Sonara
JF-Expert Member
- Oct 2, 2008
- 726
- 71
Duh, kama ni kweli basi anatakiwa kufikiria kwa mapana kauli kama hiyo!
Mkuu nani mmoja wapo kati ya wawili hao afikirie kauli hiyo ?
Duh, kama ni kweli basi anatakiwa kufikiria kwa mapana kauli kama hiyo!
Kigogo, ni kweli niko Dodoma hata sasa. Ukipenda niweke upande wowote, maana hali ilivyo kwa sasa, kubaki katikati ni hatari zaidi.
Mkuu nani mmoja wapo kati ya wawili hao afikirie kauli hiyo ?
Nikiwa mjumbe wa NEC ....
WAREMBO HUNUKA KIKWAPA
Jamani mtaniwia radhi kwani kuna vitu bado sijavielewa, kwa hiyo kosa la Sitta haswa ni nini ?
Chama Cha Mapinduzi ni chama cha wananchi. Kiongozi yeyote aliye madarakani kwa tiketi ya CCM aelewe kuwa nafasi hiyo aliyonayo ni dhamana aliyopewa kwa ridhaa ya wanachama wa CCM. Haitavumilika wala kukubalika kwa kiongozi yeyote yule anayetokea CCM kutumia nafasi hiyo kwa ajili ya kujijenga binafsi kwa gharama ya kuharibu maadili na maslahi ya chama. Pia ieleweke kuwa Chama cha Mapinduzi kina utaratibu na, viongozi na wanachama waliomakini katika kukabiliana na matatizo yanayoweza kujitokeza ndani na nje ya Chama.
Endapo kiongozi yeyote yule amekwenda kinyume na maadili au maslahi ya Chama basi hana budi kuwa muungwana na kuomba radhi na ajisahihishe. Vinginevyo, arudishe kadi!
Kigogo, ni kweli niko Dodoma hata sasa. Ukipenda niweke upande wowote, maana hali ilivyo kwa sasa, kubaki katikati ni hatari zaidi.
JK hana sasa hivi na hakuwa na kabla sifa wala uwezo wa kuingoza Tanzania .Mtabisha laini ukweli ni huo.
Mr.Baija Balobi,
Vipi wana UV-CCM wapo huko na wanamsimamo gani au tetesi zao zikoje??me hao ndio napenda kujua wana hali gani na mtazamo upi maana najua wapo huko, maana wao ndio wapiga debe full kwenye makampeni??
Yote hii ilipangwa babuuu, kama JK angetaka Sitta awe nje hakuna mtu yeyote angepinga lakini kwa ujinga wao walifikiria JK yuko nao na huu ndio mwisho wa makelele ya Sitta bungeni.
Kumbuka mkuu Sitta wa leo sii yule aliyenza na Lowassa au wakati sakata la Richmond linapingwa na Lowassa kuzungumziwa.. Sitta alikuwa mklai hata Zitto kutolewa nje ya kikao lakini baada ya kupata baraka za JK unajua yaliyofuata.
Ilibidi ionekane kuwa JK hayupo na Sitta ili kujaza kokoro..kisha ajabu kutoka kwa Sitta kulikuwa rahisi sana kwani waamuzi hawakuwa tena wajumbe wapinzani ila wazee wa CC kina Mwinyi ambao tayari wanajua kinachofuatia..
Mkuu wangu wazee wote wa CCM wanataka JK akawajibishe Mafisadi kukisafisha chama -How na ukubwa wa kundi hilo ndio ilikuwa shida kwani uchaguizi mkuu wa 2010 adui wa kwanza wa CCM ni Mtandao.. wakiwaondoa hao, kazi iliyobakia ndogo sana..
Sitta amefika mahala ameligeuza Bunge kuwa sehemu ya kuibua mashitaka, kuendesha kesi na kutoa hukumu, badala ya kuwa chombo cha kutunga sheria, alisema mmoja wa wajumbe wa NEC
Huyu jamaa (Sitta) na wapambe wake wamekuwa wakikivuruga chama na serikali ndani na nje ya Bunge kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, kwa kisingizio cha ufisadi. Leo hii wamejionea wenyewe namna damu ya watu waliowaonea kama Edward Lowassa na wenzake inavyowalilia, alisema mjumbe mwingine.
Bunge limeanza kuwa kama mchezo wa (kikundi cha televisheni cha vichekesho) The Comedy. Yaani kila mtu anafanya mambo yake mwenyewe, hali ambayo inaweza kusababisha watu kurushiana hata viatu ndani ya Ukumbi wa Bunge, sasa hali hii maana yake nini?," alisema katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, John Chiligati
Kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele. Wanaoropoka ovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo limejiona kama ni wateule wa kuzungumzia sakata hilo (la ufisadi) bila ya kujua wabunge wote wana haki ya kuzungumzia suala hilo, lakini kwa utaratibu tena kwa kupitia katika vikao vya kamati za wabunge.
aliongezea John Chiligati.
"Mkapa anastahili pongezi sio kejeli; anastahili heshima sio dharau na pia anastahili kuenziwa sio matusi," alimalizia.
Mkuu Mkandara, Mwenyekiti wa CCM na Raisi wa JMT, Mrisho Jakaya Kikwete unadai aliruhusu haya yote yasemwe kwenye kikao rasmi cha NEC ili awajue wabaya wake ! Sasa hapa atakuwa na mpango wa kumtosa nani - mafisadi au wapinga ufisadi ? Kwa maana nyingine unasema hakuwa na tatizo na Bunge kudhalilishwa maadam sasa kazi ya kuisafisha CCM inakuwa rahisi baada ya hiki kikao.
Duh, JMK ni kiboko - ana akili ya ziada ati !