Kindeena
JF-Expert Member
- Sep 27, 2017
- 9,061
- 15,805
Nilihitimu elimu ya juu kiwango cha shahada ya kwanza (Sheria).
Ajira zinazotangazwa sana na serikali ni za wenye cheti, na diploma haswa utendaji wa Mtaa ambapo kwa sasa wanahitaji Certificate NTA level 5.
Sasa shida inakuja kwamba, mfano, ikiwa kwenye kada ya Mtendaji Mtaa/Kijiji wanahitaji mwenye elimu ya Sheria ngazi ya cheti, basi mwenye degree hawezi kuajiriwa kwa sababu ya kuzidi vigezo (over qualified).
Ili kujiwekea mazingira mazuri, niliamua kwenda kujiunga chuo kusomea elimu ya jamii ngazi ya cheti, ili niombe kazi ya Mtendaji Mtaa Daraja la 3.
Sasa kinachofanyika hivi Sasa ni kwamba, nilituma maombi ya kazi huko Halmashauri kwa kutumia cheti/Certificate nilichohitimu, Halmashauri nao wanayatuma majina kwenda Sekretarieti ya Ajira, nao Sekretariet wanayachambua na kuondoa wale wenye degree.
Swali ni je, Sekretariet wanajuaje? Ni kwamba, mfano halisi Mimi nina account kwenye website Yao maarufu kama "ajira portal" na huko kuna data kwamba nina elimu ya degree, kwa hiyo wanatumia taarifa hizo kukata majina yetu na hatimaye kuyarudisha Yale ya wenye Certificate pekee kwenda Halmashauri kwa ajili ya usaili na hao hao Sekretariet ya Ajira ndiyo wasimamizi wa usaili.
Hata hivyo ikumbukwe kwamba kanuni za ajira hazizuii wenye degree kuajiriwa bali zinasema kwamba mwenye degree anaajiriwa kama Mtendaji Mtaa/Kijiji daraja la kwanza, diploma daraja la pili na cheti daraja la 3.
Lakini Sasa ngazi ya cheti ndiyo wanapata ajira na ninadhani lengo ni kuajiri watu ambao wataanza kazi na elimu ndogo na mshahara mdogo.
Swali ni kwanini tulisomeshwa na serikali halafu serikali hiyohiyo inatubagua na kutunyanyasa kwenye ajira?
====
Habarini ndugu jamaa na marafiki. naomba kushea kidogo kuna jambo limetukuta sisi tuliofanya usaili trh 9 wa utendaji wilaya ya itilima.
Wakati tupo tunakaguliwa ile siku yule mwenyekiti wa bord ya ajira akasitisha zoezi la ukaguzi akatutangazia mana alikuwa na kalatasi yenye majina mkononi.
wafuatao nawaomba hapa mbele ninajambo nataka kuzungumza nao kabla mtuhani haujaanza tukaitwa watu kama 8 hivi akatukusanya na kutuingiza ndani.
Huko ndani akaanza kutuhoji akasema nyinyi mnachangamoto upande wa vyeti vyenu kuna shida, sisi tukamwambi shida ghani? akasema wakatu tunashortlist mtaalam wetu aliingia ktk mifumo ya ajira yani ajira portal kwenye akaunt zenu mmebainika kuwa na over qualification yani mna elimu ya juu hivyo hamtaruhusiwa kufanya mtihani.
Na hili ni agizo toka serikalini sisi tukahoji mbona tumeomba kwa vigezo vilivyotolewa ktk tangazo kuambatanisha chert cha NTL LEVEL5 kama tangazo lilivyosema yule katibu katujibu kwamba nyinyi mmetoka UEFA mnakuja kuvhecha ndindo haikubaliki waachieni watoto kwa hivyo hamta fanya mtihani. ilibidi tukubaliane nao turudi majumbani je halmashauri zote waliofanya mtihani tarehe 9/9/23 walifanyiwa hivi kama tulivyofanyiwa itilima?
Ni kweli tamko kutoka serikali kuu, je ni halmashauri zote zimefanyiwa hivyo nchi nzima jamani naomba msaada afu wakati tunafanyiwa hivyo afisa usalama wapo mkuu wa takukuru yupo lkn hawakuwa pale kwa ajili ya kututetea bali walikua pale kutukandamiza na nyishoe haki yetu ya msingi inapotea mbele ya macho yao .
Ajira zinazotangazwa sana na serikali ni za wenye cheti, na diploma haswa utendaji wa Mtaa ambapo kwa sasa wanahitaji Certificate NTA level 5.
Sasa shida inakuja kwamba, mfano, ikiwa kwenye kada ya Mtendaji Mtaa/Kijiji wanahitaji mwenye elimu ya Sheria ngazi ya cheti, basi mwenye degree hawezi kuajiriwa kwa sababu ya kuzidi vigezo (over qualified).
Ili kujiwekea mazingira mazuri, niliamua kwenda kujiunga chuo kusomea elimu ya jamii ngazi ya cheti, ili niombe kazi ya Mtendaji Mtaa Daraja la 3.
Sasa kinachofanyika hivi Sasa ni kwamba, nilituma maombi ya kazi huko Halmashauri kwa kutumia cheti/Certificate nilichohitimu, Halmashauri nao wanayatuma majina kwenda Sekretarieti ya Ajira, nao Sekretariet wanayachambua na kuondoa wale wenye degree.
Swali ni je, Sekretariet wanajuaje? Ni kwamba, mfano halisi Mimi nina account kwenye website Yao maarufu kama "ajira portal" na huko kuna data kwamba nina elimu ya degree, kwa hiyo wanatumia taarifa hizo kukata majina yetu na hatimaye kuyarudisha Yale ya wenye Certificate pekee kwenda Halmashauri kwa ajili ya usaili na hao hao Sekretariet ya Ajira ndiyo wasimamizi wa usaili.
Hata hivyo ikumbukwe kwamba kanuni za ajira hazizuii wenye degree kuajiriwa bali zinasema kwamba mwenye degree anaajiriwa kama Mtendaji Mtaa/Kijiji daraja la kwanza, diploma daraja la pili na cheti daraja la 3.
Lakini Sasa ngazi ya cheti ndiyo wanapata ajira na ninadhani lengo ni kuajiri watu ambao wataanza kazi na elimu ndogo na mshahara mdogo.
Swali ni kwanini tulisomeshwa na serikali halafu serikali hiyohiyo inatubagua na kutunyanyasa kwenye ajira?
====
Habarini ndugu jamaa na marafiki. naomba kushea kidogo kuna jambo limetukuta sisi tuliofanya usaili trh 9 wa utendaji wilaya ya itilima.
Wakati tupo tunakaguliwa ile siku yule mwenyekiti wa bord ya ajira akasitisha zoezi la ukaguzi akatutangazia mana alikuwa na kalatasi yenye majina mkononi.
wafuatao nawaomba hapa mbele ninajambo nataka kuzungumza nao kabla mtuhani haujaanza tukaitwa watu kama 8 hivi akatukusanya na kutuingiza ndani.
Huko ndani akaanza kutuhoji akasema nyinyi mnachangamoto upande wa vyeti vyenu kuna shida, sisi tukamwambi shida ghani? akasema wakatu tunashortlist mtaalam wetu aliingia ktk mifumo ya ajira yani ajira portal kwenye akaunt zenu mmebainika kuwa na over qualification yani mna elimu ya juu hivyo hamtaruhusiwa kufanya mtihani.
Na hili ni agizo toka serikalini sisi tukahoji mbona tumeomba kwa vigezo vilivyotolewa ktk tangazo kuambatanisha chert cha NTL LEVEL5 kama tangazo lilivyosema yule katibu katujibu kwamba nyinyi mmetoka UEFA mnakuja kuvhecha ndindo haikubaliki waachieni watoto kwa hivyo hamta fanya mtihani. ilibidi tukubaliane nao turudi majumbani je halmashauri zote waliofanya mtihani tarehe 9/9/23 walifanyiwa hivi kama tulivyofanyiwa itilima?
Ni kweli tamko kutoka serikali kuu, je ni halmashauri zote zimefanyiwa hivyo nchi nzima jamani naomba msaada afu wakati tunafanyiwa hivyo afisa usalama wapo mkuu wa takukuru yupo lkn hawakuwa pale kwa ajili ya kututetea bali walikua pale kutukandamiza na nyishoe haki yetu ya msingi inapotea mbele ya macho yao .