Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Sasa chama cha mafisadi (ccm) kinajitokeza kwa rangi zake halisi. Jana na leo nimejaribu bila mafanikio kupata majina ya wajumbe wote wa NEC waliohongwa na kinara wa mafisadi (jina nalihifadhi kwa sasa), na kiasi cha pesa walizopewa ili wawaunge mkono katika harakati zao za kumng'oa Sitta. Naendelea na zoezi hili, likikamilika nitaweka kila kitu hadharani. Stay tuned! Lakini sisi wana wa nchi tunasema hii ni ishara nzuri, bila shaka Mungu anaongoza ili wajiumbue. Ukombozi unakaribia...
 
Madudu yaliyofanywa na hao mamluki wa akina Rostam na Lowassa Dodoma yanatusaidia sana sisi tunaopigania UHURU wa kweli. Wao wanadhani sisi Watanzania bado tumelala usingizi. Tunafuatilia hatua kwa hatua kila wanachokifanya mafisadi hawa. Wanatumia pesa walizotuibia kuwahonga MAFALA waliopo NEC eti waunge mkono hatua ya kumng'oa Sitta wamuweke mtu atakayetetea ufisadi wao unaoliangamiza taifa letu. Nasema madudu yaliyofanyika Dodoma yanatusaidia kwa sababu huo ndio mwanzo wa kusambaratika kwa CCM - Mafisadi na kuzaliwa chama cha ukombozi wa kweli wa Watanzania. Tunachotakiwa kufanya hivi sasa ni kueneza ujumbe kwa Watanzania wote wenye mapenzi ya kweli na nchi yao ili watambue kwamba nchi yao imetekwa na mafisadi wachache na wawakatae. Ujumbe kwa mafisadi wote: Mwisho wenu utakuwa mbaya sana. Saa ya Ukombozi imewadia.
 
CCM SHOULD HAVE LET SITA AND OTHERS GO

Sometime ago to be exact in February 2009 I read an article on letting go. What happened a few days ago when Speaker Sita was being asked by some of his colleagues in CCM to return the card and call it quits with the CCM woulld it not have been wise if he were to follow the advice in this article by Bishop TD Jakes? That he SHOULD HAVE LET IT GO?!!!!!

Please go ahead and read the articlle:

“And hear me when I tell you this! When people can walk away from you: let them walk. I don’t want you to try to talk another person into staying with you, loving you, calling you, caring about you, coming to see you, staying attached to you. I mean hang up the phone.
When people can walk away from you let them walk. Your destiny is never tied to anybody that left.The bible said that, they came out from us that it might be made manifest that they were not for us. For had they been of us, no doubt they would have continued with us. [1 John 2:19]
People leave you because they are not joined to you.. And if they are not joined to you, you can’t make them stay. Let them go.
And it doesn’t mean that they are a bad person it just means that their part in the story is over. And you’ve got to know when people’s part in your story is over so that you don’t keep trying to raise the dead. You’ve got to know when it’s dead.
You’ve got to know when it’s over. Let me tell you something. I’ve got the gift of good-bye. It’s the tenth spiritual gift, I believe in good-bye.. It’s not that I’m hateful, it’s that I’m faithful, and I know whatever God means for me to have He’ll give it to me. And if it takes too much sweat I don’t need it. Stop begging people to stay. Let them go!!.............................
 
Pakacha,
Mkuu hakuna serikali yoyote inayoweza kumhukumu Msika wake kwa sababu analitumia bunge kuwaadhibu viongozi wa chama chake ambao wanakiuka ilani za chama...Spika hayupo bungeni kuwakilisha chama isipokuwa kusimamia vikao vya Bunge kwa uwazi..ni kama hakimu ambaye pamoja na kuwa ni mwanasheria basi mnataka lazima awe upande wa district Attoney ktk mashtaka yote...
Nina hakika kabisa kuwa Demoktratic hawana uwezo wala nguvu ya kumnyang'anya kadi ya chama Nancy Pelosi kwa sababu tu anapingana na baadhi ya senata wa chama chake.
Binafsi sijaona kifungu wala sehemu ambayo inamweka Sitta hatiani kwa kushambulia viongozi wabaya ndani ya chama. Hajawahi kusema wala kuhoji katiba, ilani na mwongozo wa chama chake akiwa bungeni..
Mkuu wangu kumkataa Sheikh au Padre fulani haikuondoi ktk Uislaam au Ukristu...Ila nachoweza kusema JK anawachezea CCM sasa hivi. Kwa kuleta mada hii ktk kikao cha CC, JK anataka kuwajua wote waliosimama upande wa pili na walivyokuwa wajinga samaki wengi wameivaa ndoana yake. Leo hii JK anawafahamu wote waliosimama upande wake au wa Lowassa. Kazi imekwisha kilichobakia ni kuifanyia kazi report nzima na ndio maana Mzee wetu Mh. mwinyi anaifanyia kazi..

Hakika umenena!!!
 
Kama upo TZ zingatia ujumbe huu unaosambazwa kwa SMS:

Tundu Lissu azungumzia Sheria ya Haki, Mamlaka na Kinga za Bunge na masahibu ya Spika Sitta na NEC ya CCM, kesho saa 12 Asubuhi, Pambazuka ITV.
 
Kumeingia Ufa Mkubwa CCM,na hata Msamaha wa Mh.Sitta aliouomba mbele ya wana-NEC huko Dodoma sio kwamba alipanga kuuomba,bado anajiona ana haki ya kusimamia anachoamini...sasa kazi imebaki kwa Wananchi,Msiirudishe CCM kwenye Utawala,katika Uchaguzi wa 2010.......Ile CCM aliyoiongoza Mwalimu amekwenda nayo Kaburini....CCM ya leo inaongozwa na watu wenye Uwezo wa Pesa,Huyu Kikwete kamshinikiza Mh.Sitta kuomba Msamaha leo,akumbuke kuwa Kesho itakuwa zamu yake,Hao Mafisadi wanajipanga kuwashawishi wanaCCM wenzao kumuondoa Kikwete kwa kutokuwa na Uwezo wa kushinda tena...Kikwete kazungukwa na watu wenye Uwezo na akili Kumshinda yeye....Na kwa akili yake anashindwa kuligundua hilo!.....Malecela amelijua hilo,Yeye ni supporter wa Sitta kwa kuogopa Mvurugano yupo nje ya Nchi........Mzee Mwinyi ,Mzee Msekwa wote wanajua fika kuwa Sitta ni Mkweli...Sipendi kabisa Mazingaombwe haya...Kweli tanzania ni kichwa cha mwendawazimu.

Hapa ndipo ninapomkumbuka mwanachama wa JF anayejiita Mwanafalsafa kuna Tundiko moja alisema Nanukuu "Tanzania tumejaliwa kila kitu,kasoro yetu ni Uongozi".

Bila Uoga nathubutu kusema leo...Bila kuiondoa CCM kwenye Sanduku la kura...kila siku tutapiga mark time...maendeleo ya kweli yanazuiwa na Uongozi mbovu wa CCM....Ni karibu nusu karne sasa toka tupate Uhuru..lakini bado tumekuwa nyuma kwa huduma nyingi Muhimu kwa maisha ya kila siku.

Mwalimu aliwahi kusema kuwa...Upinzani Imara utatokea ndani ya CCM, Ewe Sitta,warudishie hao CCM hiyo kadi yao...Kwani CCM ni Mama yako?


Mwawado, nakubaliana nawe kwa asilimia mia moja. Lazima tutekeleze kwa vitendo kile ambacho tunaamini kitaiweka nchi hii katika mstari. Suala la kuondolewa kwa CCM sasa halihitaji tena mjadala. CCM hii ambayo inatetea ufisadi waziwazi imeshapoteza sifa ya kuendelea kuwa chama tawala. Tunafanya nini sasa? Hilo ndilo suala la kujadili humu. Kila mtu mahali alipo atafakari ni jinsi gani tutajinasua kutoka kwenye makucha ya Chama Cha Mafisadi.
 
8/18/2009

Prof Safari ataka CCM iweke bayana sera ya ufisadi

Na Waandishi Wetu

MTAALAMU wa masuala ya sheria na wakili wa kujitegemea, Profesa Abdallah Safari ameitaka CCM iweke bayana kuwa ina sera ya ufisadi baada ya chama hicho tawala kuweka mikakati ya kumdhibiti Spika Samuel Sitta ili asiruhusu mijadala inayoikosoa serikali.

Sitta, ambaye bunge lake limekuwa likiipeleka mchakamchaka serikali kiasi cha kusababisha Edward Lowassa ajiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu, aliwekwa kiti moto na kikao cha Halmashauri Kuu kwa madai ya kuruhusu mijadala inayokichafua chama na serikali na kupendelea kikundi cha wabunge wanaoshambulia baadhi ya wanachama wa CCM.

Habari zinadai kuwa wajumbe wa Nec walitaka spika arejeshe kadi ya CCM, lakini baada ya kuongea na mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete Sitta alilazimika kuomba radhi.

Akizungumza na Mwananchi jana, Prof Safari alisema chama hicho sasa kinapaswa kutangaza hadharani kwamba falsafa yake ni kutetea mafisadi.

Prof Safari alisema uamuzi huo wa kikao cha juu kabisa cha chama hicho, umeonyesha kuwa ndani ya CCM hakuna kiongozi msafi, wote ni mafisadi isipokuwa wanazidiana viwango.

Naye mhadhiri mwandamizi, Idara ya Sayansi ya Siasa na Uongozi wa Umma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema hatua iliyofikiwa na CCM ni matokeo ya kuwepo kwa makundi ndani ya chama hicho.

“Udhibiti ndani ya chama ni jambo la muhimu, lakini pia usikivu wa chama kwenye hoja za msingi ni muhimu zaidi…iweje mtu aliyepigiwa kura na CCM wenyewe kuwa spika, leo awe amegeukwa,” alihoji Bashiru.

Profesa Issa Shivji alisema kuwa kitendo cha kutaka kumpokonya spika kadi ya uanachama ambacho kingesababisha apoteze ubunge na kuvuliwa nafasi hiyo ya kuongoza moja ya mihimili mikuu mitatu ya serikali, si sahihi kwa sababu kingeweza kusababisha mgongano ndani ya chama, hivyo wajumbe wa NEC walipaswa kuangalia adhabu nyingine.

Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahimu Lipumba alimponda Spika Sitta kwa kitendo kilichoripotiwa kuwa cha kuomba radhi kwa wajumbe wa Nec, akida kimedhihirisha kuwa spika ni kiongozi laini na dhaifu.

Prof Lipumba alisema kama Sitta ni kiongozi jasiri kwa Watanzania angesimamia haki ambayo anaifanya katika kusimamia bunge.

Alisema kwa vile Sitta alikuwa anapambana na ufisadi na kuwapatia fursa wabunge kufichua ufisadi uliokuwa unafanywa na baadhi ya viongozi wa serikali na wa CCM, basi angetetea utendaji wake.

“Kama Sitta angekuwa madhubuti na jasiri angekubali kuadhibiwa na baadaye akalishitaki hilo kwa wananchi kwa kuwa alichokuwa anakifanya ni cha haki,” alisema Lipumba na kuongeza spika alishindwa kusimamia haki.

Alisema hilo linadhibitisha wazi kuwa CCM haina nia na uwezo wa kupambana na ufisadi.

“Hii ni aibu kwa CCM; badala ya kupambana na ufisadi na mafisadi, sasa wameamua kupambana na kuwapiga vita wenzao wanaopambana na ufisadi,” alisema Lipumba. Habari hii imeandaliwa na Patricia Kimelemeta, Claud Mshana, Sadick Mtulya, James Magai na Salim Said
 
Jamani mtaniwia radhi kwani kuna vitu bado sijavielewa, kwa hiyo kosa la Sitta haswa ni nini ?
 
Prof Safari ataka CCM iweke bayana sera ya ufisadi

Na Waandishi Wetu

MTAALAMU wa masuala ya sheria na wakili wa kujitegemea, Profesa Abdallah Safari ameitaka CCM iweke bayana kuwa ina sera ya ufisadi baada ya chama hicho tawala kuweka mikakati ya kumdhibiti Spika Samuel Sitta ili asiruhusu mijadala inayoikosoa serikali.

Sitta, ambaye bunge lake limekuwa likiipeleka mchakamchaka serikali kiasi cha kusababisha Edward Lowassa ajiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu, aliwekwa kiti moto na kikao cha Halmashauri Kuu kwa madai ya kuruhusu mijadala inayokichafua chama na serikali na kupendelea kikundi cha wabunge wanaoshambulia baadhi ya wanachama wa CCM.

Habari zinadai kuwa wajumbe wa Nec walitaka spika arejeshe kadi ya CCM, lakini baada ya kuongea na mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete Sitta alilazimika kuomba radhi.

Akizungumza na Mwananchi jana, Prof Safari alisema chama hicho sasa kinapaswa kutangaza hadharani kwamba falsafa yake ni kutetea mafisadi.

Prof Safari alisema uamuzi huo wa kikao cha juu kabisa cha chama hicho, umeonyesha kuwa ndani ya CCM hakuna kiongozi msafi, wote ni mafisadi isipokuwa wanazidiana viwango.

Naye mhadhiri mwandamizi, Idara ya Sayansi ya Siasa na Uongozi wa Umma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema hatua iliyofikiwa na CCM ni matokeo ya kuwepo kwa makundi ndani ya chama hicho.

"Udhibiti ndani ya chama ni jambo la muhimu, lakini pia usikivu wa chama kwenye hoja za msingi ni muhimu zaidi…iweje mtu aliyepigiwa kura na CCM wenyewe kuwa spika, leo awe amegeukwa," alihoji Bashiru.

Profesa Issa Shivji alisema kuwa kitendo cha kutaka kumpokonya spika kadi ya uanachama ambacho kingesababisha apoteze ubunge na kuvuliwa nafasi hiyo ya kuongoza moja ya mihimili mikuu mitatu ya serikali, si sahihi kwa sababu kingeweza kusababisha mgongano ndani ya chama, hivyo wajumbe wa NEC walipaswa kuangalia adhabu nyingine.

Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahimu Lipumba alimponda Spika Sitta kwa kitendo kilichoripotiwa kuwa cha kuomba radhi kwa wajumbe wa Nec, akida kimedhihirisha kuwa spika ni kiongozi laini na dhaifu.

Prof Lipumba alisema kama Sitta ni kiongozi jasiri kwa Watanzania angesimamia haki ambayo anaifanya katika kusimamia bunge.

Alisema kwa vile Sitta alikuwa anapambana na ufisadi na kuwapatia fursa wabunge kufichua ufisadi uliokuwa unafanywa na baadhi ya viongozi wa serikali na wa CCM, basi angetetea utendaji wake.

"Kama Sitta angekuwa madhubuti na jasiri angekubali kuadhibiwa na baadaye akalishitaki hilo kwa wananchi kwa kuwa alichokuwa anakifanya ni cha haki," alisema Lipumba na kuongeza spika alishindwa kusimamia haki.

Alisema hilo linadhibitisha wazi kuwa CCM haina nia na uwezo wa kupambana na ufisadi.

"Hii ni aibu kwa CCM; badala ya kupambana na ufisadi na mafisadi, sasa wameamua kupambana na kuwapiga vita wenzao wanaopambana na ufisadi," alisema Lipumba. Habari hii imeandaliwa na Patricia Kimelemeta, Claud Mshana, Sadick Mtulya, James Magai na Salim Said

Kutokana na maelezo yaliyowekwa hapo juu kuwa yalisemwa na Lipumba, inadhihirisha wazi kuwa aidha anataka kupotosha ukweli, ama hajui ukweli au alitamani matokeo tofauti na yalivyokuwa kwa Sitta.

Nadhani Lipumba anajua wazi kuwa NEC si kikao kinachoongozwa na Sitta. Anafahamu wazi kuwa ule si uwanja ambao Sitta alitakiwa kuonyesha makucha yake au msimamo wake kuhusiana na utekelezaji wa kazi zake kama spika. Hakutakiwa kabisa kufanya hivyo kwa kuwa hata mkutano ule haukuwa sahihi kujadili mambo yaliyojadiliwa ndani ya Bunge na kutaka kuyatolea hukumu. Kufanya hivyo ni kuvunja sheria/Katiba ya nchi.
 
Mkulu MkamaP kwa Tanzania mambo ni kinyume kabisa mno .Hili wazo la kuingia CCM limekuwepo na watu tumejaribu .Labda nimkumbushe Kitila .Je mkuu Kitila wakumbuka ile NYF?Tulikuwa na akina Nchimbi Naibu Waziri sasa , Zitto, kama akina Killimbah, nk .Tukasema tugawanyike kwa jina kuleta haya unayo yasema leo. Hebu ona kinacho tokea sasa .Watu wamesha pata Ulaji na hata ukimpigia simu unamuuliza bwana vipi anakueleza CCM ni nzito .

Ukiingia means umekubaliana nao muendelee kudhulumu hakika huwezi kuwa ndani ya CCM then useme nataka kuwa mjumbe wa NEC ili kupambana na wala rushwa ndani ya Chama nk .Watu walijaribu kutia kaneno tu siku hizo kama Kolimba leo wako wapi ?

Dawa ni kuwa upande wa Pili hata usipo fanikiwa lakini umetimiza wajibu wako si lazima uwe Rais hapana .Mrema did it ila alidhani he was above all Tanzanians ndiyo kosa lake .

Mkuu wangu

Nakubaliana na wewe kwa mengi ila nafikiri mbinu yenu haikuiva ,maana ya kwamba mlitaka yai la kuku lilotagwa siku hiyo na siku hiyo hiyo mpate kifaranga na kifanga huyo siku hiyo hiyo atage yai jingine,mambo haya yanahitaji mipango thabiti na ya mda mrefu.

Mkuu unapoamua ku declare vita lazima uwe umemsoma mpinzani wako ktk maeneo aliyojidhatiti na maeneo aliyo dhaifu na majumuisho yake ukiona ana ujuzi wa kutosha kukupita rudisha silahaa zako ndani ,jipange upya hadi utakapoona uko fiti.

Nafikiri ni kwenda kinyume na karne na matwakwa ya akili ya kiasili kwenda kupambana (vitani) ilihiali wafahamu bayana vita hutoshinda na hata kama uwezekano wake ni hafifu karibu na hasi ,huo utakuwa si mpambano maana hata kama mpinzani wako akikunoa ngumi utaanguka kwa hofu na utampa ushindi kirahisi mpinzani na utakuwa umepoteza resources nyingi ambazo sitakurudisha nyuma kuliko ulipokuwa.Hapa na mkumbuka mwana bondia Bruno huyu jamaa alifahamu hata mshinda Tyson na kwa hofu hiyo ile kipenga kimepulizwa tu tyson karusha kombora likamukosa Bruno lakini Bruno alianguka chini na mpambano kuisha.

Kwanini tuzidiwe utashi na akili na mnyama kama kiboko?unajuwa kiboko akizaliwa dume huwa anafichwa na mamaye maana babake akimuona atamuuwa kuhofia hapo baadae ata chukua nafasi ya baba,hivyo huyu kiboko mtoto huwa anajificha siku zote lakini kila asubuhi hutafuta alipokanyaga baba yake na yeye anakanyaga mlemle kuangalia kama kisha kuwa kama babayake na akiona unyayo wake bado mdogo hurudi mafichoni,lakini siku atakapokanyaga na kuona nyayo wake unalingana na babake ,basi siku hiyo hutoka mafichoni rasmi na huwa yuko tayari kwa zari ama tifu lolote kutoka kwa babayake.
 
- Okay the dataz ni kwamba kwanza kikao kimekwisha, ni kweli kulikuwa na njama kubwa sana ambayo imekua ikisukwa na Lowassa, ya kumn'goa Spika.

- The dataz ni kwamba jumla ya shillingi millioni 50 zilitumika hasa kuwanunua wajumbe wa visiwani, ambao wote kwa pamoja walililia kichwa cha Spika lakini hela zilizotumika hazikuwa nyingi sana, meaning kwamba hata mafisadi wameanza kupungukiwa na pesa, kundi la upande wa pili liliweza kuwazima kwa hoja nzito sana kwamba tatizo la Spika ni la CCM kwa ujumla, na kwamba chanzo ni tatizo la Taasisis za CCM na Serikali na hasa kamati ya wabunge wa CCM.


Respect.

FMEs!

du kembe mil 50 inaweza kufanya mambo mengi kiasi hicho
siamini!!!!!
kweli wajumbe wa nec ccm ni very cheap?????
ndio maana kila siku wanarudi kuwa omba omba, sasa hiyo mil 50 wakigawana itawapeleka wapi
halafu wenzao wanakamua bil 50
 
- The whole thing is a big joke, mafisadi wanataka kichwa cha mpiganaji na they almost got it kama sio Makamba factor, ambayo ilimfanya Muungwana kurudi nyuma against the plan, kwa sababu kama Muungwana hakuwa nao kina Lowassa kwenye hili la kumng'oa Spika, how come aliwaruhusu wajumbe wote waliokuwa planted na Lowassa for this job kuzungumza kwanza na kujenga hoja againts Spika kama Lowassa alivyotaka?

- Spika ameponzwa na mpiganaji mmoja mwenye mdomo mrefu sana, ambaye amekuwa akiwasiliana sana na RO na Muungwana, kuhusu mbinu za wapiganaji kumlinda Spika akidhani kwamba hawa wawili wanaunga mkono wapiganaji kumbe ni sungura wajanja! Sasa ni wakati wa huyu mpiganaji ku-shut up na Spika ku-watch his back!

- Kuna kipindi katika hicho kikao, kulikuwa na mazungumzo ya faragha kati ya marais watatu, wawili wa zamani na Muungwana, the dataz ni kwamba the subject ilikuwa how to deal with jm na his predictions, hapa ndipo Muungwana alionyesha rangi yake kamili, na alifanya hivyo akidhani yale mazungumzo ni siri! Bwa! ha! ha! Tumeshindwa hivi vita na mafisadi, lakini ni lazima kuendelea kuwakosesha japo usingizi tu!

Lakini vita vyenyewe, tumeshindwa tayari kwa sababu after this sagga uwezekano wa Spika kurudi bungeni kutoka jimboni ni almost none! Na akiondoka tu vita ndio vimezikwa rasmi!

Mungu Aibariki Tanzania.


Respect.

FMEs!
 
Field Marshall Es,
kwa sababu kama Muungwana hakuwa nao kina Lowassa kwenye hili la kumng'oa Spika, how come aliwaruhusu wajumbe wote waliokuwa planted na Lowassa for this job kuzungumza kwanza na kujenga hoja againts Spika kama Lowassa alivyotaka?
Mkuu wangu huwezi kuwajua wabaya wako bila kuwapa nafasi wakajikaanga wenyewe.. maneno mazito yaliyosemwa against Sitta ni ushahidi tosha wa watu waliopo nyuma ya Lowassa na RO..this is what JK alikuwa akihitaji siku zote.. names!..Tena basi wamepatikana na wengine waliokuwa wamejificha kwa sababu tu walifikiria JK yuko nao pamoja..

FMES, kwa lugha yetu ya kizamani unaitwa borntown,hivi kweli unaamini JK angetaka Sitta atolewe nje angekuwa na mazungumzo naye baadaye!.. Mbona asimshauri Lowassa kuomba msamaha bungeni..JK anamhitaji Sitta na kazi yake kaifanya hasa ktk mkutano huu mkuu kwani prediction za mzee Malecela zilihusiana zaidi na watu wanaotakiwa kusimama Ubunge mwaka 2010. By now wameisha jua wataanzia wapi kufanya usafi kisha mtaambiwa wananchi kuwa wachafu wote wameondolewa!..Na wananchi wasipokaa macho mshindi CCM kwa goli la kilaini utadhani Droba dakika ya 90 kuleta ushindi.
 
- The whole thing is a big joke, mafisadi wanataka kichwa cha mpiganaji na they almost got it kama sio Makamba factor, ambayo ilimfanya Muungwana kurudi nyuma against the plan, kwa sababu kama Muungwana hakuwa nao kina Lowassa kwenye hili la kumng'oa Spika, how come aliwaruhusu wajumbe wote waliokuwa planted na Lowassa for this job kuzungumza kwanza na kujenga hoja againts Spika kama Lowassa alivyotaka?

- Spika ameponzwa na mpiganaji mmoja mwenye mdomo mrefu sana, ambaye amekuwa akiwasiliana sana na RO na Muungwana, kuhusu mbinu za wapiganaji kumlinda Spika akidhani kwamba hawa wawili wanaunga mkono wapiganaji kumbe ni sungura wajanja! Sasa ni wakati wa huyu mpiganaji ku-shut up na Spika ku-watch his back!

- Kuna kipindi katika hicho kikao, kulikuwa na mazungumzo ya faragha kati ya marais watatu, wawili wa zamani na Muungwana, the dataz ni kwamba the subject ilikuwa how to deal with jm na his predictions, hapa ndipo Muungwana alionyesha rangi yake kamili, na alifanya hivyo akidhani yale mazungumzo ni siri! Bwa! ha! ha! Tumeshindwa hivi vita na mafisadi, lakini ni lazima kuendelea kuwakosesha japo usingizi tu!

Lakini vita vyenyewe, tumeshindwa tayari kwa sababu after this sagga uwezekano wa Spika kurudi bungeni kutoka jimboni ni almost none! Na akiondoka tu vita ndio vimezikwa rasmi!

Mungu Aibariki Tanzania.


Respect.

FMEs!

Naomba Mungu hadithi zako ziwe za uwongo kwani hakuna mtu anayenikatisha tamaa kama wewe. JM anayepanga mikakati ya kuiba kura (busanda) ni hatari sana. Tunapoongea kung'oa mafisadi nadhani na yeye yumo!
 
du kembe mil 50 inaweza kufanya mambo mengi kiasi hicho
siamini!!!!!
kweli wajumbe wa nec ccm ni very cheap?????
ndio maana kila siku wanarudi kuwa omba omba, sasa hiyo mil 50 wakigawana itawapeleka wapi
halafu wenzao wanakamua bil 50

Wengi wao walitoka visiwani ! Si unajua tena kuna siku hatma ya watu milioni 40 itaamuliwa na wawakilishi wa watu milioni moja. Ndio katiba yenyewe - athari za muungano ?.
 
- At this point, vyama vya upinzani vilitakiwa kutayarisha maandamano makubwa sana ya wananchi as a reaction to this conspiracy ya kuwanyamazisha wapiganaji wanaojaribu japo kidogo kulisimamia taifa, lakini wapi!

- Viongozi wa upinzani wanaongea powerlessly kama sisi tu wananchi wa kawaida, the media ndio hiyo sio siri kwamba imenunuliwa na hawa mafisadi kwa sababu ni gazeti moja tu la Raia Mwema, linalo ripoti the truth of what happened huko ndani ya kikao, wengine wote ni habari ya kupewa na the master wa media manipulations yaani DR. Nchimbi, ahhhggrrrrrrrrrr!

Respect.

FMEs!
 
Field Marshall Es,

Mkuu wangu huwezi kuwajua wabaya wako bila kuwapa nafasi wakajikaanga wenyewe.. maneno mazito yaliyosemwa against Sitta ni ushahidi tosha wa watu waliopo nyuma ya Lowassa na RO..this is what JK alikuwa akihitaji siku zote.. names!..Tena basi wamepatikana na wengine waliokuwa wamejificha kwa sababu tu walifikiria JK yuko nao pamoja..

FMES, kwa lugha yetu ya kizamani unaitwa borntown,hivi kweli unaamini JK angetaka Sitta atolewe nje angekuwa na mazungumzo naye baadaye!.. Mbona asimshauri Lowassa kuomba msamaha bungeni..JK anamhitaji Sitta na kazi yake kaifanya hasa ktk mkutano huu mkuu kwani prediction za mzee Malecela zilihusiana zaidi na watu wanaotakiwa kusimama Ubunge mwaka 2010. By now wameisha jua wataanzia wapi kufanya usafi kisha mtaambiwa wananchi kuwa wachafu wote wameondolewa!..Na wananchi wasipokaa macho mshindi CCM kwa goli la kilaini utadhani Droba dakika ya 90 kuleta ushindi.

Whaaat ? - Mkuu Mkandara tell me this is not a joke !
 
Back
Top Bottom