Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Hahaaa hata km n kuponda club sio kwa namna hii
Liver ana point tatu, unasemaje anasindikiza??
Wakat huohuo TOT hana point ila husemi kam anasindikiza
Spurs timu ndogo hamna mtu ana time nayo. sisi tuna muda na majogoo
 
Game tatu mfululizo looseful hawajashinda hata moja
Wasindikizaji kwenye haya mashindano ni liver
Ni mapema mno kusema Liverpool ni wasindikizaji, at least sio katika group stage
Bado mechi nne, moja ya kukamilisha mzunguko na tatu za marudiano.
 
Kwanza niseme wazi kuwa leo timu imecheza hovyo hovyo balaa, yaani it was extremely poor performance.

Pili niseme wazi kuwa Klopp leo maamuzi yake hayakuwa sahihi hata kidogo, especially baada ya kipindi cha pili kuanza. Mtu kama Salah hakutakiwa kurudi kipindi cha pili, ilitakiwa nafasi yake ichukuliwe na Shaqiri. Pia Firmino ndiyo angetoka nafasi yake aingie Sturridge. Kitendo cha kusubiria mpaka dakika ya 88 ndiyo unamuingiza Sturridge ni upuuzi. Mimi siyo kocha lakini niliona mapungufu ya wazi kabisa, nashangaa yeye Klopp kwa nini hakuyaona hayo.

Tatu niseme wazi kuwa mchezaji kama James Milner kwa umri wake na mechi zote anacheza siyo sahihi, ni wakati sasa wa Fabinho kuanza kucheza. Last season hatukuwa na depth kwenye squad yetu kwahiyo it was understandable wachezaji hao hao kucheza daily, this season Klopp afanye rotation ya akili.

Nne niseme wazi kuwa kwenye timu yetu kuna wachezaji washajua wao ni a must first eleven players, kwahiyo wameanza kubweteka...kocha afanye kazi yake hapo.

Mwisho niwapongeze Napoli although walitakiwa watupige kama nne hivi, maana leo tulikuwa hovyo sana!
Tukiendelea kucheza hivi tumekwisha, tutakuwa tunapigwa za kutosha.
Klopp alikuwa akibet kama mchezo wa Chelsea ndio maana kamwingiza dkd ya 88 ili dk ya 89 au 90 afunge la kusawazisha. Bad Bet
 
Kuhusu kulala mimi niko shift sa hii. Kwa hiyo niwache nikupe dozi kamili. Kuhusu kuyapokea matokeo hiyo mtajuana na mashabiki wenzenu. Napole kakutoboa na timu yako mnayoisifia ndiyo bora kwa sasa huku akiwepo Hendo uwanjani.

Pole sana. Nakutakia kila la kheri weekend
Lala mkuu acha kuwanga kwenye uzi wetu.

Matokeo yetu tumeyakubali na tumeyapokea kwa mikono miwili. Sio kama nyie mna visingizio kama washwahili
 
.
Screenshot_20181004-051552.jpeg
 
ryana fan, njoo umuone huyu mwenzako, au yeye huwa ana haki ya kuongea kabla ya mechi?!
Maana naona huwa unawakataza mashabiki wa The Reds kuongea kabla ya mechi!
Nimemuona......amekosea kidogo. Ila naona umekazwa kamoja tu. Khe khe khe khe .

Msiba umeandaliwa wapi...tulete rambi rambi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom