Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,152
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada.

Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.

Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
 
Accounting really????
Wanamaliza wahitimu zaidi elfu 20 wa Accounting kwa level ya degree hapa Tanzania kila mwaka, lakini ajira rasmi za kudumu za kuwaajiri (tena za mchongo balaa) hazifiki hata 300 kwa mwaka, hao wengine wanakwenda wapi?

Serikali haajiri wengi na wala haajiri kila mwaka, na taasisi binafsi zenye kuajiri ni chache, kwa uchache sana huajiri, tena huajiri wenye uzoefu mkubwa na mzuri. Sasa mhitimu mpya anavukaje hapo?
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
Suala la ukosefu wa ajira ni kubwa tu kwa fani zote, nafasi ni chache haziwezi kutosheleza wahitimu waliopo.

Wakati wa kutengeneza mazingira rafiki na sera nzuri ili kuvutia watu kujikita kwenye sekta zingine kama Kilimo, ujasiriamali ni sasa, huku napo sio rahisi kabisa bila mitaji au mazingira wezeshi.
 
Tunahitaji mapinduzi halisi ya viwanda(industrial revolution), hatuhitaji kuwa na wahitimu wa vyuo vikuu kwa wingi huo, tunahitaji wahitimu wa vyuo vya kati wafanye kazi kwenye viwanda.

Engineer mwenye shahada na mwenye fani yake kwa level ya diploma au cheti, atakayeleta thamani ni mwenye diploma.

Tunahitaji viwanda, otherwise tuna bomb kubwa.
 
Suala la ukosefu wa ajira ni kubwa tu kwa fani zote, nafasi ni chache haziwezi kutosheleza wahitimu waliopo.

Wakati wa kutengeneza mazingira rafiki na sera nzuri ili kuvutia watu kujikita kwenye sekta zingine kama Kilimo, ujasiriamali ni sasa, huku napo sio rahisi kabisa bila mitaji au mazingira wezeshi.
Hivyo tunarudi pale pale, kwa 90% hakuna tena ulazima wa watu kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree. Ni kupoteza rasimali tu. Maana mwisho wa siku hupati ajira wala huwezi kutumia degree yako kutengeneza kipato.
 
Civil engineering haijatajwa hapo.

Haya hizo zingine (Maths, Physics, Chemistry) ajira zake zinapatikanaje kirahisi na kwa wingi?
Kumbuka kutofautisha degree ya Ualimu wa Maths/Physics/Chemistry na Degree ya Maths/Physics/Chemistry.
Ni lazima kujiongeza, usome digrii ya maths bila kuihusisha na fani yoyote lazima uumie.
 
Civil engineering haijatajwa hapo.

Haya hizo zingine (Maths, Physics, Chemistry) ajira zake zinapatikanaje kirahisi na kwa wingi?
Kumbuka kutofautisha degree ya Ualimu wa Maths/Physics/Chemistry na Degree ya Maths/Physics/Chemistry.
Unachosema ni kweli, ajira zimekuwa ngumu Sana kupatikana, natamani kama nchi ingejikita zaidi kwenye elimu ya vitendo Kwa zaidi ya 70%.
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
Sema vyuo mnavyoenda hampati maarifa.
 
Maths, physics, chemistry?
Civil engineering?
Kwamba havina soko?
Mimi mwenyewe ni mhanga wa kozi mojawapo hapo, sema nilisoma zamani nikapata ajira ambayo haiendani na nilichosomea ndo inaniweka mjini.

Wenye ahueni ni wale waliosomea Bachelor of Science in/with education hao kwa masomo hayo ya PCM wana ajira, ila wale waliosoma Bachelor of science in Maths, phys au chem pamoja na hao wa engr wengi hakuna rangi wanaacha kuiona mtaani.
 
Ajira zipo kwa fani zote, na hazipo kwa fani zote kutegemeana na mhusika anayeitafuta, una connection?

Kama connection unayo hata kama una ufaulu mbaya ajira utapata, lakini kama una pass mark nzuri connection hauna umeumia.

So hizo kozi ulizoweka hapo zina ajira na hazina ajira pia kutegemeana na situation ya mhitimu na wazazi wake, au kama akiwa mtoto wa kike akakutana na boss anamemuelewa ajira ataipata, bahati mbaya ukiwa wa kiume....

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mimi mwenyewe ni mhanga wa kozi mojawapo hapo, sema nilisoma zamani nikapata ajira ambayo haiendani na nilichosomea ndo inaniweka mjini.

Wenye ahueni ni wale waliosomea Bachelor of Science in/with education hao kwa masomo hayo ya PCM wana ajira, ila wale waliosoma Bachelor of science in Maths, phys au chem pamoja na hao wa engr wengi hakuna rangi wanaacha kuiona mtaani.
Mimi siamini kama civil engineer atakosa cha kufanya, siamini kabisa.
 
Back
Top Bottom