Huu ni uedelezaji wa ukabaila na ukoloni mambo leo ,Spika si kwa ajili ya CCM wala wabunge wanapokuwa ndani ya bunge hawaiwakilishi CCM,inakuwaje kuwaje CC na NEC za CCM ziwe zinawashambulia na kuiwatisha ?
Hivi hawa wabunge wanaotishwa wafanye nini ? Ndio wameshatishwa kwa maana mashahara uliojaa vikolombwezo vya posho wataukosa na ikibidi kufuatiliwa na vyombo vya usalama wa CCM.
Nchi sasa inaendeshwa kidikteta ,hili halina ubishi na kitakachopatikana hapo itakuwa ni matumizi ya nguvu kuipindisha haki ya raia kumchagua anemtaka,WaTanganyika kaeni tayari maana kinachokuja safari hii sio washawasha tena bali ni risasi za moto hili halina ubishi kabisa.Mugabe style au Mwai style au yote kwa pamoja ,ila waTanzania walio wengi wakae tayari kwa kujibu kwa aina ya Odinga style ili paeleweke na hio ndio dawa peke yake haina mbadala kwa utawala huu wa kifashisti.
CCM imeshang'amua kuwa hawawezi kukubalika tena ,hivyo kwa kuanza ndio wameunda tume ili kuwajua na kuwabana wasiokuwa na wao katika kuwaunga mkono kuizamisha nchi hii.
Suali waliloulizwa wabunge ambao wapo mstari wa mbele kupinga utawala mbovu wa CCM wakiwa ndani ya CCM"...Are You with us ? If not you will see the consiquency(If correct)" Hivyo ni vitisho ,ambavyo nadhani vimekusudiwa kuwatenga wale ambao wamekusudia kujitokeza kupambana na Kikwete katika uchaguzi ujao kwa kutumia karata ya CCM ,kitu kimoja ili kuwajua waovu wa Nchi hii ni kuwatanzama wale walioitwa chemba na kummuonya spika ,hao ni watu hatari na inafaa kuepukwa wengine ni wale waliopewa jukumu la lusimamia ambao wamepewa idara maalum itanayojulikana kama Kamati ,hii si kamati ya kuiletea wala kuitetea heri hapa Tanzania bali ni kamati ya maangamizi ambayo imewekwa kuikandamiza haki pale inapotetewa kwa kuwabana na kuwadhoofisha wale watakaojitokeza kukemea na kupinga maovi yanayoonekana kufanywa na utawala wa CCM ,kwamba sasa imefika wakati kuwa litakalosemwa na CCM ndio hilo hilo hakuna wa kulipinga ,natumai waTanzania mmepata uelewa kwa hali ya mambo inavyoendeshwa na CCM ,sio jambo la mchezo hawa watu wamekusudia shari kabisa na sio kwa wabunge wao tu bali kwa wabunge waote na yeyote yule atakayeonekana analeta vya kuleta.
Hongera Wapemba kwa msimamo wenu wa kuilinda haki kwa bei yeyote ile karibu waTanganyika watawaelewa.