwanza, aliwashukuru wajumbe kwa kutumia uhuru wao kutoa maoni yao. Pili, alisema anaiachia meza kuu kutafakari yaliyosemwa na pande zote. Kisha alimaliza na kukaa.

Hata kama sikubaliani na baadhi ya misimamo yake, siwezi kusema kuwa aliomba radhi. Lakini pia siwezi sema alikosa watetezi kama inavyoripotiwa. Kulikuwa na hoja nzito, tena nyingine kutoka visiwani zilizomtetea.

Kiroja cha mjadala alikuwa Guninita, Mwenyekiti wa Mkoa wa DSM aliyechemka lakini JK akamzodoa kwa kumwambia "kama ana uchungu na chama mbona alikiacha na kwenda CHADEMA na kuitukana CCM kwa miaka miwili?"

Habari ni hiyo.

Baija
 
Kiroja cha mjadala alikuwa Guninita, Mwenyekiti wa Mkoa wa DSM aliyechemka lakini JK akamzodoa kwa kumwambia "kama ana uchungu na chama mbona alikiacha na kwenda CHADEMA na kuitukana CCM kwa miaka miwili?"
Duh, kama ni kweli basi anatakiwa kufikiria kwa mapana kauli kama hiyo!
 
Binafsi ninakubariana na uchambusi wa bwana Mkandara. Kutokana na kikao hiki Mukuu amekwishapata data kamiri za mafisadi na mutandao wao hasa viongozi na vibaraka wao ambao ni wajumbe wa NEKI. Ninalinganisha haya matukio na Mkuu alivyofanywa kuhusiana na suala la EPA ambako alifanikiwa kurudisha baadhi pesa zilizoibiwa na mafisadi.

Asingetumia strategy aliyotumia nina uhakika tungekosa kote kote. Pesa zetu zote zingepoteya/sisingerudi na mafisadi wangebaki kupeta kutokana na udhaifu na corruption katika justice systemu yetu ambayo itachukua muda murefu kuifanyia marekebisho.

Sasa tusubiri tuwone ataufanya nini huu mutandao wa mafisadi kwasababu sasa anawajuwa wabaya wake wote kama kweli alikuwa hana uhakika kabula ya hapo!

--S Horizons
 
Nidhamu hairejeshwi kwa kukumbatia ufisadi. CCM imepoteza mwelekeo, chama kilichodaiwa kuwa cha wakulima na wafanyakazi sasa kimetekwa na mafisadi na ndiyo ambao wanaongoza nchi. Ninawashangaa ambao sio mafisadi kuendelea kung'ang'ania chama ambacho kimeishaonyesha wazi kwamba mwelekeo wake ni upi.

Hao mafisadi wanaomwaga hela ili kupata support kwenye NEC na CC, hawaendi kuzomewa wakati wa kampeni na chaguzi, wala hawapazi sauti kwenye majukwaa kujitetea kwamba wao siyo mafisadi.

Tusibiri 2010 inakuja na by then wananchi watakuwa walishajua fisadi ni nani na nani achaguliwe kuwa kiongozi. CCM itakapoteza majimbo ya kutosha ndipo watakapojifunza kwamba walifanya kosa kukumbatia ufisadi.

Chama Cha Mapinduzi ni chama cha wananchi. Kiongozi yeyote aliye madarakani kwa tiketi ya CCM aelewe kuwa nafasi hiyo aliyonayo ni dhamana aliyopewa kwa ridhaa ya wanachama wa CCM. Haitavumilika wala kukubalika kwa kiongozi yeyote yule anayetokea CCM kutumia nafasi hiyo kwa ajili ya kujijenga binafsi kwa gharama ya kuharibu maadili na maslahi ya chama. Pia ieleweke kuwa Chama cha Mapinduzi kina utaratibu na, viongozi na wanachama waliomakini katika kukabiliana na matatizo yanayoweza kujitokeza ndani na nje ya Chama.
Endapo kiongozi yeyote yule amekwenda kinyume na maadili au maslahi ya Chama basi hana budi kuwa muungwana na kuomba radhi na ajisahihishe. Vinginevyo, arudishe kadi!
 
Guninita alinyweshwa chungu
Kabila fulani wanaita 'tindishubila'. Akome na kihelehele!
 
mi mbona sielewi haya mambo jamani

Ukweli ndo huo. Habari za kuwa Sitta ameomba radhi zinaenezwa na akina Rostam ambao wamehangaika usiku kucha kutugongea vyumbani wakitubembeleza tumtose Sitta. Ndio wameita magazeti mbalimbali kueneza uvumi kuwa Sitta ameomba radhi kwa NEC.
 
mhh nimechoka kabisa...Nani wa kumwamini sasa....kazi kweli kweli
 
Ukweli ndo huo. Habari za kuwa Sitta ameomba radhi zinaenezwa na akina Rostam ambao wamehangaika usiku kucha kutugongea vyumbani wakitubembeleza tumtose Sitta. Ndio wameita magazeti mbalimbali kueneza uvumi kuwa Sitta ameomba radhi kwa NEC.

haya mambo yeu ya kuegemea kundi fulani ndo yanatuchanganya hapa..mambo ya rostam yanatoka wapi..au na wewe ulikuwa dodoma.mara ngapi CCM wanakaa dodoma na vyomba vya habari vinakwenda kuripoti habari..acha ubabaishaji hapa
 
mhh nimechoka kabisa...Nani wa kumwamini sasa....kazi kweli kweli

Well, pima mwenyewe uamue. Nilikuwa ndani ya kikao. Waandishi wanaoandika kuwa kaomba radhi wanasema "Chanzo chetu cha uhakika ndani ya kikao".

Ni kweli mambo yalikuwa mazito kweli kwa sababu wabaya wa Sitta walipoona hawaungwi mkono kama walivyotaka, na hasa baada ya kuona JK hashtuki na kuwaunga mkono, wakaja na kubwa zaidi: Wakadai Sitta anautaka Urais kupitia bungeni na wakataja matukio kadhaa kuunga mkono madai yao hayo.

Tunakoenda ni giza tupu ndugu zangu. Akina mama wengi wamelia sana ukumbini.
 
haya mambo yeu ya kuegemea kundi fulani ndo yanatuchanganya hapa..mambo ya rostam yanatoka wapi..au na wewe ulikuwa dodoma.mara ngapi CCM wanakaa dodoma na vyomba vya habari vinakwenda kuripoti habari..acha ubabaishaji hapa

Kigogo, ni kweli niko Dodoma hata sasa. Ukipenda niweke upande wowote, maana hali ilivyo kwa sasa, kubaki katikati ni hatari zaidi.
 
Back
Top Bottom