Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Wazee na Waheshimiwa wana jamvi

Nikiwa mjumbe wa NEC nisiye na kundi lolote, nawajibika kuweka sawa rekodi moja katika mjadala unaoendelea kuhusu Spika Sitta na kilichotokea ndani ya ukumbi wa mkutano wa NEC.

Baada ya mjadala mrefu ulioshabikiwa sana na wajumbe wengi huku hoja zao zikijiwa bila jazba na wajumbe wachache lakini wanaoheshimika, Spika Sitta alikutana faragha na Mwenyekiti JK, Rais Mwinyi na Kinana. Baada ya faragha ile ambayo bado ni siri, Spika Sitta alipopata nafasi alisema maneno machache sana yenye pointi mbili. Kwanza, aliwashukuru wajumbe kwa kutumia uhuru wao kutoa maoni yao. Pili, alisema anaiachia meza kuu kutafakari yaliyosemwa na pande zote. Kisha alimaliza na kukaa.

Hata kama sikubaliani na baadhi ya misimamo yake, siwezi kusema kuwa aliomba radhi. Lakini pia siwezi sema alikosa watetezi kama inavyoripotiwa. Kulikuwa na hoja nzito, tena nyingine kutoka visiwani zilizomtetea.

Kiroja cha mjadala alikuwa Guninita, Mwenyekiti wa Mkoa wa DSM aliyechemka lakini JK akamzodoa kwa kumwambia "kama ana uchungu na chama mbona alikiacha na kwenda CHADEMA na kuitukana CCM kwa miaka miwili?"

Habari ni hiyo.

Baija
Asante Baija, umetufumbulia kitendawili kilichotusumbua sana. Naheshimu mchango wako. Nadhubutu kusema hapa tunapata picha halisi ya kilichotokea kuhusu suala la Spika. Kama baadhi ya wenzangu walivyosema, busara ilitumika hapa kwa sababu inaelekea watu walijipanga kummaliza kwenye NEC kama habari hizo zilivyovuja tangu kitambo.
 
pundamilia maneno yako mazuri sana. Yananikiumbusha "zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa ccm.".... Unaposema chama cha wananchi (cuf???!) halafu unarudi kusema "kiongozi yeyote aliye madarakani kwa tiketi ya ccm aelewe kuwa nafasi hiyo aliyonayo ni dhamana aliyopewa kwa ridhaa ya wanachama wa ccm" inakuwa vigumu kueleweka maana "wananchi" wote si "wanachama wa ccm"... Kuna wenye vyama tofauti na wengine wasio na vyama kabisa. Lakini pia, zile zama za kusema, "kuna utaratibu" zimepitwa na wakati na ndio maana sitta alijifunza kwa "zitto vs buzwagi" ambako mawaziri walizomewa na zitto kupokewa kama shujaa jangwani na nchini kote. Kwa hesabu za haraka haraka, sitta na wenzake wakaikomboa ccm kwa kuteka ajenda ya kina dr. Slaa na zitto na kuibeba kwamba ni ajenda yao. Ikumbukwe hoja ya vita ya ufisadi ilipata kasi mwembe yanga kwenye list of shame. Sasa yapi ni "maadili na maslahi ya chama" unayoyazungumzia? Huu upofu utawaisha lini? Hata hizo 'ajira za ngoma' kutoa burudani kwa kupigwa magumi zitawaumiza baadaye maana mwisho wa ngoma kunoga ni kupasuka na mpiga ngoma ataunda nyingine kwa kutumia maiti za ng'ombe wengine kama yule wa mwanzo. Kama maadili na maslahi ya chama ni kumsafisha lowassa na wenzake, basi mujue mumeamua kwa makusudi kukiondoa chama chenu (ccm) kutoka kwa wananchi na kukiacha solemba. Itakua vugumu sana kuwanunua (kama ilivyokua dodoma) watanzania wote na kama nilivyowahi kusema, :nchi haitatawalika jamani:
hivi ccm bado ndo chama stahili kutuongozaa?? Naona wengi wanakililiaaa...
 
- Hela zote walizi-invest kwa wajumbe wa visiwani knowing kwamba huwa wanaweza kumtishia Muungwana, lakini wakachemsha Spika ana support kubwa sana ya wabunge aliowapa marupu rupu mengi ya ajabu, lakini the damage is done na ninaamini kwamba Spika hatarudi bungeni kwani anahitaji miracle kushinda tena jimbo!

Respect.

FMES!
Unapozumgumzia hilo la Zanzibar (siyo Visiwani-tafadhali) kuwa mwangalifu sana. Wao sio cheap kama mlivyo nyinyi huko Bara. Lakini ukiwakera katika yale wanayoamini ni kweli wataunga mkono kitu kwa kauli moja- na utashangaa matokeo yake.
 
mi nadhani sasa hivi siasa ya tanzania inaelekea kubaya, halafu wanasiasa wengi hawapendi kuambiwa ukweli, kutoakana na mabaya wanayoyafanya ili kulinda maovu yao. Samweli sitta huwa hapendi unafiki, anakupa live ndio maana wanasiasa wengi hawampendi hasa wale mafisadi
si kweli sitta unafiki anao kwani ndo ngao ya kuendelea kuwa mwanachama kiongozi ndani ya ccm..
 
Mwanakijiji, ni vigumu mno kutenganisha BUNGE, SERIKALI na CCM angalau kwa sasa. Sitta anaingia CC ya CCM kwa wadhifa wake kama Spika. Serikali kwa asilimia zaidi ya 98 inaundwa na WABUNGE, Wabunge wote wa CCM ni wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa wa CCM. Kwa mchanganyiko huu na hasa ikizingatiwa kwamba hata tiketi ya kugombea USPIKA kapewa na vikao hivyohivyo vya CCM kumjadili kama Spika hakuepukiki. Kuna UJINGA mwingi sana kwenye KATIBA yetu.
nakubaliana nawe. Na kwa ufupitu Uspika alio nao Sitta ni Uspika ambao ana ubia na CCM. Na wabunge wa CCM -ubunge wao una ubia na CCM.
 
Kama kweli JK akiwa mwenyekiti wa Chama, akiwa Rais wa nchi na akiwa mtu mzima, sitegemei kama anaweza kutoa maneno ya kejeli kwa Guninita, tena ndani ya kikao kikubwa cha Chama. Sijui ni kwanini viongozi wetu wasiwe na manners za kuongea.

Inazidu kuonesha kuwa heshima ya vikao vya juu inazidi kupungua. Kama lugha ya kistaarabu haitumiki, inawezekana hata maamuzi yasiwe ya kistaarabu.

Kama hujamzoea Kikwete unaweza kushangazwa na kauli zake, lkn kwa sisi wengine tunamjua. Hebu fikiri hili: Raisi wa nchi anaulizwa chanzo cha umasikini wa nchi yake anajibu: HATA SIJUI, unategemea angemjibuje Guninita? Akiwa ziarani Muheza akasema Watanzania wavumilie shida walizonazo, kwa sbb serikali haina cha kufanya kuziondoa.
What a president!





...Jisafisheni muwe na kauli moja kama chama...


Mkuu MTM,
kwa sisiemu tunayoiongelea hapa na kwa hatua iliyofikia, suala hili la kuwa na kauli moja na kwenda nayo kwa wananchi ni ngumu sana. Hio ilikuwa ni sisiemu ya Mwalimu na aliondoka nayo.
Kwa sasa kuna:-
Sisiemu Mtandao
Sisiemu Maslahi
Sisiemu matumaini
Sisiemu Bara
Sisiemu Visiwani
Sisiemu Nyanda za juu Kusini
Sisiemu Kaskazini
Sisiemu wapinga Ufisadi
Sisiemu pro-mafisadi
Sisiemu neutral (akina Balobi)
Sisiemu.........
Wote hawa wanatoka na kauli zao kwa masuala mbalimbali ambayo wanashindwa kukubaliana ktk vikao vyao! Kumbuka suala la mafuta linavyotaka kuwatoa roho Wazanzibari, kumbuka suala la kupeana vitambulisho vya ukaazi kwa upande mmoja tu wa Muungano n.k.
 
Ndio tujadili yaliyojiri ndani ya vikao vya CCM na Mh. Spika, lakini tuwe waangalifu katika maeneo fulani. Hivi huyu Baija Bolobi ni kweli M-NEC na habari aliyoitoa ni ya kweli? Je, hakuna chanzo (source) kingine cha kutuhabarisha tukalinganisha taarifa hii?
Nje ya mh. Spika ni yapi mengine yameongelewa? Makamba je?
 
Mi naona siasa ni mchezo aliouleta shetani ili kila atakayeshiriki achukue point za dhambi alafu aishie,amiin nawaambia hakuna mkweli hata mmoja kwenye siasa za nchi ya wenye njaa kama hii yetu,we've bn f**kd by those liars and still wants 2 f**k us!!!
"He who fears death is in denial,4 death is promised"
 
Mimi naona Sita arejeshe silaha zake Bungeni mpaka Watanzania wote waelewe anasimamia nini na hapo sasa ajiuzulu hasa hapo ambapo uchaguzi wa serikali za mtaa utakua unakaribia.CCM wataumia!
We bwana 'Mkapa' chondechonde unampenda 6 au unataka afungiwe biashara zake zote?Jamani tumtetee 6 pia tuangalie maslahi yake kama 6 na si kama Redio!OOoh hawa jamaa hatari kwelikweli,muulize Masumbuko atakwambia!
 
Mkuu MTM,
kwa sisiemu tunayoiongelea hapa na kwa hatua iliyofikia, suala hili la kuwa na kauli moja na kwenda nayo kwa wananchi ni ngumu sana. Hio ilikuwa ni sisiemu ya Mwalimu na aliondoka nayo.
Kwa sasa kuna:-
Sisiemu Mtandao
Sisiemu Maslahi
Sisiemu matumaini
Sisiemu Bara
Sisiemu Visiwani
Sisiemu Nyanda za juu Kusini
Sisiemu Kaskazini
Sisiemu wapinga Ufisadi
Sisiemu pro-mafisadi
Sisiemu neutral (akina Balobi)
Sisiemu.........
Wote hawa wanatoka na kauli zao kwa masuala mbalimbali ambayo wanashindwa kukubaliana ktk vikao vyao! Kumbuka suala la mafuta linavyotaka kuwatoa roho Wazanzibari, kumbuka suala la kupeana vitambulisho vya ukaazi kwa upande mmoja tu wa Muungano n.k.

Hii yote ni sawa tu katika kujenga demokrasia. Tatizo linakuja kuwa chanzo kikuu kinacholeta makundia haya na mijadala yao ni ULAJI (UBINAFSI) na sio AJENDA za maendeleo, SERA za chama na serikali na wala sio ITIKADI ambayo ndiyo inapswa kuwa msingi mkuu wa chama kama CCM. Na hapa ndio maana naomba wasigawanyike sasa hadi vyama vingine vitakapokuwa na kukomaa kiasasi ili kuepusha Tanzania kupitia experiance ya wenzetu wa Kenya na NARC zao.

omarilyas
 
Bado naendelea kusema kuwa kutokana na hali ya sasa Tanzania na mapambano tuliyo nayo kusafisha rushwa na ufisadi, assume kama inawezekana basi Bunge letu linahitaji kuwa na Spika supavu asiyeogopa mtu kama Mr. Six. Najua kuwa mafisadi hawalali wakitafuta kila mbinu ili kumng'oa namba sita. Imagine kikao cha juzi tu mapesa yaliyomwagwa ili kuhakikisha kuwa Sitta anaamuriwa kurejesha kadi na mwishowe akose kila kitu. Nafurahi kuwa pesa zililiwa na hakuna lolote.

Na kama kwenye jimbo wanaendelea na kampeni ili wamdondoshe Mr. Six acha waendelee ila basi wajue kuwa Mr. six ataendelea kuwa Mbunge, na wala si lazima aendelee kuwa Spika. The bottom line he will remain to be our hero, the anly Spika who made the house live and active, hakuna kulala pale.

On the other hand, nakanusha kuwa Mr. Six hana support ya wana CCM wegi. Ukweli ni kwamba support anayo ila ni wachache ambao wanakubali kununuliwa na mafisadi ili kuyumbisha Bunge na serikali. Kama ambavyo wameanza kampeni kwa kupenyeza fedha kwa majimbo ya wale wabunge machachari ambao wanapinga ufisadi na rushwa ni hivyo hivyo watajitahidi kujitwalia makundi ndani ya Bunge ili kondoa kinara ambaye anaongoza mhimili huo muhimu only to safe guard the interests of Mafisadi. Hakuna fisadi yeyote aliyejihusisha na Richmond, Meremeta, Deep Green, Kagoda, IPTL, other EPAs, ..etc atafurahi kumwona Mr. Six akiwa pale kwenye kiti cha enzi akikubali wasulubiwe kupitia wapenda nchi. Kwa mantiki hii ni lazima wezi hao wajipange ili kimng'oa. Huko nyuma (miezi michache iliyopita) fisadi alitoa 2 billion ili zisambazwe kwa key constituencies!!!!! Je hizo nazo vipi???? Ni wakati umefika sasa kuelimisha wananchi zaidi madhara ya ufisadi na rushwa ili basi wafanya mabadiliko. Ni vema waambiwe kuwa hakuna anayekuwa kukushikia bunduki baadaye eti anakudai pesa, ubwabwa, tisheti au 5000 yake aliyokupa ill umchague. Hata kama watapokea hizo rushwa mwoshowe wafanye mapinduzi katika kupiga kura. Hapa nafurahi Mh. Kilango-Malecela aliwaambia wana Same Mashariki wapokee kabisa na mwishowe wamkomeshe fisadi huyo kwa kutochagua matakwa yake!!! Huu ndiyo unatakiwa uwe ni msimamao kwa wapiga kura wote.

Hii ni aibu kwa Tanzania ambayo inasema inapinga ufisadi na rushwa huku in actua fact inaukumbatia. Je tuna uongozi ambao uko serious kupinga matendo hayo ya kifisadi??? Kama kweli upo basi ungeungana na Mr. Six na si kumuita chemba ili kumkanya na kumwambia eti akisema sana anawapa nguvu wapinzani!!! What a shame. Tubadilike.
 
- The whole thing is a big joke, mafisadi wanataka kichwa cha mpiganaji na they almost got it kama sio Makamba factor, ambayo ilimfanya Muungwana kurudi nyuma against the plan, kwa sababu kama Muungwana hakuwa nao kina Lowassa kwenye hili la kumng'oa Spika, how come aliwaruhusu wajumbe wote waliokuwa planted na Lowassa for this job kuzungumza kwanza na kujenga hoja againts Spika kama Lowassa alivyotaka?
Kwa mtazamo wangu, JK aliamua kuwapa uwanja akina EL na wenzake ili watoe madukuduku yao yote kama ambavyo wamekuwa wakimuomba asaidie kuweka sawa misimamo ya Spika na wenzake. hiyo haimaanishi kuwa JK yuko upande wowote. Nadhani anatamani sana makundi haya yaishe ili mambo yaweze kuwa sawa na chama kiweze kujipanga kwa ajili ya uchaguzi ujao.
 
haya mambo yeu ya kuegemea kundi fulani ndo yanatuchanganya hapa..mambo ya rostam yanatoka wapi..au na wewe ulikuwa dodoma.mara ngapi CCM wanakaa dodoma na vyomba vya habari vinakwenda kuripoti habari..acha ubabaishaji hapa


Kigogo,

Sina hakika ukweli ni upi ila jiulize pia ni mara ngapi waandishi wamekuwa wakiripoti uongo na maneno ya kupandikizwa? Kumbuka kwamba waandishi walikuwa dodoma wengi ila hahakuruhusiwa kuingia mkutanoni hivyo wote walitegemea habari za kupewa. Tatizo ni je wamepewa taarifa na nani na mtoa taarifa ana interest na kundilipi

WEWE NDIO MBABAISHAJI NAMBA MOJA
 
Binafsi ninakubariana na uchambusi wa bwana Mkandara. Kutokana na kikao hiki Mukuu amekwishapata data kamiri za mafisadi na mutandao wao hasa viongozi na vibaraka wao ambao ni wajumbe wa NEKI. Ninalinganisha haya matukio na Mkuu alivyofanywa kuhusiana na suala la EPA ambako alifanikiwa kurudisha baadhi pesa zilizoibiwa na mafisadi.

Inawezekana pia kuwa alikuwa akiwajua wote wako upande gani, na wanataka nini. Japokuwa, kwa kuwaachia wajianike kiasi walichojianika, inaweza pia ikawa ndio njia ya kuwapunguza mafisadi nguvu zozote walizonazo. Ni dhahiri kuwa JK anajua nguvu kubwa waliyonayo Mafisadi na pia anajua nguvu kubwa iliyo nyuma ya wale wanaopambana na ufisadi (hasa kwa kuzingatia support ya wananchi). JK anajua pia kuwa wakati huu ndio wa kuamua upande wake katika sakata zima. Ni ngumu kwa kuwa inabidi awatose maswahiba wake, lakini ni muhimu kwa kuwa anaaka kushinda uchaguzi. Ndio maana, inabidi atumie busara za ma-Rais wastaafu na wazee wengine wote ndani ya CCM kufikia suluhu hilo.

Sasa tusubiri tuwone ataufanya nini huu mutandao wa mafisadi kwasababu sasa anawajuwa wabaya wake wote kama kweli alikuwa hana uhakika kabula ya hapo!

--S Horizons

Sidhani kuwa ana kubwa la kuwafanya Mafisadi kwa sasa. Hukumu yoyote anayoweza kuwapa mafisadi inaweza kufanyika katika dakika za mwisho kabisa za maandalizi ya uchaguzi kwa kujua jinsi atakavyozoa kura za wananchi. Kwa mwenendo uliojidhihirisha katika vikao hivi, ni dhahri kuwa Mafisadi watawekwa pabaya miezi michache kabla ya uchaguzi ili kukiokoa chama kutoka kwa wananchi. Ila pia, mchango wa Spika unahitajika katika kupunguza malalamiko ya Wabunge, na kuanza kuisafisha serikali machoni mwa wananchi.
 
Kigogo,

Sina hakika ukweli ni upi ila jiulize pia ni mara ngapi waandishi wamekuwa wakiripoti uongo na maneno ya kupandikizwa? Kumbuka kwamba waandishi walikuwa dodoma wengi ila hahakuruhusiwa kuingia mkutanoni hivyo wote walitegemea habari za kupewa. Tatizo ni je wamepewa taarifa na nani na mtoa taarifa ana interest na kundilipi

WEWE NDIO MBABAISHAJI NAMBA MOJA
Nikupongeze Shangazi kwa bandiko hili. nafikiri jamaa zangu nao (Waandishi) wana matatizo. Wanashabikia rumours na siyo facts. Sasa huo ni uandishi gani. Wapi Professionalism.
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 160 (54 members and 106 guests)

Jamani nyie 106 guests jiungeni na JF inawezekana mna majibu ya baadhi ya maswali tunayojiuliza hapa. Please Joine the forum of Great Thinkers pse pse.
 
Shukrani za dhati Mkuu Baija Balobi (Mjumbe wa NEC-CCM Kama ulivyojiita mwenyewe) kwa ufafanuzi wako wa nini kilichojiri huko Dodoma,Lakini pamoja na maelezo yako yote,ni ukweli usiopingika kwamba Mh.Sitta amepoteza Imani/umaarufu kwa Wabunge walio wengi haswa Wabunge wa CCM.

Kwa kuwa Wana-NEC (Haswa Wabunge wa CCM) walipendekeza Spika apokonywe kadi yake ya chama ili wamvue Ubunge na baadaye Uspika ,kushindwa njama hiyo.Nafikiri Spika kwa hiyari yake mwenyewe ajiuzulu Uspika,kwa sababu katika mazingira yaliyopo sasa,hawezi kuongoza Chombo hicho ikiwa Idadi kubwa ya Wabunge hawamkubali.

Ni wazi kuwa atabaki na Ubunge wake wa Urambo,mpaka hapo mwakani katika Uchaguzi....Atakuwa ana nafasi kubwa ya kuwashitaki Wapinzani/Wabaya wake kwa wananchi kwa jinsi walivyomfanyia Fitina kwa kutetea haki ya watanzania.....Sitomuelewa Sitta ikiwa atang'ang'ania kubaki na Uspika wake!Kule kukubali suluhisho Dodoma ilikuwa kwa Mantiki ya kutaka Kubaki na Wadhifa wa Ubunge (Anawajali watu wa Urambo waliompigia kura),Maana kama angekubali kurudisha Kadi,ni wazi kwamba angejivua Ubunge na kujiondoa kwenye Uspika.Na moja kwa moja angekuwa hajawatendea haki waliomchagua.

Hata hivyo imefika Wakati sasa kumtafuta SPIKA nje ya Bunge...Wanazuoni tuangalie sheria za Bunge zinasema vipi...Kwa sababu kwa mtindo huu wa sasa,kila wakati Spika atakuwa anaendesha Bunge kwa matakwa ya Chama chake kwa kuhofia kuwa atashitakiwa kwenye Vikao vya chama.

Utabiri wangu unaniambia kuwa Mh.Sitta atajiuzulu Uspika wa Bunge la Jamuhuri,kutokufanya hivyo itakuwa ni kufilisika Kisiasa...Huwezi kuongoza watu wasiokuwa na imani nawe.


Mwawando unanitia wasi wasi na uwezo wako wa kufikiri na kujenga hoja. Ni wabunge wangapi ambao ni wajumbe wa NEC? Una facts gani kwamba wabunge hawana imani na spika? manake naelewa hili lingeonekana bungeni kwenyewe. Niambie ni nini ulikiona bungeni kilichoonyesha hawana imani nae. Wasiwe na imani nae wakati kawaboreshea maslahi mara dufu?

Naomba nisiendelee kukuhiji manake sifanyagi mjadala na mafisadi kama wewe na usijisumbue kusema nikuombe radhi manake sitafanya hivyo wala sitatubu
 
CCM HOVYOHOVYO, UPINZANI HOHEHAHE, TANZANIA SHAGHALABAGHALA...
Unaweza kutafuta ulimwengu wako wa kuishi peke yako maana huna tumaini na hata wewe binafsi kama wewe hujiamini!
Nilitegemea kuwa wewe utakuwa mwokozi wa Tanzania lakini kama hata wewe ni Hovyo hovyo unafikiri na mimi ni hohehahe?
Naweza kuivusha Tanganyika, ila Tanzania kuivusha ni mpaka nielewane na wakina mwiba kule kwenye vinchi vilivyo baharini.
 
Hii yote ni sawa tu katika kujenga demokrasia. Tatizo linakuja kuwa chanzo kikuu kinacholeta makundia haya na mijadala yao ni ULAJI (UBINAFSI) na sio AJENDA za maendeleo, SERA za chama na serikali na wala sio ITIKADI ambayo ndiyo inapswa kuwa msingi mkuu wa chama kama CCM. Na hapa ndio maana naomba wasigawanyike sasa hadi vyama vingine vitakapokuwa na kukomaa kiasasi ili kuepusha Tanzania kupitia experiance ya wenzetu wa Kenya na NARC zao.

omarilyas

Nakubaliana na maoni yako.
Suala la kugawanyika kiitikadi kwa sisiemu lipo, ila tu inabidi wachukue kwa tahadhari angalizo lako, kwamba mgawanyiko wao uishie ndani ya chama!
 
Back
Top Bottom