Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Watu wenye fikra kama hizi ndio wapo kwenye vikao muhimu kama hivyo unategemea nini? Wanasema ili wasikiwe na upande wenye makali, waendelee kuwepo. Kama aliingia hapo kwa milioni 10 za Rostam hana la zaidi la kufanya zaidi ya yale aliyoelekezwa au anadhani wafadhili wa njaa zake watafurahia.
Napata shaka na upambanuaji wa mambo wa huyo mwenyekiti aliyekuwa akicheka tu,anachoweza yeye ni kucheka tu.
 
sitashangaa nikisikia kuna kamemo kamepita kushinikiza wajumbe wachague upande na wasione haya kujitokeza kuwa upande wa mafis**i kwani wameambiwa huo ndio upande wa ushindi.

lakini ole wao hao mafis**i kwani moto utawawikia.
 
Sasa nimeshafahamu ni kwa nini Tanzania ni masikini hivi hata baada ya miaka 50 ya uhuru. Inaniuma sana.

Hivi vikao ndio vya juu kabisa katika uongozi wa nchi. Hao wajumbe waliopo hapo ndio wanaotegemewa kuwa na upeo wa juu kabisa wa kutoa dira na uongozi wa nchi. Hivi uwezo wao wa kufikiri ndio huo jamani?

Nchi itaondokaje kwenye umasikini hii hata baada ya miaka mingine 50 kama hawa ndio viongozi wetu wa juu kabisa tunaowategemea? Tanzania kwa kweli tulichokosa ni uongozi tu, kila kitu tunacho!

Ndio maana kina Rostam wanaweza kuwanunua viongozi wetu wa juu kabisa kiurahisi sana tu. Aliiweka serikali mfukoni, baada ya kugeukwa na swahiba wake JK sasa na yeye kamzunguka na kumpiga bao la kisigino kwani kakiweka chama chao mfukoni. Hii ni laana jamani!
 
Huku ni sawa na kujidhalilisha mbele ya watu ambao siyo vilaza! Inaonesha ni kwa jinsi gani watu walivyo na upunguwa wa akili na sina uhakika kama huyu mtu ana hata darasa kidogo huenda ndo wale walio soma ngumbalo!
Mtu kama huyu huenda hata uwezo wa kuongoza familia yake tu hana! Inakuwaje aingie kwenye kikao kikubwa kama hiki? Rushwa haitaisha tz daima!
 
Wakuu tunaendelea kuchambua yaliyojiri kwenye kikao cha juzi NEC, Dodoma:-

- The More dataz ni kwamba Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Bwana Wilson Kusila, ambaye huko nyuma kuliwahi kuwa na ripoti kwamba alipewa jumla ya shillingi Millioni 10 na Rostam, ili kuweza kumshinda Bwana Masima, aliyegombea naye nafasi hiyo ya mkoa wa Dodoma, alitaka wapiganaji wote kufunguliwa kesi ya uhaini.

- Alipopewa nafasi ya kuzungumza na Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Jamhuri, alienda mbali zaidi na kutaka mashitaka ya uhaini yafunguliwe mara moja kwa Spika na wapiganaji wote, kwa sababu wanachokifanya bungeni kwa kushikiriana na Spika, ni Uhaini period!

- Huku wajumbe karibu wote wa mkutano huo wakiwa wamepigwa na mshangao, Kusila aliendelea ku-charge kwamba Uhaini huu unaanzishwa na kuendeshwa na waliokosa Urais kwenye uchaguzi wa Mwaka 2005, hawa wakamatwe mara moja na kufikishwa kwenye mkono wa sheria za jamhuri na hasa Spika Sitta, wakati wote huu Mwenyekiti wa CCM hakuficha kabisa furaha yake akimsikiliza kwa makini sana Kusila na huku akimuashiria kuendelea na hoja zake!

- Kusila aliendelea kwa kumuomba radhi Rais Mkapa, akisema kwamba "..unashambuliwa na hawa wahaini kwa sababu moja tu, nayo ni kwamba ulimchagua Kikwete kwenye urais wa 2005 na ukawaacha wengine...", hapa Mkapa akasimama juu na kupiga makofi huku akicheka sana, huku pembeni Mwenyekiti wa CCM akiendelea kucheka kwa sauti ya juu sana,

- Kusila alimalizia kwa kudai "..hata hawa wanaosema bungeni hapatatosha wote ni wahaini wakubwa na wakamtwe na kufikishwa kwenye mkono wa sheria maramoja!..."

Respect.


Field Marshall Es!

NB: Wajumbe wengi wa kikao hicho wanajiuliza swali moja muhimu, kwamba kwa nini Rais aliruhusu kutokea kwa yote yaliyojiri kwenye hiki kikao?

hahaha...sasa hivi sijui wamempa shilingi ngapi tena au ndio alikuwa analipa fadhila za kufukia mashimo yaliyopo baina ya mpasuko ambao umekuwepo tokea Waziri Mkuu EL ajiuzulu.

Kweli kazi ipo na safari bado ni ndefu sanaaaaaaa
 
Kwenye hili la Sitta's sagga na NEC, nimejifunza two important lessons, kwamba:-

1. Tanzania tutaendelea kulipia laana ya dhambi ya kumkataa Mrema, kwenye urais kwa sababu so far ana-stand tall kwa kuwa kiongozi pekee wa juu wa bara, aliyeweza kurudisha kadi ya CCM bila kufikiria mara mbili.

2. Utawala wa sasa umeanza kukubali kushindwa, kwa sababu Diria na Mwinyi walipoingia Ikulu, walijaribu sana mwanzoni kumrushia vijembe Mwalimu, lakini within time wakakwama kwa sababu hawakuwa na uwezo wa kuongoza, ndipo Mwalimu akaanza kuwachapa bakora akianzia kwenye sikuu ya wakulima Mbeya,

- Hawa Membe na Muungwana, walipoingia na wao walianza na zile zile za kumrushia vijembe Mkapa, lakini recently wamenza kunyoosha taulo la kushindwa, now Mkapa is on his way back sio siri soon na yeye ataanza kuwachapa bakora kama zile zile za Mwalimu,

Masikini ya Mungu wananchi wa Tanzania, tutawachagua tena anyways!

Respect.

Field Marshall Es
 
Kwenye hili la Sitta's sagga na NEC, nimejifunza two important lessons, kwamba:-

1. Tanzania tutaendelea kulipia laana ya dhambi ya kumkataa Mrema, kwenye urais kwa sababu so far ana-stand tall kwa kuwa kiongozi pekee wa juu wa bara, aliyeweza kurudisha kadi ya CCM bila kufikiria mara mbili.

2. Utawala wa sasa umeanza kukubali kushindwa, kwa sababu Diria na Mwinyi walipoingia Ikulu, walijaribu sana mwanzoni kumrushia vijembe Mwalimu, lakini within time wakakwama kwa sababu hawakuwa na uwezo wa kuongoza, ndipo Mwalimu akaanza kuwachapa bakora akianzia kwenye sikuu ya wakulima Mbeya,



Field Marshall Es

MZEE ES,

Mungu akubariki mkuu sina la kuongeza ...
 
Kwenye hili la Sitta's sagga na NEC, nimejifunza two important lessons, kwamba:-

1. Tanzania tutaendelea kulipia laana ya dhambi ya kumkataa Mrema, kwenye urais kwa sababu so far ana-stand tall kwa kuwa kiongozi pekee wa juu wa bara, aliyeweza kurudisha kadi ya CCM bila kufikiria mara mbili.

2. Utawala wa sasa umeanza kukubali kushindwa, kwa sababu Diria na Mwinyi walipoingia Ikulu, walijaribu sana mwanzoni kumrushia vijembe Mwalimu, lakini within time wakakwama kwa sababu hawakuwa na uwezo wa kuongoza, ndipo Mwalimu akaanza kuwachapa bakora akianzia kwenye sikukuu ya wakulima Mbeya,

- Hawa Membe na Muungwana, walipoingia na wao walianza na zile zile za kumrushia vijembe Mkapa, lakini recently wamenza kunyoosha taulo la kushindwa, now Mkapa is on his way back sio siri soon na yeye ataanza kuwachapa bakora kama zile zile za Mwalimu,

Masikini ya Mungu wananchi wa Tanzania, tutawachagua tena anyways!

Respect.

Field Marshall Es

Mkuu hiyo nyekundu ingesomeka sikukuu ya wafanyakazi. Inafurahisha sana kuona kuwa watu wazima wanasema waziwazi kuwa wapigania haki na maadili ni wahaini, na mafisadi na vibaraka na walionunuliwa wanaonekana kuwa ni watu sahihi. At the time when Mrema was trying to run, he was ridiculed and reduced to dogs. Leo sasa wanaoipigania nchi nao wanataka kuonekana kama Mrema alivyoonekana kipindi kile. Inasikitisha sana kuona chama kinajivuruga, na Rostam ni kama he is back to power again, ni kama sasa remote control yake ameweka betri mpya. Anajua kabisa akitikisa chama ametikisa serikali.

Thanks FMES kutujulisha kuwa Kusila alipewa milioni 10 na Rostam!
 
Wakuu lakini inabidi tupime maneno ya Kusila. Ni nani walioshindwa kwenye uchaguzi wa kutafuta mgombea urais kwa tikiti ya CCM? Kigoda(chaguo la Ben), Mwandosya, au Salim. Which words and what actions constitutes treason? Does fighting corruption or exposing corruption constitutes treason? or Kusila is lost.
 
"CCM ni Imara na uimara wake ni Imara sawasawa kabisa na udhaifu wake mkuu."

Uongo,majungu,fitna na fedha chafu kwa pamoja ndiyo silaha kubwa ya CCM katika harakati za kuendeleza undava wake dhidi ya Watanzania na makundi mengine ya kisiasa.
Kwa sabau silaha hiyo imefanya kazi na kuiletea CCM mafanikio makubwa zaidi ya matarajio yao;umefika wakati kila mmoja ndani ya CCM kuona umuhimu wa kuitumia silaha hiyo ndani kwa ndani ili kujijenga binafsi au katika kundi dogo ndani ya CCM.

Udhaifu mara nyingi hutumiwa kwa faida binafsi, lakini pale kundi la watumia udhaifu kwa faida zao binafsi liongezekapo, udhaifu hugeuka kuwa jiwe kubwa la kuwatweza wote.

"Uimara wa CCM ni mkubwa sawasawa na udhaifu wake mkuu"
 
Kweli hiyo ndiyo Tanzania yetu na viongozi wetu. Nilishawahi kusema hapa kuwa kuna mambo mengine hayahitaji kwenda darasani. Ni suala la busara tu. Sasa huyu Kusila anafikiri huko Mahakamani atakuta wapumbavu kama yeye. Ndiyo nimesema ni mpumbavu tu. Kama kesi za akina Zombe zinawasumbua na kuweka watu rumande for 3 yrs halafu inaonekana wana weak evidence sasa hizi kesi za uhaini watakuwa na evidence gani za ku-back up???

Mtu kama unapinga ufisadi basi wewe ni mhaini, mmh hawa ndiyo washauri wa chama?. Sasa hao wabunge wa SISIEMU hawajawahi kutaja FISADIZ publicly sasa mtu kama Mh. Slaa utamfungulia kesi gani kwa Matakwa ya huyo mpumbavu Kusila??? Narudia tena MPUMBAVU huyo Kusila. Mwenye hasira na mimi akameze nyembe.
 
- Kusila aliendelea kwa kumuomba radhi Rais Mkapa, akisema kwamba "..unashambuliwa na hawa wahaini kwa sababu moja tu, nayo ni kwamba ulimchagua Kikwete kwenye urais wa 2005 na ukawaacha wengine...", hapa Mkapa akasimama juu na kupiga makofi huku akicheka sana, huku pembeni Mwenyekiti wa CCM akiendelea kucheka kwa sauti ya juu sana,

- Kusila alimalizia kwa kudai "..hata hawa wanaosema bungeni hapatatosha wote ni wahaini wakubwa na wakamtwe na kufikishwa kwenye mkono wa sheria maramoja!..."

Hapa ndipo utaona rangi za JK. Najua kila mtu ana uhuru wa ku-express anachofikiria lakini linapokuja kwenye suala la interest for the Nation nafikiri JK alitakiwa kuonyesha leadership. Wewe ukiwa kama Prezidaa umeona Kiwira ikirudishwa serikalini kutokana na ufisadi ya huyo fisadi uliyekaa naye hapo pembeni. Vinapigwa vijembe vya kumsifia fisadi aliyekaa pembeni yako nawe unakenua meno. That was DISGUSTING. Fisadi ni fisadi tu hata umpeleke UNYAGONI is STILL FISADI.
 
Wakuu lakini inabidi tupime maneno ya Kusila. Ni nani walioshindwa kwenye uchaguzi wa kutafuta mgombea urais kwa tikiti ya CCM? Kigoda(chaguo la Ben), Mwandosya, au Salim. Which words and what actions constitutes treason? Does fighting corruption or exposing corruption constitutes treason? or Kusila is lost.

Kusila alikuwa anajipendekeza tu, hana lolote. Huyo ni Mwenyekiti wa SISIEMU Mkoa hata hakumbuki nani aligombea na JK kupata ticket ya kuwania Urais wa JMT. Ni vizuri watu kama hawa wakasoma Katiba ya nchi kuliko kuropoka tu eti kesi ya Uhaini. Unaweza ukawa kiongozi na still hujui Katiba ya nchi. Darasa linahitajika hapa, seriously.....
 
Wakuu tunaendelea kuchambua yaliyojiri kwenye kikao cha juzi NEC, Dodoma:-

- The More dataz ni kwamba Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Bwana Wilson Kusila, ambaye huko nyuma kuliwahi kuwa na ripoti kwamba alipewa jumla ya shillingi Millioni 10 na Rostam, ili kuweza kumshinda Bwana Masima, aliyegombea naye nafasi hiyo ya mkoa wa Dodoma, alitaka wapiganaji wote kufunguliwa kesi ya uhaini.

- Alipopewa nafasi ya kuzungumza na Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Jamhuri, alienda mbali zaidi na kutaka mashitaka ya uhaini yafunguliwe mara moja kwa Spika na wapiganaji wote, kwa sababu wanachokifanya bungeni kwa kushikiriana na Spika, ni Uhaini period!

- Huku wajumbe karibu wote wa mkutano huo wakiwa wamepigwa na mshangao, Kusila aliendelea ku-charge kwamba Uhaini huu unaanzishwa na kuendeshwa na waliokosa Urais kwenye uchaguzi wa Mwaka 2005, hawa wakamatwe mara moja na kufikishwa kwenye mkono wa sheria za jamhuri na hasa Spika Sitta, wakati wote huu Mwenyekiti wa CCM hakuficha kabisa furaha yake akimsikiliza kwa makini sana Kusila na huku akimuashiria kuendelea na hoja zake!

- Kusila aliendelea kwa kumuomba radhi Rais Mkapa, akisema kwamba "..unashambuliwa na hawa wahaini kwa sababu moja tu, nayo ni kwamba ulimchagua Kikwete kwenye urais wa 2005 na ukawaacha wengine...", hapa Mkapa akasimama juu na kupiga makofi huku akicheka sana, huku pembeni Mwenyekiti wa CCM akiendelea kucheka kwa sauti ya juu sana,

- Kusila alimalizia kwa kudai "..hata hawa wanaosema bungeni hapatatosha wote ni wahaini wakubwa na wakamtwe na kufikishwa kwenye mkono wa sheria maramoja!..."

Respect.

Field Marshall Es!

NB: Wajumbe wengi wa kikao hicho wanajiuliza swali moja muhimu, kwamba kwa nini Rais aliruhusu kutokea kwa yote yaliyojiri kwenye hiki kikao?

Kikwete uongozi wa nchi na chama umemshinda kabisa ndiyo maana sasa CCM na Tanzania ni bora liende tu maana nchi na chama hazina kiongozi. Mwalimu asingeruhusu machafuko ya hali ya hewa kama haya yafanyike mbele ya macho yake. Na huyu Kusila yeye na wapiga debe wote wa mafisadi ndiyo wanaostahili kukamatwa kama wahaini.
 
Wakuu lakini inabidi tupime maneno ya Kusila. Ni nani walioshindwa kwenye uchaguzi wa kutafuta mgombea urais kwa tikiti ya CCM? Kigoda(chaguo la Ben), Mwandosya, au Salim. Which words and what actions constitutes treason? Does fighting corruption or exposing corruption constitutes treason? or Kusila is lost.

Mwandosya.Kigoda,shibuda,John malecela hawashiriki kwenye mijadala ya ufisadi.
mie naona Mwakyembe,Stella Manyanya,Anna Kilango,Seleli ndio wasemaji wazuri lakini hawakugombea urais.
 
Dah!

Kusila alikuwa mwalimu wa Physics, na alikuwa bright sana. Hivi kumbe siasa zinaweza kuwafanya watu wawe wa ajabu kabisa?
 
Mwandosya.Kigoda,shibuda,John malecela hawashiriki kwenye mijadala ya ufisadi.
mie naona Mwakyembe,Stella Manyanya,Anna Kilango,Seleli ndio wasemaji wazuri lakini hawakugombea urais.

Nashukuru kwa kumkumbusha Kusila ni nani alishindana na JK kuwania Ticket kupitia SISIEMU. Sidhani kama ulihitaji darasa kukumbuka nani aliwania hiyo ticket ndani ya SISIEMU mwaka huo. Kusila kama kiongozi wa chama Mkoa alishasahau na kubaki kuropoka tu UHAINI.
 
Najua katiba inawalinda wabunge kwa matamshi yao bungeni, je matamshi ya hawa wahuni kwenye kikao cha chama chao yanalindwa na nani - serikali ? Kama nakumbuka Spika Sitta aliwahi kuwaonya wale wote wanaothubutu kuhoji maamuzi ya bunge mitaani - kama sikosei nadhani alikuwa anavishambulia vyama vya upinzani. Akiendelea kuonya, alisema bunge litachukua hatua kali kwa yeyote yule atakayerfanya hivyo kwa sababu huko ni kuvunja katiba.

Hivi itakuwaje kama hoja ikitolewa bungeni ya kuwawajibisha wahuni hawa waliokutana Dodoma, ama bunge halina ubavu huo. Watanzania tumepata nafasi nzuri ya kuwapima na kuwatolea hukumu inayostahili hawa wawakilishi wetu walioapa kuilinda na kuitetea katiba. Ja wataongozwa na matumbo yao kama siku zote au kama wanaume watahakikisha heshima ya bunge kama mhimili muhimu wa dola inalindwa. Wanaojiita wapiganaji, kazi kwenu.
 
Swali la kujiuliza hapa , ni je mheshimiwa Sitta atawezaje kuwa impartial kwenye bunge kama ameshatishiwa kiasi hiki? Nadhani kwa manufaa ya umma , na kama kweli spika anataka kutokomeza ufisadi basi itakuwa ni jambo la busara kama atajiuzuru. Hii itasend message kwamba yeye ni mtu ambaye anaheshimu values zake , na wakati huo huo ni mtu ambaye hayuko tayari ku-succumb to external pressure.
 
Jamani sisi wengine sio wazuri kwenye sheria, kuna mtu anaweza kutufafanulia katiba na sheria za nchi zinaweka bayana kesi ya uhaini inafunguliwa ukifanya makosa gani?? Halafu hiyo NEC ina power gani za kufungua mashtaka makubwa kama hayo??

Najaribu kufikiria hapa kosa la spika na wabunge wenye mapenzi ya kuzuia wizi wa rasilimali za wananchi wa jamhuri, wamefikia vipi kwenye hili janga la uhaini??

Je, mwenyekiti hakuweza kutoa mwongozo kufuatana na katiba ya nchi, hizi allegation za uhaini zilipotolewa??

Sisi wengine huku kuna kakosa ka TREASON ambakouwa tunakasikia tu kwenye malumbano kwenye FOXNEWS, lakini ni vigumu kukumbuka nani amewahi kupewa hiyo case ya treason!!

Je Treason ndio uhaini?? Kama ni ndio, du si level ya kufikia hii threshold iko very high kiasi ambacho hata sijui huyu KUSILA kama ni mzima au vipi!!
 
Back
Top Bottom