Tunapozungumzia usajili na tukasema tuna kikosi chembamba, kuna watu (Washabiki wenzetu wa Liverpool) wanatuambia kuwa hakuna Mchezaji mzuri ambaye yupo tayari kuja Liverpool kukaa Benchi kwasababu kuna Salah, Mane na Firmino.
Hivi hawa watu wanatumia hoja gani? Jamani hebu nifahamisheni kwa hili!
Kwa kigezo gani Kuwa wachezaji wetu (Mane, Bobby na Salah) hawawezi kuekwa Bench?
Kwa mfano tungemsajili Joao Felix ndiyo angekaa bench mbele ya hawa Mane, Bobby na Salah?
Tuwe wakweli bhana hao wachezaji ni wa Kawaida sana na wachezaji wa Kiwaeka Bench wapo wengi!
Hata Coutinho tuliamini hakuna mchezaji wa kumueka Benchi kumbe nje ya Liverpool ni wa kawaida sana tu.
Kwahiyo ni kwamba wachezaji wanaonekana wakali kwasababu wanafaidika na Mfumo wa Klopp tu!
Inamaana hata hao kina Timo Werner wakija Liverpool nawao watafaidika na Mfumo wa Klopp na watakuwa wakali kuwaweka benchi hao Front 3.
Klopp asajili tusilete visingizio kuwa wachezaji hawatotaka kwasababu kuna Mane, Bobby na Salah.
PSG kuna Neymar, Mbappe, Di Maria na Cavani lakini kina Icardi wameenda kujichomeka palepale.
Idriss Gana Gueye hakusema kuwa haendi PSG kwasababu kuna kina Verrati, ameenda na ameweza kutoboa.
Kwahiyo tuwe positive jamani.