Mfwatiliaji
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 1,322
- 69
Ebu tupe yaliyojiri kuhusu BoT
Mkandara!
Upo kwenye wazo Langu nafikiri tumepishana sekunde ktk kujibu hoja ya FD.
Swala si kuongelea mazuri bali ni kuyatekeleza na mafanikio kuonekana.Kuongea tu hakusaidii na wala hakuleti tija ya aina yeyote na Faida kwa Wananchi.
FD,
Tupe jibu la maswali hayo hapo juu
Ujenzi wa reli utaanza lini? 2. kiasi gani? na 3. lini inategemewa kwisha
Huo usambazaji wa Umeme unatarajiwa kufikia kiwango gani cha asilimia na mwaka gani?
hayo mengine yote ktk hotuba yaweke ktk maswali haya haya kisha tupe jibu kama hutabaki na ahadi mkononi!
FD,
Kwanza kabisa ahsante kwa mchango wako hapa jamvini. Najua unapenda kuongelea "upande wa pili wa hiyo shilingi" yetu.
Kwa kuwa umetuomba kukuuliza maswali, miye swali langu ni kuwa; Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais na M/kiti wa CCM, je ameongelea vipi kuhusu swala la Mh. Balali kuendelea kuwa Gavana wakati serikali imeamuru uchunguzi ufanyike kwa kukubali hitilafu kadhaa zilizoonyeshwa na ripoti ya CAG, na madukuduku ya wadhamini wa Bajeti yetu, hali wakati Dr. Slaa anatoa hoja Bungeni walisema hayo ni mambo ya mtandaoni (internet) na si ya kuamini. Natanguliza shukrani zangu.
Ooh, BTW, naomba uache kuwaita wote wanaohoji kuhusu CCM kuwa ni Chadema. Kwani wengine hatuna vyama ndugu yangu. Ni hilo tu.
SteveD.
FD,
Kwa hiyo alichozungumza ni nadharia tu na hakuna kitu cha maana,unajua sisi watu wa hesabu tunajua 2+2=4.haya mambo ya tunafanya kwa siri ndio tusio yataka ktk ulimwengu wa sasa.basi yote ni utumbo tu hakuna jipya punda na masikio.manu 2,arsenal 1
Steve, Ninaomba radhi kuwaita Chadema, Nilishaomba hata hivyo hapo juu, nikasema nilimaanisha Lunyungu na Phil.
OK kaka tuendelee. Hakuongelea hayo yote uliyouliza.
Ila mimi nitakujibu kuwa, unajua Gavana ni mgonjwa na yupoa Marekani muda mrefu?, unajua kwanini uchunguzi umeanza ndio na yeye anaugua na kwenda USA?, ukifikiri tena kidogo tu utagundua kua amepumzishwa kwanza mpaka uchunguzi uishe.
Unajua Tuhuma zinaweza kuwa za kweli au za uongo, sio vizuri kumharibia mtu CV yake bure. Hivyo hata hivyo jamaa hayupo .... si ndio inavyotakiwa na ndio ILIVYO.
Kwahiyo sikuona kama ni issue.
Jamani tunaomba aliyekuwa kwenye huu mkutano bila unazi wa u-chama atupe yaliyojiri, akizingatia U-Tanzania. Mood ya walioshiriki n.k.