Live: Kizota Dodoma

Live: Kizota Dodoma

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
Bunge la Muungano wa Tanzania linabadilishiwa muda, ili kupisha mkutano wa CCM, now talk about getting our priorities twisted..
haya yote ni kuchagua spika ambaye ni mwanachama wa Chama tawala,ni bora spika angekuwa mtu asiyefungamana na upande wowote,wewe unadhani kungekuwa na mkutano mkuu wa CUF wangehairisha?
 
Kada,

Watch out utashusha credibility yako humu. Kuropoka ropoka sio dili humu. Matokeo leo saa tano.

Nimeshaondoka Dodoma. Nipo dar.
 
Piga, ua, Mtazamo wangu wa matokeo ya NEC 20 bara ni hawa:

Profesa Idris Mtulia, Andrew Chenge, Edward Lowassa, Abdulrahman Kinana, Juma Kapuya, John Komba, Yusuf Makamba, Benard Membe, Kingunge Ngombale- Mwiru,John Chiligati, Hassan Ngwilizi, Emmanuel Mwambulukutu, Aggrey Mwanri,Stephen Wassira, Christopher Mwita Gachuma, Enock Chambier, Frederick Sumaye, William Lukuvi, Jaka Mwambi, na James Msekela.

hapa kuna mtu mmoja umeshamsahau,Naibu waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja,huyu lazima awemo,ni mmoja wa watu wanaoaminiwa sana na JK..na atasaidiwa na RA kuweko katika kundi hilo
 
Bunge la leo halikaliki kwa wabunge wa ccm! Shughuli za leo zitakwendakwenda tu. I believe!
 
Kama ningekuwa mwanaCCM, na mjumbe wa Mkutano Mkuu, wa Kwanza kumwonea huruma angekuwa dada Shy-Rose, nadhani anakipenda chama sana, kwa muda mfupi niliomjua nimesikia akigombea sehemu nyingi sana na akawa anapigwa chini...
kilitimie

ni sababu zipi zinakufanya useme kwamba shy anaipenda sana sisiemu?
tuache mambo ya kuusemea moyo wa mtu,sisiemu kuna nini mpaka akupende,Je ni ufisadi?watu wote walikuwa na mapenzi ya kweli na chama wamekuwa hawapewi nafasi katika kuonyesha mapenzi yao,mfano mzuri ni dr. mwakyembe..
 
Sikufanikiwa kusikiliza hotuba ya tathimini ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya 2005, ambaye ilikuwa isomwe/imeshomwa na Waziri Mkuu kwa Upande wa Jamhuri ya Muungano na Waziri Kiongozi kwa upande wa SMZ,,, wenye nakala tunaomba!!!
 
kilitimie

ni sababu zipi zinakufanya useme kwamba shy anaipenda sana sisiemu?

Kitu kimoja ni obvious,,, mtu anayegombea nafasi mbalimbali anashindwa lakini anagombea tena, anashindwa anagombea tena nadhani ni ushahidi kwamba anakipenda hicho chama, anyway... yaishe baba Ebooooooo!!!
 
Hivi wakati tunashubiri matokeo kutoka huko Dodoma,,, Baada ya kusikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri na Mwenyekiti wa CCM, naomba munisaidie kuelewa vizuri issue ya Mkataba wa Buzwaji hashwa baada ya kupata maelezo ya ziada kutoka kwa mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano,,, na kuhakikisha kwamba katika mikataba ya madani hakuna kipengele ambacho kimeachwa kwa ajili ya mtu mmoja mmoja ku-negotiate!!! kila kitu aidha kiko kwenye sheria ya madini ya sheria za kodi, kwa maana nyingine anasema Waziri Wa Nishati na Madini hakukosea lolote... sasa swali kwa Zitto, MKJJ,Mnyika, Kitila, Mwafrika wa Kike,,, and the like,,,

Hoja ya kuundwa tume huru ya uchunguzi ilikuwa kwa ajili ya :-
1. kuchunguza nini haswa?
2. Kuchunguza kwamba je mkataba umesainiwa nje ya nchi?
3. kuchunguza uharaka wa kusainiwa kwa mkataba wenyewe?
4. kuchunguzaa nini hashwa ambacho sio wazi sasa?
5. Je ni jambo gani bado lina wingu hata baada ya mkuu wa nchi kutoa maelezo ya ziada.
6. Je bado kuna ulazima wa kuunda tume huru ya uchunguzi?

Naomba Mashabiki wa CCM, muache nijibiwe swali langu objectively!!!
 
saa tano ndo hii, tupeni yaliyojiri dodoma
 
Hayo Matokeo Yameshachezewa ...mimi Mikutano Yoote Ya Ccm Tangu Enzi Za Mwalimu Nimeijua Sijawahi Kuona Kutoa Matokeo Ya Kura Za Wajumbe 1600 Inahitaji Masaa Zaidi Ya Mawili ..always ...aje Mtu Hapa Aseme Lini Kura Zimelala Hadi Kesho Yake....kuna Mkutano Ulifanyika Chimwaga Hadi Saa Kumi Za Usiku ....ilikuwa Record Lakini Hawakutawanyika Kabla Ya Matokeo...

Kwa Maoni Yangu Matokeo Tunayosubiri Leo Watapita Tu Wale Ambao System Ya Chama Inawataka....nani Anataka Kina Mwandosya Na Sumaye Wapitishe Watu Wao Wa Kuja Kuwapigia Kura 2010....

Wee Kaa Kimya Tu Ukisika Atakayelia Baada Ya Hapo Ujue Jiwe La Kina Rostam Na Nchimbi[wajumbe Wa Kamati Ya Uchaguzi ] Limempata...nani Aliwaambia Zege Linalalaga...watu 1600 Kura Zao Kuhitaji Kulala Ni Kutaniana!!!!
 
kuhesabu kura za watu 1600 zisingechukuwa zaidi ya masaa matatu. na kwa vile ilikuwa ndo kwanza saa saba usiku, tulikwa tuachiwe komba atutumbuize huku tukisubiri matokeo.

hii ya matokeo siku ya pili, inatilisha shaka na vile vile hainogi
 
Hayo Matokeo Yameshachezewa ...mimi Mikutano Yoote Ya Ccm Tangu Enzi Za Mwalimu Nimeijua Sijawahi Kuona Kutoa Matokeo Ya Kura Za Wajumbe 1600 Inahitaji Masaa Zaidi Ya Mawili ..always ...aje Mtu Hapa Aseme Lini Kura Zimelala Hadi Kesho Yake....kuna Mkutano Ulifanyika Chimwaga Hadi Saa Kumi Za Usiku ....ilikuwa Record Lakini Hawakutawanyika Kabla Ya Matokeo...

Kwa Maoni Yangu Matokeo Tunayosubiri Leo Watapita Tu Wale Ambao System Ya Chama Inawataka....nani Anataka Kina Mwandosya Na Sumaye Wapitishe Watu Wao Wa Kuja Kuwapigia Kura 2010....
Wee Kaa Kimya Tu Ukisika Atakayelia Baada Ya Hapo Ujue Jiwe La Kina Rostam Na Nchimbi[wajumbe Wa Kamati Ya Uchaguzi ] Limempata...nani Aliwaambia Zege Linalalaga...watu 1600 Kura Zao Kuhitaji Kulala Ni Kutaniana!!!!

Hivi Admin kwa nini hakuna "Kura za Maruhani" kama za kule Zanzibar?,,, walahi mtoa hoja hapa juu anastahili moja!!! naona unatuwekea tu "thanks vote" tunahitaji na negative watu wakileta za kuleta...
 
kuhesabu kura za watu 1600 zisingechukuwa zaidi ya masaa matatu. na kwa vile ilikuwa ndo kwanza saa saba usiku, tulikwa tuachiwe komba atutumbuize huku tukisubiri matokeo.

hii ya matokeo siku ya pili, inatilisha shaka na vile vile hainogi

..mbona hiyo ni rahisi kung'amua!

..ccm ina wenyewe!wengine wasindikizaji!
 
Acheni zenu, mambo yapo sawa! Nani kati yetu anaweza kukesha masaa 24?
 
FD
Heshima mkuu. tunasubiri habari kutoka kwako tuanze kukupa hongera, nadhani mambo hayatakuwa mabaya, tunakuombea
 
Acheni zenu, mambo yapo sawa! Nani kati yetu anaweza kukesha masaa 24?

..mambo yote yako sawia ndio maana watu wakaenda kupumzika,ilihali na kiroho juu!

..ila kukesha watu wanaweza kukesha,point is kusingekuwa na mahudhurio mazuri bungeni,ambapo tunategemea itakuwa hivyo in ppls minds,but physically watakuwapo!
 
Hivi Admin kwa nini hakuna "Kura za Maruhani" kama za kule Zanzibar?,,, walahi mtoa hoja hapa juu anastahili moja!!! naona unatuwekea tu "thanks vote" tunahitaji na negative watu wakileta za kuleta...


SIO LAZIMA UPIGE KURA YA MARUHANI...KURA ZA MARUHANI WANAPIGA MARUHANI ...RUHANI ANAMPIGIA RUHANI..ADMN YUKO SAWA HAWEZI KUWEKA KURA ZA MARUHANI KWA KUWA JF SIO KIJIWE CHA MARUHANI.....

ILA UKWELI UKO PALE PALE SEKRETARIETI YA UCHAGUZI IMEKOSEA KUTANGAZA MATOKEO BAADA YA WATU KUTAWANYIKA ...HATA KAMA WAMEFANYA IN GOOD FAITH WALIOSHINDWA WATALALAMIKA CHINI CHINI ..KWA KUWA WANABANWA NA ITIFAKI ZA KICHAMA....NDIO BINADAMU WALIVYO ..USIKATAE...

SASA KUEPUKA MASHAKA BORA WANGESEMA WAJUMBE WASUBIRI ...ALIYECHIKA ANGEONDOKA..UP TO HIM...AFTERALL VIKAO VYA CHAMA KUKESHA SIO AJABU ..KAMA HAYA MAMBO UNAYAJUA NADHANI UTAKUWA UMESHAPATA KUKUTANA NAYO ...KWENYE VIKAO....
 
Nataka nikiri kwamba usiri umetawala mno matokeo ya kura . Baada ya muda mfupi nitakwea gari langu kenda Dar nikiwa mtupu . Mambo nasema si shwari hapa .
 
Back
Top Bottom