Kwanini wataliban waliichukua nchi ndani ya wiki mbili tu kwenye nchi yenye askari waliofunzwa vizuri kwa miaka 20 na kupewa silaha za kisasa?
 
Mbona Magufuli alizifuta mbio za Mwenge hawa wanashindwa Nini?
Au watu wanapiga pesa ndefu kutokana na mbio hizi?
 
Mbona Magufuli alizifuta mbio za Mwenge hawa wanashindwa Nini?
Au watu wanapiga pesa ndefu kutokana na mbio hizi?
Waziri wa fedha alipaswa kumshauri Rais kukata matumizi kwa muda ya vitu kama mbio za Mwenge na sikukuu wakati huu ambao tunapambana na covid, kusambaza umeme na maji, kujenga bwawa la umeme, reli, barabara na makao makuu badala ya kupandisha mafuta na tozo za miamala. Wananchi hawawezi kuona nia nzuri kwenye mboni za macho ya serikali badala yake watu wanaona viongozi wa serikali wasiojali watu wake wanalimaje, wanauzaje, wanavuaje, kufugaje, wanakulaje, wanajengaje na kusomeshaje.

Takwimu zinatuambia kuwa 90% ya watanzania ni tegemezi, wanawategemea 10% ya watu kwa mahitaji yao. hivyo vurugu zote hizi za serikali za miamala, mafuta, PAYE, VAT, nk zinawalenga hawa 10% ya watanzania. Hawa 10% ili kumudu kuhudumia 90% itawalazimu watafute ujanjaujanja wa mbio za mwenye, sherehe za uhuru na muungano, semina nyingi, kufanya tafiti za kufoji, kusifia viongozi hata kama hawapendi, kukwepa kodi, kuiba vitu au muda wa mwajili wao, kula rushwa na ujambazi, safari za nadani na nje ya nchi. Kila mtumishi na mfanyabiashara ni mwizi wa mali, muda, ama fedha za mwajili au umma.
 
Ndoo maana teuzi haziishi,JPM teuzi zingine alitia kapuni kuokoa fedha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…